Wanaomkosoa Nyerere wana hoja?

duh hii lugha kwa kweli ngumu. I'm trying kwa kweli.


ha ha haaaa
actually nimeanza hata kujua nini utaandika next lol
since engineer bukuku alivyosema tatizo lako ni kuwa
you love nyerere too much....its love......
Naelewa usichokielewa
 
ooh noo inabidi unisome vizuri; sijasema unampenda Kikwete; nimesema Kikwete si anapendwa na hatishi kama Nyerere (ambacho ni kipimo chako wewe kuwa alikuwa anatisha!). Sasa nimesema kama Nyerere kwa maelezo yako alikuwa anatisha na kupendwa kwa wakati mmoja alikuwa mbaya kwa sababu hiyo basi Kikwete lazima awe bora kwa sababu hatishi na anapendwa. Kikwete ana tabasamu zuri, haogopwi kama alivyokuwa anaogopwa Nyerere. Ndio swali, je tumefurahi na Kikwete asiyetisha na anayependwa?

Acha spinning we mzee wangu!

unataka view zangu? Kikwete naye anatisha!

Jaribu kuandamana uone, jaribu kudai haki uone....tisho lakikwete liko so openly! anatumia mtutu kutawala na anaua na usalama wa taifa kutisha watu.

Nyerere alikuwa anatumia usalama wa taifa na anakupoteza kabisa

hawa wote mambo yao yataandikwa tu vizazi vyote
 
Eti "Emotional Intelligence-Groups EI", "Visionary", "Integrity"??? Duuh! Hayo maelezo uliyotoa yaani hayaendani kabisa na maana halisi ya dhana hizo za kiingereza na tena za kigeni. Mswahili bana akijifanya naye kaenda shule, inakuwa taabu tupu!
Mkuu acha utumwa wa kiakili, wewe ukiona mtu anajua kiingereza au kuandika basi wewe unaona eti kaenda shule! wewe ukifika Uingereza utasema Waingereza wote ni Wasomi, Kiingereza ni lugha kama kichagga tu, jibu hoja kwa wanaomkosoa Nyerere
 
Acha spinning we mzee wangu!

unataka view zangu? Kikwete naye anatisha!

Jaribu kuandamana uone, jaribu kudai haki uone....tisho lakikwete liko so openly! anatumia mtutu kutawala na anaua na usalama wa taifa kutisha watu.

Nyerere alikuwa anatumia usalama wa taifa na anakupoteza kabisa

hawa wote mambo yao yataandikwa tu vizazi vyote

Kikwete anafanana sana na Nyerere then. Ni Dikteta naye?
 
ha ha haaaa
actually nimeanza hata kujua nini utaandika next lol
since engineer bukuku alivyosema tatizo lako ni kuwa
you love nyerere too much....its love......
Naelewa usichokielewa

the opposite could be true kwako na kwa wanaomchukia Nyerere. They hate him too much.
 
sasa si tuna rahisi anayependwa na anayesikiliza sana tena ana sura nzuri kweli dr. so and so?; hatishi? are we happy?
Hahahahah.....wakanywe nae kahawa sasa!Mzee Mwanakijiji! Kwakweli mie ninapoona watu wanajaribu kutafuta vijisababu vya nguvu kuthibitisha Nyerere alikua Mtu mbaya sijui hata wanataka nini?? Hatukatai kuna aliyokosea, haya watupe basi alikuja akapatia?? Kama alikua hafai angalia leo hii vitu vyote alivyotuasa tusivifanye waliomfuata wakafanya-nini kinatokea?? Alituasa khs JK, nini kinatokea? Azimio la Arusha kwanini baadhi ya viongozi wanadai lirudi? Uongozi wa Umma alifanya ni kazi ya kutojirimbikizia mali, angalia leo marumbano ya posho-wote wanaotaka ziendelee hamna hata anaetoa mashiko ya maana zaidi ya kusingizia ni sheria, mara tuzitumia kuwasaidia wananchi, je, ndio maelekezo ya matumizi ya hizo posho mliyopewa?? Basi badilisheni jina, ili mzifanyie retirements na kuwe na justification inayokubalika kwy auditing. Katika mambo ya maendeleo, angalia kwa uchache tu vitu alivyoanzisha kama vingeendelezwa vizuri leo hii tungekua wapi? Sidhani hata kama tungehitaji vyama vingi.
 
Kikwete anafanana sana na Nyerere then. Ni Dikteta naye?

Uko huru kusema dikteta au la, definition ya u-dikteta iko kwenye mawazo na standard ya mtu personally! is not universal and it will never be!!

nadhani nimeishawahi kukujibu kama hivi mkuu!! sijawahi kusema Nyerere dikteta, ila sitampinga mtu anayemwita Nyerere dikteta, wala simtampinga wanaomwita Kikwete dikteta (lawyers wa kanada wamesema Kikwete anatawala kidikteta kwa mauaji ya Nyamongo)!

MKJJ neno dikteta wanapewa mpaka akina baba majumbani, walimu wakuu wa mashuleni...mpak wachungaji.....Kakobe juzi zmeitwa dikteta!!

sasa hizi ligi zako za kusema ikiwa A iwe B, siziwezi hizi ligi mkuu!!

pole mkuu!
 
aliwanyima watu wa pwani elimu, na kuwekeza sana arusha na kuitwa azimio la kuijenga arusha
unasikitisha ndugu!! ulitaka awashike kwa nguvu na kuwapeleka shule? pwani? hujui kama kwa sehemu kubwa (pwani) ilikaliwa na waarabu ambao hawakujali elimu dunia.Arusha hujui ni moja ya maeneo (pamoja na kilimanjaro) yaliyokaliwa na wazungu waliowekeza katika elimu kwa kujenga shule, na hospitali. Pia ujue kama Nyerere asingelitaifisha shule za wazungu kuwa za umma sijui leo ungelisema nini? maana hata hao wakazi wa pwani wachache waliosoma sijui wangelisomea wapi??? funguka na uweze kuchambua mambo kwa mapana yake na si kuingiza udini hapa.
 
the opposite could be true kwako na kwa wanaomchukia Nyerere. They hate him too much.

Hapa ndiyo ninapoanza kushawishika kuwa Nyerere hahitaji kujitetea bali maisha yake mwenyewe yanajenga utetezi mkubwa, sasa ndugu yangu Mwanakijiji sijakupata vizuri ama sijakuelewa kwa hivyo ni swala la opposite tu? kwa maana mimi siamini kuwa unampenda NYERERE nachojua unaandika ukweli kuhusu mawazo, sera na fikra za NYERERE au nimekosea mkuu?
 
Ni bora utawala Dikteta Nyerere watz maskini walienda shule bure kwa uchumi uliotegemea pamba, mkonge na mazao mengine ya kilimo kuliko leo tunategemea dhahabu, Tanzanite, Almasi, Mito na maziwa, mbuga za wanyama etc. Ni bora utawala wa Kimaskini wa Dikteta Nyerere viongozi wake hawakuwa mafisadi, wabaguzi wa dini na kabila, wabadhirifu, matajiri, waroho, wachumia tumbo, waongo kama hawa wa leo wa kidemokrasia. Nyeree was the best than Ever.
 
Nafuatilia mijadala mingi kuhusu Nyerere. Kuna kitu watu wanakiificha au hawataki kukikubali. Nyerere kama mwanadamu hakosi sura mbili . Sura hizi ni ya yale mema aliyofanya na yale mabaya aliyofanya. Mema yana sura moja ya wema, mabaya yan sura mbili za ubaya, kwanza ni je, ubaya ulikuwa wa dhamira na pili, ni kwa makosa ya kibinadamu!

Wengi ambao kwa kusema ukweli hawasomi au hawakuwahi kuishi nyakati za Nyerere wanadiriki kuongelea ya Nyerere bila kuwa na reference kwasababu tu wanahubiriwa au kufundishwa. Mapungufu haya ambayo ni sehemu kubwa ya udhahifu wetu watanzania ndiyo chanzo cha watu kuanzisha topic ile ile kila kukicha. Inashangaza wasio Watanzania wanaweza kuandika na wanaufahamu mkubwa sana kuliko sisi kuhusu Nyerere ambaye tuna access na nyaraka zote ikiwa ni pamoja na majarida, vitabu na hata watu waliofanya kazi naye kwa ukaribu sana.

Matokeo ya kusikia au kusimuliwa yanadhihirika kwa watu kushindwa kutetea hoja zao kwa ushahidi. Wengi wanapenda kujadili kwa hisia tu ili waweke nadharia zao lakini inapowekwa nyaraka ya kuthibitisha hawana uwezo wa kuitetea.
Tumeona hapa JF kila ikiwekwa nyaraka inayomhusu Nyerere watu wanakimbia na kesho yake unakuta Thread mpya iliyoanzishwa kwa nadharia. Fikiria mtu anaposema Nyerere aling'oa reli ya Dar -Mtwara hapa ni nini kama si masimulizi bila ya utafiti au uthibitisho wa aina yoyote.

Nyerere kama Icon na Beacon anachambuliwa kuliko viongozi wengine na hiyo ndiyo privilege ya great personality. Nina mambo ninayoyaeleza kila siku kuhusu mapungufu ya mwalimu, lakini hayo siwezi kuyatumia kuficha mema aliyoyafanya. Hakuna ushindani bali ni ushindanishi wa hoja.

Lile kundi linalomtetea Mwalimu, sio lazima kuwa linampenda bali linatetea rekodi yake inayoharibiwa makusudi ili kuunda rekodi iliyokusudiwa na si iliyopo. Kundi linalomchukia Nyerere linaongozwa na chuki na linatumia mbinu za kutafuta makosa ya kweli na ya uongo ili kujenga hoja zinazoshabihiana na lengo hilo. Tofauti ya makundi haya mawili ni kuwa kundi la kwanza lipo tayari kusimama na ushahidi kutetea hoja. Kundi la pili kwa bahati mbaya halipendi mjadala wenye data, takwimu au ushahidi, bali kujenga nadharia ambayo mara nyingi haiwezi kuitetea.

Mfano, mtu atasema Nyerere alikuwa dikteta, well and good! prove it, no answer. Yaani tuamini tu kwasababu imesemwa.
Nyerere alikuwa mdini, hapa amekuja Mohamed Said mwenye takwimu, hakuweza kuthibitisha zaidi ya kudai wazee wake wengine walifariki siku moja kabla hajawahoji. Mohamed said ameshindwa, kama wasivyoweza kutetea wanao amini nadharia ya udini wa Nyerere.

Nyerere alikuwa mkabali, inawezekana!!!, prove it, hakuna jibu, ila tuamini tu kwasababu fulani kasema.
Nyerere ndio chanzo cha mgao wa umeme, ok! prove it, ah ooh unajua ujamaa, kambona etc, ili mradi tu hakuna hoja bali kumsingizia.
Hakujenga viwanda, then prove vilivyojengwa baada yake, aahh aoooh unajua may be, hakuna jibu.

Kumewekwa nyaraka ya mpango wa maendeleo 1963.... wote wanaomchukia mwalimu wameingia mitini. Hakuna hata mmoja aliyethubutu kuonyesha, ukanda, ukabila au udini wa mwalimu.

Makosa ya mwalimu yasemwe, mazuri yasemwe na ikibidi yawekwe kwenye mizani, lakini tungo, mashairi yenye vibwagizo hayatusaidiii hata kidogo.
Tuangalie hoja bila kuongozwa na chuki zetu za kibinadamu au kufundishwa. Tuangalie kazi yake na tuichambue bila kuangali umbo lake.
Tujadili hoja kwa ushahidi si kusadikika, nadharia, majungu, ngano, mashairi au simulizi.
 
Nguruvi, umesema kweli kwa mfano Bukuku hapo juu kasema ati ukimpinga Nyerere "anakupotezea" tukimbana atoe mfano ataanza kutukwepesha maana ya neno "kupotezea" kwa sababu hakutaka kutumia neno "kuua!". Amesema Kikwete anatawala kwa mtutu wa Bunduki na "anaua" yaani anamtuhumi Rais wa Tanzania kuwa ni muuaji; akiambiwa atoe ushahidi wa maneno hayo makali - ambayo sisi wengine wakosoaji wakubwa wa Kikwete hatuthubutu kuyatumia kwa sababu ni charge ambayo ina criminal element - kwa maneno mengine anasema Kikwete ni mhalifu. Tukimuuliza ataanza kufafanua maana ya "kutawala kwa mtutu wa bunduki na kuua" nje ya maana ambayo hata mtoto mdogo anaelewa.

Wanasema Nyerere aliua "watu wengi" hadi leo hakuna mtu aliyekuja na idadi au mifano ya watu waliouawa na Nyerere! Wengine wanasema wakati wa Operesheni Vijijini "Maelfu ya watu waliuawa" lakini hakuna mtu ambaye amewahi kutuonesha japo orodha ya watu kumi - zaidi ya kutuambia "nilisimuliwa na baba yangu au bibi"! Na tukiwabana sana usije ukashangaa mtu anakuja na stori kuwa Nyerere "alikuwa na gas chambers huko Mtwara!"; Leo hii wapo wanaeneza kabisa kuwa Nyerere alikuwa na chuki na Waislamu, na ukiwaletea ushahidi wa kiakili na kuwahoji wanaanza -hamtaki kukubali kwa sababu mnafanya Nyerere Mungu!

Halafu cha kuudhi wenye kuendesha fikra hizo wanaamini kabisa wao ni miongoni mwa wasomi. Hii inashangaza. Sasa hawa kama wangekuwa wakati wa Mwalimu wangeweza hata kujenga hoja ikaeleweka? Wangeweza kujibu maswali ambayo wanaulizwa au watakaa kimya na kufanya kama walivyofanya wale jamaa - wakamuita Nyerere "haambiliki" kumbe sasa tunajua kwanini alikuwa haambiliki! hawakuwa na cha kumwambia zaidi ya kunung'unika. Watu wanataka kusikilizwa si kwa sababu ya uzito wa hoja zao bali uzito wa vyeo vyao, majina au nafasi zao.
 
Kupata habari kupitia TV. kwani Tv ya mwanzo ilianza wakati wa mwinyi
Chakula cha kutosha. kwani tukipanga foleni hadi za mawe.
Sabuni na bidhaa muhumi kuadimika

Hata sasa hivi watu wanakula mizizi, mbona huulizi? Mwl. RIP
 
Hapa ndiyo ninapoanza kushawishika kuwa Nyerere hahitaji kujitetea bali maisha yake mwenyewe yanajenga utetezi mkubwa, sasa ndugu yangu Mwanakijiji sijakupata vizuri ama sijakuelewa kwa hivyo ni swala la opposite tu? kwa maana mimi siamini kuwa unampenda NYERERE nachojua unaandika ukweli kuhusu mawazo, sera na fikra za NYERERE au nimekosea mkuu?

Nampenda Nyerere
Namheshimu Nyerere
Namsoma Nyerere
Napata hekima kutoka kwake
Nimejifunza mengi kuhusu yeye, udhaifu wake, mapungufu yake na makosa yake
Nimejifunza maana ya uongozi, falsafa yake, maono yake n.k

I am un-apologetically Nyerereist. Sijaanza leo, kinyume na watu wengine, sijajifunza walichoandika kina Smith na Johnson; nimefunza kwanza kabisa alichoandika na kusema yeye mwenewe Nyerere, nimejifunza vilivyoandikwa na watu wenyewe - maandishi ya Prof. Maina kuhusu Detention act, masimulizi ya watu engine mbalimbali - kama kina Prof Njozi (ambaye nilifanya naye mahojiano ya kina miaka minne iliyopita) na kina Mohammed Said ambaye tumejadiliana mengi. Badala ya kusikiliza watu tu nimekusanya vitabu vingi vya wakati wa Nyerere, hotuba zake zote muhimu, maandishi ya watu kama kina Dr. Kleruu (sijui kama kuna watu wanajua aliwahi kuandika kitu!)

Njia pekee ya kutafuta ukweli ni kuusaka, na kuwa tayari kuufuata kokote utakakokuongoza. Mapenzi yangu kwa Nyerere hayakuja hivi hivi tu. Ninaamini katika maabdiliko, aliposimama Mwanza (pale Nyamagana) kumpigia kampeni Mkapa, nilimsikiliza na nilisikiliza hoja zake lakini sikukubaliana na chaguo la Mkapa - nilimpigia kura Mrema! Ndio mbegu ya mageuzi ndani yangu ilivyowashwa. Lakini ni katika kuzidi kujua zaidi ya nchi yangu ndio nikaamua kwa makusudi kujifunza juu ya Nyerere na kuachana na masimulizi ya mitaani. Ukianza na chuki huwezi kujua uzuri wa mtu.

Ni sawasawa na mtu akaja na kukuambia "unamuona yule kijana, ni mwizi sana akiingia kwako uwe mwangalifu kweli". Sasa kijana wa watu akija nyumbani kwako utafanya nini? Utaanza kuwa mwangalifu, ukimwacha ndani ukirudi unaanza kuangalia kama kila kitu kipo. Baada ya muda unakuja kugundua kuwa yule jamaa kumbe alikuwa amegombana na huyo kijana na akataka amharibie tu ili asiaminiwe. Unamuuliza kijana anakupa stori yote na unakuja kugundua ni kijana muaminifu kweli kwani uliposahau wallet yako aliokota na kukurudishia na kila senti nawe ukashangaa - kwanini ulishangaa? kwa sababu uliamini alikuwa mwizi! kisa? uliambiwa.

So wakati mwingine kama msomi, take time to read Nyerere usitusikilize tu humu tunavyolumbana.
 
Chakula hadi sasa ni tatizo,watu wanashinda na kulala bila kula,habari hadi leo si wote wanaopata habari,tena kwa makusudi ya serikali,maana wanapoish hakuna umeme,hivyo redio na t,v ni anasa,lakini pia hata magazeti hawapati maana njia ni mbovu.......intaneti ndio anasa kabisaaaaa,kwani weeeeng wa watanzania hawazmudu gharama za kompyuta,intaneti.........
 
Hi sasa ni balaaa! Nimesoma makala moja ya gazeti la raia mwema ... mwandishi anataka kuhusisha udhaifu wa uongozi wa serikali ya awamu ya nne na Nyerere. Raia Mwema
 
Hi sasa ni balaaa! Nimesoma makala moja ya gazeti la raia mwema ... mwandishi anataka kuhusisha udhaifu wa uongozi wa serikali ya awamu ya nne na Nyerere. Raia Mwema

Na hii ndio sababu kubwa ya kushamiri kwa mijadala kuhusu failures za Nyerere sasa hivi....Kwamba matatizo yaliyopo hayakuanza sasa, hata wakati wa Nyerere yalikuwepo na akashindwa kuyamaliza! Watawala wetu wanaficha madhaifu yao kwa kuonyesha madhaifu ya wengine....
 
Agreed,but two wrongs do not make a right.Ubabaishaji na upuuzi mwingine wa Kikwete hauwezi kuhalalisha kufunika mapungufu aliyokuwa nayo Nyerere.Na JK anaweza kujitetea (katika kuficha udhaifu wake) kuwa alirithishwa nchi iliyokwishakongoroka.With exception of madhara ya the 1978-9 Kagera war,Nyerere angeweza kutupa sababu zipi za msingi za kuliacha taifa likiwa hoi bin taaban wakati anastaafu 1985?
Ndugu, Kikwete hapaswi kujitetea kwa kusema hata Mwl,Baba wa taifa aliliacha taifa likiwa hohe hahe,..arudi nyuma kidogo kwa Mkapa,aliye mtangulia. hali haikuwa mbaya kama tuliyonayo sasa.
Ukweli unabaki pale,kuwa Mwl alikosea mambo kadha wa kadha,na mwenyewe alikili hilo. Kinachonipa shida ni criticism hizo with respect to Mkweree..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom