Zipo imani na madai ya mbalimbali ya kijamii yanayobainisha namna ambavyo mama anaweza kumdhoofisha (kumbemenda) mtoto wake baadhi ya madai hayo ni:
1. Baba na Mama hawapaswi kujamiiana wakati kipindi cha unyonyeshaji kwa sababu kufanya hivyo hupelekea mtoto wao kudhoofika (kumbemendwa).
2. Lazima mama aoge ajioshe na sabuni kwanza baada ya kujamiiana ndipo amnyonyeshe mtoto wake ili asimbemende.
3. Mama akipata ujauzito wakati bado ananyonyesha anaweza kumbemenda mtoto wake.
4. Mzazi akijamiiana nje ya ndoa akishiriki tena tendo na mwanamke wake anayenyonyesha anambemenda mtoto.
Nimeona taarifa mtandaoni ikisema watumishi wa Umma na Binafsi ambao wamechangia kwa zaidi ya miezi 108 yaani miaka 9 katika NSSF au PSSSF sasa rukhsa kutumia michango yao kama dhamana ya kuchukulia mkopo wa kujenga, kuboresha au kununua nyumba nchini Tanzania.
Kanuni namba 141 za Mwaka 2024 zimeanza kazi tangu Machi 8, 2024.
JamiiCheck tusaidieni kujua ukweli wake.
Wakuu mko salama?
Nimekuwa nikisia stori nyingi kuhusu nanasi, kuwa ukila unafanya uke kuwa na harufu nzuri, wengine wanasema unaongeza "ladha", yaani ute/maji maji yanakuwa na utamu kama vile umechanganywa na sukari hivi?
Kuna ukweli kwenye hili wataalam wa JamiiCheck?
Wakuu,
Nimekutana na taarifa imepostiwa na Times FM ikiwa na maneno yanayodaiwa kutamkwa na Kiongozi Mkuu wa Korea Kaskazini Kim kuwa anashangaa jinsi wazungu walivyofaulu kuwaaminisha Waafrika kwamba mitala ni dhambi lakini LGBTQ+ ni haki ya binadamu. Waafrika wanapaswa kujifunza jinsi ya kufuata dini zao. Hadi siku Waafrika wakifuata utamaduni wao wenyewe, dini za kigeni wakizikumbatia hawataweza kamwe kujiendeleza.
Naomba kufahamu ukweli wa taarifa hii, maana nimependa sana haya maneno nataka niitumie sehemu.
Katika mitandao ya kijamii nimeona video inayohusishwa na Rais Mpya wa Senegal, Bassirou Diomaye Faye, akikemea Ufaransa kuwa ni wakati wa kuondoka bara la Afrika.
Video hiyo inamuonesha Rais Faye akiimbia Ufaransa kuwa "Inakuwa wakati wa Ufaransa kuinua magoti yake kutoka shingoni mwetu na kumaliza ukandamizaji huu usio wa haki. Karne nyingi za mateso, biashara ya binadamu, ukoloni, na ukoloni mamboleo vimesababisha mateso yasiyohesabika. Ni wakati wa kumaliza mzunguko huu wa ukandamizaji,"
Wachangiaji wengi kwenye video hizo zinazozunguka mitandaoni walionesha furaha kwamba Rais Faye ameonesha msimamo imara dhidi ya Ufaransa kulikandamiza bara la Afrika.
Video hiyo inanipa mashaka.
Kumekuwa na dhana ya kwamba ukijikata na jeraha kuanza kutoka damu basi ukipulizia Pafyumu damu inakataa na kidonda kukauka.
Je, kuna uhalisia wowote? Na kwa upande mwengine kuna madhara yeyote kwenye hili?
Picha hii inadaiwa kuwa ya Rais Mteule wa Senegal, Diomaye Faye akiwa na mke wake.
JamiiCheck naombeni ufafanuzi maana nimewahi kuiona sehemu fulani sikumbuki ni wapi, lakini ilikuwa inamzungumzia mtu mwingine kabisa.
CAF wamethibitisha kuwa kwenye michuano ya AFRICAN FOOTBALL LEAGUE hakuna kanuni ya goli la ugenini (away goal rule) hivyo mechi ya Simba na Al Ahly ni mpya kabisa kule Cairo, yani lazima timu ishinde kuvuka nusu fainali. - Farhan kihamu jr
Nimeona taarifa hiyo kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii kuwa mwanaye huyo ameteuliwa kuwa Gavana wa Benki Kuu ya Uganda.
Wengi wamehusisha uteuzi huo kuwa ni kuimarisha familia yake ambapo Mkewe Mama Janet Museveni ni Waziri wa Elimu kwenye Serikali, Mwanaye wa Kwanza Muhoozi ni Mkuu wa Majeshi ya Uganda.
Mtumiaji wa Mtandao wa Twitter anayejulikana kwa jina la MchiziMox Juni 8, 2023 amechapisha andiko linalosema kuwa aliyekuwa mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya amefariki dunia kwa kupigwa risasi.
Ukweli wa taarifa hii upoje?
Habari wakuu,
Kumekuwa na mawazo tofauti juu ya hatari ya mnyama Nungunungu. Kuna baadhi wanaamini kuwa Nungunungu hurusha miiba kujilinda na adui yake wakati wengine wanadai mnyama huyu harushi miiba bali huitegesha na adui hujichomesha mwenyewe.
Je upi ni ukweli hapa?
---
Picha: Nungunungu akiwa amesimamisha miiba yake (Credit: AnimalSandiegoZoo)
Nimesoma habari huko mtandaoni nimepata mtatiziko kidogo baada ya mwandishi kuandika watu wenye group B msile kuku, na wakati mimi kuku ndio moja ya kitoweo changu pendwa sana.
Msaada hapo wa kuhakiki taarifa hii iwapo ni kweli kuku si salama kwa wenye damu group B
Nani asiyemjua mbabe Simba mfalme wa nyika? Yaani ukutane naye paaah! Utamzame machoni aone aibu na kuondoka? Bado siamini hili jambo naona hawa vijana wa ovyo wanataka kuniingiza chaka siku nikikutana naye mbashara nisichukue njia nyingine za kujiokoa eti nimtizame.
Hivi kweli Simba huyu kweli wa kumwonea aibu binadamu kisa kumuangalia machoni ana kwa ana kwa ujasiri.
Wakuu naombeni taarifa sahihi kuhusu hili jambo, huenda mada ikawa kichekesho lakini hili jambo linasemwa sana mtaani.
Salaam ndugu zangu,
Nimekutana na video ya kusikitisha ikimuonesha raia anayesemekana kuwa ni raia wa Tanzania Bara akichapwa viboko na Raia wa Zanzibar kwa kosa la kula mchana wa Ramadhani. Je video hiyo ni ya mwaka huu?
Salaam Wakuu,
Nimekutana na stori mtaani zinadai kwamba mnamo mwaka 1990 Bondia Maarufu Muhamedi Ali alienda nchini Iraq kuzungumza na rais wa nchi hiyo wakati huo Sadam Hussein kuwaachia mateka wa Marekani na kufanikiwa.
Je, kuna ukweli wowote kuhusu sakata hili?
Tunaombeni ufafanuzi
======
Muhammad Ali alizaliwa mnamo 17 Januari 1942 na alifariki 3 Juni 2016. Muhammad Ali alikuwa mwanamasumbwi kutoka nchini Marekani.
Awali alijulikana kama Cassius Clay, lakini alibadilisha jina lake baada ya kujiunga na jumuia ya Kiislamu ya Nation of Islam mnamo mwaka wa 1964. Baadaye akabadilisha dini na kuwa Mwislamu kunako mwaka wa 1975 Ndipo alipobadili jina na kuanza kufahamika kama Muhammad Ali.
Alipata kuwa bingwa wa uzito wa juu mara...
Vifo vinavyotokana na ugonjwa wa homa ya ini vimeripotiwa Kuongezeka kwa kasi barani Afrika.
Pia, baadhi ya nyaraka zinazosambaa kwenye mitandao ya kijamii zinaonesha kuwa idadi ya visa vya ugonjwa huu vimefikia zaidi ya milioni 90.
Ukweli wa taarifa hizi upoje?
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.