Sitasahau!!!

Kwa maelezo yako Suzy inaonekana ulipitia ktk hali ngumu ya maisha, lakini bado hujaeleza ilikuwaje ukafanikiwa kutokea.
Kwa ufupi tena tupe picha inaweza kusaidia watu wengine wenye hali mbaya ili wasikate tamaa!!!!!!!! Ubarikiwe!!



nimeona habari ingekuwa ndefu sana!! lakini nitarudi tena na Part II usijali
 
niliapa kuwa sitawasamehe hasa yule wifi yangu, ila leo Mungu amenifundisha kusamehe!!! nawapenda sana! najua dhahabu safi lazima ipite kwenye moto!!

Pole Susy!

Hii hali uliyopitia ndiyo ilikufinyanga ukatoka kitu bomba kama almasi. MOVE ON USIISHI KWENYE YA KALE PLS soma signature yangu!

Mungu anajua namna ya kukulipa ukiwa mvumilivu na mstahimilivu.Hao ndugu waliokutesa sasa wanaumia zaidi maana unawalipa mema badala ya mabaya.Hakuna kitu kinaumiza hivi.ADUI MPENDE!
 
niliapa kuwa sitawasamehe hasa yule wifi yangu, ila leo Mungu amenifundisha kusamehe!!! nawapenda sana! najua dhahabu safi lazima ipite kwenye moto!!
Maajabu kabisa hayo, kweli maana kilicho safi lazima kipitie kwenye moto, uchafu wote utoke kimiminwe na kutoka kitu bora kabisa. Hayo ni madarasa ya Mungu wetu, ili akutumie lazima upimwe viwango, mwenye kuvumilia hadi mwisho ataokoka!!!!!
 
Lizy hapa ndipo ninajiuliza kwani kipindi kile chote Mungu alikuwa wapi?? lakini leo nakuja kujua jambo tu, ya kwamba hakuna jaribu lisilo na mlango wa kutokea!! na Mungu huinua maadui kwa sababu maalum!!
Mungu yupo muda wote my dear!Wakati mwingine anaacha vile ili ujifunze!Mi hua nashukuru magumu yote yanayonitokea maana najua muda ukifika na kila kitu kitakua bora kuliko hata nilivyofikiri!Na inatokea kila siku!Siunaona kama wewe..muda ukifika unapata sawa yako!
 
Pole Susy!

Hii hali uliyopitia ndiyo ilikufinyanga ukatoka kitu bomba kama almasi. MOVE ON USIISHI KWENYE YA KALE PLS soma signature yangu!

Mungu anajua namna ya kukulipa ukiwa mvumilivu na mstahimilivu.Hao ndugu waliokutesa sasa wanaumia zaidi maana unawalipa mema badala ya mabaya.Hakuna kitu kinaumiza hivi.ADUI MPENDE!
Hicho kitu safi kabisa, ushauri bomba nimependa hiyo kwenye red!!!!!!!!Ubarikiwe!!!!!!!
 
Pole Susy!

Hii hali uliyopitia ndiyo ilikufinyanga ukatoka kitu bomba kama almasi. MOVE ON USIISHI KWENYE YA KALE PLS soma signature yangu!

Mungu anajua namna ya kukulipa ukiwa mvumilivu na mstahimilivu.Hao ndugu waliokutesa sasa wanaumia zaidi maana unawalipa mema badala ya mabaya.Hakuna kitu kinaumiza hivi.ADUI MPENDE!


ha hah aaaaaaaaaa nimeisoma hiyo signature yako!!! Amen!
 
Asalam aleikum!!!

Bwana Yesu asifiwe!!

Nimesoma thread ya Lizy kuhusu unyanyasaji wa watoto ikanikumbusha mbali sana, hakika imenitoa machozi!!

Nakumbuka miaka ya nyuma sana wakati nikiwa na miaka 4 tu, mama yangu alifariki kwa ugonjwa wa cancer, hatukukaa hata mwaka baba naye alifariki na ugonjwa wa figo, hapo ndipo nilipotamani dunia igeuke chini juu.

Nakumbuka dada yangu mkubwa alikuwa ndio kwanza yupo 4m3 na kaka yangu ambaye nafatana naye alikua yupo darasa la pili, tulinyang'anywa mali zote za baba yetu, tena tukarudishwa kijijini kabisa ambapo baba aliweka mifugo yake, baada ya muda bb mdg akaja akachukua ngombe wote wakagawana na watoto wa mama mkubwa.

Hakuna aliyetujali, tuliachiwa mbuzi tu pale kijijini, nakumbuka kaka yangu ilibidi aache shule aanze kuchunga hao mbuzi kwa taabu, mimi nilikua nachota maji na kufagia, hakuna aliyejua tunakula nini, tunavaa nini wala tunalala vipi. Dada yangu alichukuliwa na dada mtoto wa mm mkubwa na kugeuzwa house girl.

