Namheshimu sana Samuel Sitta lakini kwa hili naona kachemsha. Kama waziri, ameingia kujibu masuala ambayo si ya wizara yake, yaleyale ya Lyatonga Mrema ninayosikia yakisimuliwa ya kujifanya waziri wa kila wizara (angalao Lyatonga nasikia alipewa ruksa hiyo na mzee Ruksa). Angetolea mchango wake huo kwenye baraza la mawaziri, kazi ya kusema magazetini amwachie waziri mhusika.