What Made You Stay?

King'asti ubarikiwe sana haya mambo sijui lini watu watayaacha
kuna kisa kimoja cha kweli kabisa (lakini msikitungie Script) kinamhusu dada mmoja ninayemfahu.

Huyo dada baba yake alikufa yeye akiwa na miaka 13 na mama yake akiwa na miaka 27. Kwao walizaliwa watoto watatu yeye akiwa ni wa kwanza kuzaliwa. Baba yao alikuwa na wake wanne na mama yao alikuwa ni mama wa nyumbani anayetegemea kila kitu kutoka kwa baba yao. Siku ya kufa baba yao wao walikuwa wamepangishiwa nyumba kwa sababu mama yao alikuwa ni mke wa mwisho kuolewa kwa baba yao.

Kisa cha mama yao kuolewa na huyo baba ni kuwa alikwenda kutibiwa maradhi ya tumbo. Baada ya baba yao kufariki binti akiwa na miaka 13 na miezi kadhaa alianza kufanya biashara za kwenda minadani ambako alikutana na Tingo wa gari la mnadani na akiwa na miaka 14 na ushee akajifungua mtoto wake wa kwanza na kuhamia kwa huyo tingo. Tangu hapo ndipo mateso yalipoanza.

Akiwa na mimba ya mtoto wake wa pili aliwahi kupigwa kama mbwa na kutumbukizwa kwenye mfereji wa maji machafu mchana wa jua kali,kisa chenyewe eti mumewe alikuwa anamlazimisha awataje wapenzi wake wa zamani wakati kwa maelezo ya huyo binti jamaa ndiye aliiyefungua mlango wa "nyumba"

kuna wakati akiwa mjamzito alikuwa anashindia maji kwani jamaa alikuwa anasafiri hata kwa wiki mbili wakati siku ya kuondoka anajua ameacha buku mbili za matumizi lakini mwanamke akiomba hata maharage kwa jirani jamaa akijua hicho kipondo chake kama mwizi eti mwanamke anamdhalilisha na kumwaibisha.

Keshawahi kupasuliwa kichwani kwa chupa, mwilini ana mialama kibao ya kupigwa na kuchanwachanwa ama kwa kisu au viwembe. Jamii nzima inayowazunguka walifikia kuamini kwamba hayo ni mambo ya mapenzi ya watu wawili, Hata mwanamke apige kelele mara ngapi hakuna anayeingilia. mwanaume akaamini maisha ndiyo haya.

Siku moja jamaa karudi zake kutoka kwenye safari zake na nguo zake za Grease mwanamke kakaa kizingitini mwanaume akaanza kutuhumu "wewe jana umelala wapi? mwanamke kashangaa tuu "mbona mimi jana sikutoka kabisa kwenda popote tumbo lilikuwa linaniuma" jamaa kamwambia mwanamke aingie ndani. mwanamke katimua mbio, jamaa kufukuzia kwa nyuma hakumuona kumbe wasamaria wema wanawake wenzake wa jirani wamemficha chumbani kwao.Kaka mmoja mpangaji kwenye nyumba aliyokimbilia kuulizia na kuhadithiwa tukio zima akachukua jukumu la kumpangishia chumba siku hiyo hiyo na kumpa godoro na 100,000 ya kuanzia maisha.

miezi minne baadaye jamaa akaenda kumfanyia fujo kwenye nyumba ambayo amepanga na binti akaenda polisi jamaa akakamatwa na kuwekwa ndani. tangu siku hiyo adabu na heshima No fujo No kufuatiliana. Hatimaye binti kaolewa na bwana mwingine (siyo yule mpangaji) na sasa wana mtoto wa miaka 3 na wale aliozaa na yule bwana Bouncer wa kwanza mwenye miaka 19 yuko kwa baba yake na wa pili mwenye miaka 14 ni binti yuko kwa mama yake. Bouncer tangu waachane na huyu binti keshaoa na kuacha mara sita, Believe Me!!
 
kigarama,somo kubwa sana umetupa aisee! tabia hazibadiliki! kama alikua anampiga mwanamke mwingine (ujumbe kwa saram hapa),usidhani kua ww ni bingwa zaidi! usidhani ww utamnyenyekea vya kutosha. ni same as cheating, sio kama ukiwa small house,ukiwa promoted to big house ndo utakua tofauti!
the finest,unajua nikichangia thread hii nilikua nime-disable images, hiyo picha yako inanitia hasira kwa kweli! hapo,unaweza kusema kweli huyo mwanamke amebaki hapo kwa ajili ya hao watoto? like,is she doing them kids any favors?
 
kuna kisa kimoja cha kweli kabisa (lakini msikitungie Script) kinamhusu dada mmoja ninayemfahu.

Huyo dada baba yake alikufa yeye akiwa na miaka 13 na mama yake akiwa na miaka 27. Kwao walizaliwa watoto watatu yeye akiwa ni wa kwanza kuzaliwa. Baba yao alikuwa na wake wanne na mama yao alikuwa ni mama wa nyumbani anayetegemea kila kitu kutoka kwa baba yao. Siku ya kufa baba yao wao walikuwa wamepangishiwa nyumba kwa sababu mama yao alikuwa ni mke wa mwisho kuolewa kwa baba yao.

Kisa cha mama yao kuolewa na huyo baba ni kuwa alikwenda kutibiwa maradhi ya tumbo. Baada ya baba yao kufariki binti akiwa na miaka 13 na miezi kadhaa alianza kufanya biashara za kwenda minadani ambako alikutana na Tingo wa gari la mnadani na akiwa na miaka 14 na ushee akajifungua mtoto wake wa kwanza na kuhamia kwa huyo tingo. Tangu hapo ndipo mateso yalipoanza.

Akiwa na mimba ya mtoto wake wa pili aliwahi kupigwa kama mbwa na kutumbukizwa kwenye mfereji wa maji machafu mchana wa jua kali,kisa chenyewe eti mumewe alikuwa anamlazimisha awataje wapenzi wake wa zamani wakati kwa maelezo ya huyo binti jamaa ndiye aliiyefungua mlango wa "nyumba"

kuna wakati akiwa mjamzito alikuwa anashindia maji kwani jamaa alikuwa anasafiri hata kwa wiki mbili wakati siku ya kuondoka anajua ameacha buku mbili za matumizi lakini mwanamke akiomba hata maharage kwa jirani jamaa akijua hicho kipondo chake kama mwizi eti mwanamke anamdhalilisha na kumwaibisha.

Keshawahi kupasuliwa kichwani kwa chupa, mwilini ana mialama kibao ya kupigwa na kuchanwachanwa ama kwa kisu au viwembe. Jamii nzima inayowazunguka walifikia kuamini kwamba hayo ni mambo ya mapenzi ya watu wawili, Hata mwanamke apige kelele mara ngapi hakuna anayeingilia. mwanaume akaamini maisha ndiyo haya.

Siku moja jamaa karudi zake kutoka kwenye safari zake na nguo zake za Grease mwanamke kakaa kizingitini mwanaume akaanza kutuhumu "wewe jana umelala wapi? mwanamke kashangaa tuu "mbona mimi jana sikutoka kabisa kwenda popote tumbo lilikuwa linaniuma" jamaa kamwambia mwanamke aingie ndani. mwanamke katimua mbio, jamaa kufukuzia kwa nyuma hakumuona kumbe wasamaria wema wanawake wenzake wa jirani wamemficha chumbani kwao.Kaka mmoja mpangaji kwenye nyumba aliyokimbilia kuulizia na kuhadithiwa tukio zima akachukua jukumu la kumpangishia chumba siku hiyo hiyo na kumpa godoro na 100,000 ya kuanzia maisha.

miezi minne baadaye jamaa akaenda kumfanyia fujo kwenye nyumba ambayo amepanga na binti akaenda polisi jamaa akakamatwa na kuwekwa ndani. tangu siku hiyo adabu na heshima No fujo No kufuatiliana. Hatimaye binti kaolewa na bwana mwingine (siyo yule mpangaji) na sasa wana mtoto wa miaka 3 na wale aliozaa na yule bwana Bouncer wa kwanza mwenye miaka 19 yuko kwa baba yake na wa pili mwenye miaka 14 ni binti yuko kwa mama yake. Bouncer tangu waachane na huyu binti keshaoa na kuacha mara sita, Believe Me!!
Naweza kusema huyo dada alikuwa ana sifa ya uvumilivu kwa kweli maana mateso yote hai alipoamua kukimbia si kitu kidogo, halafu hapa ndio naona wale wanaume wenye tabia hii ni vigumu sana kuacha anaendelea nayo akipata mtu mwingine
 
