Simulizi: Mwanafunzi Mchawi (A Wizard Student)

Hafi huu upuzi watu tunatenga mda wetu kuifuatilia stori hafu unaishia njiani kiukweli sojaupenda
 
duh watu mmeitafuta hadi mkaipata hiyo riwaya ilipo haya ndugu yangu babu wa kambo wananchi washaingilia tasnia yako
 
jaman si vzur kunikatisha utam mieeee....puliziii leta story na iqw ndefuu
 
SEHEMU YA KUMI NA MBILI

....DORICE alimtazama malkia yule kwa woga huku fimbo ile ya dhahabu ikiwa kifuani mwake. Alihisi kifo chake kipo njiani lakini akajipa moyo wa imani kuwa hawezi kufa kwani hakutenda kosa lolote. Malkia Yule alicheka kicheko kikali cha kutisha.

"Dorice wewe in mchawi sio?" Alisema Malkia yule huku akiwa na sura ya kutisha sana.
"Mimi sio mchawi!" Alijibu Dorice kwa kutetemeka.
"Mbona ulipovamiwa na chatu pale njiani uliongea maneno ya kichawi?"


"Ndio niliyaongea lakini mimi so mchawi, maneno hayo nilifundishwa na babu yangu ambaye ni mganga!" Dorice alishikwa na woga kupita kiasi.
"Hahah Dorice... Kuwa mkweli?"
"Kweli kabisa.. Mimi si mchawi.. Tafadhali naomba mniruhusu niende!" Alisema Dorice huku akilia.
"Unaenda wapi?"
"Naenda Singida kwa babu yangu!"

Aliomba Dorice akiwa amepiga magoti huku akilia kwa hofu.
"Huwezi kwenda Dorice... Sahau kuhusu kuondoka hapa!" Alisema malkia yule kisha akamwamrisha mlinzi wake amwondoe pale Dorice ampeleke sehemu nyingine.
Mlinzi alitii agizo la malkia akamtoa Dorice pale na kumpeleka eneo lingine.

Kilikuwa kama chumba kidogo chenye mwanga hafifu lakini kilikuwa na mapambo mengi sana ya dhahabu. Kilipendeza sana na kilivutia macho kupita kiasi, Dorice alibaki anashangaa.Aliingizwa chumbani mle bila kuambiwa kitu chochote na mlango ukafungwa. Akabaki peke yake.

Hofu ilimzidia sana alitetemeka kama MTU aliyekumbwa na baridi Kali sana, hakupata fursa ya kutazama kitu chochote ndani ya chumba kile akabaki ameinama huku akilia. Alijuta kutoroka shule kwaajili ya Doreen, aliona heri angebaki tu kuliko kuchukuliwa na viumbe wale wa ajabu.

Ghafla akiwa katika dimbwi zito la mawazo alishtuliwa na sauti nzito ya kiume ikimwita jina lake."Dorice" Dorice alishtuka sana kwani alipoingizwa mle hakukuwa na mtu yeyote wala hakusikia mlango ukifunguliwa.Aliinua kichwa na kumtazama aliyemwita.

"Usiogope Dorice.. Naitwa Mansoor, ni mtoto wa Malkia.." Alijitambulisha mwanaume Huyo mwenye sura nzuri ajabu, alinukia marashi mazuri sana yasioisha hamu kuyanusa. Dorice alishangazwa na uzuri wa kiumbe yule mwenye umbo tofauti na viumbe wengine aliowaona kwenye eneo lile. Kwa haraka alimkadiria kuwa na umri wa miaka kama 21 au 22.

"Dorice! Nimeshangazwa sana na uzuri wako uliojaaliwa.. Ama kweli umeumbika! Karibu kwenye himaya yetu!" Alisema kijana yule aliyejitambulisha kwa jina la Mansoor huku akitabasamu na kumpa mkono Dorice. Dorice alibaki ameduwaa kwa mshangao.
****
Eddy alikuwa bado ana hali mbaya iliyomliza sana mama yake kwani Hakuwa na mtoto mwingine yeyote zaidi ya Eddy. Kila Mara alimtazama Mwanaye kisha akatikisa kichwa kwa majonzi. Kwa wakati huo baba yake Eddy alikuwa hayupo nyumbani, alikuwa yupo Dubai kwaajili ya buashara zake.

"Eddy mwanangu una nini?"
"Sina tatizo mama! Naomba nirudi shule..!" Alisema Eddy huku akilia.
"Huna tatizo wakati una tatizo kubwa? Eddy mwanangu nakufahamu vizuri, hebu niambie una tatizo gani?"
"Sina tatizo... Naomba chakula!"
"Nakupa ila naomba uniambie..!"
"Nitakuambia mama ila ngoja baba arudi!"

