Mkubwa wangu
Niko hapa Dar. Mgao wa umeme eneo ninaloishi unaanza saa moja hivi. Juzi, ijumaa tulikatiwa kwa masaa kama 13. Ni balaa tupu. Kwa sisi ambao shughuli zetu nyingi tunazifanya kwa kutumia computer, you can imagine! Uzalishaji viwandani, mahospitalini, vyuoni, yaani karaha tupu. Bado watu wanathubutu kuongelea vipaumbele vya taifa!
Duh, poleni sana masaa 13 bila umeme! unajua mkuu wangu kusema kweli Bongo tuna ustaarabu wa kitumwa yaani ile ewallah bwana huku ukicharazwa bakora!..Nashindwa hata kufikiria tu hali hiyo ingetokea nchi hizi kwanza maduka yote yangevunjwa vunjwa, ujambazi ungeongezeka mara 10, billions na mabillioni ya hasara zingetokea acha mbali hasara za viwanda na biashara za watu...Nina hakika rais au waziri mkuu angetakiwa kujiuzuru mara moja!... Sii nchi ya Wadanganyika ambayo kila kitu ni Mungu hakutujalia!
Hata hivyo tumsubiri Zitto atuletee habari kamili nini Tanesco wamejibu..inashangaza sana kuona generators za Songos na mashirika mengine zilizowekwa majuzi tu (less than 4 years) tayari imekwisha haribika beyond repair!. kisha tunaambiwa mitambo hiyo ilikuwa mipya!