Mbn huelezi unapinga kwa point ipi sheria tulizo nazo zinaruhusu kunyima haki vyama vingine au una maanisha serikali niya chama kimoja tu.Mkuu,
Napinga hoja yako ya UMWAGAJI WA DAMU. Una point nzuri Ila ulipoiharibu ni hapo kwenye Hiyo kauli ya kichochezi ya umwagaji Damu. Kwanza Watanzania tumezoea kuishi kwa umoja na kushirikiana katika jamii zinazotuzunguka. WanaSiasa ndio wameleta haya matatizo yote ya chuki za Kidini, Kiukanda, Kikabila, Kiitikadi, Kijinsia n.k.
Naomba nikukumbushe tu kwamba Tanzannia ni Nchi ambayo Ina SHERIA na KANUNI. Watanzania tulio wengi tulizoea kuishi na kufanya shughuli zetu kiujanja ujanja bila kufuata taratibu za nchi.
Umekuja utawala wa awamu ya 5 ambao unarudisha mfumo wa kufuata Sheria na taratibu za nchi, matokeo yake tunaona watu wasio waadilifu na weledi kutwa kukicha wanaiponda na kuikebehi SERIKALI kwa manufaa Yao binafsi na sio kwa manufaa ya TAIFA.
Wewe Kama ni Mtanzania MZALENDO nafikiri utatafakari upya hiyo kauli yako ya UMWAGAJI WA DAMU. Kila la heri.
Serikali wameiponda kwa vipi na wewe unae sifia tu hata cuf kunyimwa haki ni sawa. Wewe kwa taarifa yako HAKI HUINUA TAIFA kwa mawazo yako watu wote ni wanachama wa ccm. Kwa hiyo ni sawa wengine kunyinwa haki zao.
Nini maana ya kuwa na vyama vingine kama haki ni ccm kutawala pekee yake. Watu wakiamua kudai haki za kisiasa kw kuingia barabarani sheria hizo unazozisema zitazuia. Nani mchochezi kati ya wewe na anaye tahadharisha ushabiki mwingine hauna maana hautapona usifikirie eti kwa kuwa mnaoshabikia ccm mtakuwa salama, wote yakiingia machafuko wote tunakuwa matatizoni saidia kuwaambia ccm wanachochea na kukaribisha uvunjifu wa amani.
Kuzuia kitu kama hicho kisitokee sikuzuia kwa kuwanyamazisha watu kwa mabunduki ni kutenda haki kwa vitendo. Kufanyia kwa vitendo usawa unao usema.