Nimemsikiliza askari aliyekuwa akihojiwa na CloudsTV anasema sheria ya mavazi ya jeshi unasema;-
"Ni marufuku raia kuvaa sare za jeshi ama mavazi yanayofanana na sare za jeshi". Ili iweje?
Yaani ktk zama hizi za sayansi na teknolojia bado jeshi letu linataka kujitofautisha na raia kwa mavazi? Mwanajeshi ajitofautishe kwa umahiri wa kung'amua na kuzima nia na jaribio la adui kutaka kuivamia nchi yetu. Baasi! Siyo hizi blah blah za kuwalingishia raia gwanda za jeshi.
Kule nchi za watu mpk walevi na mateja wanavaa mavazi yanayofanana na sare za majeshi ya nchi zao. Mbona hatujasikia wakipata shida ya kiusalama?
Tuachane na ushamba huu. Nakumbuka hata bendera ya taifa kabla ya Kikwete kuwa rais ilikuwa ni marufuku kukutwa hata na leso inayofanana na bendera yetu ya taifa. Mhe. Kikwete akaondoa ushamba huu.
Ni wakati wa kuondoa ushamba wa kuzuia raia mavazi yanayofanana na sare za kijeshi sasa.
"Ni marufuku raia kuvaa sare za jeshi ama mavazi yanayofanana na sare za jeshi". Ili iweje?
Yaani ktk zama hizi za sayansi na teknolojia bado jeshi letu linataka kujitofautisha na raia kwa mavazi? Mwanajeshi ajitofautishe kwa umahiri wa kung'amua na kuzima nia na jaribio la adui kutaka kuivamia nchi yetu. Baasi! Siyo hizi blah blah za kuwalingishia raia gwanda za jeshi.
Kule nchi za watu mpk walevi na mateja wanavaa mavazi yanayofanana na sare za majeshi ya nchi zao. Mbona hatujasikia wakipata shida ya kiusalama?
Tuachane na ushamba huu. Nakumbuka hata bendera ya taifa kabla ya Kikwete kuwa rais ilikuwa ni marufuku kukutwa hata na leso inayofanana na bendera yetu ya taifa. Mhe. Kikwete akaondoa ushamba huu.
Ni wakati wa kuondoa ushamba wa kuzuia raia mavazi yanayofanana na sare za kijeshi sasa.