Ulikuwepo enzi za DUKA LA KAYA??

Kigarama

JF-Expert Member
Apr 23, 2007
2,492
1,230
Kuna watu wanatolea mfano wa kushindwa kwa sera za Mwalimu Nyerere kwa kuhusianisha na DUKA LA KAYA. Enzi hizo wengine tulikuwa tunakimbizana na magari ya "Ugawaji" kwenye kila duka wanalosimama, wakati mwingine tukiyakimbiza magari hayo umbali wa hadi kilomita tano au sita.

Ilikuwa ni kawaida kupita kwenye maduka na kukuta msururu mreefu wa mawe yaliyopangwa kama alama ili wenye mawe hayo wakija wapate nafasi ya mbele kwenye foleni. Nakumbuka kulazimishwa kununua unga wa muhogo wenye mchanga ili tuweze kupata sukari kilo mbili na nusu kwa mujibu wa Kadi yetu ya Duka la kaya iliyokuwa inayonyesha kwamba nyumba yetu ina wanakaya 5.

Enzi hizo mgambo waliokuwa wanalinda kwenye maduka ya Kaya (Consumer's Cooperative shop) walikuwa wanaabudiwa sana mitaani kwani wao kila ukija mgao na wao hawakosi kupewa, tofauti na watu wa kawaida ambao wao ni mpaka "zamu" yao ifike. Wauzaji wa maduka haya walikuwa hawajui kabisa kubembeleza wateja kwani wateja walikuwa hawana uchaguzi kutokana na kutakiwa kununua mahitaji yao kwenye maduka walikoandikishiwa kama Wateja.

Wewe ulikuwepo enzi za DUKA LA KAYA? Na ile hali ilikuwa ni halisi au ilisababishwa na uzembe wa Mwalimu kushindwa kuona kwamba kulikuwa na hatari ya njaa inatunyemelea?
 
So???
Nyerere alijaribu kufanya alichofanya kwa kiasi chake, wewe unafanya nini?

Siamini katika kucheza 'mwathirika" (don't play victim)
 
Kuna watu wanatolea mfano wa kushindwa kwa sera za Mwalimu Nyerere kwa kuhusianisha na DUKA LA KAYA. Enzi hizo wengine tulikuwa tunakimbizana na magari ya "Ugawaji" kwenye kila duka wanalosimama, wakati mwingine tukiyakimbiza magari hayo umbali wa hadi kilomita tano au sita.

Ilikuwa ni kawaida kupita kwenye maduka na kukuta msururu mreefu wa mawe yaliyopangwa kama alama ili wenye mawe hayo wakija wapate nafasi ya mbele kwenye foleni. Nakumbuka kulazimishwa kununua unga wa muhogo wenye mchanga ili tuweze kupata sukari kilo mbili na nusu kwa mujibu wa Kadi yetu ya Duka la kaya iliyokuwa inayonyesha kwamba nyumba yetu ina wanakaya 5.

Enzi hizo mgambo waliokuwa wanalinda kwenye maduka ya Kaya (Consumer's Cooperative shop) walikuwa wanaabudiwa sana mitaani kwani wao kila ukija mgao na wao hawakosi kupewa, tofauti na watu wa kawaida ambao wao ni mpaka "zamu" yao ifike. Wauzaji wa maduka haya walikuwa hawajui kabisa kubembeleza wateja kwani wateja walikuwa hawana uchaguzi kutokana na kutakiwa kununua mahitaji yao kwenye maduka walikoandikishiwa kama Wateja.

Wewe ulikuwepo enzi za DUKA LA KAYA? Na ile hali ilikuwa ni halisi au ilisababishwa na uzembe wa Mwalimu kushindwa kuona kwamba kulikuwa na hatari ya njaa inatunyemelea?

Ninakumbuka ila nilikuwa bado mdogo, enzi hizo kuna ndugu yetu alitokea malawi alituletea Sabuni na sukari, mzee alikuwa anashauri tuvifiche maana ile product tungeulizwa imetoka wapi in case ikionekana. Lakini binafsi ninamkubali sana Nyerere amekaa madarakani kwa miaka 23 lakini Mwinyi miaka10+, Mkapa10, na sasa Kikwete miaka5 halali na Mmoja wa usio halali. Lakini mpaka sasa ukiangalia vitu tangible vilivyofanyika enzi za Nyerere ni vingi kuliko vilivyofanyika ndani ya Tawala hizi tatu.
 
So???
Nyerere alijaribu kufanya alichofanya kwa kiasi chake, wewe unafanya nini?

Siamini katika kucheza 'mwathirika" (don't play victim)
Wewe unadhani mimi namlaumu Mwalimu? Mimi kati ya watu ambao ni watetezi wakubwa wa Mwalimu lakini sikuleta hii mada ili kumhukumu Mwalimu.

Mimi nilishiriki kuiishi hali hii, nilikula unga wa YANGA, nikabugia BURGA, nikaogea MAJANI YA MPAPAI,nimekunywa chai kwa kuchemsha sukari kwa ukosefu wa majani ya chai, nimeogea sabuni ya MAGADI. Huu ni uzowefu wangu wala sina uchungu na sera za Mwalimu!!
 
Kuna watu wanatolea mfano wa kushindwa kwa sera za Mwalimu Nyerere kwa kuhusianisha na DUKA LA KAYA. Enzi hizo wengine tulikuwa tunakimbizana na magari ya "Ugawaji" kwenye kila duka wanalosimama, wakati mwingine tukiyakimbiza magari hayo umbali wa hadi kilomita tano au sita.

Ilikuwa ni kawaida kupita kwenye maduka na kukuta msururu mreefu wa mawe yaliyopangwa kama alama ili wenye mawe hayo wakija wapate nafasi ya mbele kwenye foleni. Nakumbuka kulazimishwa kununua unga wa muhogo wenye mchanga ili tuweze kupata sukari kilo mbili na nusu kwa mujibu wa Kadi yetu ya Duka la kaya iliyokuwa inayonyesha kwamba nyumba yetu ina wanakaya 5.

Enzi hizo mgambo waliokuwa wanalinda kwenye maduka ya Kaya (Consumer's Cooperative shop) walikuwa wanaabudiwa sana mitaani kwani wao kila ukija mgao na wao hawakosi kupewa, tofauti na watu wa kawaida ambao wao ni mpaka "zamu" yao ifike. Wauzaji wa maduka haya walikuwa hawajui kabisa kubembeleza wateja kwani wateja walikuwa hawana uchaguzi kutokana na kutakiwa kununua mahitaji yao kwenye maduka walikoandikishiwa kama Wateja.

Wewe ulikuwepo enzi za DUKA LA KAYA? Na ile hali ilikuwa ni halisi au ilisababishwa na uzembe wa Mwalimu kushindwa kuona kwamba kulikuwa na hatari ya njaa inatunyemelea?


Ndugu umenikumbusha mbali sana, Enzi za kuvaa mtumba toka Burundi unaonekana mhujumu wa uchumi,kuogea Sabuni ya Magwanji na kuvaa Batiki.
Mwl,alijaribu kwa kiasi chake aka prove filure ktk sera za ujamaa na sasa utandawazi.
Enzi za kusikiliza praye(santuri) na mwenye cassete memory Q tajiri?.
Ahsante kaka,
 
Du, kweli umenikumbusha mbali. Nakumbuka kijijini kwetu kulikuwa na Mama aliyekuwa muuzaji (shopkeeper) katika lile duka letu la Ujamaa alikuwa ndo star pale kijijini. Tulikuwa tunasubilia mafuta ya taa au kiberiti. Mungu bariki ugali si chakula chetu kwa hiyo atukula sana unga wa Yanga mpaka wakati wa Vita ya Tz na Uganda.
Nadhani Nyerere alikuwa na nia njema lakini strategy haikufanikiwa.
 
NMC shops models?
Hazifanani kabisa wala na yale maduka ya RTC. Duka la kaya hupati kitu mpaka mjumbe wa nyumba kumi akutambue kama wewe ni makazi wake halafu unaingizwa kwenye Leja wewe na watu wanaokutegemea. Siku ya mgao inawezekana ikawa kila siku ya jumatatu ndiyo zamu yako kama haupo basi mgao wako unahifadhiwa au mgambo kwa kushirikiana na muuzaji wanauza kwa bei ya kuruka.
 
Duka la kaya lilikuwa noma, nakumbuka la mwisho lilikuwa pale Sinza Matokeo.

Nimekunywa sana uji wa chumvi kulaleki, maana mgao wetu sisi ulikuwa kama kilo 2 za sugar hivi. Sometimes unakata.

Kuna siku mzee akarudi kazini na kiroba cha Sukari sijui alikifumania wapi wacha tufurahi.
 
Duka la kaya lilikuwa noma, nakumbuka la mwisho lilikuwa pale Sinza Matokeo.

Nimekunywa sana uji wa chumvi kulaleki, maana mgao wetu sisi ulikuwa kama kilo 2 za sugar hivi. Sometimes unakata.

Kuna siku mzee akarudi kazini na kiroba cha Sukari sijui alikifumania wapi wacha tufurahi.
Kisa kikubwa sana kinachokumbukwa wakati wa Duka la Kaya ni pale Mjumbe wa Nyumba Kumi alipozabwa kibao na kufa na kijana ambaye alikuwa anaahirishiwa "zamu" yake kila siku. Kisa hicho kilitokea maeneo ya Manzese kwa mfuga Mbwa!!
 
OMBI KWA WANWARUMERU MASHARIKI:
Ndugu zangu wana wa Arumeru mashariki kesho ni siku muhimu kwenu
kuchagua maendeleo ama ubabaishaji, Chonde Chonde chagua kiongozi unyemdhani anayajua matatizo yenu na atayafanyia kazi si wale tuliowazoea na ahadi zao toka tupate uhuru msifanye kosa CHAGUENI MTU AMBAYE AMEZALIW ARUMERU, AMESOMA ARUMERU , AMEKULIA ARUMERU NA MTAFANYA KAZI WOTE ARUMERU BAADA YA TAREHE 1/4/2012.
 
Kuna watu wanatolea mfano wa kushindwa kwa sera za Mwalimu Nyerere kwa kuhusianisha na DUKA LA KAYA. Enzi hizo wengine tulikuwa tunakimbizana na magari ya "Ugawaji" kwenye kila duka wanalosimama, wakati mwingine tukiyakimbiza magari hayo umbali wa hadi kilomita tano au sita.

Ilikuwa ni kawaida kupita kwenye maduka na kukuta msururu mreefu wa mawe yaliyopangwa kama alama ili wenye mawe hayo wakija wapate nafasi ya mbele kwenye foleni. Nakumbuka kulazimishwa kununua unga wa muhogo wenye mchanga ili tuweze kupata sukari kilo mbili na nusu kwa mujibu wa Kadi yetu ya Duka la kaya iliyokuwa inayonyesha kwamba nyumba yetu ina wanakaya 5.

Enzi hizo mgambo waliokuwa wanalinda kwenye maduka ya Kaya (Consumer's Cooperative shop) walikuwa wanaabudiwa sana mitaani kwani wao kila ukija mgao na wao hawakosi kupewa, tofauti na watu wa kawaida ambao wao ni mpaka "zamu" yao ifike. Wauzaji wa maduka haya walikuwa hawajui kabisa kubembeleza wateja kwani wateja walikuwa hawana uchaguzi kutokana na kutakiwa kununua mahitaji yao kwenye maduka walikoandikishiwa kama Wateja.

Wewe ulikuwepo enzi za DUKA LA KAYA? Na ile hali ilikuwa ni halisi au ilisababishwa na uzembe wa Mwalimu kushindwa kuona kwamba kulikuwa na hatari ya njaa inatunyemelea?


Ndugu,

Wakati huo nilikuwa ndogo wa kutumwa dukani, umenikumbusha enzi hizo. Namkumkuka mwandishi wake mahiri Mh. Ndimara I. Tegambwage, nawakumbuka baadhi ya wahusika kama vile Bibianna. Nakumbuka mzee mmoja aliyelala usingizi chini ya mti mpaka akakosa huduma ya sukari, akawa nyonge na kumwambia mkewe mara baada ya kurudi nyumbani aweke chumvi kidogo kwenye uji wa mjukuu wake.

Asante sana kwa kutukumbusha, je naweza kukipata tena
 
Ndugu,

Wakati huo nilikuwa ndogo wa kutumwa dukani, umenikumbusha enzi hizo. Namkumkuka mwandishi wake mahiri Mh. Ndimara I. Tegambwage, nawakumbuka baadhi ya wahusika kama vile Bibianna. Nakumbuka mzee mmoja aliyelala usingizi chini ya mti mpaka akakosa huduma ya sukari, akawa nyonge na kumwambia mkewe mara baada ya kurudi nyumbani aweke chumvi kidogo kwenye uji wa mjukuu wake.

Asante sana kwa kutukumbusha, je naweza kukipata tena
Mimi sizungumzii kitabu ndugu yangu. Nazungumzia hali halisi, mimi duka langu nalikumbuka mpaka leo ila bahati mbaya lilipokuwa wajanja wameuza eneo pamejengwa duka binafsi. Zilipokuja Rexona na Lifebouy watu tuliona kama tumefika mbinguni!! Dah. Mchele Kitumbo ulipapatikiwa na kina mama kama vile almasi iliyoanguka kutoka mbinguni, watu walikuwa wameshachoka kula mchele mdundiko!!
 
Wewe ulikuwepo enzi za DUKA LA KAYA? Na ile hali ilikuwa ni halisi au ilisababishwa na uzembe wa Mwalimu kushindwa kuona kwamba kulikuwa na hatari ya njaa inatunyemelea?

Mimi nilikuwepo enzi zile tukiishi Mbezi Juu, na maduka yanapatikana Kawe Ukwamani tu. Kwa kweli ilikuwa hali mbaya sana.

Lakini katu siwezi kuilaumu Serikali ya kipindi kile, kwani ile ilitokana na hali ya Hewa na uhaba wa Chakula. SErikali ilijitahidi hata kuanzisha Maduka ya Kaya, Mobile Shops (Malori ya NMC yalikuwa yanapita mitaani na kuuza chakula kama Duka)

Pia Serikali ilijitahidi hata kuagiza Unga wa Njano ili kuwanusuru wananchi wake. KWA KWELI SERIKALI ILIJITAHIDI.

Wakati ule Serikali tu ilikuwa inaruhusiwa kuuza Chakula kwa wananchi, tena nakumbuka hali ilikuwa na unafuu kwani hata chakula kilikuwa na RUZUKU ya serikali hivyo kuuzwa kwa bei ya chini sana.

Na tulikuwa hatuna Rasilimali nyingi kama tulivyo sasa huenda ingelikuwa kama sasa tunaposhuhudia rasilimali zikichimbwa basi maisha yangelikuwa mazuri zaidi na hata kuweza Serikali kuwalipa mishahara / posho wananchi wake wote. Na kula chakula bure na Waisraeli enzi hizo kule Jangwani walipokula MANA.

RIP Mwalimu J. K. Nyerere, RIP E. M. Sokoine, RIP......


MIZAMBWA
NABII MTARAJIWA!!!
 
Hazifanani kabisa wala na yale maduka ya RTC. Duka la kaya hupati kitu mpaka mjumbe wa nyumba kumi akutambue kama wewe ni makazi wake halafu unaingizwa kwenye Leja wewe na watu wanaokutegemea. Siku ya mgao inawezekana ikawa kila siku ya jumatatu ndiyo zamu yako kama haupo basi mgao wako unahifadhiwa au mgambo kwa kushirikiana na muuzaji wanauza kwa bei ya kuruka.

Usisahau ili kadi ambayo mjumbe wa shina anajaza resho yako. Nakumbuka kipindi hicho nilikuwa single basi baba mwenye nyumba akawa nampa share yangu.
 
Kigarama;

Umenikumbusha mbali sana, Kwa mtu ambaye hakuwa na utambuzi kuanzia 1984 backwards hawezi kukuelewa. Yale mawe na madebe matupu yaliyochakaa tulikuwa tunayaita 'mabandika', tuliuziwa kwa nguvu mbaazi ambazo zilikuwa haziivi, watu badala ya kuuziwa unga kwa kilo wakawa wanauziwa mahindi kwa kilo sasa jiulize ukienda kusaga kilo tatu za mahindi utapata unga kilo ngapi?, watu wakawa wanachemsha mahindi na kula. Maeneo ya nyanda za juu kusini watu walikuwa wanavaa visalfeti kama nguo, ndiyo ukawa mwanzo kwa kuruhusiwa nguo za mitumba.

Nyerere alikuwa ana uchungu hasa na watanzania na maendeleo yao tofauti na viongozi tunaowaona leo hii wenye 'on your own mentality'. Tatizo kubwa la mwalimu lilikuwa kwa watu waliomzunguuka(wasaidizi wake), wengi walikuwa ni watu wenye uelewa finyu na kujikuta wanategemea kila initiative toka kwa Ikulu, ndiyo ikawa chanzo cha kuwa na katiba mbovu iliyolididimiza Taifa kiuchumi na kimaendeleo mpaka leo. Mtu mmoja anakuwa mchumi, daktari, mwanajeshi, polisi, mkulima etc.

Nakumbuka moto aliouwasha Sokoine (RIP) uliwafanya watu kutupa viroba vya sukari na mafuta porini, kuna mtu alikuwa na shehena ya mafuta ya kupikia kaifungia akaona njia pekee ya kumlinda ni kufugia kuku kwenye store ila walimtia nguvuni. Nina hakika kama tungekuwa na mtu kama Sokoine leo hii tungekuwa mbali sana na kuna baadhi ya watu wasingeingia kwenye siasa kwani ingekuwa hailipi.
 
Mimi nilikuwepo enzi zile tukiishi Mbezi Juu, na maduka yanapatikana Kawe Ukwamani tu. Kwa kweli ilikuwa hali mbaya sana.

Lakini katu siwezi kuilaumu Serikali ya kipindi kile, kwani ile ilitokana na hali ya Hewa na uhaba wa Chakula. SErikali ilijitahidi hata kuanzisha Maduka ya Kaya, Mobile Shops (Malori ya NMC yalikuwa yanapita mitaani na kuuza chakula kama Duka)

Pia Serikali ilijitahidi hata kuagiza Unga wa Njano ili kuwanusuru wananchi wake. KWA KWELI SERIKALI ILIJITAHIDI.

Wakati ule Serikali tu ilikuwa inaruhusiwa kuuza Chakula kwa wananchi, tena nakumbuka hali ilikuwa na unafuu kwani hata chakula kilikuwa na RUZUKU ya serikali hivyo kuuzwa kwa bei ya chini sana.

Na tulikuwa hatuna Rasilimali nyingi kama tulivyo sasa huenda ingelikuwa kama sasa tunaposhuhudia rasilimali zikichimbwa basi maisha yangelikuwa mazuri zaidi na hata kuweza Serikali kuwalipa mishahara / posho wananchi wake wote. Na kula chakula bure na Waisraeli enzi hizo kule Jangwani walipokula MANA.

RIP Mwalimu J. K. Nyerere, RIP E. M. Sokoine, RIP......


MIZAMBWA
NABII MTARAJIWA!!!

Read my lips. Government is a crappy capitalist, and the shortage of goods was a man made disaster.
 
..nizikumbuka enzi za maduka ya kaya.

..Mwalimu alikuwa anadanganywa na jamaa wengine wawili.
 
Back
Top Bottom