jamaa wamepewa pesa, wamejitoa ufahamu, na kwa kuwa ni wavuta bangi, na ajira ni ngumu, walikuwa tayari kuchukua pesa na kujidharirisha. hayo mambo yako sana kenya. hata manabii wa uongo wanaojidai huponya watu wenye matatizo, hutumia ujanja huohuo kwa kuwanunua watu na kujidai wamepona, ili...
hii ni janja ya waganga wa kienyeji huko kenya. hawa jamaa ni wavuta bangi, mwenye gari ni msanii, wanachotaka ni kupata wateja kwa kutangaza biashara ya huyo mganga.
Fanyeni kazi, Rais anatimiza wajibu wake. Na kama una hoja za msingi, sidhani kutoa matusi kwa kiongozi Mkuu wa nchi ni busara.Tumieni vizuri hizi social media, zinaweza kuwasaidia badala ya kuzodoana.
Utawala wa awamu ya nne, mlikuwa siku zote kumtukana mzee kikwete kwamba anatumia pesa za umma kwa safari, kwamba yeye wakati wote ni kuchekacheka, mlilalamikia ubarifu wa mali za umma zilivyokuwa zinapondwa na wachache na mengine mengi. Leo mmepata Magufuli, hasafiri, hacheki, anabana matumizi...
Kuvunjwa kwa bodi ni kuwajibika kwa Rais. Huyu Rais anafuatlia mambo mengi, madogo kwa makubwa. Nyie mnaona kama vile anachemka, lakini ukweli ni kwamba, kwa wafanya biashara wa kitanzania walivyo, ni rahisi kucheza na bodi, ili washauri wanavyotaka wao. Tusiwe na wasiwasi, tusubiri tuone mwisho...
Watanzania wengi siku hizi tumekuwa watu wa kukatisha tamaa serikali kwa kila jambo. Tunatumiwa na wanasiasa wenye wivu binafsi kutuma ujumbe wa kukatisha tamaa.
Nafikiri ni jambo jema kuwapa pongezi TRA, maana wenye data ni wao, wakusanya kodi ni wao, kuna sababu gani kubeza wanachokifanya. Na mara nyingi tumekuwa tunalalamika hatupati taarifa toka serikalini, sasa hivi tunapewa, tunaponda, baadhi ya watanzania bhana.
Wakati nyie mnaangaika na yaliyopita kuna radio ishaanza kuongea nyakati za usiku inatisha, inatoa, inchambua usalama,polisi ,pssb na vyombo vingi vya dola hawa wa usalama wako wapi madudu yote haya yanatokea.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.