Kujiendeleza kwa Walimu wa shule za Msingi na Sekondari ni kujitia kitanzini

Mlez

New Member
Jun 6, 2023
1
4
Nawasalimu wanachama wa jukwaa hili. Niombe kwenu ushauri kuhusu walimu waliojiendeleza wa shule za msingi na sekondari.

Kuna ndugu yangu amenisimulia kuhusu kutopandishwa cheo/daraja kwa walimu waliopanda cheo kwa mara ya mwisho mwaka 2019 na walipaswa kupanda tena mwaka huu 2023 Kwa mujibu wa Sheria na taratibu za wizara husika. Sasa wamepatwa na mshangao baada ya kuona hawajapandishwa vyeo Kwa mwaka 2023 kwasababu wamejiendeleza kielimu.

Hivyo kutakiwa kutumikia muundo waliobadilishiwa. Wakati katika sekta zingine mtumishi akisoma anabadilishiwa muundo na kupandisha cheo Kwa haraka pasipo kucheleshewa.

Swali lao ni kwamba:
1. Je, ni dhambi walimu kujiendeleza kielimu? Kama sio dhambi, kwanini wanapatiwa adhabu ya muundo unaowafanya waliojiendeleza kuwa nyuma kicheo na walimu waliokuwa na cheo kimoja ambao hawakujiendeleza?

2. Kama sio dhambi, basi kwanini walimu waliojiendeleza waachwe kupandishwa vyeo Sawa na ambao hawakujiendeleza?

Pia kama ni dhambi na ili kuepuka walimu kupoteza muda na gharama za kujisomesha, itangazwe rasmi kwamba walimu hakuna kujiendeleza. Wabaki kama walivyo na kuendelea kupanda daraja lisiloathiriwa na muundo.

Pia kuna kundi la walimu waliokumbwa na kadhia hii ambao walitumia muda wao wa jioni kujisomea. Kundi lingine ni la walimu waliopata ruhusa ya kusoma lakini mwajiri hakuwalipia gharama za masomo na kusainishwa barua ya kujilipia gharama hizo.

Pia Kuna kundi la walimu ambao baada ya kuhitimu elimu ya stashahada na shahada waliandika barua ya kuomba kubadilishiwa muundo lakini hawakujibiwa Kwa wakati hivyo wote kupewa barua za muundo 2021 baada ya miaka 5 hadi 6 tangu walipopeleka barua hizo na kutopandishwa vyeo vyao Kwa mwaka 2023.

Kundi lingine ni la wale ambao hawakupeleka kabisa lkn wakakutana na adhabu ya kubadilishiwa muundo pasipokupandishwa cheo. Na asilimia kubwa haya yamefanyika Kwa Manispaa ya Kinondoni.

Niombe wataalamu wa haya mambo kuwasaidia hawa walimu kupaza sauti ili wapate stahiki zao Sawa na sekta zingine wanaowabadilishia watumishi wao mara tu baada ya kurejea toka masomoni, maana asilimia kubwa hili swala limewaathiri kisaikolojia na kushindwa kufanya KAZI Kwa weledi kutekeleza majukumu yao ya Kila siku. Huku wakirundikiwa majumu mengi kama KPI.

Nawasilisha.
 
Zamani kujiendeleza kulikuwa na maana ya kupandishwa shule kutoka msingi kwenda sekondari, kutoka sekondari kwenda chuo pamoja na kubadilishiwa muundo wa utumishi na kubadilishiwa daraja la mshahara. Kama uko kijijini unakuja mjini, wilayani unakuwa idarani au ofisa mkuu mwandamizi wilayani au mkoani na hata taifani. Siku hizi walimu wa sekondari wanashushwa kwenda kufundisha msingi na wa msingi wanakazana kusoma wapate diploma na degree na pengine wapandishiwe mshahara kulingana na elimu zao lakini wanabaki hukohuko msingi na degree zao wakicheza makidamakida na watoto.
 
Ni kwa sababu badala ya kuwa darasani kufanya kazi ya kufundisha kama wenzao wao walikuwa darasani kujiongezea elimu wakila mshahara bila kuufanyia kazi wakati wenzao wanakula vumbi la chaki. Itakuwa siyo haki wewe hufanyii kazi mwajiri akulipe mshahara wote kama aliyekazini afu ukitoka akupandishe cheo kama waliokazini kumzalishia siku zote
 
๐‡๐š๐ฉ๐š ๐ก๐ฎ๐ญ๐จ๐ฉ๐š๐ญ๐š ๐ฆ๐ฌ๐š๐š๐๐š ๐ฆ๐ค๐ฎ๐ฎ ๐ฌ๐ข๐จ ๐ฌ๐ž๐ก๐ž๐ฆ๐ฎ ๐ฌ๐š๐ก๐ข๐ก๐ข ๐ฒ๐š ๐ค๐ฎ๐ฌ๐ž๐ฆ๐ž๐š ๐ก๐š๐ฒ๐จ. ๐€๐ง๐ฒ ๐ฐ๐ž๐ข ๐ฐ๐š๐ค๐š๐ญ๐ข๐ฌ๐ก๐ž ๐ญ๐š๐ฆ๐š๐š ๐ฐ๐š๐ฌ๐ข๐ฌ๐จ๐ฆ๐ž ๐ค๐ฐ๐š ๐ฌ๐š๐›๐š๐›๐ฎ ๐ง๐ข ๐ฐ๐š๐จ๐ ๐š ๐ฉ๐ข๐š ๐ฐ๐š ๐ค๐ฎ๐ฌ๐จ๐ฆ๐š.@Mpwayungu Village
 
Ni kwa sababu badala ya kuwa darasani kufanya kazi ya kufundisha kama wenzao wao walikuwa darasani kujiongezea elimu wakila mshahara bila kuufanyia kazi wakati wenzao wanakula vumbi la chaki. Itakuwa siyo haki wewe hufanyii kazi mwajiri akulipe mshahara wote kama aliyekazini afu ukitoka akupandishe cheo kama waliokazini kumzalishia siku zote
Mawazo ya kijinga sana haya, kwani mtu anapokuwa masomoni anasoma kwa manufaa ya nani?

Mm nipo idara ya mazingira, mtu anapokwenda masomoni (iwe kwa kujilipia au kulipia na mwajiri) anapata mshahara wake kama kawaida, na soon baada ya kurudi kutoka masomoni anakuwa promoted kwa daraja moja!

N'a hiyo ni hamasa ya wengine waliokuwa wamebaki kazini kwenda kusoma ili kuongeza ufanisi wa kazi kwa maslahi mapana ya nchi.

Sasa hiyo nadharia yako kwamba kwa kuwa alipokuwa masomoni wengine walikuwa wanafanya kazi kwa hiyo asipewe haki ya kupandishwa cheo/mshahara ni dalili za uchawi, na wivu dhidi ya wenzako, acha!

Sheria ya ajira na mahusiano kazini 2004, pamoja na standing order ina-apply kwa watumishi wote wa serikali, japo Kuna mijitu ya aina yako huwa inanza kutumia logic za kijinga kuumiza wengine, haifai!
 
Ukitaka kufanya kitu pata muda wa kujielewesha juu ya kitu hicho,waraka upo ,na uko wazi kabisa,sio tu mwalimu Bali mtumishi yeyote akienda masomoni kwa zaidi ya mika mitatu hawezi kupanda daraja,sasa wewe unalilia kupannda daraja wakati hujalitumikia.


Hii imeanza kipndi cha magufuli,kiufupi magufuli katenda mazuri lakini na mabaya pia katenda,enzi za kikwete haikuwa hivi,ngoja tumuone mama samia labda anaweza badilisha.

Mzilankende ndo wakulaumia na Sera yake ya kubana matumizi,mimi nimetumikia daraja moja kwa miaka saba enzi zake
 
Inaumiza, inakatisha tamaa, na kwa(kwa maoni yangu) sio haki kwa mtumishi kufanyiwa hivi. Kuna mwalimu kamaliza Bachelor yake mwaka2017,akapeleka barua yamuundo 2018 akajibiwa 2021.Najiuliza huku kucheleweshewa kujibiwa barua kupo kikanuni au nibaadhi tu yaHalmashauri?
Kwa ushauri wangu ukimaliza ngazi flani ya elimu tulia Kwanza na vyeti vyako nyumbani usiharakishe kuomba muundo, vinginevyo uwe umefikia daraja la mwisho ambalo ili lifunguke daraja lingine elimu mpya inahitajika
 
Ni kwa sababu badala ya kuwa darasani kufanya kazi ya kufundisha kama wenzao wao walikuwa darasani kujiongezea elimu wakila mshahara bila kuufanyia kazi wakati wenzao wanakula vumbi la chaki. Itakuwa siyo haki wewe hufanyii kazi mwajiri akulipe mshahara wote kama aliyekazini afu ukitoka akupandishe cheo kama waliokazini kumzalishia siku zote
Huo ndo ukweli na Sheria Iko hivo kupanda daraja maana yake uwe umelitumikia ndio maana Kwa wasiotaka hayo wanaendanzao kusoma open
 
Inaumiza, inakatisha tamaa, na kwa(kwa maoni yangu) sio haki kwa mtumishi kufanyiwa hivi. Kuna mwalimu kamaliza Bachelor yake mwaka2017,akapeleka barua yamuundo 2018 akajibiwa 2021.Najiuliza huku kucheleweshewa kujibiwa barua kupo kikanuni au nibaadhi tu yaHalmashauri?
Kwa ushauri wangu ukimaliza ngazi flani ya elimu tulia Kwanza na vyeti vyako nyumbani usiharakishe kuomba muundo, vinginevyo uwe umefikia daraja la mwisho ambalo ili lifunguke daraja lingine elimu mpya inahitajika
Kwelj kabisa sahiz kujiendealeza nako ili uwe na maslah nako nafikir nayo inahitahi connection๐Ÿ˜€
 
Hukutafuta kazi kwenda kuwa mwanafunzi bali kwenda kufanya kazi. Mwajiri alitoa vigezo vya kuwa na sifa ya kukuajiri. Ukapeleka vyeti ukafanyiwa usahili akakuajiri baada ya kuridhika nawe kuwa kwa elimu yako utamudu level hiyo ya kazi. Swala la kujiendeleza ili upande madaraja haraka ni mbwembwe na ni kwa masilahi yako binafsi. Kama Mwajiri angetaka mtu mwenye elimu hiyo uliyojiendeleza angetangaza kipindi anaajiri maana wamejaa mtaani.

Sasa wewe uliomba kazi umepewa fanya kazi acha tamaa ya kwenda kusoma kisa uwe juu ya wenzako wanaotumikia kazini. Ukirudi kutoka masomoni fundisha kwanza kwa kipindi kinachohitajika kama wengine ili upande daraja. Hiyo elimu yako ya kujiendeleza inatakiwa iwe sifa ya ziada kama ikitokea kwenye ushindani nani apewe madaraka kwenye cheo fulani ila siyo kuwa kigezo cha kurushwa kupanda daraja bila kufanyia kazi daraja husika.

Na hii ingewekwa kigezo cha kupanda madaraja wafanyakazi wote wangerudi darasani nani angefundisha?
 
Nasikia wengi wa viongozi ngazi za juu waliwahi kuwa walimu. Hivi ni kweli? Mpwayungu unasemaje juu ya uvumi huu!
Eeeh walimu wapo pia wasanii na watu wa kada tofauti tofauti zenye kuelekeana na ualimu
 
Ujue ifikie hatua walimu muache kua mnalalamika lalamika ovyo kwanza mnapaswa kutambua walimu ndo sekta ilioajili watu weng kulko kitengo kingne chochote kile
Leo hii kila kata, kitongoji , tarafa ata kijiji lazma utakuta mwalimu akiishi ila sio kla kata kijiji kitongoji wala tarafa ukakuta polisi daktar mwasibu iyo inaonyesha walimu ni weng sana kizidi waajiriwa wa sekta zingne

Na ndo maana leo serikal inaweza jengea polisi au madaktari nyumba ila sio walimu sababu ni weng ata pia kwenye suala la mishahara ni ivyo ivyo wing wenu ndo ttzo

Sasa tuje kwenye ishu yako ya vyeo leo hii asilimia kubwa ya walimu wenye vyeo ni vijana na ukizunguka shule nying vyeo ving ni waalimu vijana sasa ww unaenda kusoma unakuja unategemea upande cheo sasa unataka cheo gan wakat vyeo vying vimeshikiliwa na walimu vijana na idadi ya shule haijaongezeka sasa unataka upandishwe cheo upelekwe wap.
 
Back
Top Bottom