Mziwanda,
Kila naposoma maandishi yetu ktk vyombo mbali mbali, Uzalendo umechukuliwa kama kitambulisho cha Uraia (Uhuru wa Bendera) kwani taifa lote bado linatawaliwa kifikra. Mtu akihamia Ulaya na kuchukua Uraia basi huyo sii Mzalendo! Mtu akikipinga chama CCM huyo sii Mzalendo hata kama uongozi ni mbaya. Mikataba mibovu sii matokeo ya wananchi kukosa Uzalendo isipokuwa ni matokeo ya kutokuwa na itikadi ambayo sote tunahitajika kuwa devoted to (Uzalendo)
Na ndio maana Mkandara akipiga kelele hapa kulaani Ufisadi wa Mkapa wapo wengine wataniona mchawi kwa sababu Ufisadi wake kulingana na Katiba (msahafu wa kuiga) sii HARAMU..ingawa consciousness yetu ya Uzalendo inatuambia kabisa kuwa kitendo hicho ni Haramu na mtu kama huyu anahitaji kufia Jela..Tumeshindwa kutenganisha Patrotism na Natinalism ktk matetezi yetu ya Uhuru wa Mtanzania kama vile watu wasiokuwa na dini.
Na hakuna mafundisho yoyote ya Kijamii yanayolaani Ufisadi. Kwa hiyo hata Ukimchagua kiongozi ambaye haamini Ufisadi ni haramu utaweza vipi kumpima Uzalendo wake ili hali wewe mwenyewe huamini kama Ufisadi ni haramu.
Mkuu nitakuuliza wewe UZALENDO ni kitu gani?..devotion to what?..Ni nini haswa context inayojenga neno hili ktk jamii yetu? Unaweza vipi kuomba uzalendo toka kwa wananchi ikiwa hatuna Utamaduni hata huo wa kujenga Nationalism. Hatuna itikadi inayounda sheria na ethics kiasi kwamba kipimo halali cha Uzalendo wa Mtanzania kitatokana na mila na desturi za watu hawa..Nambie mkuu wangu pengine mimi natzama upande usokuwa na tija kabisa lakini ukweli ni kwamba Taifa bila mwongozo ni sawa na Merikebu inayokwenda pasipo dira..Chief mkandara. Kiongozi anatoka ndani ya jamii husika, na uzalendo si lazima uanzie na uongozi, bali kwa mtu mmoja mmoja. Suala la uhuru lina upana wake. Uhuru wa bendera kwa mtazamo wangu ulikuwa na nguvu miaka ya mwanzo ya uhuru. Miaka ya 90 hadi leo mambo mengi ni ya kujitakia. Mikataba mibovu na uwekezaji holela na soko huria ndio vimetufikisha hapa. Uzalendo tangu ngazi ya mwanajamii hadi mtawala ungetumika, hayo mambo hapo juu yangetujenga. Uhuru tulio nao unatosha sana kujiletea maendeleo
Kila naposoma maandishi yetu ktk vyombo mbali mbali, Uzalendo umechukuliwa kama kitambulisho cha Uraia (Uhuru wa Bendera) kwani taifa lote bado linatawaliwa kifikra. Mtu akihamia Ulaya na kuchukua Uraia basi huyo sii Mzalendo! Mtu akikipinga chama CCM huyo sii Mzalendo hata kama uongozi ni mbaya. Mikataba mibovu sii matokeo ya wananchi kukosa Uzalendo isipokuwa ni matokeo ya kutokuwa na itikadi ambayo sote tunahitajika kuwa devoted to (Uzalendo)
Na ndio maana Mkandara akipiga kelele hapa kulaani Ufisadi wa Mkapa wapo wengine wataniona mchawi kwa sababu Ufisadi wake kulingana na Katiba (msahafu wa kuiga) sii HARAMU..ingawa consciousness yetu ya Uzalendo inatuambia kabisa kuwa kitendo hicho ni Haramu na mtu kama huyu anahitaji kufia Jela..Tumeshindwa kutenganisha Patrotism na Natinalism ktk matetezi yetu ya Uhuru wa Mtanzania kama vile watu wasiokuwa na dini.
Na hakuna mafundisho yoyote ya Kijamii yanayolaani Ufisadi. Kwa hiyo hata Ukimchagua kiongozi ambaye haamini Ufisadi ni haramu utaweza vipi kumpima Uzalendo wake ili hali wewe mwenyewe huamini kama Ufisadi ni haramu.