Zitto kugombea urais 2015?

Status
Not open for further replies.
km anajua katiba basi umri haumruhusu na hivyo hawezi, alishawaambia hata wananchi yake jimboni kuwa 2015 atagombea uraisi ana haki kikatiba ya kuchagua na kuchaguliwa
 
kwa kusema ukweli kutoka moyoni mimi sio mshabiki wa CHADEMA ila kama ZITTO KABWE angekuwa ametimiza umri wa kugombea urais na angeteuliwa na chama chake kugombea mi naona angefaa kwa mtazamo wangu
 
Nakisikitikia chama kitakachompa zito ridhaa ya kugombea kwa tiketi yake, maana kitapigwa mweleka mkali sana sana. Zito hajawa na busara za kutosha kuweza kuongoza nchi. Kwanza ana papara sana na ni mtu wa kuuma huku na huku. Kwa ujumla hana msimamo kabisaa.
 
kwa kusema ukweli kutoka moyoni mimi sio mshabiki wa CHADEMA ila kama ZITTO KABWE angekuwa ametimiza umri wa kugombea urais na angeteuliwa na chama chake kugombea mi naona angefaa kwa mtazamo wangu

Mkuu naona una maslahi binafsi na zito wewe, hatuwezi kukubali zito akagombea. Wanaotaka Zitto agombee ni wale waliotufilisi waTZ wanahofu simba wa vita Dr W. Slaa akiingia madarakani watakuwa wana hali mbaya kiuchumi na kisiasa kwa watarudisha vitu vyote walivyovikwapua enzi zao.
 
I dont think if Zitto can afford that position; He better leave that chance to the one trusted by the citizens:

Ask people how do they think of Zitto? Zitto is good th*for the current position and not otherwise:
 
Kuna taarifa (toka TBC1) kuwa leo Zitto katoa tamko rasmi kuwa ana mpango wa kugombea urais wa Tanzania mwaka 2015 na akawaomba wananchi wampe kura nyingi ili apate hadhi ya kuweza kugombea urais wa nchi hii.

Kila la heri mkuu Zitto, walau una nia! Je, katiba itabadilisha


UKWELI UKO WAZI,KULIKO KMPA ZITTO URAIS BOORA LOWASA...
 
kwa kweli huyu kijana nimemfuatilia kwa muda mrefu na kugundua ni miongoni mwa viongozi wa chache ambao wana nia ya dhati ya kuwakombania wananchi wa nchi hii ya Tanzania


pia ni kijana mwenye maono na uwezo wa kujenga hoja, ni mtu mwenye kujiamini na kuwa tayari kuusimamia na kuutetea msimamo wake

ni mtu asiendeshwa na emotion kama viongozi wengine, ni kiongozi pekee karibu vyama vyote vya siasa na wasiokuwa na vyama wanamuheshimu na kumpenda


kwa kweli zitto anafaa Lowassa pia ni mchapa kazi na ana maono ya mbali. Kama ndiyo vigezo vyako ni hivyo.
 
Hivi Watanzania mna tatizo gani?
Zitto kweli anaweza kufananishwa na Lowassa? kwa kipi hasa kwa Ufisadi au hapendeki kwa sababu mnafikiria hapendiki hivyo yeye na Lowassa lao moja.

Nimeyasoma maelezo mengihapa na la msingi poengine ni hilo la Umri lakini haya mengine jamani mbona mnamchukia Zitto kiasi hicho kwani yeye kafanya nini hasa ambalo hastahili kugombea Urais! au kwa sababu chaguo lenu ni Dr.Slaa ambaye nina hakika hawezi tena kugombea urais hata kama mtapenda agombee kwani nafasi yake kuchukua ushindi ilikuwa mwaka 2010 na sidhani kama nafasi hiyo itatokea tena kirahisi ikiwa siasa za Chadema zitaendelea kuwa na jazba kiasi hiki..

Labda niwafahamishe tu kwamba siku zote ushindi ktk chaguzi nyingi humfuata mtu asiyekuwa na jazba, mtu wa watu na maarufu kwa uwezo wake ktk kukabiri matatizo na sii kujihami ama kulaumu..Na kama Chadema tutaendelea kujibizana ktk malumbana ambayo hayana tija kwa wananchi mtapoteza hata umaarufu uliojengwa kwa muda mfupi sana.

Kama kweli Zitto ametangaza nia ya kugombea mwaka 2015 ni jukumu letu kumtakia kila la kheri wa sababu tunajua katiba hamruhusu..Lakini kama inamruhusu sioni tatizo hata kidogo ikiwa yeye mwenyewe anajiamini na hizo sababu zenu za kushindwa kwake ziwe sababu ya nyie kutompa kura zenu lakini msitumie sababu zenu kuwa ndio hitimisho la nukuu za Fareed ambaye nina hakika ameandika haya makusudi kumkashifu Zitto.

Mimi huandika jinsi navyomtazama Zitto, na nimewahi kusema Zitto bado hajakomaa kisiasa ni mtumishi mzuri wa Umma lakini bado anashindwa kuelewa kwamba Siasa ni mrengo ambao una Principal zake na uwezo wa kuongoza hautunukiwi na binadamu bali majawaliwa. Huwezi ku force watu wakuelewe kisiasa bali siasa ni kama taa inayotoa mwanga wa mafanikio badala ya uwezo wa mtu mmoja. Tofauti na fikra hizi Zitto amekuwa akijiamini sana yeye badala ya kusimamia nguzo za Uchadema. Ni hizi nguzo ndizo zilimpa umaarufu na hizi nguzo ndizo pekee zitaweza kuondoa umaarufu wake kama atashindwa kuzisimamia..

