Black Butterfly
Member
- Aug 31, 2022
- 54
- 99
Naomba kufikisha kero yangu ambayo inanigusa binafsi pamoja na Watumishi wa Kada ya Ualimu katika Halmashauri ya Wilaya ya Moshi huku Mkoa wa Kilimanjaro.
Sisi Walimu ambao tulipandishwa madaraja tangu Mwaka 2021 hadi kufikia leo ninavyoweka malalamiko haya hatujapewa Barua za Uthibitishi wa kupanda Madara licha ya kuwa tumekuwa tukifuatilia kwa muda mrefu bila mafanikio yoyote.
Wahusika wa suala hili ni Ofisi ya Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) lakini hawatoi msaada wowote zaidi ya kutuzungusha tu.
Barua hizo ni muhimu sana kwetu kwasababu zinatumika katika kuwasilisha madai mbalimbali Serikalini na ni haki yetu kuwa nayo.
Tunaomba TAMISEMI itusaidie kupata barua hizi kwasababu tunaanza kupata mashaka juu ya kupata stahiki zetu.
Kawaida unapokuwa na barua hiyo ya kupandishwa ajira inakurahisishia akati unapotaka kupandishwa cheo katika ngazi inayofuata, kwa kuwa huku Serikalini Walimu huwa tunatakiwa kupandishwa cheo kila baada ya miaka mitatu, hivyo basi itakapofika mwakani inamaanisha sisi tuliopandishwa vyeo Mwaka 2021 lazima tutaingia kwenye changamoto ya kuanza kusumbuana na mamlaka.
Nakumbuka kabla ya Mwaka 2021 utaratibu uliokuwepo ilikuwa ni unapandishwa cheo kwa barua kisha mshahara unachelewa kupandishwa, baada ya malalamiko kuwa mengi ikaonekana Serikali inachelewa kupandisha mshahara licha ya barua kuwa zimefika mapema, utaratibu ukabadilika kuanzia Aprili 2021.
Kilichokuwa kinafanyika ni Walimu kupandishiwa mshahara kisha barua inakuja baadaye, hata mimi mshahara umepanda kulingana na cheo changu lakini changamoto ni hiyo barua ambayo naweza kuitumia kwenye matumizi yangu mbalimbali ya kiofisi.
Sisi Walimu ambao tulipandishwa madaraja tangu Mwaka 2021 hadi kufikia leo ninavyoweka malalamiko haya hatujapewa Barua za Uthibitishi wa kupanda Madara licha ya kuwa tumekuwa tukifuatilia kwa muda mrefu bila mafanikio yoyote.
Wahusika wa suala hili ni Ofisi ya Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) lakini hawatoi msaada wowote zaidi ya kutuzungusha tu.
Barua hizo ni muhimu sana kwetu kwasababu zinatumika katika kuwasilisha madai mbalimbali Serikalini na ni haki yetu kuwa nayo.
Tunaomba TAMISEMI itusaidie kupata barua hizi kwasababu tunaanza kupata mashaka juu ya kupata stahiki zetu.
Kawaida unapokuwa na barua hiyo ya kupandishwa ajira inakurahisishia akati unapotaka kupandishwa cheo katika ngazi inayofuata, kwa kuwa huku Serikalini Walimu huwa tunatakiwa kupandishwa cheo kila baada ya miaka mitatu, hivyo basi itakapofika mwakani inamaanisha sisi tuliopandishwa vyeo Mwaka 2021 lazima tutaingia kwenye changamoto ya kuanza kusumbuana na mamlaka.
Nakumbuka kabla ya Mwaka 2021 utaratibu uliokuwepo ilikuwa ni unapandishwa cheo kwa barua kisha mshahara unachelewa kupandishwa, baada ya malalamiko kuwa mengi ikaonekana Serikali inachelewa kupandisha mshahara licha ya barua kuwa zimefika mapema, utaratibu ukabadilika kuanzia Aprili 2021.
Kilichokuwa kinafanyika ni Walimu kupandishiwa mshahara kisha barua inakuja baadaye, hata mimi mshahara umepanda kulingana na cheo changu lakini changamoto ni hiyo barua ambayo naweza kuitumia kwenye matumizi yangu mbalimbali ya kiofisi.