Uzembe wa madaktari waua tena Hospitali ya DDH Bunda

Basi mwaka 1996 nilipeleka mwanagu hapo Bunda DDH alikuwa anaumwa homa Kali sana.nikaonana na Dkt nikaandikiwa vipimo nikaenda maabara mtoto akapimwa nikapewa majibu kuwa ana homa Kali sana lakini hana Maji kabisa muda wowote anaweza kufa.
Ikabidi Dkt aache watu wako mwenye foleni akaondoka na mgonjwa wangu mpaka hodini akamwambia nesi mwekee huyu mtoto drip sasa hivi Fanya haraka.nesi kaleta drip yule Dkt akaondoka akawahi wagonjwa aliowaacho foleni.
Alipoondoka tu nesi akaning'iniza chupa ya Maji mwenye stand bila kumwekea mtoto ,nesi akaenda kukaa kwenye kichumba chao akatutelekeza
Hapo.kila nikimfata ananijibu kwa hasira INA maana unatufundisha kazi.
Kikaona hapa nikizubaa mwanangu anakufa basi nikamfata nesi kwa hasira nikamukwida nimpe vibao ,ghafula Dkt mkuu WA hospt Dkt Sweya akatokea alikuwa anatembea hodini anasalimia wagonjwa ,akaona nilivyo mkwida akaja nikamweleza kila kitu nesi akakoromewa akatolewa akaletwa mwingine mwanangu Dkt sweya akamwekea drip.
Ajabu hata nesi aliyeletwa nae ni jipu Muda kidogo kitanda nilicholazwa akaletwa mtoto mmoja toka kijiji kung'ombe ameishiwa damu ,wakamtoa babaake damu ,ikaletwa ikatundikwa kwenye stand ikatelekezwa hapo .
Nikawa namsihi baba MTU nenda wafate anaogopa .zaidi ya SAA moja hajawekewa damu yule mtoto akafa.nesi akachukua ile CHUPA ya damu akaondoka nayo sijui alienda kuiuza.
Ukifikiria utadhani hawa manesi wana mkataba na kuzimu WA kuchomoa roho zetu.hawana huruma
Mimi mkuu katika masuala yanayohusu roho ya mtu sina huruma na masihara....huyo jamaa ni mzembe kwa kushuhudia kifo cha mwanae kwa uzembe wa nesi....alafu unamuacha nesi atambe kwa kauli ya bahati mbaya huku wewe umeshapoteza mtoto huku akipokea mshahara kama kawaida....
 
Tusisahau kutokujali hakuko afya tu, hata benki, ardhi, polisi, simu n.k. Tusiwalaumu sana hawa watu. Kila mtu awajibike eneo lake.
Tuanze na afya kwanza mengine yatafuata........


Ardhi inatafutwa maisha ya mtu yanatafutiwa wapi???
 
Mimi sitaweza kuvumilia kumpoteza mpendwa wangu kwa uzembe wa mtu mwenye jukumu la kuokoa maisha ya mpendwa wangu na analipwa kwa kazi hiyo......wakati home wanapanga mazishi na wao kwao lazima wapange mazishi na nitakuwa naendelea na kesi ya kuua kwa bahati mbaya.....
Hizi kesi zimekuwa nyingi sana acha zile zisizo ripotiwa na wahusika wamekuwa wakitoa maelezo kama kwamba waliopoteza maisha ni midoli tu nasio binaadamu...

Nakumbuka kisa kimoja cha mtu fulani aliyekuwa amelazwa kwenye kituo fulani cha afya.....
Nesi alipomkuta kazimia akawaambia ndugu zake kuwa amefariki na ndugu wakaanza kuangua kilio.....ikawa wanaandaa mipango ya mazishi na maiti wakaipeleka nyumbani.....wakati wanamuaandaa maiti kwa ajili ya mazishi mara ghafla marehemu akazinduka na kuwashangaa wao....

Sasa jiulize kesi kama hizo zipo ngapi....??na ni wangapi wanazikwa hai....kama jamaa asingezinduka si ndio angefukiwa moja kwa moja.......???

Pole sana mkuu. Hii Africa yetu bado ni majanga sana aisee. Ebu imagine mgonjwa anawekewa dripu ya sukari bila ya kipimo kwanza cha haraka. Yani muuguzi (sijuwi ndo nesi) anakisia tu na kufanya maamuzi afanye hiki. Hapo hakuna tofauti na ramli.

Unabunia tu na kumuwekea mtu dripu ya sukari ilihali kumbe mwili wake hauhitaji hicho kitu, then kwa uzembe huo mgonjwa anakufa! Afu eti ooh bahati mbaya, ooh mipango ya Mungu, and blah blah! Inaumiza sana walahi.

Ifike mahala watu waanze kushtakiwa kwa kosa la 'professional negligence' kama nchi zilizoendelea. Otherwise watu hawatakuwa makini wala kufuata guidelines za profession zao ktk kuhudumia watu.

Ndo maana mimi binafsi huwa naamini kwamba majanga na vifo vingi hapa Africa ni kutokana na UZEMBE (negligence/recklessness) tu, wala hakunaga bahati mbaya!! Na hii 'bahati mbaya' ndo ishakuwa utetezi wetu wa kila siku.

Poleni sana
Halafu hatuko makini na post mortam(spelling sijui kama ni sahihi)
 
Mungu amlaze pema, jambo la kushangaza kwanini hospital za tz kila mgonjwa anatundikiwa drip tu kila akionekana yuko hoi?

Ni ajabu sana kiasi unaongea doc anaandika utumbo
Niliwauliza hili swali wakasema 'kwa kawaida' mgonjwa aliye hoi cha kwanza huwa ni drip ya sukari....kwahiyo kazi zinafanyika kwa mazoea
 
kuna tatizo kubwa kwenye sekta ya afya siku hizi unapeleka mgonjwa dakteri anamkimbia anaacha nesi anamhudumia sijui kwa sababu kuna vyuo vingi vya kibiashara au maadili yameshuka tukiendelea kukaa kimya tutakuwa tunapoteza wapendwa wetu na kusingizia mapenzi ya Mungu
 
Sheria zipo, lakini wananchi hawazijui haki zao. Nilipokuwa Chuo tulifundishwa na kutahadharishwa kuhusu uzembe katika kuhudumia wagonjwa; Tatizo ndo hilo, wananchi wetu hawazijui haki zao.

Nchi za wenzetu mawakili ndo dili zao hizi, Mtumishi wa AFYA afanye kosa la kugharimu uhai au kiungo cha raia aone fidia atakayotozwa!!!
 
Ndio matatizo ya kusajili vyuo vingi vya afya na kushindwa kusimamia ipasavyo ethics zinazotolewa hapo chuoni kwa wahitimu. Wauguzi wengi ni graduates wa vyuo private ambavyo hata hao walimu wao ni wababaishaji tu.
 
Huenda pia kukawa na Manesi feki hapo DDH, tahadhari inahitajika ili kunusuru hali za wagonjwa.
Pumzika kwa Amani ndgu Sostenes Mitti.
 
Bado sijaona details za kumuhukumu mtoa huduma...naona watu wanajadili experiences zao kwenye huduma za afya in a negative thinking...
Kuna scenario za ndugu kuongeza kasi ya drip wakidhani ndio dawa inaenda haraka ili mgonjwa apone kumbe hupelekea majanga...pengine hao ndugu walifanya hivyo ....who knows?

Kuna scenario za ugomvi wa majumbani kuletwa hadi mahospitalini....mtu anabeba maziwa yenye sumu na kuja kumywesha mgonjwa ili afe apate urithi...kifo kikotokea atalaumiwa daktari ....

So far naona tunajadili hisia za mleta mada badala ya facts!!
 
Kiukweli hili tatizo sio Mara ya kwanza au ya pili but imekua nimazoea hospital I nyingi zimekua ziki Fanya kazi kwa mazoea mabaya
 
Ndio matatizo ya kusajili vyuo vingi vya afya na kushindwa kusimamia ipasavyo ethics zinazotolewa hapo chuoni kwa wahitimu. Wauguzi wengi ni graduates wa vyuo private ambavyo hata hao walimu wao ni wababaishaji tu.
Unashutumu vipi chuo wakati hujui waliomhudumia wana elimu gani?
 
Tusisahau kutokujali hakuko afya tu, hata benki, ardhi, polisi, simu n.k. Tusiwalaumu sana hawa watu. Kila mtu awajibike eneo lake.
Nakubaliana nawe kabisa ni lazima watu wawajibike kwa taaluma zao, mara nyingi wajenzi wamewekwa kitimoto na serikali, hata wafanyakazi wengine kama watumishi wa ardhi nao wamekumbwa na kadhia hii ya kushitakiwa kwa maamuzi mabovu.

Ifike mahali na madokta washtakiwe pia
 
Sina hamu na Manesi kabisa maana nilimpoteza mama mdogo wangu, kaendaa kujifungulia hospitali ya Magu na baada ya kujifungua akakoswa huduma na kufariki dunia.
Mwishoni mwa mwaka jana 2015 mama mmoja amepelekwa kwenda kujifungua akakoswa huduma baada ya nesi wa zamu kutokuwepo mda wa kazi majira ya usiku na kupelekea mama huyo kufariki dunia.
 
Back
Top Bottom