Habarini
Nimeona hii kitu ikanistua, naomba kujuzwa juu ya huu undugu na kama kweli, wanyama wetu watabaki kweli?
Maana enzi za awamu ya mzee ruksa, mkewe alituhumiwa/shutumiwa kusafirisha wanyama hai kwenda arabuni saivi Rais Samia anasema ataimarisha usafiri wa majini ili kusafirisha wanyama hai.
Nijuzeni kuhusu hili swala
Tangu nikiwa mdogo nilisikia na kuamini kwamba ute/ mapovu yanayokuwa kwenye mimea ni mate ya nyoka. Mpaka kufika wakati huu bado sijajua kama suala hili lina ukweli ama la.
Naomba wataalamu mnisaidie kujua uhalisia wa jambo hili
Kielelezo 1: Picha ikionesha mmea umeachiwa mapovu
Kielelezo 2: Picha ikionesha mdudu aina ya Spittlebugs anayetengeneza Povu kwenye mimea
Video ikionesha namna wadudu aina ya Spittlebugs wanavyotengeneza povu
Picha moja iliyosambaa mtandaoni – ikiwemo hapa JamiiForums – inamuonesha mwanaume mmoja akiwa katika hali mbaya ya kiafya. Maelezo katika picha hiyo yameandikwa kwa lugha ya Kiarabu yakieleza: “Kutoka tetemeko la ardhi la Februari 6, leo ametolewa chini ya vifusi huko Antakya, Uturuki hai na akiwa vizuri. Utukufu ni wa Mungu.”
Picha ya sasa ya Ahmed Al-Sousi (Chanzo: An-Nahar)
Kuna madai mengi mtaani yanayosema kuwa mwanamke akiwa kwenye hedhi husababisha kunyauka kwa mboga na matunda ikitokea amechuma. Mdau mmoja wa JamiiForums amenadika pia kuhusu suala hili.
Baadhi ya tamaduni huwazuia kabisa wanawake wasichume vitu hivyo. Kisayansi, madai haya yana ukweli?
Salaam Ndugu zangu,
Zipo tetesi zimesambaa katika maeneno mbalimbali kwamba ugonjwa wa Covid-19 umerejea nchi. Kwa sisi tunaoishi Dar tunashuhudia kulipuka kwa mafua makali yakiambatana na kikohozi fulani na homa.
Je kuna ukweli kiasi gani kwenye hili?
Jamiiforums tunaomba mtusaidie kuuliza kwa mamlaka ili tahadhari ichukuliwe mapema.
Madai:
Yapo madai kutoka katika jamii mbalimbali yakihusisha rangi nyekundu na radi. Baadhi ya jamii zinaamini kwamba kuvaa mavazi yenye rangi nyekundu wakati wa mvua ni hatari kwa sababu yanaweza kusababisha ukapigwa na radi. Sambamba na hilo jamii nyingine zinaamini Mjusi kafiri na Kondoo wana uwezo wa kupambana na radi.
---
Kumezuka tabia ya waandishi wa habari mkoani Kilimanjaro kujihusisha na utapeli kwa kuchukua fedha za watu (wadau) wakidai ni gharama za kutuma habari lakini kinachotokea ni wizi mtupu.
Juzi mama mmoja wa Uru Mjini wilaya ya Moshi Vijijini ametoa Tsh. laki 4 kwa waandishi wa habari wanne ili waripoti tukio la mtoto wake mwenye Utindio wa ubongo kubakwa na kupewa ujauzito, mpaka sasa waandhi hao watatu wa TV na mmoja wa gazeti wameshindwa kutoa habari yake.
Huu ni utapeli wa aina yake, ni jukumu la viongozi wa Press Club kilimanjaro kuchukua hatua dhidi ya waandishi hawa ambao ni wanachama wenu na hata kama si wanachama wenu wanachafua tasnia ya habari.
Ni hayo tu kwa leo, wasiporudisha tunawaanika chap ili vyombo vya vichukue...
Kuna mwanamama aliwahi nipa ushuhuda kuwa matiti yake yalianza kuanguka akiwa na miaka 23 kutokana na mitomaso aliyokuwa anafanyiwa na mpenzi wake wa kwanza. Aliendelea kwa kusema kuwa, kabla ya kuanza michezo na wanaume alikuwa na chuchu dodo zilizosimama na kuchoma.
Hivi ni kweli kuwa matiti ya mwanamke yanapopapaswa na viganja vya mwanaume hupelekea kuanguka na kuwa ndala?
Hivi ni kweli kuwa watumiaji wa kompyuta mpakato huku wameipakata mapajani, pamoja na sisi tunaotumbukiza simu zetu zikiwa on air kwenye mifuko yetu ya mbele ya suruali tupo kwenye hatari ya kupoteza nguvu za kiume?
Miaka kadhaa nyuma niliwahi kusikia mwanamke mmoja nchini Uganda kajifungua watoto wawili (mapacha) wenye baba tofauti, hali hii ilinishangaza sana.
Hali kama hii iliripotiwa pia Septemba 9, 2022 kwenye jarida la CNBC ambapo mwanamama mmoja kutoka Minerois, Brazil alithibitika kuwa na ujauzito wa mapacha ambao baada ya kupimwa DNA zao ilibainika kuwa walikuwa wa baba tofauti.
Kisayansi, ni kweli kuwa jambo hili linaweza kutokea? Kama jibu ni ndio, linatokeaje?
Hivi ni kweli kuwa ukomo wa kurefuka na kunenepa kwa uume ni miaka 20?
Yaani mtu mwanaume mwenye umri wa miaka 25 au 30, kamwe hawezi ku experience ongezeko la ukubwa wa uume wake?
Kwa maana nyingine, ukubwa wa uume wa mwanaume akiwa na miaka 20, ndio atakaokuwa nao akifikisha miaka 35?
Salaam Wandugu,
Nimepata taarifa mtandaoni kuwa ndege ya Malaysia iliyopotea miaka tisa iliyopita imekutwa kwenye maji ikiwa haina abiria.
Habari hiyo ilichapishwa kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii ikiwamo Twitter linaonesha picha ya mbele ya ndege yenye kutu inayosomeka: “Ndege ya Malaysia MH370 iliyotoweka miaka 9 iliyopita imepatikana chini ikiwa haina abiria. Ndege hiyo ilikuwa na abiria 239.”
Je, kuna ukweli wowote?
Picha inayoenea kwenye mitandao
Picha ya ndege ya Lockheed Martin L1011 Tristar kwa upande wa pembeni
Source: Deepbluedivecenter
Video credit: Deepbluedivecenter
Ikatokea mwanaume amemwaga manii kwenye taulo ambalo muda mchache baadae mwanamke akalitumia kukaushia uke wake.
Kuna uwezekano akapata ujauzito kupitia taulo hilo?
Kwa muda mrefu sasa yamekuwepo madai yanayosema kuwa Mtoto mchanga ukimtazamisha kwenye kioo au Mwanga wa jua kabla ya siku 40 hupata Makengeza.
Naomba kufahamu ukweli kuhusu jambo hili.