pappilon
JF-Expert Member
- Jan 27, 2015
- 3,192
- 3,556
Utakuwa mkutano mkubwa wa aina yake kuwahi kufanyika kwa siku za hivi karibuni katika shughuli za kisiasa nchini.
Mkutano huo utakaofanyika Jumatano, Julai 22, 2015 kuanzia majira ya saa 8 mchana utahudhuriwa na Viongozi wakuu wa Chama wakiongozwa na Mwenyekiti wa Chama Taifa Freeman Mbowe, Katibu Mkuu Dk. Slaa, Makamu Mwenyekiti Bara Prof. Abdallah Safari.
Viongozi wengine waandamizi watakaokuwepo ni; NKMZ John Mnyika, NKMZ Salum Mwalimu, Mjumbe wa KK Prof. Baregu, Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini Arcado Ntagazwa na Mwenyekiti wa BAWACHA Taifa Halima Mdee, ambao wote watahutubia taifa kutokea Uwanja wa Magomeni jijini Mwanza.
Waliokuwa wabunge wa CCM, wapiganaji Mzee James Lembeli na Easter Bulaya watakuwepo Uwanja wa Magomeni. Tusimalize utamu hapa kuhusu watakachosema.
Mkutano utatangazwa live kwa masaa 3 kupitia ITV na Radio One.
Wakati Watanzania wengine watapata fursa ya kufuatilia matangazo ya moja kwa moja kupitia tv na radio, wakazi wa mikoa ya Kanda ya Ziwa watawakilisha kwa kufika kwa wingi uwanjani hapo kusikia hotuba zitakazotoa mwelekeo wa taifa hasa tunapoelekea kwenye Uchaguzi mkuu.
Wametangulia na kufuli, tutakuja na ufunguo.
Makene
Updates...
Maandamano ni makubwa mno. Haijawahi kutokea. Kutokea Uwanja wa Ndege wa Mwanza kuelekea mjini ambapo ni mwendo kama wa dakika 10 hivi hadi sasa msafara umetumia masaa mawili na bado haujafika mjini.
Mji mzima unanukia CHADEMA, Kanda ya Ziwa at its peak for changes.
Clear signs of quest for changes for the better future under safe hands of the committed and responsible leaders.
Tutaanza kuwawekea picha punde. Hapa hapa
Mapokezi ya mapadlocks mbona pikipiki zilikuwa chache sana...au wafuasi wake hawana pikipiki...???