Sitta: Katiba Inaniruhusu Kugombea Urais 2015

Boflo

JF-Expert Member
Jan 20, 2010
4,384
4,409
[h=2][/h] [h=3]Sitta: Katiba Inaniruhusu Kugombea Urais 2015[/h]

Mh Samuel Sitta alikuwa mgeni rasmi leo kwenye bonanza la wanahabari


Waziri wa Africa Mashariki, Samuel Sitta, amesema yupo huru kugombea Urais licha ya kuwa katika umri wa uzee.
Amesema yeye ni raia mwenye umri unaokubalika kikatiba kugombea nafasi hiyo iliyo kubwa kuliko zote za uongozi wa nchi, hivyo anawashangaa wanaopata kiwewe kuhusu suala hilo. Ameyasema hayo wakati akizungumza kwenye bonanza la waandishi wa habari linaloandaliwa na chama cha waandishi wa habari za michezo (TASWA) linalofanyika kwenye ufukwe wa Msasani jijini Dar es Salaam leo. Hata hivyo, Sitta anayeheshimika kwa kuwa kiongozi wa 'kasi na viwango' Hivi karibuni, kuliibuka hoja ya umri wa watu wanaostahili kuwania uraia nchini ambapo mbali na Rais Jakaya Kikwete, wabunge Zuberi Zitto (Chadema) na Januari Makamba (CCM), wamekaririwa wakisema ni wakati kwa vijana kupewa fursa ya urais katika Uchaguzi Mkuu wa 2015. Sitta ameongeza kuwa wanasiasa wanapokuwa wameandikwa tofauti kwenye magazeti na vyombo vingine wasikasirike bali wawe wawazi kuzungumza ukweli kuliko kukasrikia vyombo vya habari. Ameongeza kwamba kama una chunusi usoni na umejiangalia kwenye kioo ukaiona inakukera usikimbilie kuvunja kioo ila tafuta dawa ya kuitibu ile chunusi. Mbali na urais, Sitta ameibua hoja ya kuwepo mkusanyiko wa waandishi wa habari katika kanda hiyo, ili kubadilishana uzoefu na kufanikisha utekelezaji wa majukumu yao kwa jamii. Sitta ambaye pia ni Spika wa Bunge la Tisa la Tanzania amesema atawashawishi mawaziri wenzake katika ukanda wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kuunga mkono wa la kuwakutanisha waandishi wa habari kwa kupeana uenyeji wa kutoka nchi moja hadi nyingine. "Kwa kuanzia mjumuiko huo utaanzia hapa Tanzania na ninatarajia kuwa utafanyika kabla ya mwisho wa mwaka huu," alisema. Sitta alisema uwezo wa kufanyika kwa matamasha yatakayowajumuisha waandishi wa habari wa Africa Mashariki upo hasa kwa kushirikisha makampuni ya kibiashara yanayofanya shughuli zao kwenye nchi wanachama.
 
JAMANI HAYA MASHINDANO YOTE YA ULIMBWENDE WA KISIASA 'MABINTI' KUJIPITISHA OVYO JUKWANI HATA KABLA HAKUJAGOTA SAA SITA TUME YA UCHAGUZI, JE HUKO MAGOGONI KUNANI???????????

Zitto, Lowassa, Sioi, Membe, Migiro, Lusinde, Januari, Nchimbi, Wasira na sasa hivi Sitta kila mmoja kila mmoja ANAUTAKA Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;

jamani Wana-CCM tuambieni ukweli kama kiti hiki kikubwa kuliko vyote nchini kikatiba tayari kipo VACANT tangu mwaka huu 2012 wakati wengine wengi tu huku uswahilini hatuna habari.

Wenzetu tayari mnafahamu nini huko Magogoni wengine tusioijulikana kwetu? Wenzetu mumebaini kitu gani chini ya uvungu msiotuweka wazi mpaka hata wengine wakaja wakaonelea njia ya mkato ki-umri yaweza kutoa jibu la mapema?

Enyi ndugu zetu wachambuzi wa mambo ya siasa nchini, dalili zote hizi si za bure wala wa kupuuza hivi hivi hebu katudadavulieni haraka, kiundani zaidi na bila kupapazapapazi kitu hapo.
 
