Luteni
JF-Expert Member
- Jan 9, 2010
- 2,274
- 302
WAHISANI wamepunguza mchango wao kwenye bajeti ya serikali kwa mwaka 2010/2011 kwa sababu mbalimbali, ikiwamo kasi ndogo ya serikali katika kutekeleza mageuzi katika sekta za umma.
Taarifa ya Wahisani hao iliyotolewa jijini Dar es Salaam jana, imesema katika mwaka huo watatoa Dola za Marekani 534 milioni sawa na (Sh721bilioni), ambazo ni pungufu kwa Dola za Marekani 220 milioni (sawa na Sh297 bilioni) walizotoa mwaka 2009/2010.
Wahisani wa bajeti ya serikali ni Benki ya Maendeleo Afrika (ADB), Canada, Denmark, Jumuiya ya Ulaya (EU), Finland, Ujerumani, Ireland, Japan, Uholanzi, Norway, Sweden, Uswisi, Uingereza na Benki ya Dunia (WB) ambao mwaka jana walichangia Sh1.9 trilioni katika bajeti ya serikali kupitia miradi ya maendeleo na mifuko ya kisekta.
Katika bajeti hiyo ya mwaka 2009/2010 Sh milioni 968,028 zilitokana na mikopo ya ndani na sehemu ya mchango wa wahisani hao kupitia misaada ya kibajeti.
ADB ambayo ndiyo mwenyekiti wa wahisani hao jana, ilieleza katika taarifa yake kwa vyombo vya habari kuwa uamuzi wa kupunguza fedha za kusaidia bajeti ya serikali, umetokana na mambo mengi, ikiwemo serikali kushindwa kufikia malengo kadhaa ya maendeleo.
Taarifa hiyo ilitaja maeneo ambayo serikali ilishindwa kufikia malengo kuwa ni mabadiliko ya haraka katika menejimenti ya sekta ya fedha za umma, mategemeo ya kuboreka kwa hali ya mazingira ya uwekezaji na uwekezaji na uboreshaji wa huduma kwa kutoka sekta za umma.
Hii ni mara ya nne kwa wahisani hao kuiwekea ngumu serikali katika kuchangia bajeti yake kila inapofikia mwisho wa mwaka, kwa kushindwa kutekeleza mambo yanayowavutia kutoa fedha.
Mwaka juzi wahisani hao waligoma kutoa fedha baada ya serikali kusuasua kuchukua hatua dhidi ya watuhumiwa wa ufisadi wakiwemo wa fedha za EPA mpaka zilipofunguliwa kesi kadhaa ambazo mpaka sasa zinanguruma mahakamani.
Akizungumza katika mkutano huo, ambao ulihusisha nchi wahisani na taasisi za kimataifa, Mwenyekiti wa Nchi Wahisani wa Bajeti ya Serikali (DPG), Peeter Dorst alisema nchi wahisani zinaamini kuwa ni muhimu kwa serikali kuonyesha wanachukua hatua katika suala zima la rushwa zikiwemo rushwa ndogo na kubwa.
Alisema hali hiyo inatokana na habari za hivi karibuni kuonyesha kuwa Tanzania imeshuka nafasi 24 katika suala zima la uwazi katika mapambano dhidi ya rushwa.
Source: Gazeti la Mwananchi
Taarifa ya Wahisani hao iliyotolewa jijini Dar es Salaam jana, imesema katika mwaka huo watatoa Dola za Marekani 534 milioni sawa na (Sh721bilioni), ambazo ni pungufu kwa Dola za Marekani 220 milioni (sawa na Sh297 bilioni) walizotoa mwaka 2009/2010.
Wahisani wa bajeti ya serikali ni Benki ya Maendeleo Afrika (ADB), Canada, Denmark, Jumuiya ya Ulaya (EU), Finland, Ujerumani, Ireland, Japan, Uholanzi, Norway, Sweden, Uswisi, Uingereza na Benki ya Dunia (WB) ambao mwaka jana walichangia Sh1.9 trilioni katika bajeti ya serikali kupitia miradi ya maendeleo na mifuko ya kisekta.
Katika bajeti hiyo ya mwaka 2009/2010 Sh milioni 968,028 zilitokana na mikopo ya ndani na sehemu ya mchango wa wahisani hao kupitia misaada ya kibajeti.
ADB ambayo ndiyo mwenyekiti wa wahisani hao jana, ilieleza katika taarifa yake kwa vyombo vya habari kuwa uamuzi wa kupunguza fedha za kusaidia bajeti ya serikali, umetokana na mambo mengi, ikiwemo serikali kushindwa kufikia malengo kadhaa ya maendeleo.
Taarifa hiyo ilitaja maeneo ambayo serikali ilishindwa kufikia malengo kuwa ni mabadiliko ya haraka katika menejimenti ya sekta ya fedha za umma, mategemeo ya kuboreka kwa hali ya mazingira ya uwekezaji na uwekezaji na uboreshaji wa huduma kwa kutoka sekta za umma.
Hii ni mara ya nne kwa wahisani hao kuiwekea ngumu serikali katika kuchangia bajeti yake kila inapofikia mwisho wa mwaka, kwa kushindwa kutekeleza mambo yanayowavutia kutoa fedha.
Mwaka juzi wahisani hao waligoma kutoa fedha baada ya serikali kusuasua kuchukua hatua dhidi ya watuhumiwa wa ufisadi wakiwemo wa fedha za EPA mpaka zilipofunguliwa kesi kadhaa ambazo mpaka sasa zinanguruma mahakamani.
Akizungumza katika mkutano huo, ambao ulihusisha nchi wahisani na taasisi za kimataifa, Mwenyekiti wa Nchi Wahisani wa Bajeti ya Serikali (DPG), Peeter Dorst alisema nchi wahisani zinaamini kuwa ni muhimu kwa serikali kuonyesha wanachukua hatua katika suala zima la rushwa zikiwemo rushwa ndogo na kubwa.
Alisema hali hiyo inatokana na habari za hivi karibuni kuonyesha kuwa Tanzania imeshuka nafasi 24 katika suala zima la uwazi katika mapambano dhidi ya rushwa.
Source: Gazeti la Mwananchi