kigarama,somo kubwa sana umetupa aisee! tabia hazibadiliki! kama alikua anampiga mwanamke mwingine (ujumbe kwa saram hapa),usidhani kua ww ni bingwa zaidi! usidhani ww utamnyenyekea vya kutosha. ni same as cheating, sio kama ukiwa small house,ukiwa promoted to big house ndo utakua tofauti!
the finest,unajua nikichangia thread hii nilikua nime-disable images, hiyo picha yako inanitia hasira kwa kweli! hapo,unaweza kusema kweli huyo mwanamke amebaki hapo kwa ajili ya hao watoto? like,is she doing them kids any favors?
King'asti sijui hata nisemeje mtu unapigwa mbele ya watoto wako, kama hawa watoto hawajaathirika kisaikolojia sijui kwa kweli maana hata mimi imeniwia vigumu sana kuandika mtu ambaye namfahamu alikuwa binti mzuri mwenye afya njema leo hii unamuona ana makovu ya mikanda kwenye mwwili wake yakiwemo ya visu, hata ukikaa naye ukiongea anachukua muda sana kukujibu sababu she's not herself anymore anachobakia kusema ni kuwa Mungu naomba unionyeshe njia, the only thing ambacho aliniuliza and i almost shed tears ni kuwa "Are you going to do the same thing to your wife when you get married". King'asti sijui kwa kweli i just wish you people could understand ni kitu gani nakieleza hapa regarding my friend i mean she has been traumatized, ngoja niishie tu hapa maana kuna kitu kimenishika kooni kinanifanya nisikie hasira
 
Kwakweli simulizi zote zinatia huruma sana; ila Faraja kubwa niliyoipata ni kuwa almost wanaume wote waliochangia huu Uzi wanasikitishwa na unyanyasaji huu!

Big up to you Real Men wa humu; you all will be blessed with happy homes! Love you all from my heart!
 
Kwakweli simulizi zote zinatia huruma sana; ila Faraja kubwa niliyoipata ni kuwa almost wanaume wote waliochangia huu Uzi wanasikitishwa na unyanyasaji huu!

Big up to you Real Men wa humu; you all will be blessed with happy homes! Love you all from my heart!
Kaunga i pray that God will show this woman a way and as well to all other women who are going through the same situation, it does hurt so much
 
The Finest..............this is so touchy jamani. Hivi wanaume wengine wamelelewaje/ hivi jamii yetu inafikiria je?.
Ni kweli kuwa hii inachangiwa na kutokujitambua lakini naamini pia malezi na jamii zetu kwa kiasi kikubwa zinachangia na kama kuwajibika basi a major transformation need to be done. Maneno ya ndoa ni kuvumilia yawe na mipaka i.e. limit? kuvumilia vitu gani na gani vya kutovumilia.

I have been there. Yes in a very abusive relationship tena ya mtu ambaye nilimpenda kiasi cha kusacrifice mambo mengi sana including elimu yangu and all that (najua mpo mtakaosema MWJ1 ulikuwa mjinga, unaacha elimu ikupite kushoto kwa ajili ya mwanaume!!? nitawaelewa). Sacriface nyingi sana ambazo nilizifanya kwa jina la mapenzi ! The Sacrifice ambayo ilinibidi niiweke katika moja wapo ya items muhimu na endelevu kwenye maisha yangu. Nikiwa kama binadamu ambaye siko perfect ninakiri na ninaamini kuwa nilikuwa na part yangu lakini kwa mtazamo wa nje na yale yote muhimu nilijitahidi (na yeye anakiri leo kuwa ali'pitiwa na shetani) nilikuwa mjinga na ilinichukua muda kurealize kuwa ninakuwa abused. (Ninapenda kuwajulisha kuwa MWJ1 wa enzi hizo ni yule alokuwa anafahamika kama mlokole....... yule ambaye alikuwa akimaliza kugawa tunda pamoja na kuwa ni halali anahisi anatakiwa kutubu!) Kila siku ikawa ni sacrifice, sacrifice only to realize kuwa haitokaa siku akatosheka na wala akabadilika. Ilinichukua muda kuamua kwanza kuuvunja ukimya na kisha kuchukua hatua ambayo nakiri haikuwa kazi rahisi hata kidogo na hii ilichangiwa na jamii niishiyo ambapo mpaka wazazi wangu (ambao si kuwa tu mimi ni mtoto wao wa kwanza, bali pia mtoto pekee kati ya watoto 5) ambaye angalau nilikuwa na kajidiploma kangu ualimu, hata hao wazazi walinifukuza wakitoa sharti la kurudi kwenye uhusiano wangu na huyo mwenza. Katika mwaka ambao sitakaa niusahau humu duniani ni mwaka ule. Nilijuta kuingia katika kifungo nikingali msichana (si mdogo sana) but nikingali mchanga ambaye sikuwa na pa kusimamia. Pocket money niliyokuwa napewa na wazazi ilikatwa, nikaishi maisha ya kuhangaika na kudowea kwa marafiki (namshukuru MUNGU sikuwahi kuwaza maovu zaidi lakini shukrani zangu za maisha ziende kwa rafiki yangu wa kike ambaye yeye pamoja na kuwa si tajiri bali aliwezakunikimu kwa kugawana pocket money aliyokuwa akichangiwa na dada zake na kunipa kalazi na chakula mpaka nilipomaliza chuo).

Haikuishia hao, chuoni nilipokuwa nasoma nilionekana msichana niliyeshindikana, anawezaje kuondoka kwenye mahusiano madhubiti kama yale! anataka awe huru ili awe changudoa, ameona anabanwa na maneno chungu mbovu kiasi cha kuona kabisa unapopita unanyooshewa vidole na unaposogelea kundi lal marafiki wanatawanyika. ! Mtaani ndio usiseme. Maisha yalikuwa magumu kupindikia mpaka MUNGU aliponibariki kazi yangu ya kwanza ambapo nilifanikiwa kuhama mtaa na chuo na kuanza maisha mapya, nikiwa nimetengwa na ndugu, jamnaa na marafiki isipokuwa rafiki yangu alitenivumilia nilipoanguka!

Mtu ukiyafikiria haya yote utagundua kuwa kujitambua peke yake hakutoshi bila kuwa na ujasiri na a hand to hold you on maana it is not easy at all. Mchana utatembea kichwa juu macho miita mia kujifanya u strong but usiku hulali kwa kulia na wengine kujiingiza kwenye ulevi kama si kunusuriwa na mauti.

unapoisoma hii post ninakuomba wewe mwanamke utafakari, ujiweke kwenye nafasi ya huyu MwJ1 (wa enzi hizo). Fikiria mazingira yote yanayoukuzunguka kuanzia thamani yake (kwa jinsi unavyoidefine wewe, wazazi wako na jamii inayokuzunguka)
2. Ukikumbuka kuwa decision making at household inatawaliwa na baba, mama anawezakuumia sana juu ya maumivu yako lakini kumbuka uamuzi wa mwisho unatolewa na mzazi wako wa kiume (wangapi ambao wazazi wao wa kiume wanasymphasize nao achilia mbali wale ambao hawana wazazi wa kiume au wana wazazi ambao si wazazi wa kumzaa)
3. Fikiria nafasi ya mwanamke mwenzioa ambaye hana kazi nzuri ya kumsustain yeye na wanae kama ataamua kuondoka kimoja; na mazingira yote yanayomzunguka..wanawake wengine hawana elimu, hawajui haki zao n.k

So ninawaomba ndugu zangu kabla ya kufanya "Victim blaming' ninawaomba tuwaangalie hawa wanawake wanaokuwa abused kutoka katika mazingira halisi wanayoishi. Am telling you wanawake ambao wana ujasiri wa kusimama na kuamua 'enough is enogh' wabebe misalaba yao na majukumu ya watoto wao ni 3 kati ya kumi.
Karibuni
Mhh!!! Inasikitisha sana pole MwanajamiiOne
 
...kwa kuungama kiukweli tu [individual cases] ndipo utapoweza tambua mzizi wa fitna wa tatizo hili,...lakini
tatizo juu ya tatizo ni kwamba katika wanaume kumi [10] utaobahatika kuwauliza sababu ya kufikia kutumia
ngumi, mateke na makofi kwa wapenzi/wake zao...huenda ni mmoja au wawili anayeweza kukupa jibu la kueleweka.

...the rest, either kwa aibu atasema si kweli kama anatabia hiyo, hupitikiwa tu na shetani, au atasema bila
"kuonyesha" nani ni mwanaume ndani ya mahusiano mwanamke atampandia kichwani.
Hebu tujiangalie sisi wenyewe
tunachangia vipi kwenye matatizo haya...

tukianzia kwenye malezi;.....

wewe kama mzazi, unamuandaa vipi mtoto wako wa kiume kuja kupambana na maisha ya mapenzi, mahusiano?
kila mtu kwa experience yake, tujadiliane umri muafaka wa kuanzia malezi hayo...

-wazazi wengi mnachangia ku create monsters !!!-




...nipo bro,...udhuru kidogo.

Kweli Mbu malezi ni jambo la msingi sana la kuliangalia pia, maana akifanyiwa wa kwako lazima tuangalie mtu utajisikiaje
 
Mamushka nafikiri watu wanahitaji kujitambua wao ni nani na hatua anayokuwa amefikia inabidi kuchukua maamuzi bila kujali nani atasema nini na kitu gani

The Finest, unachosema ni kweli, kunasaa mtu inabidi ajilipue tu na kufanya maamuzi magumu sana kwenye life. Ila maamuzi ambayo yataleta manufaa mbeleni.
 
Mkuu, hapo nilipokuza, kukozesha na kupigia mstari, ninakubaliana nawe kwa kiasi kikubwa, lakini udhalilishaji wa wanawake si tabia ya wabantu tu. Hata sisi wabantu tumeanza kubadilika. Wengine wanaona kama mabadiliko haya ni kuwalea vibaya wasichana, pale mama anapomwambia mwanawe m/mke arejee nyumbani, au anpomkemea mume kwa kumwambia "huyu ana kwao, hukumwokota jaani".

Udhalilishaji wa wanawake upo ulimwenguni pote miongoni mwa races zote - Waafrika weusi na weupe, waarabu, wahindi, wachina, wazungu wa mabara yote, na response ya wanawake wengi inakuwa kama hii ya Angela. Ni juzi tu rafiki yangu mzungu alinisikitikia mateso anayopata toka kwa mume wake - wivu, gubu, kisago - na bado anabakia kwa kisingizio cha watoto lakini ukweli ni kuwa anafikiri iko siku mume atabadilika.

Imefikia wakati, kwa takwimu nilizonazo za nchi moja ya Ulaya, wastani wa wanawake watano kwa mwezi huuliwa na waume au ex-wao, ukiwachia mbali ya maelfu wanaojulikana na wasiojulikana rasmi kesi zao; ukilinganisha na 1/45 ya wanawake wanaoua waume zao pale maji yanapowafika shingoni. Imefika wakati pia wanaume/wanawake wanavishwa vilinzi (GPRS) ili kuwakinga mahasimu zao wasiwasogelee.

Tatizo lipo kwenye mfumo dume, toka majumbani hadi serikalini. Angalau kwa nchi zinazoendelea wanajaribu kulipunguza. Mfano ni EU ambapo wamo wanaandaa sheria ya kuwasakama wanaume watesaji na wauwaji. Hata hivyo mitaani, bado mke akiteswa inaonekana kama ni stahiki yake.

Ninachowashauri wasichana wasimame wenyewao kujilinda na hii hali. Mkisubiri huruma ya mume, serikali na familia zetu, mtaendelea kuteswa. Ikiwa sula ni la watoto, watoto si wako peke yako. Na ikiwa ni tamaa ya kumbadilisha mume siku moja, kumbuka kuwa walishishashindwa wazazi wake kumbadilisha. AMKENI

Ulichoongea ni point tupu kakaangu, tusipoamka wenyewe hakuna atakae tusaidia.
 
Mkuu, hapo nilipokuza, kukozesha na kupigia mstari, ninakubaliana nawe kwa kiasi kikubwa, lakini udhalilishaji wa wanawake si tabia ya wabantu tu. Hata sisi wabantu tumeanza kubadilika. Wengine wanaona kama mabadiliko haya ni kuwalea vibaya wasichana, pale mama anapomwambia mwanawe m/mke arejee nyumbani, au anpomkemea mume kwa kumwambia "huyu ana kwao, hukumwokota jaani".

Udhalilishaji wa wanawake upo ulimwenguni pote miongoni mwa races zote - Waafrika weusi na weupe, waarabu, wahindi, wachina, wazungu wa mabara yote, na response ya wanawake wengi inakuwa kama hii ya Angela. Ni juzi tu rafiki yangu mzungu alinisikitikia mateso anayopata toka kwa mume wake - wivu, gubu, kisago - na bado anabakia kwa kisingizio cha watoto lakini ukweli ni kuwa anafikiri iko siku mume atabadilika.

Imefikia wakati, kwa takwimu nilizonazo za nchi moja ya Ulaya, wastani wa wanawake watano kwa mwezi huuliwa na waume au ex-wao, ukiwachia mbali ya maelfu wanaojulikana na wasiojulikana rasmi kesi zao; ukilinganisha na 1/45 ya wanawake wanaoua waume zao pale maji yanapowafika shingoni. Imefika wakati pia wanaume/wanawake wanavishwa vilinzi (GPRS) ili kuwakinga mahasimu zao wasiwasogelee.

Tatizo lipo kwenye mfumo dume, toka majumbani hadi serikalini. Angalau kwa nchi zinazoendelea wanajaribu kulipunguza. Mfano ni EU ambapo wamo wanaandaa sheria ya kuwasakama wanaume watesaji na wauwaji. Hata hivyo mitaani, bado mke akiteswa inaonekana kama ni stahiki yake.

Ninachowashauri wasichana wasimame wenyewao kujilinda na hii hali. Mkisubiri huruma ya mume, serikali na familia zetu, mtaendelea kuteswa. Ikiwa sula ni la watoto, watoto si wako peke yako. Na ikiwa ni tamaa ya kumbadilisha mume siku moja, kumbuka kuwa walishishashindwa wazazi wake kumbadilisha. AMKENI

Halafu nimekumiso cha kukaa kimya hivyo, mzima kweli?
 
Mkuu, hapo nilipokuza, kukozesha na kupigia mstari, ninakubaliana nawe kwa kiasi kikubwa, lakini udhalilishaji wa wanawake si tabia ya wabantu tu. Hata sisi wabantu tumeanza kubadilika. Wengine wanaona kama mabadiliko haya ni kuwalea vibaya wasichana, pale mama anapomwambia mwanawe m/mke arejee nyumbani, au anpomkemea mume kwa kumwambia "huyu ana kwao, hukumwokota jaani".

Udhalilishaji wa wanawake upo ulimwenguni pote miongoni mwa races zote - Waafrika weusi na weupe, waarabu, wahindi, wachina, wazungu wa mabara yote, na response ya wanawake wengi inakuwa kama hii ya Angela. Ni juzi tu rafiki yangu mzungu alinisikitikia mateso anayopata toka kwa mume wake - wivu, gubu, kisago - na bado anabakia kwa kisingizio cha watoto lakini ukweli ni kuwa anafikiri iko siku mume atabadilika.

Imefikia wakati, kwa takwimu nilizonazo za nchi moja ya Ulaya, wastani wa wanawake watano kwa mwezi huuliwa na waume au ex-wao, ukiwachia mbali ya maelfu wanaojulikana na wasiojulikana rasmi kesi zao; ukilinganisha na 1/45 ya wanawake wanaoua waume zao pale maji yanapowafika shingoni. Imefika wakati pia wanaume/wanawake wanavishwa vilinzi (GPRS) ili kuwakinga mahasimu zao wasiwasogelee.

Tatizo lipo kwenye mfumo dume, toka majumbani hadi serikalini. Angalau kwa nchi zinazoendelea wanajaribu kulipunguza. Mfano ni EU ambapo wamo wanaandaa sheria ya kuwasakama wanaume watesaji na wauwaji. Hata hivyo mitaani, bado mke akiteswa inaonekana kama ni stahiki yake.

Ninachowashauri wasichana wasimame wenyewao kujilinda na hii hali. Mkisubiri huruma ya mume, serikali na familia zetu, mtaendelea kuteswa. Ikiwa sula ni la watoto, watoto si wako peke yako. Na ikiwa ni tamaa ya kumbadilisha mume siku moja, kumbuka kuwa walishishashindwa wazazi wake kumbadilisha. AMKENI

Mkuu thanks for your analysis maana hapa wote tunajifunza maana kwa hali ya namna hii kwa kweli it's so disappointing
 
domestic-violence.jpg


Hiki ni kisa cha kweli cha rafiki yangu ila jina la muhusika ndio nimelibadilisha. Naandika kwa masikitiko sana kwa jinsi hali aliyonayo sasa hivi inasikitisha sana nafikiria ila kichwani mwangu maswali ndio mengi kuliko majibu, najiuliza ni kwanini lakini??

Ukimuona Angela sio yeye ile hali ya uanamke haipo tena, nguo anazovaa yeye ni zile zinazofunika mwili kuanzia juu hadi chini. Angela is not confident anymore anaonekana kama vile ana miaka 40. Angela amekuwa kwenye abusive relationship kwa muda mrefu amekuwa akipigwa na mumewe mara kwa mara na kumfukuza nje ya nyumba kwa kuwa ana watoto na huyu mume Angela ilikuwa inambidi arudi kwa mumewe kumuomba msamaha hii yote alikuwa anafanya kwa ajili ya watoto wake, alikuwa anataka watoto wake wamalize shule kabla hajachukua uamuzi mwingine.

Mumewe alikuwa ameishajua udhaifu wake uko wapi na ndio akaamua kuwa anatumia nafasi hiyo kumdhalilisha, Angela naye aliendelea kuishi na hali hiyo akitegemea iko siku labda mambo yatabadilika, ila siku mambo yalipokuwa magumu ndipo aliamua kuchukua uamuzi wa kuondoka hii ni baada ya mumewe kumjeruhi kwa kisu na mpaka sasa Angela ana makovu ya visu mwilini, natamani laiti kama mngeweza kumuona jinsi alivyo sasa hivi inasikitisha sana swali nililomuuliza ni kuwa pamoja na haya yote kwanini aliendelea kukaa kwenye ndoa ya namna hiyo akanijibu ni kwasababu ya watoto.

Nashindwa kueleza mambo mengine zaidi sababu ni ya aibu na ya kusikitisha sana mwanaume ambaye umezaa naye watoto leo hii anakuuliza "Kama wewe ni mwanamke kweli basi nionyeshe huo uanamke wako uko sehemu gani"? hivi sielewi.

NB: Mume wake ameishafikishwa kwenye vyombo vya kisheria kwa kosa la kumjeruhi

Najua ni wengi sana wako katika hali kama hii lakini hawasemi kwa kuhofia wakiacha ndoa zao jamii itawaelewa vibaya, ni kitu gani kinachokufanya uendelee kukaa kwenye ndoa ya namna hiyo????
Inasikitisha sana mambo haya yapo katika familia nyingi wengi wamekuwa hawasemi
 
inauma sana wanawake wengi wanapitia magumu ambayo hayaelezeki bahati mbaya hubadilisha maisha yao kabisa na sio lazima iwe kipigo
Kwa kweli Chauro inasikitisha sana ni wachache sana wanaoweza kuelezea unyama wanaofanyiwa ndani ya ndoa wengi wao wamekuwa ni waoga sana wanaishi chini ya hicho kivuli huku wakiendelea kupigwa kila kukicha
 
Not that much simple bebii.... Je umesahau ule usemi kuwa 'kofi la mpenzi haliumi'? Ni usemi mfupi lakini ukitumia japo dk tano kuuwaza utajifunza mengi. Kifupi ni kuwa, ukishafikia steji ya kumuita mtu mpenzi (na mara nyingi hapa ndipo unapopata nafasi ya kujua mambo yake), hutaona uovu wake kamwe, unakuwa kama umelishwa limbwata. kila afanyalo unaliona jema, hata akikupiga unaona kama anakutania, watu wakikuasa unaona wanakuonea wivu. Ukishaingia kwenye ndoa ndipo unakuwa na akili ya kupambanua mema na mabaya, na 'kofi la mume/mke linauma le mbaya' lakini la mpenzi haliumi...
Hahaha!!! Tuko umenifanya nicheke asubuhi hii
 
JAmani polen wote mliotoa visa vyenu kwa wale wenye ndoa za furaha basi endeleeni kumshukuru mungu wale wenye ndoa zenye mateso Fanya maamuzi sahihi haraka iwezekanavyo,watoto isiwe kigeziokwan ukikaa hapo kwa kateso hayo na ukafa si wataishi tu? sembuse uhai ungalipo...say u can!kwa wale wenzangu na mie kama bado hujapata mwenza basi maombi ni silaha muhimu pia STOP and THINK before you enter in marriage!asanteni jamani nawapenda wote
 
domestic-violence.jpg


Hiki ni kisa cha kweli cha rafiki yangu ila jina la muhusika ndio nimelibadilisha. Naandika kwa masikitiko sana kwa jinsi hali aliyonayo sasa hivi inasikitisha sana nafikiria ila kichwani mwangu maswali ndio mengi kuliko majibu, najiuliza ni kwanini lakini??

