JamiiCheck

A citizen-centered approach in countering misinformation and disinformation Online and Offline by JamiiForums

On JF:

Salaam Wakuu, Nimekutana na maandiko yanadai kuwa Lissu akiwa kwenye mkutano Singida alisema mtoto wa Rais Samia aitwaye Abdul aliwahi kumpelekea rushwa akamfukuza. Je, kauli hii ni kweli? Tunaomba mtusaidie kutafuta uhakika --- Video 1: Lissu akiwa Mkutanoni Singida akielezea kufuatwa na Abdul Video 2: Lissu akieleza kufuatwa na Abdul katika Spaces ya Maria Sarungi
Kumetokea uvumi unaosambaa sana kwenye mitandao ya kijamii kuhusiana na uwepo wa ugonjwa hatari nchini CONGO DRC. Ugonjwa huo unasemekana kuenea na kuambukizwa zaidi kwa njia ya ngono. Pia inasemwa muathirika huugua kwa kipindi Cha muda mfupi sana (kati ya siku 4 Hadi wiki 2) Hadi kupoteza maisha. Naomba wanajukwaa na JamiiForums kwa ujumla tusaidiane kuhakiki habari hii ambayo imekuwa ikisambaa kwa kuambatana na sauti inayoelezea ugonjwa huo pamoja na picha za waathirika na watu wakifanya mazishi (ya anayesemekana kafariki kwa ugonjwa huo) huku wakiwa wamevalia mavazi ya kujikinga mawili mzma na kuacha sehemu ya uso tu. TAHADHARI: Baadhi ya picha sio nzuri kutazama hadharani. Naomba radhi kwa hilo, nazi-attach kama nilivyozipokea...
Kamanda Tundu Lissu amekanusha madai yaliyotolewa hapo nyuma kidogo na Lema kwamba Mbowe ndio aliyeshika chupa ya damu wakati akipelekwa Nairobi kwa matibabu. Amesema aliyeshika chupa ya damu aliyokuwa akiongezewa ni Mchungaji Peter Msigwa mwanasiasa nguli asiyeogopa hila na figisu. Wataalam wa mambo ya siasa za kusini mwa jangwa la sahara wanasema hii kauli imebeba maana kubwa sana.
Katika jamii yetu ya kitanzania asilimia kubwa inatumia vyombo vya plastiki kunywea na kulia chakula, lakini nimekuwa nikisikia kuwa plastiki ina madhara makubwa kwa afya ya binadamu, wapo wanaodai inasababisha saratani, wengine inamaliza nguvu za kiume kwa wanaume na mambo mengi. Je, ni kweli ina madhara? Maana napata mashaka kwani sijawahi kusikia serikali ikisema kuhusu madhara hayo au kukemea matumizi yake wala kutoa elimu ya namna ya kuvitumia.
Alhamisi ya pili ya Mwezi Machi kila mwaka, Dunia huadhimisha Siku ya Figo Duniani ili kutoa ufahamu na kuelimisha umma kuhusu umuhimu wa afya ya figo na magonjwa yanayohusiana na figo. Kupitia maadhimisho haya, watu hupata fursa ya kujifunza kuhusu njia za kuzuia magonjwa ya figo, kudhibiti magonjwa ya figo, na umuhimu wa kuwa na maisha yenye afya ya figo. Aidha, maadhimisho haya huchangia katika kuongeza uelewa wa umma kuhusu haja ya kuchangia katika juhudi za kuzuia na kutibu magonjwa ya figo, pamoja na kusaidia watu wenye matatizo ya figo kupata msaada unaohitajika. Hata hivyo, ugonjwa huu huambatana na dhana nyingi potofu zinazofifisha kasi ya kupambana nao hivyo JamiiCheck imekuandalia ufafanuzi wa Dhana hizo kama sehemu ya...
Imezoeleka kuona watoto wachanga wakiwa wamefunikwa manguo mengi sana, hii sio shida iwapo hali ya hewa inaruhusu yaani ya ubaridi au ya kawaida. IIa kunaweza kuwa na hali ya joto kali watu wazima mnatamani kukaa kwenye feni ila mtoto mchanga bado kafunikwa mablanketi na kavishwa sweta, ukihoji unajibiwa watoto wachanga hawahisi joto. Wapo wanaotetea hoja hii kwa madai tumboni kulikuwa na joto hivyo mtoto hawezi hisi joto bali huhisi baridi muda wote. Je, hii ni kweli?
Kuna video inasambaa twiter na Instagram ikimuonesha mwanaume akiruka dirisha na kukimbia huku akiwa mtu kabisa bila nguo, watu hao wamekuwa wakishare video hiyo na kuweka ujumbe wa MKE WA MTU SUMU wakimaanisha mtu huyo alikuwa na mke wa mtu kisha akafumaniwa ndio anakimbia. Je, ni kweli mtu huyo anakimbia fumanizi na tukio hilo limetokea Tanzania? JamiiCheck, msaada wa kujua ukweli.
Salaam Wakuu, Ikiwa Ligi Kuu ya NBC imeisha leo 28/05/2024 huku Yanga akiwa Bingwa Azam nafasi ya pili na Simba nafasi ya tatu. Kuna tetesi kuwa Simba Sports Club na Yanga SC zitacheza African Football League, Azam FC watacheza CAF Champions League pamoja na Coastal Union. Taarifa hiyo inadai Kombe la Shirikisho limefutwa. Je, kuna ukweli wowote wa taarifa hii?
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…