Mama Eddy hakuishiwa maswali kwa mwanaye, alitamani ajue anasumbuliwa na nini lakini jitihada zake ziligonga mwamba. Eddy hakuwa tayari kumweleza chochote.

Mama Eddy alimwandalia chakula akipendacho mwanaye. Wali na samaki aina ya Sato vilikuwa tayari vipo mezani vikimsubiri Eddy avishughulikie. Eddy alikitazama chakula kile kisha akaachia sonyo Kali.

"Mama! Hivyo ndio nini? Ntakulaje chakula kina harufu kama nini? Huoni hao funza walivyojaa humo au ndio chakula chenu siku hizi?"
Alisema Eddy akiwa amekunja sura kama amekula ndimu iliyooza.

"Funza? Funza wako wapi?" Mama Eddy alishangaa kwani chakula kile ndio kwanza alitoka kupika mda ule.
"Funza hao! Huoni wanavyotembea tembea humo kwenye bakuli? Mama toaaaa..!" Alisema Eddy kwa sauti.
"Mmh! Mwanangu we umerogwa.. Sio Bure..!" Alisema mama Eddy huku akiondoa chakula kile mezani.
"Eddy kweli umeona funza?"
"Ndio kwani we hujaziona?" Eddy Alisisitiza na kuzidi kumshangaza mama yake.

Mama Eddy alizidi kuchanganyikiwa, akachukua simu na kumtafuta baba yake Eddy.
"Hebu achana na hizo biashara baba Eddy! Mtoto ana hali mbaya sana!" Alisema mama Eddy kwa msisitizo.
"Kwani ananini?"
"We njoo mume wangu, uje haraka sana!"
"Mh! Leo nakata tiketi ya ndege nakuja!"
Mama Eddy alikata simu kwani alikuwa amempigia mumewe kupitia mtandao wa IMO.

Kesho yake baba Eddy aliwasili nchini na kufika nyumbani kwake haraka.
Alipomtazama Eddy hakuona kama ana tatizo sana. Aliona yupo kwaida na alishindwa kuelewa ni kwanini mkewe alichanganyikiwa kiasi cha kumfanya aache biashara zake na kurudi nyumbani.

"Wanawake bhana mbona Eddy mzima kabisa?"
"Mzima? Amerogwa huyu mume wangu tangu.. afike Jana hajala kitu anasema eti anaona funza?"
"Eti nini? Mbona sielewi? Hujazoea utani wa Eddy mke wangu!?" Baba Eddy alichukulia kimasihara suala la Eddy. Ikabidi wamkalishe chini na kumuuliza vizuri kilichomsibu kijana wao.

Sikh hiyo Eddy alikuwa mpole kupita kiasi, ni kama vile akili zilirudi kichwani mwake.
"Baba! Mama! Hapa nilipo sio MTU tena, siwezi kuishi tena kwani nikiishi sitakuwa mkamilifu.. Bora nife!"
Maneno hayo ya Eddy yalikuwa kama upanga kwani yalichoma mioyo ya wazazi wake na kuiachana katikati huku damu zikichuruzika bila kikomo.

"Eti nini Eddy!"
"Bora nife!" Aliridia Eddy
"Kwasababu gani? Tumekukosea nini? Kuna kitu hatujakupa?"baba Eddy alichanganyikiwa na kuinuka sofani kama amechomwa na mwiba.
"Wazazi wangu! Nimefanywa vibaya na binadamu katili, nimechukuliwa.. .. Ah.. Nime..!" Eddy aliangua kilio na kushindwa kuendelea kuongea.
"Sema tu.. Umechukuliwa pesa? Au umebiwa vitu vyote sema tu.."


****
"Doreen unataka nini kwangu?" Aliuliza Nadia Joseph.
"Sitaki kitu.. Nataka tupige stori..."
"Stori zipi za kutaka kuniwangia mchana kweupeee?"
Maneno ya Nadia yalimshtua sana Doreen, hakutaka kuamini kama Nadia amejua lengo lake alistaajabu kidogo lakini hakutaka kushindwa.


"Doreen unataka kuniwangia? Usitake kunijaribu nitakuaibisha!" Alisema Nadia kwa sauti ndogo iliyosikika vizuri.

Doreen bado hakumuamini akajiweka sawa, akataka atumie ufundi na nguvu za uchawi wake ili amtulize kimya Nadia. Akaachia kombora lake la kichawi lakini....

Itaendelea....
 
