Mwanasiasa mkongwe William Lukuvi amefariki Dunia, asubuhi ya Machi 25, 2026 katika Hospitali ya Benjamin Mkapa, Dodoma alipokuwa akipatiwa matibabu ya ugonjwa wa mshtuko wa moyo.
Taarifa ya msiba wa William Lukuvi, aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) na Mbunge wa Jimbo la Isimani, imetangazwa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Kusiluka. Lukuvi, alizaliwa Agosti 15, 1955 na amewahi kuwa Mbunge kwa vipindi saba tangu mwaka 1995.