kapotolo
JF-Expert Member
- Sep 19, 2010
- 3,727
- 2,214
Kuna tangazo la Hakielimu ambalo mwalimu anafundisha somo la computer kwenye shule ambayo jengo lake linakaribia kuangua, wanafunzi wanaona mchoro wanaulizana ile sijui nini iko kama video, wanalalamika mwalimu angekuja nayo labda wangeelewa. Lakini masikini shule haina umeme wala haijulikani lini itapata umeme, kwa sababu hata jengo lenyewe ukiweka umeme umeweka mtego kwa watoto, kwa hiyo somo la computer practically ni ndoto.
Nikiliangalia Tangazo hili naona kama wanamdhihaki JK na ahadi yake ya kueneza computer katika mashule nchini kwa ajili ya kujifunzia. Kwamba hili haliwezekani kwa kuwa shule hazina miundombinu ya kusupport matumizi ya computer.
Sijui wenzangu mnalionaje tangazo lile.
Nikiliangalia Tangazo hili naona kama wanamdhihaki JK na ahadi yake ya kueneza computer katika mashule nchini kwa ajili ya kujifunzia. Kwamba hili haliwezekani kwa kuwa shule hazina miundombinu ya kusupport matumizi ya computer.
Sijui wenzangu mnalionaje tangazo lile.