Nakumbuka wale rafikize baba walipoona hivyo, wakamlipia dada yangu ada tena kwa kuchangiwa na kijiji dada akarudi shule, jirani yetu mmoja akasema tuchanganye mbuzi zetu na zake ili kaka asiende kuchunga tena awe anaenda shule.

kutokana na baridi ya mkoa ambao tulikuwepo, na hatukuwa na blanket siku moja nilishikwa na naimonia ikiambatana na homa kali, yule bb mkubwa rafikiye baba akamtuma aende kwa ba-mdogo akamweleze, kaka yangu akapanda gari kwenda mjini kumwambia baba mdogo, baba mdogo akamwambia kama baba yake na mama yake wamekufa yeye anafaida gani, mwache afe akupunguzieni taabu!! kaka alirudi kijijini na kuomba msaada kwa yule rafiki yake na baba (ba-mkubwa) ndipo nikapelekwa hospitali na kulazwa, ikimlazimu kufanya vibarua vya kulima wakati akiwa mdogo ili kutupatia fedha za matumizi na kuniuguza.

kaka yangu mtoto wa m.mkubwa akaoa kule kijijini akatuchukua lakini niliona bora tulivyokuwa tunakaa wenyewe maana wifi alitunyanyasa sana, jina langu lilikua mbwa, nakumbuka alikua ananiita hivi, "we mbwa mkubwa njoo hapa" ukifika tu unakutana na kibao kizito alafu ndio maagizo mengine yanafuatia!!!

Baada ya muda, wale wote waliotudhulumu alikufa mmoja baada ya mwingine, wale waliotunyanyasa kwa chakula leo ndio wanatuomba chakula, waliotulaza chini leo wanatembea wameinamisha vichwa vyao!!

"usimnyanyase yatima wala kumuonea mjane, mkono wa Mungu utakuwa juu yako"

bwana yesu apewe sifa Amen,kama kweli awo waliyowanyia kama nikweli kama ulivyoandka,basi mungu ni mkubwa daima.
 
Mungu yupo muda wote my dear!Wakati mwingine anaacha vile ili ujifunze!Mi hua nashukuru magumu yote yanayonitokea maana najua muda ukifika na kila kitu kitakua bora kuliko hata nilivyofikiri!Na inatokea kila siku!Siunaona kama wewe..muda ukifika unapata sawa yako!

ni kweli Lizy,

nakumbuka siku moja kaka alisafiri alivyorudi wifi alinisemelea uongo kwa kaka nilichapwa sana na kaka mpaka katibu kata akaja kunichukua na kunipeleka kwake, Lizy wifi yangu alikuwa ni zaidi ya mateso, alinichotesha maji mbali tena wakati wa usiku alafu kijijini siunajua tena hakuna hata umeme sa moja tu kila mtu kajifungia kwenye kibanda chake!!
 
bwana yesu apewe sifa Amen,kama kweli awo waliyowanyia kama nikweli kama ulivyoandka,basi mungu ni mkubwa daima.

hii ni kweli tupu, haina hata chembe ya uongo kaka tena mambo mengi tu sijayaweka humu!!! mambo ya aibu!!
 
Kwenye thread ya Lizzy nilishindwa kuchangia, hii imeniliza na kunikumbusha zaidi hata siku yangu leo imeharibika kabisa.

Nakumbuka maneno haya tu "Washenzi mbwa nyie nani aliwaleta hapa kazi kula ugali wangu tu wakati kwenu mlikuwa mmezoea mlenda"

Nimeshindwa......................kuendelea
 
machozi yamenilenga lenga baada ya kusoma thread hii.........kweli Mungu hamtupi nja wake.
sifa na utukufu ni vyake
 
Kwenye thread ya Lizzy nilishindwa kuchangia, hii imeniliza na kunikumbusha zaidi hata siku yangu leo imeharibika kabisa.

Nakumbuka maneno haya tu "Washenzi mbwa nyie nani aliwaleta hapa kazi kula ugali wangu tu wakati kwenu mlikuwa mmezoea mlenda"
Dah!Nxt time sitaanzisha thread yenye kuleta hisia sana!Hata hivyo pole mpendwa!Pole sana..ila yote ni mapito!Masumango yanauma kweli..najua uchungu wake ila mwisho wa siku wewe ndo mshindi wao wanabaki kukushangaa
 
ni kweli Lizy,
nakumbuka siku moja kaka alisafiri alivyorudi wifi alinisemelea uongo kwa kaka nilichapwa sana na kaka mpaka katibu kata akaja kunichukua na kunipeleka kwake, Lizy wifi yangu alikuwa ni zaidi ya mateso, alinichotesha maji mbali tena wakati wa usiku alafu kijijini!!
Yani nachukia kweli mtu anapomwadhibu mtoto kwa msukumo wa mtu mwingine!Utakuta huyo kaka yako wala hakua na chuki na wewe ila alikua anafanya kumridhisha mke wake!
 
Da Dena!!

huna haja ya kuumia moyo, leo imeshabakia historia tu, leo naishi maisha mazuri, nakula nitakacho, naena nitakapo, navaa nitakacho, naishi nipendavyo, Mungu ameyabadilisha maisha yangu, tena ameyabadilisha sana tu!!!

Hivyo tumshukuru kwa pamoja tumrudishie sifa na utukufu kwa maana yeye huviinua vilivyo vinyonge!!
 
Yani nachukia kweli mtu anapomwadhibu mtoto kwa msukumo wa mtu mwingine!Utakuta huyo kaka yako wala hakua na chuki na wewe ila alikua anafanya kumridhisha mke wake!

nikweli Lizy maana nakumbuka alisema hawa watoto wataishi hivi mpaka lini? ngoja nioe wasome, kaka alioa kwa ajili yangu na ya kaka yangu, alitupenda sana, nakumbuka kaka alikua akija kutoka safari, Lizzy wifi ananiiogesha tena ananivalisha nguo safi ila kaka akiondoka tu, navalishwa gauni nikitembea ****** yote yako nje. na nguo kaka alizokuja nazo wifi anampa mdogo wake.
 
Asalam aleikum!!!

Bwana Yesu asifiwe!!

Nimesoma thread ya Lizy kuhusu unyanyasaji wa watoto ikanikumbusha mbali sana, hakika imenitoa machozi!!

Nakumbuka miaka ya nyuma sana wakati nikiwa na miaka 4 tu, mama yangu alifariki kwa ugonjwa wa cancer, hatukukaa hata mwaka baba naye alifariki na ugonjwa wa figo, hapo ndipo nilipotamani dunia igeuke chini juu.

Nakumbuka dada yangu mkubwa alikuwa ndio kwanza yupo 4m3 na kaka yangu ambaye nafatana naye alikua yupo darasa la pili, tulinyang'anywa mali zote za baba yetu, tena tukarudishwa kijijini kabisa ambapo baba aliweka mifugo yake, baada ya muda bb mdg akaja akachukua ngombe wote wakagawana na watoto wa mama mkubwa.

Hakuna aliyetujali, tuliachiwa mbuzi tu pale kijijini, nakumbuka kaka yangu ilibidi aache shule aanze kuchunga hao mbuzi kwa taabu, mimi nilikua nachota maji na kufagia, hakuna aliyejua tunakula nini, tunavaa nini wala tunalala vipi. Dada yangu alichukuliwa na dada mtoto wa mm mkubwa na kugeuzwa house girl.

Nakumbuka wale rafikize baba walipoona hivyo, wakamlipia dada yangu ada tena kwa kuchangiwa na kijiji dada akarudi shule, jirani yetu mmoja akasema tuchanganye mbuzi zetu na zake ili kaka asiende kuchunga tena awe anaenda shule.

kutokana na baridi ya mkoa ambao tulikuwepo, na hatukuwa na blanket siku moja nilishikwa na naimonia ikiambatana na homa kali, yule bb mkubwa rafikiye baba akamtuma kaka yangu aende kwa ba-mdogo akamweleze, kaka yangu akapanda gari kwenda mjini kumwambia baba mdogo, baba mdogo akamwambia kama baba yake na mama yake wamekufa yeye anafaida gani, mwache afe akupunguzieni taabu!! kaka alirudi kijijini na kuomba msaada kwa yule rafiki yake na baba (ba-mkubwa) ndipo nikapelekwa hospitali na kulazwa, ikimlazimu kufanya vibarua vya kulima wakati akiwa mdogo ili kutupatia fedha za matumizi na kuniuguza.

kaka yangu mtoto wa m.mkubwa akaoa kule kijijini akatuchukua lakini niliona bora tulivyokuwa tunakaa wenyewe maana wifi alitunyanyasa sana, jina langu lilibadilika ghafla, nikawa naitwa mbwa, nakumbuka alikua ananiita hivi, "we mbwa mkubwa njoo hapa" ukifika tu unakutana na kibao kizito alafu ndio maagizo mengine yanafuatia!!!

Baada ya muda, wale wote waliotudhulumu alikufa mmoja baada ya mwingine, wale waliotunyanyasa kwa chakula leo ndio wanatuomba chakula, waliotulaza chini leo wanatembea wameinamisha vichwa vyao!!

"usimnyanyase yatima wala kumuonea mjane, mkono wa Mungu utakuwa juu yako"

as if am watching movie.anyway everything has a reason in this world.al i can tell you today is jus 4get the past and move on with your lyfe,and praise almight God 4 making you whoever u r today.
 
as if am watching movie.anyway everything has a reason in this world.al i can tell you today is jus 4get the past and move on with your lyfe,and praise almight God 4 making you whoever u r today.

Thanks my dia!!
 
Susy kuna wimbo naupenda sana bila shaka unaujua;

Muombee adui yako aishi siku nyingi............Asije akafa kabla hajaona baraka ambazo Mungu ameweka juu yako. Kwa yanayokutokea ni Mungu anadhihirisha uumbaji wake. Na ww unapaswa kumtukuza na kumsifu maana amekuinua toka kwa watesi wako. Ni watu wengi wamepitia mambo mengi sana, lakini Mungu ni mwaminifu na anawapigania kila siku.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom