MNAFU
Member
- Jan 16, 2014
- 99
- 24
Mara ziende chadema, mara ziende ACT, mara zirudi CCM tunachoka kwa kweli hawa wanachama wenu wafundisheni kuwa na misimamo..
Yaani inaudhi. Watu wanakuwa kama bendera? Upepo ukivuma hivi wanageukia huko, ukibadilika wanageukia huku.
Kabla hujajiunga na Chama fulani Chukua muda kusoma KATIBA, ilani na machapisho ya vyama ili ujue misingi ya vyama hivyo na ndipo uchague unapoona panakufaa. Sio Mara leo CCM, Kesho CHADEMA, keshokutwa ACT, n.k. Ukweli ni kuwa wengi ya hao wanaohamahama hawajui kitu kuhusu misingi ya vyama wanavyohamia kutwa kucha!
Watanzania tujifunze kuwa na msimamo!