Uzembe wa madaktari waua tena Hospitali ya DDH Bunda

Nilimpeleka ndugu yangu ocean road hospital alikuwa na shida ya cancer. ..kufika Pale kuonekana yuko dhaifu saana akapewa drip ya sukari bila vipimo
Baadae doctor alipokuja kufanya vipimo akakuta sugar iko 32 normal ni 4-7 , wakastopisha ile drip haraka sana but it was too late alifariki siku ileile jioni...hii imetokea mwezi uliopita


Pole sana mkuu. Hii Africa yetu bado ni majanga sana aisee. Ebu imagine mgonjwa anawekewa dripu ya sukari bila ya kipimo kwanza cha haraka. Yani muuguzi (sijuwi ndo nesi) anakisia tu na kufanya maamuzi afanye hiki. Hapo hakuna tofauti na ramli.

Unabunia tu na kumuwekea mtu dripu ya sukari ilihali kumbe mwili wake hauhitaji hicho kitu, then kwa uzembe huo mgonjwa anakufa! Afu eti ooh bahati mbaya, ooh mipango ya Mungu, and blah blah! Inaumiza sana walahi.

Ifike mahala watu waanze kushtakiwa kwa kosa la 'professional negligence' kama nchi zilizoendelea. Otherwise watu hawatakuwa makini wala kufuata guidelines za profession zao ktk kuhudumia watu.

Ndo maana mimi binafsi huwa naamini kwamba majanga na vifo vingi hapa Africa ni kutokana na UZEMBE (negligence/recklessness) tu, wala hakunaga bahati mbaya!! Na hii 'bahati mbaya' ndo ishakuwa utetezi wetu wa kila siku.

Poleni sana
 
Mungu amlaze pema, jambo la kushangaza kwanini hospital za tz kila mgonjwa anatundikiwa drip tu kila akionekana yuko hoi?

Ni ajabu sana kiasi unaongea doc anaandika utumbo
 
Inahuzunisha sana kumpoteza mtu kwa uzembe kama huu. Mungu amlaze mahala pema peponi. Amen.
Lakini wakuu kila mtu katika eneo lake la kazi awe muwajibikaji. Unaweza ukawa wamlalamikia mtumishi wa afya kwa uzembe, hadi ukatamani kumtoa roho, lakini wewe pia waweza ukawa mtumishi jipu sehemu nyingine. Tunaweza walaumu watumishi wa afya kwa sababu wao wakikosea wanaweza wakasabisha kifo, ila sisi tukikosea labda watu wanakosa haki zao, wajane wananyang'anywa mali, na mambo mengi maeneo ya kazi yetu. Tukumbuke kwamba watumishi wa afya nao ni watu kama sisi, wao si malaika na hawatakuwa malaika. Na kwamba kazi zote tunazofanya ni wito, si kwa daktari, mwalimu na polisi tu. Tukiwa maeneo yetu ya kazi tumhudumie vizuri mteja, atoke akitabasamu.
 
Basi mwaka 1996 nilipeleka mwanagu hapo Bunda DDH alikuwa anaumwa homa Kali sana.nikaonana na Dkt nikaandikiwa vipimo nikaenda maabara mtoto akapimwa nikapewa majibu kuwa ana homa Kali sana lakini hana Maji kabisa muda wowote anaweza kufa.
Ikabidi Dkt aache watu wako mwenye foleni akaondoka na mgonjwa wangu mpaka hodini akamwambia nesi mwekee huyu mtoto drip sasa hivi Fanya haraka.nesi kaleta drip yule Dkt akaondoka akawahi wagonjwa aliowaacho foleni.
Alipoondoka tu nesi akaning'iniza chupa ya Maji mwenye stand bila kumwekea mtoto ,nesi akaenda kukaa kwenye kichumba chao akatutelekeza
Hapo.kila nikimfata ananijibu kwa hasira INA maana unatufundisha kazi.
Kikaona hapa nikizubaa mwanangu anakufa basi nikamfata nesi kwa hasira nikamukwida nimpe vibao ,ghafula Dkt mkuu WA hospt Dkt Sweya akatokea alikuwa anatembea hodini anasalimia wagonjwa ,akaona nilivyo mkwida akaja nikamweleza kila kitu nesi akakoromewa akatolewa akaletwa mwingine mwanangu Dkt sweya akamwekea drip.
Ajabu hata nesi aliyeletwa nae ni jipu Muda kidogo kitanda nilicholazwa akaletwa mtoto mmoja toka kijiji kung'ombe ameishiwa damu ,wakamtoa babaake damu ,ikaletwa ikatundikwa kwenye stand ikatelekezwa hapo .
Nikawa namsihi baba MTU nenda wafate anaogopa .zaidi ya SAA moja hajawekewa damu yule mtoto akafa.nesi akachukua ile CHUPA ya damu akaondoka nayo sijui alienda kuiuza.
Ukifikiria utadhani hawa manesi wana mkataba na kuzimu WA kuchomoa roho zetu.hawana huruma
 
