Tunahitaji chama kipya?

Najiuliza kama kuna watu wameanza kuwa kama mimi; vyama vyote vya kisiasa vilivyopo nchini haviwezi kutupatia kile tunachohitaji kama taifa.

Siyo CCM, CHADEMA, CUF au TLP ambacho kilivyo sasa kinaweza kuwa tumaini la Watanzania.

Je, kuanzisha chama kingine ambacho kitatoka kwa wananchi na chenye ajenda ya mabadiliko ya kweli na kikiongozwa na watu wenye mwelekeo wa mabadiliko na wasioogopa political confrontation na ambacho hakitasita kufanya what is necessary to restore law and order and a constitutional rule kitaweza kuwa na nafasi.

Chama ambacho mrengo wake itakuwa ni kuhakikisha kuwa hakuna kurembuliana macho na mafisadi tena wala kuufafanua ufisadi bali kuushughulikia moja kwa moja.

Chama ambacho kitalenga kuleta mabadiliko ya kimfumo na kimuundo wa serikali yetu ndani ya miaka mitano ya kuingia madarakani kikibeba ajenda ya mabadiliko ya kweli (kikatiba, kisiasa, na kiutendaji) huku kikiwashughulikia kama simba mkali wale wote ambao wamelifikisha taifa letu hapa ikiwemo kutaifisha mali zao, kuwasweka jela na wale ambao ni vigogo wa ufisadi "kunyongwa" kama wanavyofanya huko China!

Chama ambacho hakitawabembeleza wawekezaji kama wakwe zetu!

Au ndiyo tubanane mumu kwa mumu huku tukiulizana "kajamba nani'!

Mpaka wewe unatumika Na Zitto? mwambie aanzishe hicho chama chake kipya.
 
Hakuna vyama vizuri kama ccm na cdm ila tatizo ni tabia za wanachama walio kwenye vyama hivi,hawajui katiba za vyama wala sera za vyama hivi ila wanafanya kazi kwa upepo.mfano ccm wanajiua wenyewe maana watendaji wao ndio wanafanya kazi kwa mazoea badala ya utekelezaji wa sera zao.
 
Hatuitaji chama kipya bali tunaitaji kuitoa CCM na kuingiza chama chochote madarakani. Hata ASP Na TANU ambavyo ndio CCM sasa vilikuwa vichovu wakati vinachukuwa madaraka. Chama chochote hatakama kidogo kitafanya vizuri kuliko CCM kwasababu kitaangaliwa na raia na CCM iliyo nnje ya madaraka kuliko CCM iliyokwenye madaraka ambayo haina wa kuirekebisha ilipofika sasa. Kwaujumla tulitakiwa kumchagua mrema na NCCR maana kinachotakiwa ni kuitoa CCM madarakani japo hata kwa mwaka mmoja ili wajisafishe.
 
Najiuliza kama kuna watu wameanza kuwa kama mimi; vyama vyote vya kisiasa vilivyopo nchini haviwezi kutupatia kile tunachohitaji kama taifa.

Siyo CCM, CHADEMA, CUF au TLP ambacho kilivyo sasa kinaweza kuwa tumaini la Watanzania.

Je, kuanzisha chama kingine ambacho kitatoka kwa wananchi na chenye ajenda ya mabadiliko ya kweli na kikiongozwa na watu wenye mwelekeo wa mabadiliko na wasioogopa political confrontation na ambacho hakitasita kufanya what is necessary to restore law and order and a constitutional rule kitaweza kuwa na nafasi.

Chama ambacho mrengo wake itakuwa ni kuhakikisha kuwa hakuna kurembuliana macho na mafisadi tena wala kuufafanua ufisadi bali kuushughulikia moja kwa moja.

Chama ambacho kitalenga kuleta mabadiliko ya kimfumo na kimuundo wa serikali yetu ndani ya miaka mitano ya kuingia madarakani kikibeba ajenda ya mabadiliko ya kweli (kikatiba, kisiasa, na kiutendaji) huku kikiwashughulikia kama simba mkali wale wote ambao wamelifikisha taifa letu hapa ikiwemo kutaifisha mali zao, kuwasweka jela na wale ambao ni vigogo wa ufisadi "kunyongwa" kama wanavyofanya huko China!

Chama ambacho hakitawabembeleza wawekezaji kama wakwe zetu!

Au ndiyo tubanane mumu kwa mumu huku tukiulizana "kajamba nani'!


MM, naomba urdi TZ uje tufanye hayo utamaniyo may be utakuwa chachu ya kuwa na chama chenye siasa zenye utofauti, siasa za kujadili issues na solutions na sio sisa za kuishi kwenye matamko na matukio, siasa za kutafutana ili tumalizane na ili tuonekane sisi wa maana ...njoo home kaka njooo, usiwe kama tshangari wa zimbabwe alipopiga kelele akiwa nje hakueleweka kabisa mpaka aliporudi kwao ndo wakamuelewa
 
Siku zote wazo hutoka kwa mtu mmoja na kufanyiwa marekebisho na wengi! Wengi hawawezi kutoa wazo moja kwa wakati mmoja!

Kitila Mkumbo katoa wazo, kwamba tunahitaji mbadala wa CCM na CHADEMA, katoa na hoja alizodhani zinatetea wazo lake, wengi tulimuunga mkono na wengi hawakumuunga mkono, wale tuliomuunga mkono naamini tulikubaliana naye na wale ambao hawakumuunga mkono hawakukubaliana naye!

Naamini, sasa ni wakati wa wale tuliokubalina naye kujitoa kwa ajili ya kuboresha wazo lake ili hata wale wanaomuona kwa mtazamo hasi basi waweze kuungana na sisi tuliokubaliana naye katika kuifikia Tanzania tuitakayo!

>Tunapokubali kuwa sasa tunahitaji mbadala wa CCM na CHADEMA hatumaanishi kuwa tunahitaji chama chenye jina tofauti na CCM au CHADEMA! Bali tunamaanisha tunauhitaji wa chama cha siasa chenye kuwaza, kunena na kutenda tofauti na CCM na CHADEMA.

Sasa swali la msingi linakuja, je tutakipataje chama kitakachowaza, kunena na kutenda tofauti na CCM au CHADEMA?!

Binafsi nimepata majibu haya:-

1) Tunahitaji chama ambacho mtu binafsi au kikundi cha watu fulani hawatajiona kuwa wao wanachembechembe za umiliki wa hicho chama! Mfano, tunaamua kulifanyia kazi hili wazo na kufanikiwa kutengeneza chama mbadala, baada ya muda hatutapenda kumuona Dr. Kitila Mkumbo akijipa umiliki kisa tu eti yeye ndiye aliyetoa wazo! au kuona kikundi cha watu wakijipa umiliki kisa tu eti wao ndiyo waasisi wa chama! Tunahitaji kuunda chama ambacho kitakuwa mali halisi ya wanachama kidhahania na kialisia!

2) Tunahitaji chama kinakachoundwa kutokana na mawazo ya wanachama/watanzania. Vyama vingi vya kiafrika uundwa kuwa kuiga aidha kutoka vyama vikongwe (kama vilivyo vyama vyetu hapa Tanzania karibia vyote vimeundwa kwa kufuata muundo wa CCM) Au kutoka vyama vya mataifa yaliyoendelea. Chama hiki mbadala kinatakiwa kiundwe kutokana na mawazo ya wananchi, utafiti ufanyike, wananchi waulizwe na wajibu yao yafanyiwe kazi!

3) Misingi na Sera za chama mbadala, Vyama vingi vya kiafrika ni vizuri katika kuhubiri mapungufu ya chama pinzani kama chama na si kuhubiri madhaifu ya ya sera na misingi ya chama pinzani, lakini pia vyama hivi vya kiafrika ni vizuri katika kuhubiri shida za waafrika kuliko kuhubiri ni namna gani misingi na sera zao zitawanufaisha na kuwasaidia waafrika, Mfano, ".... CCM ni chama cha kifisadi kimeuza nchi yote ndio maana pamoja na utajiri wetu wote sisi bado ni maskini....... mkikichagua chama chetu tunapitia mikataba yote ya madini ili rasilimali zetu zitunufaishe sisi wenyewe....." kwa hotuba hii naamini wafuasi wako tu na wale walioichoka CCM ambao wako tayari kuiona CCM ikitoka madarakani bila kujali nani anaingia badala ya CCM ndio watakaokuunga mkono, lakini kwa jamii ya waelewa wataona kwa hali hii ni bora CCM iendelee kubaki madarakani tu! na kwa aina hii ya hotuba ndio maana hakuna mwananchi wa kawaida asiyejisumbua na kusoma anayejua misingi na sera za vyama vyetu! Tunahitaji chama mbadala kiwe na misingi na sera kwanza, zenye maneno machache na pili zenye kueleweka na tatu rahisi kuhubirika, Tutamani kiongozi wa chama mbadala atakaposimama jukwaani kuhutubia aseme "........Pamoja na utajiri tulionao, tunaendelea kuwa maskini kwa sababu ya sera na misingi inayosimamiwa na CCM, Msingi wa CCM unaegemea kwenye .......... na ndiyo maana sera zao za uchumi zinawafanya wafanye 1,2,3 mfano sera yao ya uchumi inasema ..........., hii sera ina madhaifu 1,2,3 na ndio maana hali hii iko hivi lakini mkitupa ridhaa sisi (chama mbadala) ambao msingi wetu umeegemea kwenye ........... hii inatufanya tuwe na sera 1,2,3 kutokana na hizi sera zetu ni lazima tukiingia madarakani tutafanya 1,2,3 na tukifanya haya wewe kama mtanzania wa kawaida utanufaika kwa ..........!

Kwa kifupi chama mbadala kiwe chama kitakachofanya mapinduzi katika siasa za kitanzania/kiafrika, kiwe chama cha kuwafanya watanzania kuchagua chama kutokana na uhitaji wa muda husika na si kuchagua chama ilimradi, kwamba kama uchumi umelegea legea basi watanzania tuchague chama chenye sera nzuri zaidi za uchumi, kama huduma za jamii zimelegea legea basi tubadilishe chama na kuchagua chenye sera nzuri zaidi za huduma za jamii au kama tutaona sasa ni wakati wa kuimalisha ulinzi na usalama basi chama chenye sera nzuri zaidi za ulinzi na usalama kipewe dola.
 
jaribu kulinganisha mambo aliyofanya Dr Slaa na Dr Mkumbo katika taifa hili. Utakuja kuona Dr mkumbo si kitu si lolote. Ifike kipindi tukubali chini ya uongozi wa Dr Slaa na Mbowe Watanzania wameamka na wamepata hamasa na wanazidi kupata hamasa na kujua haki zao kwa elimu waliyopata toka kwa viongozi hawa thus why matukio ya watu kutolewa kucha na meno pamoja na kuuliwa yanafanywa na CCM kwa sababu ya harakati za viongozi hawa.
 
Hivi watanzania wenzangu ni nani hasa aliewaloga? Maana kila anayekuja na mawazo tofauti na ccm ni mpinzani na hasa cdm. Ukija na wazo mbadala wa chadema wewe umetumwa.

Wekeni mawazo yenu huru. Hao wanaowalipa vijisenti kidogo kuandika hapa mambo ya kishabiki yasiyo na mshiko mnajua wamechukua shs ngapi kwenye chama?

Jalini utaifa. Kuiondoa ccm madarakani bila kua na chama kilicho tayari ni majanga matupu.

Tujaribu kua na mawazo huru kama chama chako kina mapungufu basi huko ndani ya chama yarekebishe. Nasi watanzania tusio na vyama tutakuunga mkono.

Ni hayo tu wakuu wajuvi wa mambo ya vyama
 
Hivi watanzania wenzangu ni nani hasa aliewaloga? Maana kila anayekuja na mawazo tofauti na ccm ni mpinzani na hasa cdm. Ukija na wazo mbadala wa chadema wewe umetumwa.

Wekeni mawazo yenu huru. Hao wanaowalipa vijisenti kidogo kuandika hapa mambo ya kishabiki yasiyo na mshiko mnajua wamechukua shs ngapi kwenye chama?

Jalini utaifa. Kuiondoa ccm madarakani bila kua na chama kilicho tayari ni majanga matupu.

Tujaribu kua na mawazo huru kama chama chako kina mapungufu basi huko ndani ya chama yarekebishe. Nasi watanzania tusio na vyama tutakuunga mkono.

Ni hayo tu wakuu wajuvi wa mambo ya vyama
Ndugu yangu wewe una mawazo sahihi na unavyowashangaa watanzania nami pia huwa ninajiuliza hivyo, sasa huwa ninashindwa kuelewa hawa watu wanaelewa wanakwenda na wanatenda nini, wanajua wanachokipenda? lakini jibu rahisi hapa nikuwa wengi wao wanaongozwa na chuki na ushabiki tu na kuwaacha wenyewe wanafaidi katika vyama vyao.
 
Kazi kweli, mbona hakuna tofaut ya ccm na cdm. Mifumo yao kiuongozi ni ile ile tu... Ni kubebana kwa kwenda mbele. Ebu angalia cdm et mpaka leo Mtei ana sauti katika chama kisa muasisi ni ujinga huu....
 
utofauti upo ccccm ni wezi wa fedha za umma, wauwaji, wabakaji,wanawauza watanzania kwa wadhungu, ila chadema wanatetea na kuyapigania maisha ya watanzania kwa kuwajenga kifikra na kimtazano juu ya nchi yao tajili inayodhulumiwa na wachache

nawasilisha
 
Kila nikisoma maoni hapa JF na kwingineko, inazidi kunipa nguvu zaidi kuendelea na hoja yangu. Inatia moyo kwamba angalau baadhi ya watu wameanza kujadili hoja na kuachana na mambo ya mipasho, kejeli na wakati mwingine matusi.

Kejeli, mipasho na Matusi sio jambo baya sana kwa sababu linamsaidia mtu kutoa hasira zake, lakini mwisho wa siku inabidi turudi kwenye hoja na hoja ijibiwe kwa hoja. Sio lazima tukubaliane, na ni mbaya sana kukubaliana kila kitu, lakini lazima tujifunze kama taifa kujadiliana kihoja na kujenga utamaduni wa kukubaliana kutokukubaliana. Hakuna namna tutakayoweza kulazimisha kila mtu afikiri kama sisi, hilo halipo, madamu tunaendelea kuwa binadamu.

Mfumo wa vyama vingi unataka vyama vishindane katika kutoa mawazo mbadala. Bahati mbaya hapa kwetu vyama vinashindana katika kutoa kejeli na mipasho. Ndio maana wananchi wanalazimika kuwa washabiki wa viongozi, badala kuwa washabiki wa mawazo, kwa sababu mawazo hayapo. Tunahitaji mbadala wa chama ambacho kitajipambanua kimawazo ili watu wakiunge mkono au wakipinge kwa sababu ya mawazo hayo.

Wiki ijayo nitaendelea na hii mada, nikieleza aina ya chama tunachokihitaji na mbadala ninaongelea ni katika mambo yapi.
 
jaribu kulinganisha mambo aliyofanya Dr Slaa na Dr Mkumbo katika taifa hili. Utakuja kuona Dr mkumbo si kitu si lolote. Ifike kipindi tukubali chini ya uongozi wa Dr Slaa na Mbowe Watanzania wameamka na wamepata hamasa na wanazidi kupata hamasa na kujua haki zao kwa elimu waliyopata toka kwa viongozi hawa thus why matukio ya watu kutolewa kucha na meno pamoja na kuuliwa yanafanywa na CCM kwa sababu ya harakati za viongozi hawa

Hapa nilikuwa siangalii nani ni nani na nani kafanya nini! hapa nilikuwa naangalia wazo lililotolewa na kiliboresha hata wewe ukitoa wazo nitaangalia wazo lako na si kukulinganisha na kina fulan!
 
utofauti upo ccccm ni wezi wa fedha za umma, wauwaji, wabakaji,wanawauza watanzania kwa wadhungu, ila chadema wanatetea na kuyapigania maisha ya watanzania kwa kuwajenga kifikra na kimtazano juu ya nchi yao tajili inayodhulumiwa na wachache

nawasilisha

chadema wanatetea na kuyapigania maisha ya watanzania kwa kuwajenga kifikra na kimtazano juu ya nchi yao tajiri inayodhulumiwa na wachache kwa kutumia sera na misingi ipi na CCM ni wezi wa fedha za umma, wauwaji, wabakaji,wanawauza watanzania kwa wadhungu kwa kutumia sera au misingi ipi?!
 
Mnahangaika tu bure wenafiki wanajulikana na wazalendo wanajulikana. Muongeze vyam msiongeze taifa litakombolewa na wazalendo tu. Niishie hapo Mungu alishatubariki ila wanafiki wanaharibu baraka hiyo
 
Mtu yeyote anayeweza kuilinganidha CCM iliyokaa madarakani miaka 52 sasa na vyama vingine vya upinzani( Chadema ikiwamo), kama sio MWENDAWAZIMU basi atakuwa ni KICHAA au bac atakuwa MwanaCCM anayetafuta huruma kutoka kwa watanzania kwa chama chake kwa kuchafua vyama vingine!

Mwanakijiji ni wazi ana wivu na hatua waliyopiga Chadema,kwa hiyo ameona ni bora "Tukose wote!"
 
Najiuliza kama kuna watu wameanza kuwa kama mimi; vyama vyote vya kisiasa vilivyopo nchini haviwezi kutupatia kile tunachohitaji kama taifa.

Siyo CCM, CHADEMA, CUF au TLP ambacho kilivyo sasa kinaweza kuwa tumaini la Watanzania.

Je, kuanzisha chama kingine ambacho kitatoka kwa wananchi na chenye ajenda ya mabadiliko ya kweli na kikiongozwa na watu wenye mwelekeo wa mabadiliko na wasioogopa political confrontation na ambacho hakitasita kufanya what is necessary to restore law and order and a constitutional rule kitaweza kuwa na nafasi.

Chama ambacho mrengo wake itakuwa ni kuhakikisha kuwa hakuna kurembuliana macho na mafisadi tena wala kuufafanua ufisadi bali kuushughulikia moja kwa moja.

Chama ambacho kitalenga kuleta mabadiliko ya kimfumo na kimuundo wa serikali yetu ndani ya miaka mitano ya kuingia madarakani kikibeba ajenda ya mabadiliko ya kweli (kikatiba, kisiasa, na kiutendaji) huku kikiwashughulikia kama simba mkali wale wote ambao wamelifikisha taifa letu hapa ikiwemo kutaifisha mali zao, kuwasweka jela na wale ambao ni vigogo wa ufisadi "kunyongwa" kama wanavyofanya huko China!

Chama ambacho hakitawabembeleza wawekezaji kama wakwe zetu!

Au ndiyo tubanane mumu kwa mumu huku tukiulizana "kajamba nani'!

Mtu yeyote anayeweza kuilinganidha CCM iliyokaa madarakani miaka 52 sasa na vyama vingine vya upinzani( Chadema ikiwamo), kama sio MWENDAWAZIMU basi atakuwa ni KICHAA au bac atakuwa MwanaCCM anayetafuta huruma kutoka kwa watanzania kwa chama chake kwa kuchafua vyama vingine!

Mwanakijiji ni wazi ana wivu na hatua waliyopiga Chadema,kwa hiyo ameona ni bora "Tukose wote!"
 
Back
Top Bottom