Missile of the Nation
JF-Expert Member
- May 24, 2018
- 13,505
- 51,108
Pengine tunaweza kujiuliza, kwa nini serikali ya raisi Samia wakati huu imeamua kupotezea na kuruhusu CHADEMA wafanye maandamano wakati inafahamika kuwa siku zote unapoleta ajenda ya maandamano basi serikali ya CCM huwa wanakuwa wagumu na wakali kama pilipili kuyaruhusu. Nitaeleza hapa chini kwa nini safari hii Samia na serikali yake wameamua kuyaacha yafanyike. Sababu zenyewe ni hizi.
1. Sababu ya kwanza ni kuwa, ajenda kuu za maandamano hazina athari kubwa kisiasa kwa Samia na CCM yake.
Kwa mujibu wa taarifa iliyosonwa na katibu mkuu John Mnyika mbele ya waandishi wa habari, Ajenda kuu za maandamano ambazo waliwaandikia Polisi wa Dar ni mbili
a) Miswada ya sheria mbovu za mambo ya uchaguzi
b) Hali ya ugumu wa maisha ya Wananchi.
Katika Ajenda hizo hakuna kabisa suala la KATIBA mpya
Sasa ukiangalia hizo Ajenda, kisiasa hakuna hata moja yenye uzito wa kisiasa wa kuitetemesha CCM. Tena ukichunguza vizuri ajenda ya kwanza inawaportray CHADEMA kama wenye uchu na chaguzi ili wapate nafasi za ubunge udiwani, ruzuku n.k
Tegemea kuanza kuona CCM wakiwageuzia kibao CHADEMA kwenye ajenda yao hiyo ya mambo ya uchaguzi, kwamba CHADEMA ni wasaka madaraka tu lakini hawako serious na mambo makubwa ya mabadiliko ya kweli.
2. Sababu ya Pili ni Kumuonyesha Samia kama mwanademokrasia.
Haya maandamano, yakifanyika, kitakachofuata baada ya hapo ni kumtengenezea taswira rais Samia kama mwanademokrasia, mwanasiasa mkomavu ambaye yuko tayari kuvumilia vyama vingine kutumia haki yao ya kidemokrasia kuandamana n.k. Itamjengea taswira chanya ndani na nje.
3. Sababu ya tatu, ni kupunguza fukuto la Wataka maandamano.
Yamekuwepo majaribio ya watu kutaka kuandamana kwa muda mrefu huku Jeshi la polisi likiyazima kikatili. Safari hii naona wameona wayaache ili kuoffload steam ( fukuto lipumue). Hii itasaidia kupunguza joto, mshawasha wa kutaka kuandamana, kitu ambacho ni dream ya wanadiasa na wanaharakati nchini.
4. Kwa kuruhusu maandamano katika ajenda nyepesi kunaipa serikali mtaji wa kukataa maandamano ya ajenda ngumu bila lawama kiviiile!
Zipo ajenda kuu nchini za mambo ya msingi.
1. Ajenda ya dhulma kwa Wamasai huko ngorongoro
2. Ajenda ya Katiba mpya
3. Ajenda ya Ufisadi, ubadhirifu na kutowajibishwa ipasavyo wanaofanya hayo
4. Ajenda ya Elimu mbovu
5. Ajenda ya kutapanya rasilimali za nchi kwa kuziuza bei chee na kuingua mikataba mibovu
6. Ajenda ya kumnyonya mkulima.
Hizo ni Ajenda ambazo CCM wanaziogopa na siyo mambo ya miswada ya uchaguzi. Kwa hiyo, kwa kuruhusu maandamano ya Ajenda dhaifu, Wanajiwekea kigingi cha kuzuia maandamano ya ajenda nzito zaidi kwa hojs za kiintelijensia.
5. Maandamano haya, yanawasaidia CCM kuwashusha mzuka watu ambao wako serious kuandamana kwa ajili ya katiba mpya.
Katika nchi yetu, jinsi mifumo ya kisiasa ilivyo. Ni vigumu kumobilise watu, au kufanya jambo lenye mguso wa kisiasa bila kupitia platform za kisiasa. Ndiyo maana akina Mwabukusi walipata shida sana kuandaa maadamano yao ya kudai katiba mpya na kupinga ugawaji wa bandari yetu. Hata hivyo fukuto la madai yao lilikuwa kubwa miongoni mwa Watanzania, kwa hiyo kingetokea chama cha siasa kikawa na guts za kuandamana kwa ajenda hizo bila shaka ingeweka pressure kubwa zaidi kwa serikali ya CCM. Sasa hakuna Chama kilichojitokeza kubeba ajenda hizo, bali CHADEMA imekuja na ajenda za kupapasapapasa bila kuifanya KATIBA MPYA kuwa ni AJENDA kuu. Matokeo yake watu watashushwa mzuka, Na hii itaisaidia CCM kubuy time katika danadana zake za kutotupatia katiba mpya!. Mpaka Joto la kuwapush watu kuingua barabarani tena kwa ajili ya katiba mpya lipande, itakuwa labda miaka mingine 10 ijayo!
KWA KUMALIZIA.
1. Maandamano ya Chadema yatamjenga Samia aonekane mwanademokrasia.
2. Maandamano ya CHADEMA yasiyobeba Katiba mpya kama ajenda kuu ni kama Controlled demolition ya kuzima hasira ya watu kimkakati ya kuingia barabarani kwa ajili ya katiba mpya.
3. Maandamano yasiyoogopwa na CCM hayo siyo maandamano halisi.
4. Maandamano haya yanaweza kutumika kuwaportray CHADEMA kama Flip-Floppers wakubwa. Leo wanazungumza habari za sheria za uchaguzi, wakati miaka michache iliyopita walikuwa wanasema kuwa hakuna reform yoyote ya sheria za kawaida inayoweza kusaidia uchaguzi huru na haki. Leo wanaandamana kwa ajili ya reform ya sheria hizohizo!.
Kwa maoni yangu, bila ya KATIBA MPYA kuwa ndiyo Ajenda kuu ya kila kitu, basi madai yetu yote mengine ni bure!
1. Sababu ya kwanza ni kuwa, ajenda kuu za maandamano hazina athari kubwa kisiasa kwa Samia na CCM yake.
Kwa mujibu wa taarifa iliyosonwa na katibu mkuu John Mnyika mbele ya waandishi wa habari, Ajenda kuu za maandamano ambazo waliwaandikia Polisi wa Dar ni mbili
a) Miswada ya sheria mbovu za mambo ya uchaguzi
b) Hali ya ugumu wa maisha ya Wananchi.
Katika Ajenda hizo hakuna kabisa suala la KATIBA mpya
Sasa ukiangalia hizo Ajenda, kisiasa hakuna hata moja yenye uzito wa kisiasa wa kuitetemesha CCM. Tena ukichunguza vizuri ajenda ya kwanza inawaportray CHADEMA kama wenye uchu na chaguzi ili wapate nafasi za ubunge udiwani, ruzuku n.k
Tegemea kuanza kuona CCM wakiwageuzia kibao CHADEMA kwenye ajenda yao hiyo ya mambo ya uchaguzi, kwamba CHADEMA ni wasaka madaraka tu lakini hawako serious na mambo makubwa ya mabadiliko ya kweli.
2. Sababu ya Pili ni Kumuonyesha Samia kama mwanademokrasia.
Haya maandamano, yakifanyika, kitakachofuata baada ya hapo ni kumtengenezea taswira rais Samia kama mwanademokrasia, mwanasiasa mkomavu ambaye yuko tayari kuvumilia vyama vingine kutumia haki yao ya kidemokrasia kuandamana n.k. Itamjengea taswira chanya ndani na nje.
3. Sababu ya tatu, ni kupunguza fukuto la Wataka maandamano.
Yamekuwepo majaribio ya watu kutaka kuandamana kwa muda mrefu huku Jeshi la polisi likiyazima kikatili. Safari hii naona wameona wayaache ili kuoffload steam ( fukuto lipumue). Hii itasaidia kupunguza joto, mshawasha wa kutaka kuandamana, kitu ambacho ni dream ya wanadiasa na wanaharakati nchini.
4. Kwa kuruhusu maandamano katika ajenda nyepesi kunaipa serikali mtaji wa kukataa maandamano ya ajenda ngumu bila lawama kiviiile!
Zipo ajenda kuu nchini za mambo ya msingi.
1. Ajenda ya dhulma kwa Wamasai huko ngorongoro
2. Ajenda ya Katiba mpya
3. Ajenda ya Ufisadi, ubadhirifu na kutowajibishwa ipasavyo wanaofanya hayo
4. Ajenda ya Elimu mbovu
5. Ajenda ya kutapanya rasilimali za nchi kwa kuziuza bei chee na kuingua mikataba mibovu
6. Ajenda ya kumnyonya mkulima.
Hizo ni Ajenda ambazo CCM wanaziogopa na siyo mambo ya miswada ya uchaguzi. Kwa hiyo, kwa kuruhusu maandamano ya Ajenda dhaifu, Wanajiwekea kigingi cha kuzuia maandamano ya ajenda nzito zaidi kwa hojs za kiintelijensia.
5. Maandamano haya, yanawasaidia CCM kuwashusha mzuka watu ambao wako serious kuandamana kwa ajili ya katiba mpya.
Katika nchi yetu, jinsi mifumo ya kisiasa ilivyo. Ni vigumu kumobilise watu, au kufanya jambo lenye mguso wa kisiasa bila kupitia platform za kisiasa. Ndiyo maana akina Mwabukusi walipata shida sana kuandaa maadamano yao ya kudai katiba mpya na kupinga ugawaji wa bandari yetu. Hata hivyo fukuto la madai yao lilikuwa kubwa miongoni mwa Watanzania, kwa hiyo kingetokea chama cha siasa kikawa na guts za kuandamana kwa ajenda hizo bila shaka ingeweka pressure kubwa zaidi kwa serikali ya CCM. Sasa hakuna Chama kilichojitokeza kubeba ajenda hizo, bali CHADEMA imekuja na ajenda za kupapasapapasa bila kuifanya KATIBA MPYA kuwa ni AJENDA kuu. Matokeo yake watu watashushwa mzuka, Na hii itaisaidia CCM kubuy time katika danadana zake za kutotupatia katiba mpya!. Mpaka Joto la kuwapush watu kuingua barabarani tena kwa ajili ya katiba mpya lipande, itakuwa labda miaka mingine 10 ijayo!
KWA KUMALIZIA.
1. Maandamano ya Chadema yatamjenga Samia aonekane mwanademokrasia.
2. Maandamano ya CHADEMA yasiyobeba Katiba mpya kama ajenda kuu ni kama Controlled demolition ya kuzima hasira ya watu kimkakati ya kuingia barabarani kwa ajili ya katiba mpya.
3. Maandamano yasiyoogopwa na CCM hayo siyo maandamano halisi.
4. Maandamano haya yanaweza kutumika kuwaportray CHADEMA kama Flip-Floppers wakubwa. Leo wanazungumza habari za sheria za uchaguzi, wakati miaka michache iliyopita walikuwa wanasema kuwa hakuna reform yoyote ya sheria za kawaida inayoweza kusaidia uchaguzi huru na haki. Leo wanaandamana kwa ajili ya reform ya sheria hizohizo!.
Kwa maoni yangu, bila ya KATIBA MPYA kuwa ndiyo Ajenda kuu ya kila kitu, basi madai yetu yote mengine ni bure!