  • Thanks
Reactions: FJM
i luv mzee sitta.nchi hii ingekuwa na wazalendo wa kutosha kama huyu mzee na utajiri huu tulionao ardhini tungesonga mbele sana.
 
inasikitisha sana,juzi tumefanya uchaguzi tayari watu wanawaza urais badala kufikiria jinsi kupata maendeleo
 
inaonekana tatizo kubwa la tanzania ni uraisi..labda wanaona pale ikulu kuna koti tu la rais kwa hiyo raisi atakuja 2015...kikwete angekua mchapa kazi hakuna mpuuzi yoyote ambaye angijitokeza kuutaka urais.
 
suala la urais wa nchi yoyote dunia si suala la kushitukiza,ni suala endelevu,inakupa shida gani kwa sasa kuwafahamu wagombea urais,mimi nina uhakika kuwa watanzania watatumia fursa hii kuelekea 2015 wakiwa wamewapima na kujua ni mtu wa aina gani wanahitaji.

hongera sana Mh.Sitta kwani unastahili kuongoza nchi yetu na taifa linakuhitaji kulivusha katika hili vimbi la umasikini,ujinga ,naradhi na ufisadi unaolimaliza taifa letu.
 
Hongera sana Mh.Sitta,tunakuunga mkono katika hili mbali na katiba kukurushu lakini pia mioyo yetu sisi watanzania tuna kiu ya kukupa katika uongozi huu mkubwa wa taifa ili kututoa kwenye hili vyumbi na giza nene linalolimaliza taifa letu.

hongera kwa kuweka bayana,kwani ni nani huwasha taa na kuweka uvunguni,umeweka taa yako kwenye kilima cha ukweli.
 
source: ippmedia.com , NIPASHE JUMAPILI

Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, amevunja ukimya na kutema cheche kuhusu suala la kugombea urais katika uchaguzi wa 2015 na kusema kuwa wanaomkataza kuzungumzia suala hilo wameingiwa kiwewe.
Sitta ambaye amekuwa akitajwa kuonyesha nia ya kuwania nafasi hiyo, amesema itakapofika wakati wa kutangaza nia yake hakuna mtu atakayemzuia.
Alisema hayo wakati akifungua Bonanza la Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam jana, lililofanyika Msasani Beach.
"Linapoingia suala la Urais kuna watu wanapata kiwewe, wanaposikia ninataka kugombea, lakini hiyo ni haki ya kila Mtanzania mwenye sifa anaruhusiwa kugombea," alisema Sitta.
Alisema muda utakapowadia wa yeye kufanya hivyo, hakuna atakayemzuia kugombea nafasi hiyo kwa sababu atakuwa anatumia haki yake kikatiba.
Alisema kuna baadhi ya watu wanatumia vibaya maneno ya Rais Jakaya Kikwete kwa kueleza kiongozi atakayemfuata lazima awe kijana, kitu ambacho Sitta alisema kamwe Rais hakumaanisha hivyo.
Alisema Watanzania wamechoshwa kila siku kusikia habari za rushwa na ubadhilifu wa mali ya umma na kusababisha gharama za ujenzi wa miradi mbalimbali kuwa juu kwa manufaa ya watu wachache.
Sitta alisema wakati umefika kwa Taifa kuwa na mwelekeo mpya wenye viongozi wasio na longolongo, rushwa na ubadhilifu.
Aliongeza kwa kusema kuwa hata watoto wadogo hivi sasa wanafahamu mazingira ya rushwa kitu ambacho si kizuri kwa ustawi wa Taifa.
"Hivi karibuni kuna mwanamke mmoja alikuwa akimpeleka mwanawe kwenda shule, alipofika eneo la Mwenge alikamatwa na polisi lakini wakati wanajibizana yule mtoto akamwambia mama yake mpe hela tuwahi," alisema.
Hata hivyo, aliwataka waandishi kuendelea kutoa taarifa zinazoibua ufisadi kwa viongozi wasio waadilifu, ambapo mara nyingi watu hao wanapoona wameng'atwa wanawahukumu ili kuwakatisha tamaa.
Waziri Sitta alikipongeza Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo (TASWA) kwa kuandaa bonanza hilo na kuahidi kuwa Wizara yake itafanya juhudi ya kuomba udhamini katika Makampuni ya Afrika Mashariki ili kuandaa bonanza litakalowajumuisha waandishi wa nchi zote wanachama.
 
chadema wameonyesha nia ya kumtumia Sitta mwaka 2015 kugombea Urais ndiyo maana anasema hakuna wa kumzuia CCM asipopita atakwenda chadema na kule chadema kuna kambi ya Dk. Slaa, Mbowe na Zitto patakuwa hapatoshi nguo kuchanika kila kambi ikitaka kushika hatamu ya kwenda Ikulu
 
Wanaogombea Ubunge sijawaona kutangaza mapema kulikoni? kila mtu anatangaza kuwania Urais!!!!!!!! Kuna nini Ikulu akina Mama porojo, Zitto, Sitta, Lowassa, Mbowe, Dk. Slaa wanapakimbilia?
 
Hata uspika 2010-2015 hakuzuiwa na alitumia haki yake ya kikatiba. Tulipoona manyoya tukajua tayari 6...
 
SittaSamwel(1).jpg

Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana.


Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, amevunja ukimya na kutema cheche kuhusu suala la kugombea urais katika uchaguzi wa 2015 na kusema kuwa wanaomkataza kuzungumzia suala hilo wameingiwa kiwewe.

Sitta ambaye amekuwa akitajwa kuonyesha nia ya kuwania nafasi hiyo, amesema itakapofika wakati wa kutangaza nia yake hakuna mtu atakayemzuia.

Alisema hayo wakati akifungua Bonanza la Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam jana, lililofanyika Msasani Beach.

"Linapoingia suala la Urais kuna watu wanapata kiwewe, wanaposikia ninataka kugombea, lakini hiyo ni haki ya kila Mtanzania mwenye sifa anaruhusiwa kugombea," alisema Sitta.

Alisema muda utakapowadia wa yeye kufanya hivyo, hakuna atakayemzuia kugombea nafasi hiyo kwa sababu atakuwa anatumia haki yake kikatiba.

Alisema kuna baadhi ya watu wanatumia vibaya maneno ya Rais Jakaya Kikwete kwa kueleza kiongozi atakayemfuata lazima awe kijana, kitu ambacho Sitta alisema kamwe Rais hakumaanisha hivyo.

Alisema Watanzania wamechoshwa kila siku kusikia habari za rushwa na ubadhilifu wa mali ya umma na kusababisha gharama za ujenzi wa miradi mbalimbali kuwa juu kwa manufaa ya watu wachache.
Sitta alisema wakati umefika kwa Taifa kuwa na mwelekeo mpya wenye viongozi wasio na longolongo, rushwa na ubadhilifu.

Aliongeza kwa kusema kuwa hata watoto wadogo hivi sasa wanafahamu mazingira ya rushwa kitu ambacho si kizuri kwa ustawi wa Taifa.

"Hivi karibuni kuna mwanamke mmoja alikuwa akimpeleka mwanawe kwenda shule, alipofika eneo la Mwenge alikamatwa na polisi lakini wakati wanajibizana yule mtoto akamwambia mama yake mpe hela tuwahi," alisema.

Hata hivyo, aliwataka waandishi kuendelea kutoa taarifa zinazoibua ufisadi kwa viongozi wasio waadilifu, ambapo mara nyingi watu hao wanapoona wameng'atwa wanawahukumu ili kuwakatisha tamaa.

Waziri Sitta alikipongeza Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo (TASWA) kwa kuandaa bonanza hilo na kuahidi kuwa Wizara yake itafanya juhudi ya kuomba udhamini katika Makampuni ya Afrika Mashariki ili kuandaa bonanza litakalowajumuisha waandishi wa nchi zote wanachama.



CHANZO: NIPASHE JUMAPILI

Babu Mzee Samuel Sita waachie vijana washindanie kuongoza nchi wewe umeshakuwa Mzee kila kitu kina mwanzo wake na mwisho wake jikalie pembeni ule mpunga wako ehhh
 
unafiki@home.sitta.mwakyembe

Umezoea kukariri lini utajifunza kujibu hoja badala ya hivi viroja vyako ?.

Ana haki kisheria, mimi ndicho nilichomuelewa, unafiki unatoka wapi? hivi unajua kwamba kisheria hata Rostam ana haki hiyo?

Mkuu tuko ukurasa mmoja Sitta ana haki ya kugombea kiti cha magogoni sisi wananchi kwa maana ya wapiga kura tuna haki ya kumpima kama anaweza kushika madaraka ya urais mpaka hapo siajaoana tatizo la Mheshimiwa Sitta.
 
Ana haki kisheria, mimi ndicho nilichomuelewa, unafiki unatoka wapi? hivi unajua kwamba kisheria hata Rostam ana haki hiyo?
...hata vijisenti ana haki hiyo na soon mtasikia anawapasua nyoyo zenu..nitacheka kweli kwelii!!
 
Back
Top Bottom