Basi mwaka 1996 nilipeleka mwanagu hapo Bunda DDH alikuwa anaumwa homa Kali sana.nikaonana na Dkt nikaandikiwa vipimo nikaenda maabara mtoto akapimwa nikapewa majibu kuwa ana homa Kali sana lakini hana Maji kabisa muda wowote anaweza kufa.
Ikabidi Dkt aache watu wako mwenye foleni akaondoka na mgonjwa wangu mpaka hodini akamwambia nesi mwekee huyu mtoto drip sasa hivi Fanya haraka.nesi kaleta drip yule Dkt akaondoka akawahi wagonjwa aliowaacho foleni.
Alipoondoka tu nesi akaning'iniza chupa ya Maji mwenye stand bila kumwekea mtoto ,nesi akaenda kukaa kwenye kichumba chao akatutelekeza
Hapo.kila nikimfata ananijibu kwa hasira INA maana unatufundisha kazi.
Kikaona hapa nikizubaa mwanangu anakufa basi nikamfata nesi kwa hasira nikamukwida nimpe vibao ,ghafula Dkt mkuu WA hospt Dkt Sweya akatokea alikuwa anatembea hodini anasalimia wagonjwa ,akaona nilivyo mkwida akaja nikamweleza kila kitu nesi akakoromewa akatolewa akaletwa mwingine mwanangu Dkt sweya akamwekea drip.
Ajabu hata nesi aliyeletwa nae ni jipu Muda kidogo kitanda nilicholazwa akaletwa mtoto mmoja toka kijiji kung'ombe ameishiwa damu ,wakamtoa babaake damu ,ikaletwa ikatundikwa kwenye stand ikatelekezwa hapo .
Nikawa namsihi baba MTU nenda wafate anaogopa .zaidi ya SAA moja hajawekewa damu yule mtoto akafa.nesi akachukua ile CHUPA ya damu akaondoka nayo sijui alienda kuiuza.
Ukifikiria utadhani hawa manesi wana mkataba na kuzimu WA kuchomoa roho zetu.hawana huruma
 
Kumbe alipata huduma? Ni mapenzi ya Mungu tu hapo, acha kutafuta mchawi.

Tumuombe marehemu Mungu amrehemu. Ameen.
 
Mungu amlaze pema, jambo la kushangaza kwanini hospital za tz kila mgonjwa anatundikiwa drip tu kila akionekana yuko hoi?

Ni ajabu sana kiasi unaongea doc anaandika utumbo
Mkuu huwezi ukasema kwanini kwa sababu wagonjwa ni tofauti na watumishi wa afya wanaowatibu ni tofauti kitaaluma na uwezo. Hilo swali inatakiwa unamuuliza indication aliye order hizo fluids apewe mgonjwa, ili walau akupe sababu. Ila kwa uelewa wangu mdogo si kila mgonjwa anahitaji hayo maji yao.
 
Kifo ni mpango ya mungu,mi nilishawah kulazwa hapo siku tatu tena private ward enzi nikikuwa BUNDA TC,nilipenda huduma za DDH,Manesi na madoctor wakalimu
 
Kumbe alipata huduma? Ni mapenzi ya Mungu tu hapo, acha kutafuta mchawi.

Tumuombe marehemu Mungu amrehemu. Ameen.
hakupata huduma shtahiki , mtu anakuwekea drip alafu anaenda nyumbani kufanya mapenzi, tatizo kubwa linaonekana lipo kwa uongozi wa hospital hiyo, watumishi wanajifanyia wanavyotaka hakuna wa kuwaajibisha, serikali iwachukulie hatua hawa watu, bahati nzuri mashahidi wapo
 
Mkuu Urio kimiroI
Pole sana kwa msiba.
Naamini kichwa UZEMBE WA MADAKTARI UMEUA TENA ni hukumu.
Tunaona madaktari wengi wakiwa hawajali, lakini kutokujali kwao si chanzo cha kifo siku zote. Mfano nilisikia ugonjwa wa kichaa cha mbwa hautibiki. Sasa mgonjwa anaweza akalazwa na kichaa cha mbwa, madaktari wasioneshe kujali na akafa. Issue inakuja, je kutojali mgonjwa ndio kumeua au pia mgonjwa alikuwa na ugonjwa ambao death ilikuwa inevitable.
Wenzetu huwa na kitu wanaita death inquest, sijui kama Tz tunafanya.
 
Mkuu, unaushahidi wauguzi walienda kufanya "mapenzi?"
Punguza mihemuko ya kisiasa, muombeeni Kada kapumzike kwa Aman.
 
Imefikia wakati Wa Madaktari wetu kushtakiwa wanaposababisha Vifo vya watu kwa Makusudi au uzembe katika matumizi ya Taaluma yao.

Tunahitaji kuleta nidhamu katika matumizi ya Taaluma.Huwa tunapenda kukimbilia ni mapenzi ya Mungu hata kwa watu tuliowaharakishia mauti.

Sostenes Mitti Majira ya Saa kumi na Moja Jioni Jana tarehe 06 February 2016 Alijihisi vibaya akaondoka mwenyewe kwenda Hospital ya DDH Bunda kucheck Afya yake.Madaktari walimuattend na kumwekea Drip ya Maji kushusha Pressure,wakaendelea na shughuli zao wakimuacha ,mpaka marafiki walipokuja kumuona na kukuta amefariki ndipo wakawaita madaktari na wao kuanza kushangaa tu.Unawezaje kumwekea mgonjwa aliyeserious drip nawe ukaenda mbali.Kifo hiki kimeniumiza na naamini ni uzembe kwani kilichotokea kwa Mitti miaka miwili iliyopita nikiwa Bunda niliugua nikamwomba Mitti anisindikize,wakanilaza kwenye private ward zao hapo hospitalini kwao,wakanitundikia drip.Usiku akaja nesi mwanafunzi akabadilisha ile drip ya Quinine na kuongeza spidi ya follow,Akaondoka baada ya kama dakika kumi Hali yangu ilibadirika nikaita nesi nesi nesi hakukuwa na dalili ya MTU kuitikia.Nikampigia Sostenesi nikiwa siwezi kupumua vizuri,watafute uwezekano wa madaktari maana nimetelekezwa.

Hali ilizidi kuwa mbaya,nilichokumbuka nikuomba nakujua muda wangu umekwisha.Ndipo ghafla akaingia mama Mdogo ambaye ni daktari hospital hiyo hakuwa zamu,na hakujua kama nipo hospitalini pale alipigiwa simu na Mitti,akaja anakimbia akanikuta nimelowa na sina uwezo Wa kuongea kwa sauti,nikamwonyesha Drip akaona tatizo akaichomoa drip na kuleta oksjeni na kuniwekea baada ya kama nusu saa nikapata nafuu na akina Mitti walikuwa tayari wapo wamezunguka kitandani wasijue kinachotokea.

Niliwaeleza kilichotokea kuhusu Yule nesi alitafutwa hakupatikana kabisa.Tulifuatilia na Mitti,hakutokea na Daktari Wa zamu hakuweza kumtambua,.

Ninapoambiwa Sosteness katuacha katika Mazingira Yale Yale inaumiza sana.Tunahitaji kufuatilia kwa karibu utoaji huduma za Afya katika Hospital ya DDH ,Vinginevyo wananchi watakatiliwa Maisha kila kukicha.

Tangulia Mdogo wangu Mitti uliokoa maisha yangu,nimeshindwa kuwepo kukuokoa.Bwana alitoa na BWANA ametwaa.Jina la Mungu wetu lihimidiwe.
Pole sana mkuu......
 
Pole kwa mfiwa...RIP Mitti!

Nasikitika na title ya thread yako ya kusema uzembe wa madaktari wakati hujatuambia yafuatayo....

1-Tatizo la presha kwa marehemu lilianza lini?aligundulika siku hiyo hiyo au lilikuwako kwa muda mrefu na alikuwa akitumia dawa na kwenda kliniki?

2-Alipofika hospitali na kupimwa presha ilikuwa kiasi gani?na je alichopewa ni hiyo drip pekee ama kuna dawa nyingine?

3-Unaweza kuitambua aina ya drip aliyowekewa kwa jina?nauliza hili kwa sababu hakuna drip ya maji ya kushusha presha duniani bali kuna dawa ya kushusha presha inayoweza kuwekwa kwenye drip

4- Aliyesema kuwa hakuonwa mpaka ndugu walipofika ni nani?Ndugu walifika muda gani kwani kwa taratibu za hospitali nyingi huwezi kumuona mgonjwa mida ya usiku...kama alienda saa 11 jioni naamini ndugu hawakuwa na fursa ya kuingia kumuona iwapo utaratibu umefuatwa.

5-Unaweza kutaja cheo cha mhudumu aliyemhudumia ili tujue kama ni daktari au muuguzi au mganga....kwani sio kila aliyeko hospitali ni daktari....unaweza kuwa unalaumu madaktari kumbe aliyemuona ni muuguzi wa kiume.

Nasisitiza kukupa pole lakini ili shutuma zako ziwe za haki ni vyema ukaja na ushahidi wa kutosha kwani ninavyoamini hakuna daktari aliyekula kiapo akawa na nia ya kupoteaza maisha ya mgonjwa....!

Uzembe huwa unatokea lakini inabidi uelezee kwa ufasaha ili usiwakute wengine!

RIP MITTI
 
Ndio maana wengine wanakimbilia kwa waganga tu.....

Ila tatizo ni kukosa uwajibikaji

Na manesi kwenye hospitali za serikali ni majanga sana
 
Imeniuma sana utafikiri yamenikuta mimi, hivyo na bugando ni zaidi ya hao, yaanikupeleka mgonjwa wako akiwa mahuhuti bugando ni sawasawa na kumzika kabla hajakata roho. Juzi kati nilikuwa pale kwenye folen mama mmoja alionekana mtu wa kijijini sana, akanivuta mkono akaniambia naomba elfu 70 mama yake yuko hoi anataka kufanyiwa operation tho operation ni laki 3 nikamwambia mbona sina? Akanambia watamtumia baadae mpesa kwanza nimsaidie hiyo,kweli nilikuwa sina iyo 70 kwa mda huo maana nami nilikuwa na mtoto wa dada ana tatizo la mguu na ndo tulikuwa tunaingia kwa dr, nikwamwambia ebu wambie home wakutumie hela nikupeleke mpesa utoe, akanambia hana mpesa yeye anatumia halotel na pale bugando hakuna iyo huduma, dah nikaitwa kwa dr, mama alivyoona nimeondoka alimwaga machozi kumbe alikuwa alishaomba msaada kila mmoja anamkwepa. Nilivyoingia kwa dr nikamwacha dada na mtoto nikarudi kumwona huyo mama alikuwa anatoka tarime,hata kiswahili tulikuwa hatuelewani vizuri, kujielezea ni sheeda, nikamwomba no ya mtu ambae anataka kumtumia simu, nikamwomba atume hiyo hela kwangu ili nimtolee, siku hiyo mtandao ulikuwa mbovu mpaka sa 11 za jion ndo hela iliingia, nikamtolea nikampa,akashukuru nikaenda home, kumbe ambe mgonjwa wake alikuwa hoi hakojoi ni maumivu makari, akalipa 250000 ili mgonjwa afanyiwe operation elfu 50 atazilipa baadae maana iyo 50 alibaki nayo kwa matumizi ya chakula, mwee usiku ananipigia, kuwa hela amelipa mpaka sasa hawajamuhudumia na kumbuka mgonjwa hapo alikuwa na siku 3 anapewa panado. Aliponipig niende kumsaidia niongee na ma dr akanambia mtoto wake ana njaa sasa ikabidi kwa nipike hili niende kumdaidia nafika bugando tu akafariki, hela alishalipa huduma hakuna, tukaanza kulia, kwenda kuomba arudishiwe hela imsaidie kusafilisha mwili wakasema hiyo hela ataishugulikia baadae kwanza aende azike atarudi loh bugando mmelaaniwa yule mama hakufa kwa mapenzi ya mungu. Ma dr wa bugando kama mko humu hii ni laana mnapenda hela kuliko uhai wa mtu???
 
Vifo kama hivi vinahuzunisha sana, ni matokeo ya kutojali utu na ubinadamu. Ni wakati sasa wa kuwachukulia hatua, kuna elements za professional negligence na ukiangalia mtiririko wa threads utagundua kuwa sekta ya afya hasa ya umma ina tatizo la ubora wa huduma zitolewazo.

Mungu akupe roho ya ustahimilivu katika kipindi hichi.
 
Vifo kama hivi vinahuzunisha sana, ni matokeo ya kutojali utu na ubinadamu. Ni wakati sasa wa kuwachukulia hatua, kuna elements za professional negligence na ukiangalia mtiririko wa threads utagundua kuwa sekta ya afya hasa ya umma ina tatizo la ubora wa huduma zitolewazo.

Mungu akupe roho ya ustahimilivu katika kipindi hichi.
Tusisahau kutokujali hakuko afya tu, hata benki, ardhi, polisi, simu n.k. Tusiwalaumu sana hawa watu. Kila mtu awajibike eneo lake.
 
Back
Top Bottom