Na ni makosa haya haya yanatumiwa leo na Viongozi wa Chadema ambao kama Zitto wanataka sana wananchi wakubali uwezo wamtu mmoja mmoja kama Dr.Slaa na kina Lissu badala ya kusimamia mwongozo ambao ndio nguzo ya chama. Na ndio maana unawakuta ktk malumbano na mijhadala mikali isiyohusu kabisa mwelekeo wa chama bali nafsi zao ktk ujenzi wa majina yao. Again ni mwongozo wa chama ndio umewapa Chadema umaarufu na pasipo nguzo hizi Chadema itaanguka kama watashindwa kuzisimamia wakaingia ktk malumbano yasiyokuwa na tija ila kuunda makundi ya chuki na unafiki.

Wakuu zangu, tunapoteza kabisa tunu hii ya demokrasia kwa dhana kwamba demokrasia inatupa haki na nafasi ya kutoa maoni yetu pasipo kufikiria athari za maoni binafsi ktk jamii. Na hakika tunaruhusiwa kutoa maoni yetu kama yetu na sii kujumuisha watu wote kuwa na upinzani na mtu ambaye wewe humpendi ama huoni uwezo wake kutokana upinzani wake..Ila tunachotakiwa ktk maoni yetu ni kuainisha yale mabaya anayosimamia mtu huyo iwe Zitto au Dr.Slaa na kuyapinga kwa kutumia ushahidi unaodhihirisha kinyume..

Lakini maajabu ni kwamba ktk uwanja huu wa great thinkers watu wanapinga tu ili mradi wanampinga mtu pasipo uorodhesha yapi mabaya yenye mantiki ambayo yanaonyesha udhaifu wa hoja ama uwezo wa mhusika. Dr.Slaa analaumiwa kwa Ukristu wake, ati kwa sababu alikuwa Padre basi hafai kuwa rais!.. hii kweli ni akili za watu wanaojiita great thinkers! kisha Ati Zitto ni sawa na Lowassa mara Mbowe ni Mchagga ili mradi tu kuonyesha udhaifu wetu ktk kujenga hoja..

Mbona hao wagombea wa CCM kina Lowassa mnawapa nafasi kubwa ya ushindi ingawa hawatakiwi na wananchi? ni vigezo gani mnavyotumia jamani ama utasikia Mwandosya, Magufuli, na wengine wakitajwa kwa fahari kana kwamba CCM haina mwongozo isipokuwa watu kama hawa ndio wataleta mageuzi na kuboresha maisha ya wananchi. Hawa wote ni wanaCCM kama alivyokuwa JK hawawezi kufanya lolote kinyume cha Azimio la Zanzibar ambalo wote hawa wanalitetea na wataendelea kulitetea kwa nguvu zote.
 
Nilikuwa pale kijiweni maeneo ya kariakoo kuna wajamaa fulani walikuwa wanajadili kuhusu fununu zilizotanda kuwa Zitto amewahi kusema jukwaani kuwa.."nikija tena 2015 sio tena ubunge bali nakuja kuomba kura za urais.." mimi sikumbuki kuwahi kusikia kauli kama hii hivi ina ukweli wowote? je ni kweli Zitto anataka kuwania urais? na imani kuwa Mh Zitto upo humu jamvini hebu tujuze mkuu.

Kwa maana naandaa documentary juu ya mbio za urais 2015 kuhusu Tanzania inahitaji mtu wa namna gani? sasa ili nisije kukuonea au kukupendelea Mh Zitto naomba uniambie hapa mbele ya wanajamvi hivi kuna ukweli juu ya fununu hizi? au ni mambo ya kuzusha tu?
 
Nilikuwa pale kijiweni maeneo ya kariakoo kuna wajamaa fulani walikuwa wanajadili kuhusu fununu zilizotanda kuwa Zitto amewahi kusema jukwaani kuwa.."nikija tena 2015 sio tena ubunge bali nakuja kuomba kura za urais.." mimi sikumbuki kuwahi kusikia kauli kama hii hivi ina ukweli wowote? je ni kweli Zitto anataka kuwania urais? na imani kuwa Mh Zitto upo humu jamvini hebu tujuze mkuu.

Kwa maana naandaa documentary juu ya mbio za urais 2015 kuhusu Tanzania inahitaji mtu wa namna gani? sasa ili nisije kukuonea au kukupendelea Mh Zitto naomba uniambie hapa mbele ya wanajamvi hivi kuna ukweli juu ya fununu hizi? au ni mambo ya kuzusha tu?

Kwa hiyo unaandaa documentary kupitia JF?

You mustbe crazy, kuna siku ulisema unahitaji msaada una kipaji cha kuandika nakala, bado sijaona hicho kipaji, is just because you have time to do so.

Sasa kupata number ya simu ya Zito ni rahisi sana, mwombe Invisible atakupa, nenda ofisi za bunge, nenda ofisi za chadema, tafuta osifi yake..ANDAA INTERVIEW NA ZITO muulize, kila kitu

acha huu utoto na ujinga wa kuuliza mambo personal ya mtu kupitia thread za JF!! title iko clear unamuuliza Zito, kwa nini unamuulizia humu?

sidhani kama ww ni mwandishi wa habari, sidhani kama umesomea, ila COMMON sense is what counts!
 
Mpaka mwaka 2015 sitampigia kura yeyote tofauti na Dr.SLAA. Kama hatokuwepo ktk karatasi ya kupiga kura,mi ntaandika jina na kuweka tiki.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom