MWANAKIJI,leo nimepata fursa kidogo.Najiuliza kama kuna watu wameanza kuwa kama mimi; vyama vyote vya kisiasa vilivyopo nchini haviwezi kutupatia kile tunachohitaji kama taifa.
Siyo CCM, CHADEMA, CUF au TLP ambacho kilivyo sasa kinaweza kuwa tumaini la Watanzania.
Je, kuanzisha chama kingine ambacho kitatoka kwa wananchi na chenye ajenda ya mabadiliko ya kweli na kikiongozwa na watu wenye mwelekeo wa mabadiliko na wasioogopa political confrontation na ambacho hakitasita kufanya what is necessary to restore law and order and a constitutional rule kitaweza kuwa na nafasi.
Chama ambacho mrengo wake itakuwa ni kuhakikisha kuwa hakuna kurembuliana macho na mafisadi tena wala kuufafanua ufisadi bali kuushughulikia moja kwa moja.
Chama ambacho kitalenga kuleta mabadiliko ya kimfumo na kimuundo wa serikali yetu ndani ya miaka mitano ya kuingia madarakani kikibeba ajenda ya mabadiliko ya kweli (kikatiba, kisiasa, na kiutendaji) huku kikiwashughulikia kama simba mkali wale wote ambao wamelifikisha taifa letu hapa ikiwemo kutaifisha mali zao, kuwasweka jela na wale ambao ni vigogo wa ufisadi "kunyongwa" kama wanavyofanya huko China!
Chama ambacho hakitawabembeleza wawekezaji kama wakwe zetu!
Au ndiyo tubanane mumu kwa mumu huku tukiulizana "kajamba nani'!
Tuendelee Kusupport hivi hivi vilivyopo.....hakuna haja ya kukata tama. Siku zote ukombozi ni mgumu sana. Najua kwamba kila mtanzania anahamu ya mabadiliko, hali iliyopo CHADEMA ni nzuri kwetu kwani itatusaidia kujua makosa yaliyopo na kuyarekebisha, TUTAVUKA TU HIKI KIHUNZI.Watanzania wakibadilika kifikra basi vyama hivyo hivyo vilivyopo vya upinzani (vikiengezeka vizuri) vitafaa mradi vitakuwa disciplined na watu ambao wamebadilika kifikra.Kama vichwa vya Watanzania wengi vitaendelea kuamini kuwa CCM ndo nambari wani hata kama hakina jipya...basi tunaweza kuwa na vya zaidi ya 300 kama Congo kinshasa...na itakuwa Katibu wa Chama kimoja ni Mwenyekiti wa Chama kingine...
Watanzania wabadilike kifikra na kila kitu kitabadilika...Obama alipokuja na "Change Policy" aliwakuta Wamarekani tayari wameshabadilika kifikra na walikuwa tayari kwa chama au system nyengine ambayo itakwenda sambamba na fikra zao mbadala...hawakuhitaji chama kipya bali kile ambacho kitakua tayari kukubaliana na fikra zao...
Watanzania wabadilike...CCM ya jana si ya leo.
na hayo mapambano ukiyaanzisha ndiyo yanakupata ya liyowapata akina ZZK na wenzakeMzee Mwanakijiji,
Tatizo sio vyama bali ni watu, tatizo ni Watanzania ambao wengi ni wababaishaji, wezi, mafisadi.
Tunayoyasema hapa JF hatuyaamini kabisa.
Kama kuna watu wanataka kuleta mabadiliko, tayari tuna vyama vingi, ingieni kwenye hivyo vyama na anzeni mapambano kuanzia chini.