Waziri Sitta: Dowans ni genge la ulaji wa vigogo watatu; tusiwalipe!

haya sasa,watu wako kazini kuganga njaa zao hapo hakuna uchungu wa nchi wala nini
 
Kama kuna kundi linatakiwa kunyamaza sasa ni hawa wanaojikanyaga katika CCM kwa majina ya makamanda wa ufisadi na wale waitwao mafisadi. wote hawa kwa umoja wao wametufikisha katika giza lilopo kwa ajili ya maslahi yao. Ndio maana leo nionapo wanajifanya kutoa vimanneo vya kisiasa nasikitika sana kwa kuwa walitufanya mpira wa kona tangu Richmond na walicheza siasa hata walipojuakuwa Dowans watashinda kesi. Sasa ni wakati tunataka Sitta atutajie ni akina nani wamiliki wa Dowans maana anawajua na hatakiwi kuishia kusema vigogo watatu. Kisha kama kauli yake inatokana na yeye kuwa waziri nashawishika sasa ni wakati tuwabomoe CCM na kuwanyima kura kabisa ikibidi kwa maandamano maana 2015 ni mbalin sana.
 
Time will tell!

Maneno matamu na yenye matumaini tuliyapata kwenye hotuba ya JK wakati wa ufunguzi wa Bunge mwaka 2006, lakin je yalitekelezwa? Six tunataka tuone matokeo ya moto uliouwasha!
 
Hivi Six si ni mwanasheria? Sasa nina wasiwasi na taaluma yake.haya ni mambo ya kisheria hayahitaji blaablaa za kisiasa kutafuta umaarufu.Yeye kama ana dhamira ya kweli alete hiyo ishu kwenye baraza la mawaziri ijadiliwe wafikie suluhisho la kisheria na si la kisiasa.Yeye wakati akiwa mwenyekiti wa TIC si ndie aliyekuwa anakaribisha hao wawekezaji?
sitta ni ccm na ccm ni sitta.kama sio kweli na atoke huko tuone.Acheni kutulughai bwana
 
Watawala wanayajua haya yote ndio maana wanang'anga'ana kukaa madarakani at any cost ili mambo kama haya yakifumuka basi wanacheza nayo wenyewe na hakuna wa kuswekwa ndani
 
Re: Ujumbe toka kwa samwel sitta...

Hivi Six si ni mwanasheria? Sasa nina wasiwasi na taaluma yake.haya ni mambo ya kisheria hayahitaji blaablaa za kisiasa kutafuta umaarufu.Yeye kama ana dhamira ya kweli alete hiyo ishu kwenye baraza la mawaziri ijadiliwe wafikie suluhisho la kisheria na si la kisiasa.Yeye wakati akiwa mwenyekiti wa TIC si ndie aliyekuwa anakaribisha hao wawekezaji?
sitta ni ccm na ccm ni sitta.kama sio kweli na atoke huko tuone.Acheni kutulughai bwana​


KALAMAZOO: Wakati wote lazima tuwe na wapiganaji wa kutoka ndani. Six abaki huko; nasikia raha akiwa anawawasha tokea Africa Mashariki
:whoo::whoo::whoo::whoo::whoo::whoo::whoo::whoo:
 
MUNGU ATUOKOE TU NA BALAA HILI.. TUKUMBUKE SITTA YUKO RIGHT.. ALISHAKUWA WAZIRI WA SHERIA KITAMBO KWA HIYO JK ASIMFUNDISHE KAZI... HE IS CAPABLE..... JAMANI RA, EL, EC, Y MANJI, LAW MARSH KEGOR STUP WOTE WANAFAA KUJIBU TUHUMA LA SIVYO 'people's redemption council' led by chadema tutawafunua tu... look on what now Ayadema, Bongo families wanavyoface hunting of the international justice lobbies.... tutawapata tu hata kama ni 2025 watafungwa.... nimeshangaa kusikia Bongo alikuwa na account 80 tofauti ulaya, ana mtaa mzima ufaransa una flat kama 40.. du KUNA KITABU KITWACHO ...HOW TANZANIAN LEADERS ARE UNDER DEVELOPING TANZANIA.... KINAKUJA EARLY 2011.. GET READY
 
Nimesoma gazeti la mwananchi la leo ukurasa wa kwanza kuhusu kauli ya Sita kuhusiana na hukumu ya kesi ya Dowans. Anasema hakuna haja ya kulipa hizo pesa na kwamba kuna genge ndani ya CCM ndio walichora mpango huo wapate fedha kwa ajili ya uchaguzi wa 2015. Namuunga mkono kwamba kama serikali tunaweza kukataa kulipa na kusema wazi kuwa mkataba huo ulikuwa una harufu ya rushwa na hivyo ni batili. Tumeambia Richmond ilikuwa hata haijasajiliwa wakati inaingia mkataba hivyo hakukuwa na mkataba halali. Kama hakuna mkataba halali Richmond hawakuwa na kitu cha kuwauzia Dowans.

Ila kilichonifurahisha ni kumkuta Waziri anaweza kutoa kauli za kishujaa na kizalendo namna hii. Kumbe viongozi wazalendo wapo ila wachache na katika hao wachache wapo waoga. Wenye uwezo wa kuzungumza ni wachache, wengi wanalinda ugali. Kikubwa kama jamii tumuunge mkono Sita na viongozi wengine wenye uzalendo ndani ya mioyo yao. Ningekuwa na uwezo ningeandaa maandamano ya kuunga mkono kauli ya kishujaa na kizalendo ya Sita. Nadhani 2015 bila kujali chama TZ inahitaji kiongozi mwenye dhamira ya kupambana na rushwa wa aina ya Sita.
 
Wadau,
Sidhani kama anachokizungumza Sitta kinaweza kukubalika kwa Watanzania walio wengi. Ni abiria anayesafiri kwenye meli ya ufisadi. Hivyo ndivyo ninavyoamini mimi.Dhana ya kuwa na chakula kisafi kwenye sahani chafu huenda sambamba na mtazamo wa kuendelea kupiga kelele kwenye boti linalozama badala ya kutafuta njia ya kujiokoa. Sitta yupo ndani ya mfumo huu kwa muda mrefu na anajua wazi mambo yanavyofanyika. Nina wasiwasi na tamko lake. Yawezekana ni kutaka kutuchanganya wananchi tuliopoteza matumaini ya maisha haya na kumtafuta hata malaika mmoja anayeweza kutuvuta mkono. Tunamkubali kwa kudhani kuwa Sitta ni mkombozi aliyedondoka kwa ajili ya kutubadilishia mfumo wa maisha tunayoyalilia. Hizo ni mbwembwe tu,hana nafasi ya kufanya maamuzi. Analeta propaganda kwa kuwa naye ana machungu yake mengi aliyoyabeba moyoni. Tunapaswa kujiuliza: Je, kelele za Dowans na Richmond zimeanza leo? Alikuwa wapi siku zote?


Awali nilitamani SS akatae uwaziri alopewa lakini baada ya kusoma maoni ya watu hapa kwenye jamvi ninashawishika kwamba ni busara abaki huko ili hata serikalini kuwe na kambi zinazikinzana. Maana wakibaki wote ndio mzee kule ndani mauti yetu ya pili itakuwa imewadia.
Na ukweli watanzania tumshukuru huyu mzee maana bila yeye kuruhusu bunge kuchunguza tulikuwa tumeshapigwa changa la macho na kina EL kwenye Richmond. At least we should be grateful for that!!

Mie nadhani tuzidishe kelele hata hao watoto wao ni vema kuwanyanyapaa tu hata tukikutana nao mtaani maana ni wabaya kuliko ukimwi wenyewe. Tatizo sie watz tunawashobokea sana sasa sijui ni njaa zetu. Maana mtu akimwona Riz1 basi mimacho yamtoka.

Vita vipigananwe kutoka kila kona mpaka wasalimu amri!
 
Mafisadi walifikiri kwamba akiwa waziri atazibwa mdomo. They were very wrong. Kwa kumtoa kwenye u-spika ndio wamenfyatua zaidi. Sitta ni shujaa katika mashujaa. Nadhani wafisadi sasa wanakuna vichwa, kulia na kusaga meno!
 
Mkerio unasema Mh. Sitta ni mzalendo!!!

Sijui, binafsi sina uhakika!! Ila ningependa kukutahadhalisha kuwa tegemea kuona mengi sana kuelekea uchaguzi mkuu wa 2015. Viongozi watakuja kwa sura za hadaa ili mradi wajitengenezee mazingira ya kuteuliwa kugombea Urais come 2015.

Jiulize yule yule Sitta aliyeizima na kuizika hoja ya Richmond (Dowarns) bungeni (tena akiwa na nguvu zaidi kama Spika wa Bunge la JMT leo anatoa nguvu wapi ya kusema Dowans ni ya Mafisadi wa Tanzania?

Nilitegemea kipindi kile akiwa Spika wa Bunge ndo alikuwa well placed kuonyesha uzalendo wake kwa Tanzania.

Kinyume na hapo........namuona msanii na mtu anayetafuta cheap populality mbele ya macho ya wadanganyika!!
 
Kila nikiona Mtanzania mwenzangu anatoa such comments...... Huwa nakata tamaa kabisa, na kuona Safari bado ni ndefu sana... Na huenda hatutafika in any near future

Halafu itokee bahati uone huyu mtu jamii yake inavyoishi ndio utalia kabisa. Yeye anaweza kuwa kafanikiwa kuweka mkate tu mezani, kibanda na kitoyota cha mwaka 2000 anadhani amewin maisha. Kuna ndugu zetu huko vijijini wanatia huruma, aende skuli za huko shamba aone kama atakuja na comment za kipuuzi hapa.

VoiceofReason naomba wasitukatishe tamaa, we are fighting for something bigger than putting bread on the table.
 
Mkerio unasema Mh. Sitta ni mzalendo!!!

Sijui, binafsi sina uhakika!! Ila ningependa kukutahadhalisha kuwa tegemea kuona mengi sana kuelekea uchaguzi mkuu wa 2015. Viongozi watakuja kwa sura za hadaa ili mradi wajitengenezee mazingira ya kuteuliwa kugombea Urais come 2015.

Jiulize yule yule Sitta aliyeizima na kuizika hoja ya Richmond (Dowarns) bungeni (tena akiwa na nguvu zaidi kama Spika wa Bunge la JMT leo anatoa nguvu wapi ya kusema Dowans ni ya Mafisadi wa Tanzania?

Nilitegemea kipindi kile akiwa Spika wa Bunge ndo alikuwa well placed kuonyesha uzalendo wake kwa Tanzania.

Kinyume na hapo........namuona msanii na mtu anayetafuta cheap populality mbele ya macho ya wadanganyika!!

-Sita + +Sita = Zero

Nakubaliana na hoja zako uncle.
 
Kwenye ile kesi ya CityWater na DAWASA kwenye mahakama hiyohiyo, DAWASA ilishinda na wakili alikuwa ni huyohuyo. Alilipwa over 5bn. Mara hii kwenye DOWANS/TANESCO, TANESCO imeshindwa. Anaijua sana mahakama ile.

Pale ilibidi DAWASA ishinde kwa vile aliyewafukuza Citywater alikuwa EL. Lakini kwa hili la Dowan EL ni mdau dhidi ya Tanesco. These people are just too much
 
Back
Top Bottom