Ukimuona Angela sio yeye ile hali ya uanamke haipo tena, nguo anazovaa yeye ni zile zinazofunika mwili kuanzia juu hadi chini. Angela is not confident anymore anaonekana kama vile ana miaka 40. Angela amekuwa kwenye abusive relationship kwa muda mrefu amekuwa akipigwa na mumewe mara kwa mara na kumfukuza nje ya nyumba kwa kuwa ana watoto na huyu mume Angela ilikuwa inambidi arudi kwa mumewe kumuomba msamaha hii yote alikuwa anafanya kwa ajili ya watoto wake, alikuwa anataka watoto wake wamalize shule kabla hajachukua uamuzi mwingine.

Mumewe alikuwa ameishajua udhaifu wake uko wapi na ndio akaamua kuwa anatumia nafasi hiyo kumdhalilisha, Angela naye aliendelea kuishi na hali hiyo akitegemea iko siku labda mambo yatabadilika, ila siku mambo yalipokuwa magumu ndipo aliamua kuchukua uamuzi wa kuondoka hii ni baada ya mumewe kumjeruhi kwa kisu na mpaka sasa Angela ana makovu ya visu mwilini, natamani laiti kama mngeweza kumuona jinsi alivyo sasa hivi inasikitisha sana swali nililomuuliza ni kuwa pamoja na haya yote kwanini aliendelea kukaa kwenye ndoa ya namna hiyo akanijibu ni kwasababu ya watoto.

Nashindwa kueleza mambo mengine zaidi sababu ni ya aibu na ya kusikitisha sana mwanaume ambaye umezaa naye watoto leo hii anakuuliza "Kama wewe ni mwanamke kweli basi nionyeshe huo uanamke wako uko sehemu gani"? hivi sielewi.

NB: Mume wake ameishafikishwa kwenye vyombo vya kisheria kwa kosa la kumjeruhi

Najua ni wengi sana wako katika hali kama hii lakini hawasemi kwa kuhofia wakiacha ndoa zao jamii itawaelewa vibaya, ni kitu gani kinachokufanya uendelee kukaa kwenye ndoa ya namna hiyo????

hiyo picha imeniumiza sana na kunikumbusha mbali.siwezi kommenti from women's angle ila nikiwa mtoto niliishi kwenye familia ya hivyo....it's HELL!saa tisa usiku,mvua kali inapiga,mimi,my beautiful mama na my two sisters tuko kwa kiambaza cha nyumba tumezuia vichwa tu visilowe ila mili yetu ikitandikwa na mvua mercilessly sababu tu ndani hakukaliki kwa kipigo na manyanyaso!

it came a day ambapo nilitayarisha kisu changu kikali vizuri na nikasema moyoni 'leo akirudi saa saba na kuanza kutupiga sisi na mama i will stangle him to death...'.that day hakurudi kabisa nyumbani!sijui kwanini mama alichelewa kuondoka kwa yule mzee.nasikia aibu kwamba yeye ni baba yangu!
 
.hii mbaya sana,hivi ni kwa nini mungu naye anawapa waume binti kama angela?aende tu kwao,aachana nae huyo hafai
 
hiyo picha imeniumiza sana na kunikumbusha mbali.siwezi kommenti from women's angle ila nikiwa mtoto niliishi kwenye familia ya hivyo....it's HELL!saa tisa usiku,mvua kali inapiga,mimi,my beautiful mama na my two sisters tuko kwa kiambaza cha nyumba tumezuia vichwa tu visilowe ila mili yetu ikitandikwa na mvua mercilessly sababu tu ndani hakukaliki kwa kipigo na manyanyaso!

it came a day ambapo nilitayarisha kisu changu kikali vizuri na nikasema moyoni 'leo akirudi saa saba na kuanza kutupiga sisi na mama i will stangle him to death...'.that day hakurudi kabisa nyumbani!sijui kwanini mama alichelewa kuondoka kwa yule mzee.nasikia aibu kwamba yeye ni baba yangu!
Mkuu pole sana kwa matatizo yaliyokupata
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom