Ulikuwepo enzi za DUKA LA KAYA??

Duh umenikumbusha mbali nakumbuka enzi hizo nilikuwa mdogo natumwa kukaa nje kusubiri gari la sukari likisimama niwastue ndani gari ina mlango nyuma ina mifuko ya kilo moja moja ya kaki na huruhusiwi kununia zaidi ya mfuko mmoja.
 
Ndugu umenikumbusha mbali sana, Enzi za kuvaa mtumba toka Burundi unaonekana mhujumu wa uchumi,kuogea Sabuni ya Magwanji na kuvaa Batiki.
Mwl,alijaribu kwa kiasi chake aka prove filure ktk sera za ujamaa na sasa utandawazi.
Enzi za kusikiliza praye(santuri) na mwenye cassete memory Q tajiri?.
Ahsante kaka,

National Radio Cassette Memory Q, Viatu ilikuwa ni Bora peke yake tena kwa mgao. Jamaa wa RTC walikuwa kama Miungu watu miaka hiyo. Mitumba ilikuwa ikiiitwa kafa ulaya.
 
Ninakumbuka ila nilikuwa bado mdogo, enzi hizo kuna ndugu yetu alitokea malawi alituletea Sabuni na sukari, mzee alikuwa anashauri tuvifiche maana ile product tungeulizwa imetoka wapi in case ikionekana. Lakini binafsi ninamkubali sana Nyerere amekaa madarakani kwa miaka 23 lakini Mwinyi miaka10+, Mkapa10, na sasa Kikwete miaka5 halali na Mmoja wa usio halali. Lakini mpaka sasa ukiangalia vitu tangible vilivyofanyika enzi za Nyerere ni vingi kuliko vilivyofanyika ndani ya Tawala hizi tatu.

Hakuna kitu tangible alichofanya Nyerere zaidi ya kumaliza akiba ya Taifa lenu kwa kujijengea hishma ya kisiasa kuwa yupo mstari wa mbele katika ukombozi wa Afrika na kuuwa uchumi wenu kabisa.

Nchi alipewa ikiwa na akiba kubwa ya fedha, haikuwa na njaa hata kidogo, uchumi wake ulikuwa mzuri, hakukuwa na ulanguzi wala mwendo wa kuruka na kila kitu kilipatikana madukani. Yeye ndie muasisi wa Rushwa na Ulanguzi huko Tgk.

 
Kweli watu wametoka mbali. Nakumbuka kaka yangu alivunjika mkono wakti akigombea katika foleni kutaka kununua sababu ya mbuni pale mtaa wa Aggrey kariakoo.

Nakumbuka ilikuwa mkiwa mnakwenda kuswali alfajr tunaweka mawe katika duka la kaya pale Aggrey na ukitoka msikitini tunapangiana zamu kulinda jiwe letu maana mkiondoka tu watu wanalitupa. Na gari la Ugawaji linakuja saa sabaa au nane alasiri.

Kila mtu alikuwa lazima amjue Mkurugenzi mkuu wa NMC mzee Mollel au Mkurugenzi wake wa utawala Mz Uwesu msumi kwa ajili ya kupata kibali cha kununua vitu kwa wingi.

Kweli kila watu na zama zao.
 
Ukibahatika ukawa na ndugu yako akaenda Ulaya lazima umuagize viatu aina ya raba wakati huo tukuviita RABA MTONI. Kama huyo nduguyo alikuwa anakaa sana Ulaya basi akikutumia RABA MTONI lazima kwanza atume kiatu cha mguu mmoja, ukishakipata ndio anatuma tena kiatu cha mguu wa pili. Akifanya makosa akatuma viatu vya miguu yote miwili kwa pamoja, LAZIMA VIIBIWE POSTA. Pia jamaa yako akienda Kenya lazima umtume akuletea dawa ya meno ya COLGATE na sabuni ya IMPERIAL. Siku ukiogea sabuni ya imperial unajipaka pia mwilini kama mafuta ili kila utakapokwenda watu wajue kwamba umeogea sabuni ya IMPERIAL. Ndiyo maana tangia wakati huo mindset yangu ni kwamba the best tooth paste and washing soap is Colgate and imperial respectively!

Wee acha tu ndugu yangu enzi hizo!!! Ukimsimulia kijana wa dot com hawezi kuelewa mambo yalikuwaje.
 
Kuna watu wanatolea mfano wa kushindwa kwa sera za Mwalimu Nyerere kwa kuhusianisha na DUKA LA KAYA. Enzi hizo wengine tulikuwa tunakimbizana na magari ya "Ugawaji" kwenye kila duka wanalosimama, wakati mwingine tukiyakimbiza magari hayo umbali wa hadi kilomita tano au sita.

Ilikuwa ni kawaida kupita kwenye maduka na kukuta msururu mreefu wa mawe yaliyopangwa kama alama ili wenye mawe hayo wakija wapate nafasi ya mbele kwenye foleni. Nakumbuka kulazimishwa kununua unga wa muhogo wenye mchanga ili tuweze kupata sukari kilo mbili na nusu kwa mujibu wa Kadi yetu ya Duka la kaya iliyokuwa inayonyesha kwamba nyumba yetu ina wanakaya 5.

Enzi hizo mgambo waliokuwa wanalinda kwenye maduka ya Kaya (Consumer's Cooperative shop) walikuwa wanaabudiwa sana mitaani kwani wao kila ukija mgao na wao hawakosi kupewa, tofauti na watu wa kawaida ambao wao ni mpaka "zamu" yao ifike. Wauzaji wa maduka haya walikuwa hawajui kabisa kubembeleza wateja kwani wateja walikuwa hawana uchaguzi kutokana na kutakiwa kununua mahitaji yao kwenye maduka walikoandikishiwa kama Wateja.

Wewe ulikuwepo enzi za DUKA LA KAYA? Na ile hali ilikuwa ni halisi au ilisababishwa na uzembe wa Mwalimu kushindwa kuona kwamba kulikuwa na hatari ya njaa inatunyemelea?
Na mwisho akakimbia kwa staili ya kung'atuka.
 
National Radio Cassette Memory Q, Viatu ilikuwa ni Bora peke yake tena kwa mgao. Jamaa wa RTC walikuwa kama Miungu watu miaka hiyo. Mitumba ilikuwa ikiiitwa kafa ulaya.
Duh unanikumbusha raba za pua ya ng'ombe. Mgambo wakikukuta na raba za mtumba wanakuvua.
 
Mimi nakumbuka mgao wa bia, ambapo bia zilikuwa zinapatikana mwisho wa mwezi. Kila mtu alipangiwa kunywa bia 3 tu. wakati unakunywa bia USALAMA WA TAIFA wanaokata vizibo vya bia ulizokunywa. Ukimaliza magao wako wa bia 3 unakwenda nyumbani kulala. Ukijifanya mjanja ukahamia baa nyingine kuongeza, ukifika baa mhudumu anakunusa mdomo akikuta unanuka bia unakufukuzwa kwasababu atajua kwamba ulikotoka tayari utakuwa umeshakunywa mgao wako wa bia 3. Pia ninakumbuka MARUFUKU ya kutembeza gari la binafsi siku ya JUMAPILI baaada ya saa 7 mchana. Siku ya Jumapili mwisho wa kuendesha gari la binafsi ilikuwa saa 7 mchana, baada ya mda huo gari la binafsi likionekana barabarani linakamatwa na traffic na kupigwa heavy penalty. Mambo niliyoyaona kipindi hicho yalinifanya NIUCHUKUE UJAMAA HADI LEO, mimi huniambii kitu kuhusu SIASA YA UJAMAA!

Duh! Mkuu unajua kutia chumvi kama mahindi ya kuchoma ya kileo? Pombe watu walikua wanapiga ila wanawahi kama sanduku mbili mnanunua mnaweka chini ya meza mkiogopa zisiishe. Na pia magari ya Serikali yalikua siku za Jumapili kutembea mwisho saa 8 na hii ilifanywa ili watu wasitumie magari ya serikali kwa starehe zao na ilikua gari la Serikali halitakiwi kuonekana limepaki Bar ukionekana unakamatwa na Polisi ilikua ni suala la maadili sio kama sasa .
 
Kuna watu wanatolea mfano wa kushindwa kwa sera za Mwalimu Nyerere kwa kuhusianisha na DUKA LA KAYA. Enzi hizo wengine tulikuwa tunakimbizana na magari ya "Ugawaji" kwenye kila duka wanalosimama, wakati mwingine tukiyakimbiza magari hayo umbali wa hadi kilomita tano au sita.

Ilikuwa ni kawaida kupita kwenye maduka na kukuta msururu mreefu wa mawe yaliyopangwa kama alama ili wenye mawe hayo wakija wapate nafasi ya mbele kwenye foleni. Nakumbuka kulazimishwa kununua unga wa muhogo wenye mchanga ili tuweze kupata sukari kilo mbili na nusu kwa mujibu wa Kadi yetu ya Duka la kaya iliyokuwa inayonyesha kwamba nyumba yetu ina wanakaya 5.

Enzi hizo mgambo waliokuwa wanalinda kwenye maduka ya Kaya (Consumer's Cooperative shop) walikuwa wanaabudiwa sana mitaani kwani wao kila ukija mgao na wao hawakosi kupewa, tofauti na watu wa kawaida ambao wao ni mpaka "zamu" yao ifike. Wauzaji wa maduka haya walikuwa hawajui kabisa kubembeleza wateja kwani wateja walikuwa hawana uchaguzi kutokana na kutakiwa kununua mahitaji yao kwenye maduka walikoandikishiwa kama Wateja.

Wewe ulikuwepo enzi za DUKA LA KAYA? Na ile hali ilikuwa ni halisi au ilisababishwa na uzembe wa Mwalimu kushindwa kuona kwamba kulikuwa na hatari ya njaa inatunyemelea?

Ndio ujamaa huo
 
[FONT=comic sans

Kila mtu alikuwa lazima amjue Mkurugenzi mkuu wa NMC mzee Mollel au Mkurugenzi wake wa utawala Mz Uwesu msumi

FONT]
Hspo ni Dar. Kwa wakazi WA Dodoma tunamkumbuka Shekifu. Na huo ndo ulikuwa mwanzo wake kung'ara hadi alipo sasa.
 
Yaani nimecheka sana! Enzi hizo wajumbe wa nyumba kumi walikuwa wa maana sana maana wao ndiyo walikuwa wanapanga ration!!!! Ukikuta foleni unasimama tu bila kuuliza na unauliza wa mbele yako anakuambai hata yeye hajui ameikuta akasimama tu!! Duh!! Mungu apishilie mablai hali hiyo!!!
Kuna watu wanatolea mfano wa kushindwa kwa sera za Mwalimu Nyerere kwa kuhusianisha na DUKA LA KAYA. Enzi hizo wengine tulikuwa tunakimbizana na magari ya "Ugawaji" kwenye kila duka wanalosimama, wakati mwingine tukiyakimbiza magari hayo umbali wa hadi kilomita tano au sita.

Ilikuwa ni kawaida kupita kwenye maduka na kukuta msururu mreefu wa mawe yaliyopangwa kama alama ili wenye mawe hayo wakija wapate nafasi ya mbele kwenye foleni. Nakumbuka kulazimishwa kununua unga wa muhogo wenye mchanga ili tuweze kupata sukari kilo mbili na nusu kwa mujibu wa Kadi yetu ya Duka la kaya iliyokuwa inayonyesha kwamba nyumba yetu ina wanakaya 5.

Enzi hizo mgambo waliokuwa wanalinda kwenye maduka ya Kaya (Consumer's Cooperative shop) walikuwa wanaabudiwa sana mitaani kwani wao kila ukija mgao na wao hawakosi kupewa, tofauti na watu wa kawaida ambao wao ni mpaka "zamu" yao ifike. Wauzaji wa maduka haya walikuwa hawajui kabisa kubembeleza wateja kwani wateja walikuwa hawana uchaguzi kutokana na kutakiwa kununua mahitaji yao kwenye maduka walikoandikishiwa kama Wateja.

Wewe ulikuwepo enzi za DUKA LA KAYA? Na ile hali ilikuwa ni halisi au ilisababishwa na uzembe wa Mwalimu kushindwa kuona kwamba kulikuwa na hatari ya njaa inatunyemelea?
 
Duh! Enzi hizo ilikuwa unaponunua sukari lazima ununue majani ya chai na unga wa UKURA au wa Yanga.
 
Ninakumbuka ila nilikuwa bado mdogo, enzi hizo kuna ndugu yetu alitokea malawi alituletea Sabuni na sukari, mzee alikuwa anashauri tuvifiche maana ile product tungeulizwa imetoka wapi in case ikionekana. Lakini binafsi ninamkubali sana Nyerere amekaa madarakani kwa miaka 23 lakini Mwinyi miaka10+, Mkapa10, na sasa Kikwete miaka5 halali na Mmoja wa usio halali. Lakini mpaka sasa ukiangalia vitu tangible vilivyofanyika enzi za Nyerere ni vingi kuliko vilivyofanyika ndani ya Tawala hizi tatu.

Weka mfano wa hivyo vitu kuandika tu vitu "tangible" ni so vague.

Nilikuwepo wakati huo, kabla ya huo na Alhamdulillah nipo sasa. Tusiandikie mate na wino upo.
 
Kikwete na familia yake wameteseka vipi? Wanatajirika kwa kuuza madini na ardhi yetu kwa wazungu. Kawaulize.

Kikwete na mkapa nani kauza madini? Na nyerere na mwadui hebu tueleze ilikuaje?. Wee ni mtu mzima hebu weka ukatoliki wako kando useme ukweli
 
Kikwete na mkapa nani kauza madini? Na nyerere na mwadui hebu tueleze ilikuaje?. Wee ni mtu mzima hebu weka ukatoliki wako kando useme ukweli

Soma hotuba aliyoitoa Kikwete Afrika Kusini 2007 kuhusu vile alivyokata mbuga kuwatafuta akina Sinclair ndio uulize swali lako. Mwadui ilikuwepo enzi za ukoloni na usitake kuniambia kuwa Nyerere ndiye aliyeleta ukoloni.
Mimi si Mkatoliki. Ni Methodist.
 
Soma hotuba aliyoitoa Kikwete Afrika Kusini 2007 kuhusu vile alivyokata mbuga kuwatafuta akina Sinclair ndio uulize swali lako. Mwadui ilikuwepo enzi za ukoloni na usitake kuniambia kuwa Nyerere ndiye aliyeleta ukoloni.
Mimi si Mkatoliki. Ni Methodist.

Mwadui ilikuwepo Toka enzi za ukoloni kwa hiyo nyerere asingeweza kufanya kitu.asingeweza kufanya kitu?..hustuki?..we unashtushwa na hotuba ya 2007?...Hii suppott yenu hata kwenye upuuzi uliofanywa na nyerere na mkapa ndio unaotufanya tuamini kuwa chuki dhidi ya kikwete inaanzia kanisani
 
Wewe unadhani mimi namlaumu Mwalimu? Mimi kati ya watu ambao ni watetezi wakubwa wa Mwalimu lakini sikuleta hii mada ili kumhukumu Mwalimu.

Mimi nilishiriki kuiishi hali hii, nilikula unga wa YANGA, nikabugia BURGA, nikaogea MAJANI YA MPAPAI,nimekunywa chai kwa kuchemsha sukari kwa ukosefu wa majani ya chai, nimeogea sabuni ya MAGADI. Huu ni uzowefu wangu wala sina uchungu na sera za Mwalimu!!
Khaaa wewe nakukubali,yote hayo na bado unamkubali mwalimu!!?,we mwenzangu japo mi sikula hiyo Yanga wala Burga
 
Mshukuruni Mwinyi na team yake.

Duka la kaya huchezi mbali na mjumbe.

Kidaftari lazima kitiwe tick sehemu husika.

Bada utalijua tu hata kama kwenu hamli.

Na ugali wa Yanga juu.
 
Back
Top Bottom