Safari za Kikwete zazaa matunda...

Kama hayo ndio mafanikio umeyaona inabidi tukupeleke milembe tukapime brain huenda akili ina hitirafu!

Hayo ni baadhi ya mafanikio, kuweza kuwapata waalimu wa sayansi kutoka nchi iliyopia hatua kubwa kisayansi ni mafanikio makubwa sana hata kwa uchache wake. Ni punguani tu ambae anaweza kuyabeza hayo.

Fikiri kama watatawanywa shule 47 zenye wanafunzi 100 tu wa sayansi kila moja, ni wangapi watafaidika hapo?

Halafu unasema sio mafanikio? unaskitisha sana. Kwako labda mafanikio ni kukopa na kujengea hawara pesa za chama.
 
Matunda gani ..zaid ya hasara ametupa huyo mshenzi..muhuni huyo hakuna disco ambaya hajawahi kuingia anafanya kwa siri anawadanganya wajinga wenzake kwamba safari zimezaa matunda

Bilicanas?
 
teh teh teh...zomba, are you serious on what you say? Ngoja niangalie movie mie maana ndio ile hadithi niliyosimuliwa na shupavu mmoja aliyekuwa anawinda mende na bunduki. Hiyo kazi ya kuleta hao walimu kama kweli ni walimu kama anafanya Rais, wasaidizi wake wa wizara wanafanya kazi gani?

Unachoshindwa kuelewa kuwa hiyo ni ahadi aliitowa bungeni na bandiko nimeweka juu huko, pitia pitia. Wasaidizi wake wanahakikisha hao wanapelekwa kufundisha bila kubughudhiwa wala kero.

Hivi wewe sio msaidizi wake?
 
Mineral and gas explorers

Hao wapo wengi sana na kisha wataja sana kuwa sasa wapo wale wababe wenye kina exxon na kina petrobras na wengineo kama makampuni 22 makubwa na yanaongezeka. Kaa mkao wa kula, lakini kwa kufanya kazi au kusoma na huko wanatakiwa wana sayansi na Kikwete ndio hivyo anaonesha mfano. Kalagabaho.
 
Hayo ni baadhi ya mafanikio, kuweza kuwapata waalimu wa sayansi kutoka nchi iliyopia hatua kubwa kisayansi ni mafanikio makubwa sana hata kwa uchache wake. Ni punguani tu ambae anaweza kuyabeza hayo.

Fikiri kama watatawanywa shule 47 zenye wanafunzi 100 tu wa sayansi kila moja, ni wangapi watafaidika hapo?

Halafu unasema sio mafanikio? unaskitisha sana. Kwako labda mafanikio ni kukopa na kujengea hawara pesa za chama.


ha ha ha zombaaaa kweli we kilaza

hawa peacecorps wako siku nyingi tu tangu miaka ya 1990's enzi za mwinyi, kwa kifupi ni walimu wanaojitolea na USA government na mashirika husika yanafacilitate ujio wao na jinsi watakavyoishi hapa nchini tena kwa gharama nafuu

cha kupongeza hapa ni ujio wao tena na kwamba labda wakasaidie hizo shule za kata zisizo na walimu kusogeza siku

ila hili sio jambo jipya, pia mfumo wa elimu wa marekani ni tofauti sana na tanzania kwa wale wanaoufahamu vizuri....walimu hawa wangekua wametoka uingereza ingekua ni sawa..... wengi hawa vitu wanavyoweza kufundisha ni vya level ya chini sana..... nakupa mfano sisi tuliwahi kupata mmoja miaka ya 90 pale shule ya sekondari ilboru kwa ajili ya Advanced Mathematics, muhula mzima alikua anachora chora tu ubaoni hamna la maana alilokua akifundisha maana mambo mengi aliyoyaona alikua anasema marekani yanasomwa chuo kikuu....kwa kifupi alikuja kuondolewa

walimu hawa wa marekani ni msaada mkubwa kwa masomo mengine lakini sio masomo ya sayansi na hesabu!
 
Kuna wengine 47 kutoka Brazil wao niwataalamu wakilimo cha NYANYA,nawengine 47 kutoka Ghana wao wamebobea kwenye kilimo cha MANANASI safi sana jk.
 
Walikuwepo kabla ya Nyerere na Keneddy au hulijui hilo?

PEACE CORPS ni programu iliyoasisiwa na Rais JFK. Mapisko (wajulikanavyo mitaani) huwa wanakuja kila mwaka na sio TZ tu bali pia nchi mbalimbali duniani. Sasa kama hii ni mojawapo ya mafanikio ya safari za Mkulu basi mimi najiendea kurara!!!!!!!!!!!!!!!
 
PEACE CORPS ni programu iliyoasisiwa na Rais JFK. Mapisko (wajulikanavyo mitaani) huwa wanakuja kila mwaka na sio TZ tu bali pia nchi mbalimbali duniani. Sasa kama hii ni mojawapo ya mafanikio ya safari za Mkulu basi mimi najiendea kurara!!!!!!!!!!!!!!!

Wala hilo halina shida, ni mpango ulioanzisha na JFK lakini nisemalo kuwa Waalimu wa Kimerekani walikuwepo toka kabla ya Kennedy na Nyerere hata nyerere mwenyewe kwao huko alisomeshwa na Mmerekani. Ungefatilia nyuzi kabla hujakurupuka ungekuta jibu.
 
PEACE CORPS ni programu iliyoasisiwa na Rais JFK. Mapisko (wajulikanavyo mitaani) huwa wanakuja kila mwaka na sio TZ tu bali pia nchi mbalimbali duniani. Sasa kama hii ni mojawapo ya mafanikio ya safari za Mkulu basi mimi najiendea kurara!!!!!!!!!!!!!!!
Mkuu unamaanisha JK kaokota DODO kwenye muarobaini?
 
Hao waalim toka Marekani wanakuja Tanzania kwa sababu hatuna waalimu wa kutosha, au kwa sababu tumeshindwa kulipa waalim vizuri na hivyo watu kukumbia hiyo taaluma? Na pindi wakiondoka hali itakuwaje?

NB: CIA 47, sio mbaya!
 
WAlimu 47 kwa shule zilizopo mkoa wa kilimanjaro tuu hawatoshi sembuse inchi nzima
 
Hao waalim toka Marekani wanakuja Tanzania kwa sababu hatuna waalimu wa kutosha, au kwa sababu tumeshindwa kulipa waalim vizuri na hivyo watu kukumbia hiyo taaluma? Na pindi wakiondoka hali itakuwaje?

NB: CIA 47, sio mbaya!

Hao waalimu wamekuja kufindisha sayansi, somo ambalo tuko nyuma kulinganisha na nchi zingine. Na hizi ni jitihada za Kikwete kuimarisha hilo somo alizozitoa bungeni Dodoma, pitia juu kuna link.
 
Unachoshindwa kuelewa kuwa hiyo ni ahadi aliitowa bungeni na bandiko nimeweka juu huko, pitia pitia. Wasaidizi wake wanahakikisha hao wanapelekwa kufundisha bila kubughudhiwa wala kero.

Hivi wewe sio msaidizi wake?

Usinichekeshe zomba. Namsaidia katika hizi porojo za hapa na pale labda. Lakini ukitaka kuniajiri nifanye hiyo kazi hilo suala lingine...tatizo umri kaka...
 
Last edited by a moderator:
Mkuu unamaanisha JK kaokota DODO kwenye muarobaini?

Nyerere aliwaleta waalimu wa sayansi? au aliiuwa sayansi na kuleta ujamaa usiokuwa na tija, eti kulima kwa mkono kutamkomboa Mtanzania, hiyo ndio sayansi ya Nyerere. Kwi kwi kwi teh teh teh! Akajenga kiwanda cha majembe UFI akawafukuza LONRHO waliokuwa na kiwanda cha matrekta, hiyo ndio sayansi ya mchonga. Ukistaajabu ya Mussa utayakuta ya Firauni.
 
Waalim wa sayansi 47 kutoka USA wameapishwa leo ubalozi wa Merekani. Wamejitolea kuja kufundisha shule za Sekondari za Tanzania baada ya kuombwa rasmi na Mheshimiwa Rais Kikwete.

Ahsante Kikwete. Inanikumbusha wakati nasoma, enzi hizo, tulikuwa na Waalim kutoka Australia, India, Uingereza kwa uchache na mambo yallikuwa swaafi kabisa,

Hii ni fursa kubwa kwa Waalim wetu kujifundisha mbinu za wenzetu nasi kuwaonesha uwezo wetu nao wajifunze kutoka kwetu.

Haya wanafunzi, kazi kwenu na Mungu awasaidie muwe wanafunzi wazuri wa kuigwa na hawa Wamerekani wapeleke salaam njema kwao ili waje na wengine wanaosuasua.

Zomba ni janga na laaana kubwa hapa JF phew!!!!!!!
 
Usinichekeshe zomba. Namsaidia katika hizi porojo za hapa na pale labda. Lakini ukitaka kuniajiri nifanye hiyo kazi hilo suala lingine...tatizo umri kaka...

Kama umri umekutupa mkono unafaa kuwa mshauri mzuri sana kwa jamii. Watu kama wewe na mimi (umri wangu si mdogo, nimezaliwa Tanganyika, nimeanza kusoma Tanganyika kwa hiyo nnaelewa kuhusu elimu ilivyokuwa wakati wa Tanganyika na ilivyoharibika baada ya Azimio la Arusha.) Utu uzima ni dawa, akiondoka mzee mmoja ni kama imeondoka encyclopedia nzima.

Tumia umri wako na ujuzi wako kwa ukweli na kwa nia njema kuwaeleza vijana mambo ya ukweli, Kuna wanaoelimika kupitia ubishi wao. Usikate tamaa.
 
Back
Top Bottom