Tetesi: Lissu adaiwa kumponza Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji

radika

JF-Expert Member
Jul 15, 2014
20,427
32,196
Lissu.png

Toka chanzo changu nyeti cha habari kimedadavua habari hii kwa uhakika kabisa kwamba kisa cha kutolewa ubalozi mtoto wa sokoine nchini ubelgiji na kurudishwa nchini ni kile kitendo cha yeye kwenda kumjulia hali mheshimiwa Tundu lissu.

Inasemekana bwana mkubwa hakufarahishwa na kitendo cha balozi wetu kwenda kumuona ndugu lissu na kumuona ni msaliti akaenda mbali zaidi na kusema hali kama hiyo aliipitia ndugu Lazaro Nyalundu alipokwenda kumuona lissu kwani wabunge wa ccm walizuiwa kwenda na ndicho chanzo kikuu cha Nyalandu kuamua kuachia ubunge wake na kujitoa ndani ya chama cha mapinduzi ( ccm) kwa kuwa hakuridhishwa na namna ya hilo jambo lilivyokuwa likiendeshwa na mwenyekiti wao.

Kahitimisha kwa kusema kwamba wanachama wao kwa sasa wanahali ngumu mno katika vipindi vyote ambayo wapo ndani ya chama hicho kikongwe.

My take:

Kwa upande wangu naona hili jambo si zuri hasa kwa sisi Watanzania tulishazoea kuishi kwa upendo kwani siasa sio uadui lakini inashangaza bwana mkubwa anapogeuza siasa ni uadui hasa kwa yale majibu yake ya kuomba aachwe afanye atakavyo aje kuulizwa mbele hii kitu inatia shaka mno,

Inakuwaje mtu anasema siasa nazifungia kwa kuwa natukanwa huku nikiwajengea barabara je hizo pesa ni za hisani toka mfukoni kwake? Nakumbuka wanafunzi wa udom waliitwa vilaza sijui kama anakumbuka hizi kauli za kuudhi.

Ukipenda kusifiwa kubali kunakukosolewa hata shilingi ina pande mbili.
 
Pamoja na kwamba anayejua ukweli wa huo uamuzi wa kumrudisha nchini ni Mh.rais, tungejiuliza kwanza hivi kutoka kuwa balozi mpaka kuwa naibu katibu mkuu ikulu ni Demotion (kushushwa cheo) au promotion (kupandishwa cheo) both interms of opportunity and exposure, labda kuanzia hapo ndo tuanze kuunganisha dot.
 
Pamoja na kwamba anayejua ukweli wa huo uamuzi wa kumrudisha nchini ni Mh.rais, tungejiuliza kwanza hivi kutoka kuwa balozi mpaka kuwa naibu katibu mkuu ikulu ni Demotion (kushushwa cheo) au promotion (kupandishwa cheo) both interms of opportunity and exposure, labda kuanzia hapo ndo tuanze kuunganisha dot.
Balozi wa nchi ya marekani na msemaji wa ikulu unamaanisha hivyo au balozi wa Angola na msemaji wa ikulu sio au?
 
Balozi wa nchi ya marekani na msemaji wa ikulu unamaanisha hivyo au balozi wa Angola na msemaji wa ikulu sio au?
Hilo la sijui Marekani na Angola limetoka wapi Mkuu, lakini mada uliyoleta inamzungumzia mtoto wa Sokoine ambaye alikuwa balozi wa Tanzania umoja wa Ulaya ila kupitia mabadiliko madogo yaliyofanyika juzi akahamishiwa ikulu kuwa naibu katibu mkuu, swali langu ni kutaka kujua huko ni kupandishwa cheo ama kushushwa cheo? Naomba unijibu kama ikikupendeza
 
Hilo la sijui Marekani na Angola limetoka wapi Mkuu, lakini mada uliyoleta inamzungumzia mtoto wa Sokoine ambaye alikuwa balozi wa Tanzania umoja wa Ulaya ila kupitia mabadiliko madogo yaliyofanyika juzi akahamishiwa ikulu kuwa naibu katibu mkuu, swali langu ni kutaka kujua huko ni kupandishwa cheo ama kushushwa cheo? Naomba unijibu kama ikikupendeza
Balozi ni mkubwa mkuu.
 
Pamoja na kwamba anayejua ukweli wa huo uamuzi wa kumrudisha nchini ni Mh.rais, tungejiuliza kwanza hivi kutoka kuwa balozi mpaka kuwa naibu katibu mkuu ikulu ni Demotion (kushushwa cheo) au promotion (kupandishwa cheo) both interms of opportunity and exposure, labda kuanzia hapo ndo tuanze kuunganisha dot.
Kwa tafsiri za kikwetu kutolewa Ulaya kurudishwa Bongo ni demotion tosha, haijalishi umerudi kuwa Waziri.
 
Back
Top Bottom