Kwa heshima na taadhima, ninaandika kama mdau wa elimu nchini. Tangu kufunguliwa kwa dirisha la maombi ya mkopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu, waombaji wanashindwa kuwasilisha maombi yao kwa wakati. Wengi wanaishia hatua ya demographic information tu.
Wanapowasilisha (submit) hakuna mrejesho wowote. Waombaji wanafuata hatua zote kama vile kufungua account OLAMS, kulipia shilingi 30,000/= za kitanzania, kuchagua Local Undergraduate n.k. kuset picha ukubwa wa pasi ya kusafiria 120px kwa 150px isiyozidi ukubwa wa MB1.
Kuweka Verification code inayotolewa na RITA inayoishia na BV kama ilivyo, kuingiza namba ya NIDA bila kuweka alama ya deshi (-). Yote haya waombaji wanazingatia. Ila hakuna wanashindwa kuendelea.
Jambo hili linahitaji uharaka na kushughulikiwa na HESLB mapema iwezekanavyo. Haiwezekani nchi nzima wapate tatizo kama hilo muda wote.
Pengine Computers (SERVER COMPUTERS) zinazopokea na kuchakata taarifa za maombi ya mkopo zina uwezo mdogo ukilinganisha na mahitaji, au kuna hujuma inayofanywa dhidi ya Bodi ya Mikopo, au kuna matatizo ya kimitambo (technical challenges) au kuna uzembe wa kibinadamu pahala.
Wanombaji wengi wanategemea mikopo ili waweze kufikia ndoto zao kitaaluma hasa wanaotoka kwenye familia zenye kipato cha chini, na waombaji wengine ni yatima wa wazazi wote au mmoja.
Hivyo, ninasihi mamlaka husika akiwemo ndugu Abdul- Razaq- Badru (Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB) na timu yake kulifanyia kazi jambo hili. Pengine mfumo huu mpya una changamoto ambazo ziko nje ya uwezo wa kibinadamu.
Ushauri wangu ni kuwa, ili kujiridhisha kama mfumo uko sawa, wangetathmini kwa mwaka jana tarehe kama ya leo 15/08/2022 ni wanafunzi wangapi walikuwa wamekwishakuwasilisha maombi, na tarehe kama ya leo 15/08/2023 ni wanafunzi wangapi wamekwishakuwasilisha maombi. Hii, itawasaidia watendaji wa HESLB kugundua tofauti na kujiridhisha kuwa kuna jambo halipo sawa.
Ninaamini kuwa watendaji wa HESLB ni binadamu na sio malaika, wanaweza kukosea kiutendaji na hata vifaa kama Server Computers zao zimeundwa na biinadamu, zinaweza kuwa na dosari.
Ninaamini Higher Education Students' Loan Board (HESLB) will do all humanly possible means to address this issue of national importance as adequately as possible so much that those who deserve can acquire loans to further their education for a better Tanzania than ever before.
Regards,
Julius E Julius (0712830357)
Wanapowasilisha (submit) hakuna mrejesho wowote. Waombaji wanafuata hatua zote kama vile kufungua account OLAMS, kulipia shilingi 30,000/= za kitanzania, kuchagua Local Undergraduate n.k. kuset picha ukubwa wa pasi ya kusafiria 120px kwa 150px isiyozidi ukubwa wa MB1.
Kuweka Verification code inayotolewa na RITA inayoishia na BV kama ilivyo, kuingiza namba ya NIDA bila kuweka alama ya deshi (-). Yote haya waombaji wanazingatia. Ila hakuna wanashindwa kuendelea.
Jambo hili linahitaji uharaka na kushughulikiwa na HESLB mapema iwezekanavyo. Haiwezekani nchi nzima wapate tatizo kama hilo muda wote.
Pengine Computers (SERVER COMPUTERS) zinazopokea na kuchakata taarifa za maombi ya mkopo zina uwezo mdogo ukilinganisha na mahitaji, au kuna hujuma inayofanywa dhidi ya Bodi ya Mikopo, au kuna matatizo ya kimitambo (technical challenges) au kuna uzembe wa kibinadamu pahala.
Wanombaji wengi wanategemea mikopo ili waweze kufikia ndoto zao kitaaluma hasa wanaotoka kwenye familia zenye kipato cha chini, na waombaji wengine ni yatima wa wazazi wote au mmoja.
Hivyo, ninasihi mamlaka husika akiwemo ndugu Abdul- Razaq- Badru (Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB) na timu yake kulifanyia kazi jambo hili. Pengine mfumo huu mpya una changamoto ambazo ziko nje ya uwezo wa kibinadamu.
Ushauri wangu ni kuwa, ili kujiridhisha kama mfumo uko sawa, wangetathmini kwa mwaka jana tarehe kama ya leo 15/08/2022 ni wanafunzi wangapi walikuwa wamekwishakuwasilisha maombi, na tarehe kama ya leo 15/08/2023 ni wanafunzi wangapi wamekwishakuwasilisha maombi. Hii, itawasaidia watendaji wa HESLB kugundua tofauti na kujiridhisha kuwa kuna jambo halipo sawa.
Ninaamini kuwa watendaji wa HESLB ni binadamu na sio malaika, wanaweza kukosea kiutendaji na hata vifaa kama Server Computers zao zimeundwa na biinadamu, zinaweza kuwa na dosari.
Ninaamini Higher Education Students' Loan Board (HESLB) will do all humanly possible means to address this issue of national importance as adequately as possible so much that those who deserve can acquire loans to further their education for a better Tanzania than ever before.
Regards,
Julius E Julius (0712830357)