FEBIANI BABUYA
JF-Expert Member
- Mar 5, 2022
- 1,035
- 1,925
Once again tunakutana kwenye mchezo bora huu hapa. Tukapate kumsoma secret agent mmoja ambaye alikuwa assigned kuwa mlinzi wa raisi.
Lakini baadae anagundua kwamba mfumo hauko sawa na yeye ndiye alikuwa amechaguliwa na watu wasio julikana kwa ajili ya kuufuta huo mfumo. Anakuja kushtuka wakati yeye mwenyewe yupo ndani ya mfumo tayari hivyo anakuwa hana namna zaidi ya kudili na watu ambao hakuwa akiwajua na nyuma yao kulikuwa na mambo mazito sana.
Max (jina la kazi) huku jina lake halisi akijulikana kama DONALD DANIEL (DONNY) code no 001. Anaanza kuyafunua yale ambayo alipewa kazi kuyafanya ndipo anagundua kwamba kuna mlima mzito sana wa kuupanda lakini wakati anaanza kuyajua hayo mazito anakutana na jambo baya sana.
Ananasa kwenye HONEY TRAP na kuunguza mchezo mzima hali ambayo inamfanya kuishia kwenye umauti huku akishuhudia raisi ambaye ndiye alitakiwa kumlinda na raisi huyo ndiye alimpa kazi ya kuufuta huo mfumo akiwa anauawa ndani ya ofisi yake.
Muuaji anamuua raisi huku 001 akiwa ma risasi 6 mwilini hana cha kufanya hivyo yeye ndiye anauziwa kesi kwa kuhusika na mauaji ya raisi wa nchi, rasmi anavishwa taji la ugaidi huku ikionekana kwamba ameuliwa akiwa kahusika na mauaji ya raisi wake tena akiwa ndiye mlinzi mkuu wa raisi huyo.
Mwanaume huyo baada ya raisi kufa naye akiwa ana risasi sita kwenye mwili wake, anabebwa na kwenda kuzikwa akiwa bado hai hajakata roho.
001 anafukiwa na kushindiliwa ndani ya shimo la futi sita porini huku mvua ikiwa inausindikiza umauti wake na jina lake linafutwa kwenye idadi ya watu ambao waliwahi kuishi.
Lakini jambo la kutisha zaidi ni kwamba mwanaume huyo ambaye dunia iliamini kwamba alipatwa na umauti na ilithibitishwa kwamba ni gaidi ambaye aliuawa baada ya kumuua raisi akitaka kushambulia na watu wengine, alikuja kuonekana akiwa hai baada ya miaka kumi na mbili kupita.
Sasa alikufaje halafu akaja kuonekana tena akiwa hai miaka kumi na miwili baadae? Baada ya yeye kuonekana ni kipi kilitokea kwa watu wake ambao alifeli kuwafuta na mfumo wao kwa ujumla? Binafsi majibu yote nimekuandalia ndani ya hili andiko bora sana.
Ni muda wako ndio utakufanya uyapate majibu sahihi kwenye moja kati ya simulizi bora sana ya mapigano ya hali ya juu na ya kutisha muda mwingine bila kusahau stori iliyo pangiliwa unono kabisa.
Kwenye kalamu nimesimama mwenyewe Febiani Babuya wengine wapenda kuniita Bux the storyteller.
Here we go
Lakini baadae anagundua kwamba mfumo hauko sawa na yeye ndiye alikuwa amechaguliwa na watu wasio julikana kwa ajili ya kuufuta huo mfumo. Anakuja kushtuka wakati yeye mwenyewe yupo ndani ya mfumo tayari hivyo anakuwa hana namna zaidi ya kudili na watu ambao hakuwa akiwajua na nyuma yao kulikuwa na mambo mazito sana.
Max (jina la kazi) huku jina lake halisi akijulikana kama DONALD DANIEL (DONNY) code no 001. Anaanza kuyafunua yale ambayo alipewa kazi kuyafanya ndipo anagundua kwamba kuna mlima mzito sana wa kuupanda lakini wakati anaanza kuyajua hayo mazito anakutana na jambo baya sana.
Ananasa kwenye HONEY TRAP na kuunguza mchezo mzima hali ambayo inamfanya kuishia kwenye umauti huku akishuhudia raisi ambaye ndiye alitakiwa kumlinda na raisi huyo ndiye alimpa kazi ya kuufuta huo mfumo akiwa anauawa ndani ya ofisi yake.
Muuaji anamuua raisi huku 001 akiwa ma risasi 6 mwilini hana cha kufanya hivyo yeye ndiye anauziwa kesi kwa kuhusika na mauaji ya raisi wa nchi, rasmi anavishwa taji la ugaidi huku ikionekana kwamba ameuliwa akiwa kahusika na mauaji ya raisi wake tena akiwa ndiye mlinzi mkuu wa raisi huyo.
Mwanaume huyo baada ya raisi kufa naye akiwa ana risasi sita kwenye mwili wake, anabebwa na kwenda kuzikwa akiwa bado hai hajakata roho.
001 anafukiwa na kushindiliwa ndani ya shimo la futi sita porini huku mvua ikiwa inausindikiza umauti wake na jina lake linafutwa kwenye idadi ya watu ambao waliwahi kuishi.
Lakini jambo la kutisha zaidi ni kwamba mwanaume huyo ambaye dunia iliamini kwamba alipatwa na umauti na ilithibitishwa kwamba ni gaidi ambaye aliuawa baada ya kumuua raisi akitaka kushambulia na watu wengine, alikuja kuonekana akiwa hai baada ya miaka kumi na mbili kupita.
Sasa alikufaje halafu akaja kuonekana tena akiwa hai miaka kumi na miwili baadae? Baada ya yeye kuonekana ni kipi kilitokea kwa watu wake ambao alifeli kuwafuta na mfumo wao kwa ujumla? Binafsi majibu yote nimekuandalia ndani ya hili andiko bora sana.
Ni muda wako ndio utakufanya uyapate majibu sahihi kwenye moja kati ya simulizi bora sana ya mapigano ya hali ya juu na ya kutisha muda mwingine bila kusahau stori iliyo pangiliwa unono kabisa.
Kwenye kalamu nimesimama mwenyewe Febiani Babuya wengine wapenda kuniita Bux the storyteller.
Here we go