Ulikuwepo enzi za DUKA LA KAYA??

Duh umenikumbusha mbali nakumbuka enzi hizo nilikuwa mdogo natumwa kukaa nje kusubiri gari la sukari likisimama niwastue ndani gari ina mlango nyuma ina mifuko ya kilo moja moja ya kaki na huruhusiwi kununia zaidi ya mfuko mmoja.

Shikamoo mama.
 
mkuu mimi niliambulia kuona hayo maduka ya RTC sukari, vyombo kwa foleni, kijijini huko naenda na mama kupanga foleni ya kununua robo kilo ya sukari, daftari niliwahi kununua kwa senti 5 1986,
Acha uongo basi. 1986 hata shilingi yenyewe usingeweza kununua kitu. Eti senti tano? Bongo fleva
 
Mwadui ilikuwepo Toka enzi za ukoloni kwa hiyo nyerere asingeweza kufanya kitu.asingeweza kufanya kitu?..hustuki?..we unashtushwa na hotuba ya 2007?...Hii suppott yenu hata kwenye upuuzi uliofanywa na nyerere na mkapa ndio unaotufanya tuamini kuwa chuki dhidi ya kikwete inaanzia kanisani

Nimegundua wewe ni mdini sana; angalia sana usije jikuta jehanamu ya moto.
 
Wewe ulikuwepo enzi za DUKA LA KAYA? Na ile hali ilikuwa ni halisi au ilisababishwa na uzembe wa Mwalimu kushindwa kuona kwamba kulikuwa na hatari ya njaa inatunyemelea?

Swali lako hapa ni rahisi sana; lakini labda uliulize kivingine... unakumbuka ni Watanzania wangapi walikufa kwa baa la njaa wakati wa duka la kaya? Kule mtaani kwenu au kijijini unakumbuka kuwaona watu wanatembea mbavu nje kwa njaa; au hata kama unakumbuka watu waliokuwa wanakula mizizi yenye sumu ili kupata angalau chochote mdomoni...?? Labda kama kuna mtu mwingine anaweza kutusaidia katika haya...

Unachoita "uzembe" wengine tunakiona "the genius of Mwalimu". Hivi unajua leo hii kuna Watanzania wanatatizo la njaa na hii imekuwa ni kila mwaka licha ya kwamba hakuna tena "duka la kaya"?

Ukisoma wote "wanaokumbuka" kwenda kupanga foleni, kupewa mgao wao utaona kuwa hakuna hata mmoja ambaye anasimama na kusema kuwa kwenye familia yao kuna mtu alikufa kwa njaa...!!

Think about it.. je bila ya duka la kaya tungekuwaje?
 
Kweli watu wametoka mbali. Nakumbuka kaka yangu alivunjika mkono wakti akigombea katika foleni kutaka kununua sababu ya mbuni pale mtaa wa Aggrey kariakoo.

Nakumbuka ilikuwa mkiwa mnakwenda kuswali alfajr tunaweka mawe katika duka la kaya pale Aggrey na ukitoka msikitini tunapangiana zamu kulinda jiwe letu maana mkiondoka tu watu wanalitupa. Na gari la Ugawaji linakuja saa sabaa au nane alasiri.

Kila mtu alikuwa lazima amjue Mkurugenzi mkuu wa NMC mzee Mollel au Mkurugenzi wake wa utawala Mz Uwesu msumi kwa ajili ya kupata kibali cha kununua vitu kwa wingi.

Kweli kila watu na zama zao.
Kumbe wewe ni muislam?
 
Weka mfano wa hivyo vitu kuandika tu vitu "tangible" ni so vague.

Nilikuwepo wakati huo, kabla ya huo na Alhamdulillah nipo sasa. Tusiandikie mate na wino upo.

Penye nyekundu hapo sijakuelewa weka sawa ili nielewe unataka nini.
 
Penye nyekundu hapo sijakuelewa weka sawa ili nielewe unataka nini.

Pole sana kwa kutokuelewa kwako maana ya AlhamduliLlah. Wala usipate taabu ya kuelewa, achana na huo mstari wa pili, jibu mstari wa kwanza, hiyo nyekundu haikuwa swali kwako. Hiyo ni expression ya kumshukuru Allah alieniwezesha kuwepo wakati huo wa maduka ya "kata" mpaka hii leo.

Nasubiri.
 
Duh! Mkuu unajua kutia chumvi kama mahindi ya kuchoma ya kileo? Pombe watu walikua wanapiga ila wanawahi kama sanduku mbili mnanunua mnaweka chini ya meza mkiogopa zisiishe. Na pia magari ya Serikali yalikua siku za Jumapili kutembea mwisho saa 8 na hii ilifanywa ili watu wasitumie magari ya serikali kwa starehe zao na ilikua gari la Serikali halitakiwi kuonekana limepaki Bar ukionekana unakamatwa na Polisi ilikua ni suala la maadili sio kama sasa .

NAdhani wewe ndio unatia chumvi! Binafsi baba yangu alikuwa na gari miaka hiyo ya 1960s mpaka 1980s, tukitaka kwenda mahali siku ya Jumapili NI LAZIMA UOMBE KIBALI MAALUM... sijui kuhusu bia, ila ya kuendesha gari siku ya Jumapili ni ukweli ulio wazi na mimi kama shahidi! labda kama familia yako haikuwa ikimiliki gari miaka hiyo huwezi litambua hilo.

Kuhusu Folen nilishawahi kuminywa mitaa ya Mkunguni kwenye duka la kaya Mh! sisahau! kweli tuliteseka! na mguuni una katambuga la kigogo! matairi yalikuwa ni mali ghafi enzi hizo! machicha hayakuwa nyuma kwa kutenegezwa sabuni za kuogea! kuna miti siikumbuki ukiogea matunda yake na kufulia yalikuwa yanatoka mapovu! hahah Nyerere banaaa!
 
NAdhani wewe ndio unatia chumvi! Binafsi baba yangu alikuwa na gari miaka hiyo ya 1960s mpaka 1980s, tukitaka kwenda mahali siku ya Jumapili NI LAZIMA UOMBE KIBALI MAALUM... sijui kuhusu bia, ila ya kuendesha gari siku ya Jumapili ni ukweli ulio wazi na mimi kama shahidi! labda kama familia yako haikuwa ikimiliki gari miaka hiyo huwezi litambua hilo.

Mkuu ahsante kwa kumjibu huyo jamaa limbogamboga. Mimi mwenyewe ni shahidi kwamba tuliwahi kukamatwa na Traffic na baba yangu tukitoka kanisani baada ya saa saba mchana na gari la baba yangu likapelekwa kituo cha kati. Nilishangaa sana huyo jamaa kunibishia kwamba magari ya BINAFSI yalikuwa hayazuiliwi kutembea siku ya jumapili.
 
umenikumbusha mbali sana.miaka ya themanini mwanzoni nikiwa primary school.enzi hizo duka let LA kaya likiwa ofisi za SHIHATA.KWA sasa ofisi za tume ya mawasiliano.wengi wetu tuliudharau unga WA njano tukadhani chakula cha mifugo ughaibuni..kumbe umejaa tele madukani kwao!
 
Mkuu ahsante kwa kumjibu huyo jamaa limbogamboga. Mimi mwenyewe ni shahidi kwamba tuliwahi kukamatwa na Traffic na baba yangu tukitoka kanisani baada ya saa saba mchana na gari la baba yangu likapelekwa kituo cha kati. Nilishangaa sana huyo jamaa kunibishia kwamba magari ya BINAFSI yalikuwa hayazuiliwi kutembea siku ya jumapili.
Ilikuwa shauri ya kuchunga matumizi ya mafuta hali ilikuwa mbaya sana na hata mashindano ya magari E.African rally yalipigwa marufuku nchini

 
Swali lako hapa ni rahisi sana; lakini labda uliulize kivingine... unakumbuka ni Watanzania wangapi walikufa kwa baa la njaa wakati wa duka la kaya? Kule mtaani kwenu au kijijini unakumbuka kuwaona watu wanatembea mbavu nje kwa njaa; au hata kama unakumbuka watu waliokuwa wanakula mizizi yenye sumu ili kupata angalau chochote mdomoni...?? Labda kama kuna mtu mwingine anaweza kutusaidia katika haya...

Unachoita "uzembe" wengine tunakiona "the genius of Mwalimu". Hivi unajua leo hii kuna Watanzania wanatatizo la njaa na hii imekuwa ni kila mwaka licha ya kwamba hakuna tena "duka la kaya"?

Ukisoma wote "wanaokumbuka" kwenda kupanga foleni, kupewa mgao wao utaona kuwa hakuna hata mmoja ambaye anasimama na kusema kuwa kwenye familia yao kuna mtu alikufa kwa njaa...!!

Think about it.. je bila ya duka la kaya tungekuwaje?
Nakumbuka Nyerere alinusurika kupinduliwa mara 5 shauri ya kuchokwa.

 
Nakumbuka dukani mnalazimishwa kununua sigara zilikuwa zinaitwa zakuchuja na zaraa, pamoja na tube ya baiskeli wakati hauna baiskeli huku tumevaa makatambunga.
 
Swali lako hapa ni rahisi sana; lakini labda uliulize kivingine... unakumbuka ni Watanzania wangapi walikufa kwa baa la njaa wakati wa duka la kaya? Kule mtaani kwenu au kijijini unakumbuka kuwaona watu wanatembea mbavu nje kwa njaa; au hata kama unakumbuka watu waliokuwa wanakula mizizi yenye sumu ili kupata angalau chochote mdomoni...?? Labda kama kuna mtu mwingine anaweza kutusaidia katika haya...

Unachoita "uzembe" wengine tunakiona "the genius of Mwalimu". Hivi unajua leo hii kuna Watanzania wanatatizo la njaa na hii imekuwa ni kila mwaka licha ya kwamba hakuna tena "duka la kaya"?

Ukisoma wote "wanaokumbuka" kwenda kupanga foleni, kupewa mgao wao utaona kuwa hakuna hata mmoja ambaye anasimama na kusema kuwa kwenye familia yao kuna mtu alikufa kwa njaa...!!

Think about it.. je bila ya duka la kaya tungekuwaje?

Ni kweli usemacho mimi sijawahi binafsi kusikia watu wakilalamika kufa kwa njaa ila kwa ujasiri wanasifu kuwa wote walipata na walijifunza kutumia kwa makini isingekuwa vl kuna uwezekano wachache wangepata huku wengi wangekosa.kwani soko lingeshikwa na wachache kwa maslai ya wachache.
Kwa wakati ule ilibidi mwalimu kufanya vl na ilifaa kwa wakati huo hata mie sioni kosa.
 
Back
Top Bottom