Zitto kugombea urais 2015?

Status
Not open for further replies.
Nimeona clip ya kampeni zake kwenye face book ya zito akiwauliza wananchi waliohudhiria kampeni zake "2015" wao wanajibu "Urais"
 
Kama hizi taarifa ni za ukweli, Zitto atakuwa amechemsha! Kugombea kiti cha uraisi labda kama atagombea binafsi, lakini yeye anajua mchakato mzima wa kugombea uraisi katika chama chake Chadema.

Huu sio wakati wake kugombea uraisi kupitia CHADEMA, lazima apate ridhaa ya Chama, sio kujiamulia yeye mwenyewe. Zitto, saa nyingine unakua mropokaji na kukosa busara...which leaves me with so many questions for your drive to become a president!!
 
Nafikiri zitto atatoa taharifa rasimi kuhusu hili mimi nilipoona anaongea nilishutuka kabisa urais haukimbiliwi hivi hivi. namshauri asubiri miaka ishilini ijayo. Na pia azungumzie sana ubunge maana bado hajachaguliwa kuwa mbunge. halafu hiilo la kutokuwa jangwani ni swala zito sana.
 
Mbwembwe, Kiburi, ujuaji na majivuno ya Zitto yataishia mwaka huu kwani vichwa kama Tundu, Rwakatare, Nyimbo Thomas vinaingia CHADEMA huku kijana muadilifu na mchapakazi Myika JJ akiukwaa Ubunge kwa kishindo. sasa CHADEMA itakuwa na vichwa vya kutosha na huyu bwana itabidi ama ajirekebishe au akimbie chama maana CHADEMA si chama cha kubebana. wapi walipo akina Shaibu Akwilombe, Walid Amaan kabouru, Danda na David Kafulila? hawa wameondoka na CHADEMA imezidi kupaa na kupata vichwa vipya kama akina CHACHA WAITARA MWITA MWIKABE

NAJUA zitto ni mwana JF

Tafadhari jirekebishe maana wananchi hawakuamini tena!

Have some respect kwa watu na wakubwa zako hasa MBOWE mtu aliyewekeza sana kwako akiamini utakuwa mrithi sahihi na msaada wa mageuzi. Nakumbuka enzi zetu za siasa za DARUSO na jinsi MBOWE alivyokuwa akitinga chuoni kukusupport niliposikia unataka kumchallenge nilishtuka na kusema wahenga walikuwa sahihi.

SHUKRANI ZA PUNDA NI MATEKE
 
Nimemchoka kweli nahuyu kijana, kweli ngoma ivumayo sana haidumu. Nilitazama TBC sikuamini macho yangu, nikajiuliza ni chama gani? anataka Slaa amsafishie njia? au ana hama Chama? huyu kijana anahitaji washauri wa karibu wenye busara. au nataka kukubaliana na mwandishi mmoja wa habari alipata kuandika kuwa vijana ni taifa la kesho alipokuwa akimchambua marehemu Amina Chifupa, miaka kadhaa iliyopita, busara hamna kabisa, tunaongozwa na sifa na ushabiki wa watu tu. Ni wazi kwamba si upiganaji au kutetea haki za wananchi ni ubinafsi tu, iliyobaki nipige tu kazi siasa ni longolongo. Ama kweli dunia hadaa ulimwengu shujaa.
 
Source tafadhari.....
kuna taarifa kuwa leo zitto katoa tamko rasmi kuwa ana mpango wa kugombea urais wa tanzania mwaka 2015 na akawaomba wananchi wampe kura nyingi ili apate hadhi ya kuweza kugombea urais wa nchi hii.

Kila la heri mkuu zitto, walau una nia!
 
Siamini km kweli kuna baadhi ya watu bado wanamwamini zitto.............anaonekana ni mtu anayefanya kitu fulani kwa malengo fulani....mimi binafsi sijawahi kumuamini tena kwa mara ya pili pale nilipositukia kuwa kumbe alinunuliwa na wazee wanne (lowasa,rostam,kikwete,hosea) wa richmond ili atumie kukubalika kwake kuwashwishi watz kununua mitambo ya richmond..................yaani pale tu ndipo nilipomuona zitto ni kijana wa aina gani.........kwa maana nyingine zitto hayupo kwa maslahi ya taifa ni mtaka sifa fulani tu na mvurugaji na wakati wowote anaweza kuhamia ccm kwani hana msimamo huwa anaangalia upepo unavyovuma....ni kweli anaweza kugombea 2015 lakini naamini ana vision kali sana kwani anajua lazima atahamia ccm...........ni mchokonozi kwa maslahi yake tu na kwa kweli ilimsaidia sana lakini watu wanstuka kutokana na mwenendo na anavyoyachukulia mambo...................
Nilitegemea kipindi kile angekuwa mtu wa kwanza kabisa kuishauri serikali kubinafsisha mitambo hiyo ya kampuni feki na ambayop haipo lakini badala yake alikuwa tayari hata tuvunje kanuni/sheria za manunuzi za umma kwa kilekile anacholilia lowasa kwa ilikuwa lazima kulipa tenda kampuni hii ya kwake binafsi aliyoamua kuipa jina la richmond (richard monduli) yaani mtotowake.....
 
Kigezo cha umri tayari ni kikwazo by 2015 hatakuwa na 40 years.
Nina wasi wasi nae sana bse mbona ata Jangwani hakuwepo siku ya ufunguzi?
Jina nilishuhudia live via TBC akitangaza nia ya kugombea 2015 au alijua bse ameiongela uko mwisho wa reli hatutaipata?
 
Siamini km kweli kuna baadhi ya watu bado wanamwamini zitto.............anaonekana ni mtu anayefanya kitu fulani kwa malengo fulani....mimi binafsi sijawahi kumuamini tena kwa mara ya pili pale nilipositukia kuwa kumbe alinunuliwa na wazee wanne (lowasa,rostam,kikwete,hosea) wa richmond ili atumie kukubalika kwake kuwashwishi watz kununua mitambo ya richmond..................yaani pale tu ndipo nilipomuona zitto ni kijana wa aina gani.........kwa maana nyingine zitto hayupo kwa maslahi ya taifa ni mtaka sifa fulani tu na mvurugaji na wakati wowote anaweza kuhamia ccm kwani hana msimamo huwa anaangalia upepo unavyovuma....ni kweli anaweza kugombea 2015 lakini naamini ana vision kali sana kwani anajua lazima atahamia ccm............

Hivi niwaulize wana JF mlisha kaaa mkajiuliza hawa watu na kuangalia back ground zao.(Lowassa,Rostam,Kikwete,Hosea,Mbowe,Zitto) hizi kesi ni danganya toto nawambieni

 
Jamani
Mimi naona msubiri kidogo kumhukumu Zitto. Yeye kawauliza watu waliohudhuria mkutano, na wao wakajibu "urais", TBC wakadaka ili kukuza mpasuko ndani ya Chadema. Mimi naona suala hili linakuzwa na vyombo vya habari tu. Mwacheni Zitto apambane kurudi mjengoni, mengine tuwaachie wananchi. Kutokuwepo Jangwani, ni wengi hawakuwepo.
 
Zitto hajui kuwa ktk siasa usiangalie mbele na kuruka kihunzi kilichopo mbele yako sasa. Badala ya kulenga ktk kushinda ubunge kwenye uchaguzi ujao yeye anaanza kutangaza nia za mwaka 2015.....to me that demonstrates poor judgment. Hafai kuwa raisi huyu kwa sababu nyingi tu.....
Mkuu unamdisregard Zitto very unfair.
kwa hiyo unasema mwaka 2015 akisimama Zitto hautampa kura yako hata kama CCM wamesimamisha jiwe? na vyama vingine havitasimamisha wagombea
just to say!!!
 
heee.............hata kikwete alikuwa aling'anag'ania hivyohivyo..matokeo yake kila mtz anajuuta kumjua
Hivi niwaulize wana JF mlisha kaaa mkajiuliza hawa watu na kuangalia back ground zao.(Lowassa,Rostam,Kikwete,Hosea,Mbowe,Zitto) hizi kesi ni danganya toto nawambieni
 
Mkuu unamdisregard Zitto very unfair.
kwa hiyo unasema mwaka 2015 akisimama Zitto hautampa kura yako hata kama CCM wamesimamisha jiwe? na vyama vingine havitasimamisha wagombea
just to say!!!

Kwanza kabisa, huyo Zitto hawezi kuwa nominee wa chama chochote.

Pili, ikitokea miujiza amekuwa nominee kura yangu hatapata.
 
Jamani
Mimi naona msubiri kidogo kumhukumu Zitto. Yeye kawauliza watu waliohudhuria mkutano, na wao wakajibu "urais", TBC wakadaka ili kukuza mpasuko ndani ya Chadema. Mimi naona suala hili linakuzwa na vyombo vya habari tu. Mwacheni Zitto apambane kurudi mjengoni, mengine tuwaachie wananchi. Kutokuwepo Jangwani, ni wengi hawakuwepo.
It si true kwa nini TBC waone hiyo ndiyo habari na kuacha mambo mengine, mbona hawarushi habari nyingi za mikutano ya Slaa, wenyewe wakiona kitu controversial kwa Chadema ndiyo inakuwa habari ili waonekane wanaripoti habari za Chadema. Ni sawa na gazeti la Habari Leo wao wanachoona ni mambo ya ndoa ya Slaa tu huo si uandishi bora ni bora uandishi.
 
Mkuu unamdisregard Zitto very unfair.
kwa hiyo unasema mwaka 2015 akisimama Zitto hautampa kura yako hata kama CCM wamesimamisha jiwe? na vyama vingine havitasimamisha wagombea
just to say!!!
Zitto ana wafuasi wengi sana KIgoma. Kama kweli Zitto kasema hayo maneno yatamaliza Dr Slaa kwa wana Kigoma na kumjenga Kikwette.Wafuasi wake wengi wataona ni bora wamchague Kikwette ili Zitto apate nafasi ya kugombea 2015
 
Huyu Zitto huyu na mambo yake yenye kuacha maswali mengi;

-Alipendekeza mitambo ya Dowans itaifishwe, baadae akasema inunuliwe.
-Alipendekeza liundwe jopo la majaji kuchunguza Richmond...Rostam naye ali support
-Atafanya maamuzi makubwa ambayo hayajawahi kufanywa na mtu yoyote Tanzania
-Kusifia uongozi wa Kikwete kila kukicha.
-Alisema atamsaidia mgombea wa NCCR kwenye kampeni.
-Role models wake wote ni ccm.

This guy is a time bomb just waiting to go off


Naomba niongeze hapo kidogo Mkuu. Siku tatu ama mbili kabla ya Uzinduzi wa kampeni ya Chadema pale Jangwani, Kabwe Zito alitoa tangazo la Nusu Ukurasa kwenye gazeti la Mwananchi akiomba michango kutoka kwa Watanzania wanaotaka mabadiliko. Akaunti za kuingiza michango hiyo zilikuwa za kwake binafsi CRDB na NMB kama sikosei. Fair enough, some of you might say.

Lakini katika toleo hilo hilo Chama cha CUF nacho kilikuwa kimetoa tangazo la ukurasa mzima la kuwaomba wanachama na wananchi kwa ujumla kuchangia CHAMA akaunti mbili zilizotangazwa za kupokea michango zilikuwa za CHAMA na sio Maalim Seif ama Profesa.
Hili mimi lilinichanganya mno.

Ilikuwaje Zito atoe tangazo la nusu ukurasa gazeti la Mwananchi kuomba mchango binafsi kwa ajili ya kutetea ubunge wake kutoka kwa wanachama na wananchi siku mbili/tatu kabla Uzinduzi wa Kampeni ya Chadema badala ya kufanya kama walivyofanya CUF cha kuomba michango kama Chama na sio mtu binafsi??

Haiwezekani kwamba kuna wanachama na wananchi walimchangia wakidhani kuwa wanachangia Chama na kumbe walikuwa wanachangia Mbunge mmoja?

Kama aliona wazo la kutoa tangazo gazetini ni jema kwa nini hakufanya juhudi za kufanya tangazo hilo kuwa la Kichama zaidi, kama lilivyokuwa la CUF, na badala yake akalifanya la kibinafsi zaidi??
Kwa hakika, na mimi naanza kuwa na wasiwasi kuwa the Guy is literally a Time Bomb just waiting to go off.
 
that is kigoma........kigoma wana nini cha ajabu....wakimkubali kigoma NDIYO BASIIIIII...............KUNA SEHEMU ZA MUHIMU KWA MGOMBEA KUKUBALIKA KWANZA NDIPO USEME FULANI ANAKUBALIKA SEHEMU FULANI NA WALA SIO KIGOMA..............
It si true kwa nini TBC waone hiyo ndiyo habari na kuacha mambo mengine, mbona hawarushi habari nyingi za mikutano ya Slaa, wenyewe wakiona kitu controversial kwa Chadema ndiyo inakuwa habari ili waonekane wanaripoti habari za Chadema. Ni sawa na gazeti la Habari Leo wao wanachoona ni mambo ya ndoa ya Slaa tu huo si uandishi bora ni bora uandishi.
 
Ni vizuri kujua mapema zaidi maana nitakuwa nyuma yake na pia ni vizuri kujua azma ya mtu mwenyewe, kwa hilo sina wasiwasi na Zitto
 
Zitto ana wafuasi wengi sana KIgoma. Kama kweli Zitto kasema hayo maneno yatamaliza Dr Slaa kwa wana Kigoma na kumjenga Kikwette.Wafuasi wake wengi wataona ni bora wamchague Kikwette ili Zitto apate nafasi ya kugombea 2015
Conclusion yako butu, unamaana wafuasi wa Zitto wakimpa kura Kikwete ndipo Zitto atapata nafasi ya kugombea 2015, mbona havina uhusiano.
 
Mnampaisha bure......there are many thingsajendas hiden on the back of zitto..........what out!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom