kazi za polisi zinafuata sheria na kanuni vile vile mazingira ndio yanaongoza ukamataji na upekuzi.tambua kuna waizi wa kuku na waizi wenye kutumia bunduki na makosa madogo kama lugha ya matusi .huo ni mfano tu yapo mazingira mengi hatarishi na rafiki
vipi kuhusu upekuzi wa dharula.vipi kumkamata jambazi mwenye silaha .inakuaje kama utapata taarifa kuna vitu vya hatari ktk nyumba au gari kama mabomu ,bunduki nk
suala la ulinzi halina siasa jitafakari mwenyewe ni mambo mangapi yanatokea mbele yako na ukatoa taarifa ili kuzuia uhalifu usitendeke au uvunjaji wa amani .tuwe wazalendo sio kulalamika kwani lazima tushiriki japo kwa kutoa taarifa
jeshi la polisi linafanya kazi kwa kupokea taarifa kutoka kwa raia wote wa nchi.kuwa mzalendo ni pamoja na kutoa taarifa zote zinazoatarisha amani na utulivu,polisi ni watoto kaka dada zetu kamwe hawawezi kutusaliti cha muhimu tushirikiane nao ,lazima wahalifu wapatikane tunaishi nao hawakai porini.
ni muda wa kuungana pamoja kuwabaini wahalifu kwani hata katiba inasema kila mtu ana jukumu la kushiriki ktk ulinzi na kudumisha amani .maadui tunaishi nao ,na kama wanatoka nje tunawapokea sasa tuwe wazalendo kupambana nao kwani wanaweza kumdhuru yeyote.tuungane pamoja kuwatokomeza
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.