Uzembe wa madaktari waua tena Hospitali ya DDH Bunda

Urio kimiroI

Senior Member
Jan 2, 2016
146
74
Imefikia wakati Wa Madaktari wetu kushtakiwa wanaposababisha Vifo vya watu kwa Makusudi au uzembe katika matumizi ya Taaluma yao.

Tunahitaji kuleta nidhamu katika matumizi ya Taaluma.Huwa tunapenda kukimbilia ni mapenzi ya Mungu hata kwa watu tuliowaharakishia mauti.

Sostenes Mitti Majira ya Saa kumi na Moja Jioni Jana tarehe 06 February 2016 Alijihisi vibaya akaondoka mwenyewe kwenda Hospital ya DDH Bunda kucheck Afya yake.Madaktari walimuattend na kumwekea Drip ya Maji kushusha Pressure,wakaendelea na shughuli zao wakimuacha ,mpaka marafiki walipokuja kumuona na kukuta amefariki ndipo wakawaita madaktari na wao kuanza kushangaa tu.Unawezaje kumwekea mgonjwa aliyeserious drip nawe ukaenda mbali.Kifo hiki kimeniumiza na naamini ni uzembe kwani kilichotokea kwa Mitti miaka miwili iliyopita nikiwa Bunda niliugua nikamwomba Mitti anisindikize,wakanilaza kwenye private ward zao hapo hospitalini kwao,wakanitundikia drip.Usiku akaja nesi mwanafunzi akabadilisha ile drip ya Quinine na kuongeza spidi ya follow,Akaondoka baada ya kama dakika kumi Hali yangu ilibadirika nikaita nesi nesi nesi hakukuwa na dalili ya MTU kuitikia.Nikampigia Sostenesi nikiwa siwezi kupumua vizuri,watafute uwezekano wa madaktari maana nimetelekezwa.

Hali ilizidi kuwa mbaya,nilichokumbuka nikuomba nakujua muda wangu umekwisha.Ndipo ghafla akaingia mama Mdogo ambaye ni daktari hospital hiyo hakuwa zamu,na hakujua kama nipo hospitalini pale alipigiwa simu na Mitti,akaja anakimbia akanikuta nimelowa na sina uwezo Wa kuongea kwa sauti,nikamwonyesha Drip akaona tatizo akaichomoa drip na kuleta oksjeni na kuniwekea baada ya kama nusu saa nikapata nafuu na akina Mitti walikuwa tayari wapo wamezunguka kitandani wasijue kinachotokea.

Niliwaeleza kilichotokea kuhusu Yule nesi alitafutwa hakupatikana kabisa.Tulifuatilia na Mitti,hakutokea na Daktari Wa zamu hakuweza kumtambua,.

Ninapoambiwa Sosteness katuacha katika Mazingira Yale Yale inaumiza sana.Tunahitaji kufuatilia kwa karibu utoaji huduma za Afya katika Hospital ya DDH ,Vinginevyo wananchi watakatiliwa Maisha kila kukicha.

Tangulia Mdogo wangu Mitti uliokoa maisha yangu,nimeshindwa kuwepo kukuokoa.Bwana alitoa na BWANA ametwaa.Jina la Mungu wetu lihimidiwe.
 
You knew about that DDH and why did you allow that to happen to your friend? Or you assumed things have changed? We should always not take chances

RIP Mitti
 
Pole sana mkuu kwa msiba,nimehuzunika sana kwa kisa hiki cha nduguyo Mitti.
MUNGU na akupe subira katika kipindi hiki kigumu kwako.
 
Nilimpeleka ndugu yangu ocean road hospital alikuwa na shida ya cancer. ..kufika Pale kuonekana yuko dhaifu saana akapewa drip ya sukari bila vipimo
Baadae doctor alipokuja kufanya vipimo akakuta sugar iko 32 normal ni 4-7 , wakastopisha ile drip haraka sana but it was too late alifariki siku ileile jioni...hii imetokea mwezi uliopita
 
Nilimpeleka ndugu yangu ocean road hospital alikuwa na shida ya cancer. ..kufika Pale kuonekana yuko dhaifu saana akapewa drip ya sukari bila vipimo
Baadae doctor alipokuja kufanya vipimo akakuta sugar iko 32 normal ni 4-7 , wakastopisha ile drip haraka sana but it was too late alifariki siku ileile jioni...hii imetokea mwezi uliopita
pole kaka
 
Ishu kama hizi ndio mtu unajikuta kizimbani kwa kesi ya kuua bila kukusudia. :hatari:
 
Daaaah,nimesikitika sana!Hasa kwenye hiyo paragraph ya mwisho.
R.I.P Mitti
 
Mimi sitaweza kuvumilia kumpoteza mpendwa wangu kwa uzembe wa mtu mwenye jukumu la kuokoa maisha ya mpendwa wangu na analipwa kwa kazi hiyo......wakati home wanapanga mazishi na wao kwao lazima wapange mazishi na nitakuwa naendelea na kesi ya kuua kwa bahati mbaya.....
Hizi kesi zimekuwa nyingi sana acha zile zisizo ripotiwa na wahusika wamekuwa wakitoa maelezo kama kwamba waliopoteza maisha ni midoli tu nasio binaadamu...
 
Nakumbuka kisa kimoja cha mtu fulani aliyekuwa amelazwa kwenye kituo fulani cha afya.....
Nesi alipomkuta kazimia akawaambia ndugu zake kuwa amefariki na ndugu wakaanza kuangua kilio.....ikawa wanaandaa mipango ya mazishi na maiti wakaipeleka nyumbani.....wakati wanamuaandaa maiti kwa ajili ya mazishi mara ghafla marehemu akazinduka na kuwashangaa wao....

Sasa jiulize kesi kama hizo zipo ngapi....??na ni wangapi wanazikwa hai....kama jamaa asingezinduka si ndio angefukiwa moja kwa moja.......???
 
R.I.P MITTI, ungejua usingempeleka pale as long as unajua sio mahali pazuri, au hospital ipo moja tu huko? Poleni
 
Kuna siku tutachoka kuandika 'R.I.P' kwa vifovvya kizembe zembe kama hivi, tukifika hapo itabidi hao watoa huduma za afya wajengewe makambi ya kuishi.
 
Back
Top Bottom