SEHEMU YA KUMI NA TATU

....EDDY hakuwa na jinsi kwani aliona hana sababu yoyote ya kuwaficha wazazi wake juu ya tatizo lake.Aliamua kuwaambia ukweli Ili kama kuna uwezekano wa kumsaidia basi wamsaidie. Kwa kilio cha kwikwi kilichoonesha huzuni kuu iliyotawala moyo wake, Eddy alifungua kinywa na kusema ukweli.

"Sehemu zangu za siri... Zimepotea.. Sielewi zilikoenda!" Maneno ya Eddy yaliibua sura mpya kwa wazazi wake. Walishtuka mshtuko ambao haukuwahi kuwatokea maishani. "Ati nini? Hebu rudia tena..!" Mr.Alloyce hakuamini maneno ya mwanaye. Mama yake Eddy hakueweza hata kufumbua kinywa chake kwani alikuwa amechanganyikiwa kupita maelezo.

"Ndio hivyo baba yangu.. Sina raha ya kuwa hai..!" Eddy alizidi kulia pindi alipozungumza maneno hayo.

Kiukweli kisa kile kiliwakata maini wazazi wa Eddy. Walihisi kuishiwa nguvu kabisa mwilini, walibaki kimya wakiwa wameinamisha vichwa vyao. Huzuni iliyochanganyika na mshangao ndiyo iliyotawala katika jumba lile la kifahari la Mr.Alloyce. Zilipita dakika tano kukiwa na ukimya wa kuogofya. Hatimaye Mr.Alloyce alivunja ukimya ule kwa kumdadisi mwanaye kwa maswali.

"Kuna mtu ulimkosea?"
"Hapana baba!" Alijibu Eddy.
"Sasa ilikuwaje mwanangu?" Mr.Alloyce aliuliza kwa sauti ya upole sana.
"Sijamkosea mtu ila kuna binti anaitwa Doreen..!" Eddy alitaka kusimulia jinsi ilivyokuwa lakini baada tu ya kutaja jina la Doreen hakuweza kuendelea kuzungumza kwani alipigwa Kofi moja zito, likamyumnisha pale kitini, kichwa kikamzunguka akahisi kama radi imempiga. Alipiga ukelele uliowashtua wazazi wake na kufanya wahamaki.

"Eddy nini?"Mr.Alloyce aliuliza kwa mshangao kwani alimuona Mwanaye akidondoka kitini bila kujua kinachoendelea.

Wakazidi kuchanganyikiwa sana, wakamsogelea Eddy na kumwinua lakini Eddy hakuwa na habari, alikuwa kama mzoga ambao unapelekwapelekwa kokote bila kutoa ushirikiano. Hali hiyo ilimtisha sana mama Eddy, akashindwa kuvumilia akaangua kilio kikali.

*******
Dorice aliendelea kumshangaa Mansoor bila kutia neno lolote, ingawa moyoni alibaki kumsifia kwa uzuri alionao mwanakaka yule bila shaka hakuna mwanamke ambaye kwa hali ya kawaida asingevutiwa nae. Yote hayo yalibaki moyoni mwa Dorice na asingeweza kusema lolote kwa kijana yule.

"Dorice mbona upo kimya wala hutaki kunijibu lolote.. Hata salamu?" Alisema Mansoor huku akiachia tabasamu mwanana.
"Mh! Umesemaje?" Dorice akajifanya hakusikia lolote.
"Ina maana hukunisikia kabisa..?"
"Ndio"
"Inawezekana kweli.. Maana unaonekana una mawazo mengi.. Unawaza nini?" Mansoor alimsogelea kwa ukaribu zaidi Dorice na kuketi.
"Nataka kurudi nyumbani!"
"Unataka kurudi? Kwasababu gani?"
"Siwezi kukaa huku! Nataka nirudi nyumbani!" Alisema Dorice huku machozi yakimlengalenga.
"Dorice! Utarudi vipi wakati mama yangu ameniambia amenitafutia mke? Nataraji kufunga ndoa nawewe hivi karibuni.." Maneno hayo ya Mansoor yalimshtua Sana Dorice akatoa macho kwa mshangao.

"Unasemaje wewe?" Dorice aliuvua woga akajikuta ameropoka kwa hasira.
"Sikiliza Dorice.. Kwa muda mrefu sana nilikuwa natafuta mke, sikumpata. Nilitamani sana kuoa binadamu ili niishi nae, na kwakuwa mama yangu ananipenda amenitafutia wewe na ninakupenda. Nataka nikuoe..!"

"Toka hapa.. Usinisogelee... " Alifoka Dorice na kumsukuma Mansoor.
Mansoor alihuzunika sana kwa kitendo alichofanyiwa na Dorice, akatikisa kichwa na kupiga hatua za taratibu kisha akatoweka ghafla machoni kwa Dorice. Dorice alishtuka sana akabaki ametumbua macho tu.

"Mungu wangu nisaidie niondoke huku, mkosi gani huu? Nitafanywa vibaya na viumbe hawa sijui majini... Bila shaka ni majini! Niolewe na jini? Siwezi Mimi...!" Alizidi kuwaza Dorice huku kijasho chembamba kikimtoka kwa kasi.

Ghafla mlango wa chumba alichokuwamo Dorice ukafunguka ghafla, Dorice alishtuka sana kukutana na sura ya malkia akiwa na hasira kupita maelezo.

"Dorice binadamu! Ungekuwa umeuwawa masaa mengi yaliyopita.. Lakini kutokana na mapenzi ya mwanangu Mansoor kwako ndio maana upo hai mpaka sasa.. Ni kitu gani kinakupa jeuri ya kumtesa mwanangu wa pekee?" Malkia alizungumza kwa sauti Kali iliyoambatana na radi. Alionekana mwenye hasira sana.

Dorice aliogopa sana wala hakuthubutu hata kunyanyua kinywa chake akabaki kimya huku akitetemeka.
"Dorice! Una machaguo mawili tu! Chagua moja... KUOLEWA NA MANSOOR AU KIFO!"
Alisema malkia yule kwa ukali, Hofu ikamzidia Dorice.

********
Doreen alipoathubutu kutumia uchawi wake kumdhuru Nadia Joseph, ghafla akakumbana na kichomi kikali sana ubavuni mwake. Akahisi maumivu makali yaliyomfanya apige kelele sana zilizowashtua darasa zima. Wanafunzi wote wakamgeukia yeye lakini kwa kukwepa aibu akajifanya kujinyoosha akiwa bado anaugulia maumivu yale makali. Baada ya hapo wanafunzi wale wakaendelea na shughuli zao.

"Doreen.. Nakupa onyo, acha kuwachezea wenzio! Unajivunia uchawi lakini Mimi nina MUNGU.. Hunitishi kwa lolote maana niliyenaye ni mkuu kuliko nguvu zote.. Nimemwomba Mungu anioneshe MTU anayevuruga shule nashukuru sasa amenionesha! Achana na Uchawi!" Alisema Nadia kwa ujasiri sana ingawa aliongea kwa sauti ndogo ili asisikike sana.

Doreen aliumbuka sana, akaondoka bila kuaga.
Kengele iligongwa wanafunzi wote walitakiwa waende mstarini. Baada ya mkusanyiko wa wanafunzi wote alisimama mwalimu mmoja kwaajili ya matangazo muhimu.

"Kuuna taarifa za kusikitisha sana! Kiufupi ni kwamba Mwalimu Mkuu msaidizi na mwalimu wa taaluma hatuko nao tena. Wameaga dunia Leo asubuhi.. Pia kuhusu mwalimu John kuna sintofamu imetokea kiufupi ni kwamba hajafa bado yuko hai..." Wanafunzi walisikitishwa sana na taarifa zile ila walipigwa butwaa kuhusu mwalimu John kwani walikwisha tangaziwa kuwa amefariki lakini iweje waambiwe yuko hai? Walishindwa kuelewa.

Baada ya mwalimu kutoa matangazo aliondoka zake pale mstarini. Ndipo Nadia Joseph alipoomba nafasi ya kuzungumza na akapewa.

"Jamani wanafunzi wenzangu, hali hapa shule ni mbaya sana... Acheni masikhara hebu fanyeni maombi ya kweli! Mkisali kwa uaminifu MUNGU atajibu tu... Msichukulie mazoea tafadhali..." Aliposema hivyo kuna wanafunzi waliguna lakini Nadia hakujali hilo akaendelea.

"Sasa hivi wanataka titi la msichana.. Usipokua makini unaweza ukachukuliwa lako..!" Nadia aliposema hivyo, alimwona Doreen kwa mbali akiwa amenuna sana huku akimtazama Nadia utadhani anataka kummeza.
Wanafunzi wote wakataharuki, walianza kuogopa sana.
Nadia akaondoka pale mbele kisha wanafunzi wote wakatawanyishwa.

Doreen alikuwa na hasira za kuua MTU. Alimchukia Nadia kupita kawaida, akaahidi kumfanyia kitu kibaya sana....

Itaendelea....
 
Jamani eeh mimi nawawekea Simulizi kadri ninavyoipata, so kuingilia thead ni kuvurugiana utaratibu

Naomba mlioanzisha thread juu ya thread mziondoe tafadhali, la sivyo nitafuta thread yote

Natoa muda mchache post zisizo na utaratibu ziwe zimefutwa
 
Back
Top Bottom