kwani amesema nini huyo Sitta? thread imeanza as if kila mtu alimsikia alichozungumza huyo Sitta. iweke vizuri post yako mkuu!
KWA HAWA MAFISADI WA DOWANS NA WAFADHILI WAO 'MWENDO WA KUWANYATIA MMOJA BAADA YA MWINGINE, FAMILIA ZAO PAMOJA NA MALI ZAO NDIO JIBU KWETU VIJANA TANGU SASA:
Wenye magendo na nia ya dhati kuendelea kuhujumu uchumi na KUTAFUNA RASILMALI YA TAIFA BILA HURUMA, nadhani siku si nyingi sana Wa-Tanzania tutalazimika kidogo kuweka AMANI yetu kabatini na UTAWALA WA KIJANJA WA SHERIA na kuzipitia baadaye kidogo ili vijana kwanza tukamalizane kiaina na nyie. Hapo adabu itakwepo.
Ndio, nadhani njia pekee tuliobaki nayo ni hii hapa. Hakika, itabidi na familia zenu popote pale walipo nao kama hawaoni kwamba mnafanya KUFURU vitendo vyenu vinatuelekeza kuchukua hatua za makusudi kabisa ili sasa tuanze tu na nyinyi pamoja na familia zenu popote pale mlipo - KWA MWENDO WA KUWANYATIENI BILA YA KELELE ZOZOTE ZA MWIZI MWIZI - halafu matamu yake yatakua fundisho tosha kwa wengine wengi wa aina yenu.
Nyinyi si ni wajanja, na wanasheria wote mnao, taasisi zote muhimu tayari mmezinunua ndani na nje ya nchi sio??????????? Sawa basi!!! Huu ujinga tutaufumbia macho hadi lini. Ole wake mtu atumie sehemu ya KODI YANGU kuwalipeni ninyi MASHETANI WAKUBWA!!!!!!!!!!
Nao wanafamilia zenu wamekataa katakata kuwashaurini kutufanyia taifa letu huu UBAKAJI WA KUTISHA WA AINA HII, OK!!!!!!!!!! Hivi kwanza wanachi mnaowakilishwa na watu kama hawa mnajisikieje????
Nimrodi alijenga mji wa Ninawi! (Mwa. 10:9,11).
If Sitta is being patriotic,he should then resign. Otherwise he is just a POLLUTER by MAKING NOISE.
Wadau,
Sidhani kama anachokizungumza Sitta kinaweza kukubalika kwa Watanzania walio wengi. Ni abiria anayesafiri kwenye meli ya ufisadi. Hivyo ndivyo ninavyoamini mimi.Dhana ya kuwa na chakula kisafi kwenye sahani chafu huenda sambamba na mtazamo wa kuendelea kupiga kelele kwenye boti linalozama badala ya kutafuta njia ya kujiokoa. Sitta yupo ndani ya mfumo huu kwa muda mrefu na anajua wazi mambo yanavyofanyika. Nina wasiwasi na tamko lake. Yawezekana ni kutaka kutuchanganya wananchi tuliopoteza matumaini ya maisha haya na kumtafuta hata malaika mmoja anayeweza kutuvuta mkono. Tunamkubali kwa kudhani kuwa Sitta ni mkombozi aliyedondoka kwa ajili ya kutubadilishia mfumo wa maisha tunayoyalilia. Hizo ni mbwembwe tu,hana nafasi ya kufanya maamuzi. Analeta propaganda kwa kuwa naye ana machungu yake mengi aliyoyabeba moyoni. Tunapaswa kujiuliza: Je, kelele za Dowans na Richmond zimeanza leo? Alikuwa wapi siku zote?
Six anajaribu kujikosha lakini yeye sasa hivi ni mmoja wa genge hilo. Hatudanganyikiiiiii
Kila nikiona Mtanzania mwenzangu anatoa such comments...... Huwa nakata tamaa kabisa, na kuona Safari bado ni ndefu sana... Na huenda hatutafika in any near future
SITTA bado hajachelewa, anaweza kujinasua kwa kujiuzulu uwaziri na kuamua kubakia kama mbunge. Bila ya shaka kwa uamuzi huo, CCM watamvua uwanachama na kwa hivyo kukosa sifa ya kuwa mbunge, na bila shaka hatua hiyo itazidi kuwathibitishia Watanzania udikteta, ufisadi na ulafi wa CCM, na Watanzania watamuunga mkono Sitta. Uchaguzi mdogo ukiitishwa agombee kupitia chama chengine. Hapa falsafa ya "Ukishindwa kupigana nao, ungana nao" haitekelezeki, bali "Ukishindwa kupigana nao, tengana nao".Sitta hana pa kuponea
Hivi hayo magazeti ya serikali (habari leo na Daily newz) kwa nini hayaandiki habari hii ya Dowans kushinda kesi na kutakiwa kulipwa mabilioni?
Mimi yangu macho. Tusubiri tuene kitakacho mpata 6