Safari za Kikwete zazaa matunda...

Hata aibu huna!!!!!!hivi waalimu 47 wanaweza kutoa elimu kwenye shule ngapi nchi hii?kwann asiboreshe maslah ya waalimu wazalendo walioko kwenye mgomo baridi ili wafanye kazi yao vizuri?kwann asijenge maabara zinazokidhi ili wanafunzi wa masomo ya sayansi wafanye practical?sasa hao wamarekani 47 wamekuja na maabara zao?hebu tubadilike tuwe na uchungu na mustakabali wa elimu katika nchi yetu,sio kusifia UJINGA.

Hivi wewe unaakili sawasawa? kama unazo, pitia nyuma huko, umekurupuka, hilo lishajadiliwa. Usidandie treni kwa mbele.
 
Waalim wa sayansi 47 kutoka USA wameapishwa leo ubalozi wa Merekani. Wamejitolea kuja kufundisha shule za Sekondari za Tanzania baada ya kuombwa rasmi na Mheshimiwa Rais Kikwete.

Ahsante Kikwete. Inanikumbusha wakati nasoma, enzi hizo, tulikuwa na Waalim kutoka Australia, India, Uingereza kwa uchache na mambo yallikuwa swaafi kabisa,

Hii ni fursa kubwa kwa Waalim wetu kujifundisha mbinu za wenzetu nasi kuwaonesha uwezo wetu nao wajifunze kutoka kwetu.

Haya wanafunzi, kazi kwenu na Mungu awasaidie muwe wanafunzi wazuri wa kuigwa na hawa Wamerekani wapeleke salaam njema kwao ili waje na wengine wanaosuasua.


Mtamtetea sana lakini hateteeki, mtambeba sana lakini habebeki.............................. Kwenye zile ahadi za Kigoma kuwa Dubai, Mwanza kuwa California, Kujenga uwanja wa ndege Bukoba, Kununua Meli Ziwa Nyasa (ambalo siyo letu).......................n.k. Hii ya kuleta walimu kutoka Marekani aliitolea mkoa gani vile???
 
We Zomba kweli unaona ni sahihi kuleta mamluki wa kuiangamiza elimu yetu kabisa!! Curriculum ya Tanzania ni tofauti na ya US, hawa walimu watafundisha kitu gani walichosoma US? Ukitazama hawa walimu kutoka US, mara nyingi wanakuwa shallow sana. Bora wangekuwa wametoka UK! Kuna ugumu gani kuandaa hawa walimu wa science na kuwalipa vizuri ili waweze kuitumikia Nchi yao?? Huku naona ni kuwapoteza kabisa watoto wa maskini. Hawa walimu wengi wanakuwa wanafundisha mamichezo tu!! Je hawa walimu watalipwa au kujitolea?? Zomba jiulize swali moja, "watafundisha mjini au ni hadi vijijini"? Kama watafika hadi vijijini, mtawaweka wapi, ni kule walimu wetu waliozea shida wanakoishi au?? Hapa mnazidi kutupoteza ndg yangu!!
Tujadili kwa kina Mkuu!

Kama hujui aliyeiangamiza elimu, tuulize tuliokuwepo. Pitia juu huko tumeelezea kwa uchache.

Kwa kukujuza tu, somo la sayansi, ni moja uwe China uwe USA, uwe Tanzania, unaonesha hujui science ni nini.
 
Wale ni watalii sio walimu,wamekuja kuangalia namna bora ya kuvuna URANIUM toka kwenye nchi waliouziwa, fuatilia wanafunzi wanaokwenda kusoma marekani wa kidato cha tatu kwa mwaka mmoja wakirudi wanapelekeshwa sana na wenzao waliowaacha tanzania, timizeni na wapeni walimu wazawakipaumbele kwa kuwalipa stahiki zao na maslahi bora muone performance itakavyokuwa sio kupiga siasa tu

Uranium imeshaanza kuchimbwa, umelala?
 
Waalim wa sayansi 47 kutoka USA wameapishwa leo ubalozi wa Merekani. Wamejitolea kuja kufundisha shule za Sekondari za Tanzania baada ya kuombwa rasmi na Mheshimiwa Rais Kikwete.

Ahsante Kikwete. Inanikumbusha wakati nasoma, enzi hizo, tulikuwa na Waalim kutoka Australia, India, Uingereza kwa uchache na mambo yallikuwa swaafi kabisa,

Hii ni fursa kubwa kwa Waalim wetu kujifundisha mbinu za wenzetu nasi kuwaonesha uwezo wetu nao wajifunze kutoka kwetu.

Haya wanafunzi, kazi kwenu na Mungu awasaidie muwe wanafunzi wazuri wa kuigwa na hawa Wamerekani wapeleke salaam njema kwao ili waje na wengine wanaosuasua.

Zomba unauhakika gani kama hawa ni walimu kweli na si majasusi wakupeleleza kujua vizuri rasilimali zetu waje waibe. Binafsi nilishapoteza imani na Wamarekani.
 
Kama hujui aliyeiangamiza elimu, tuulize tuliokuwepo. Pitia juu huko tumeelezea kwa uchache.

Kwa kukujuza tu, somo la sayansi, ni moja uwe China uwe USA, uwe Tanzania, unaonesha hujui science ni nini.

Waulize waliosoma Mkwawa High School miaka ya 90 watakuambia vizuri habari za mwalimu mmoja wa kemia kutoka Uingereza Mr. Gordon alivyokua "mweupe" na kituko darasani. Aliiona syllabus ya A-level ya TZ kama Chuo kikuu kwao, mambo yalikuwa yanamwia vigumu.
 
zomba your in possession of counterfeted brain in your head. Which fruits are talking about? those maembe from tanga? Or which one! Can 47 teachers cover the gape? Nhaa be serious friend. Or that one of transfaring our few survived animals to arab emirate? Or which one or that of iranian vessels fraging with our frag? How poor you are. I didnt see the kidness ever before. Ha ha ha ha let make a small justerposion between we and our fellow Rwanda it is fun to head of state dont know even simple question that why your people are poor. Dont make your head patient of religious foliousity try to help your country without point of religious control. The time when you will walkout frow day dreaming it will be to rate to your country. Who is your real enemy? If you known join him to fight withn his womb .my friend it is time renew your thnught and come up with a new sensable thread other wise you bf with malicious error to your presiden and if some one is behind your though tell enough is enough. Or are happy to see many restondings to your thread?
 
Waalim wa sayansi 47 kutoka USA wameapishwa leo ubalozi wa Merekani. Wamejitolea kuja kufundisha shule za Sekondari za Tanzania baada ya kuombwa rasmi na Mheshimiwa Rais Kikwete.

Ahsante Kikwete. Inanikumbusha wakati nasoma, enzi hizo, tulikuwa na Waalim kutoka Australia, India, Uingereza kwa uchache na mambo yallikuwa swaafi kabisa,

Hii ni fursa kubwa kwa Waalim wetu kujifundisha mbinu za wenzetu nasi kuwaonesha uwezo wetu nao wajifunze kutoka kwetu.

Haya wanafunzi, kazi kwenu na Mungu awasaidie muwe wanafunzi wazuri wa kuigwa na hawa Wamerekani wapeleke salaam njema kwao ili waje na wengine wanaosuasua.

Nyerere alikuwa hafanyi ziara Nje tulikuwa na Waalimu wa Kinorway; Kiswidish; Australia; Kirusi; Kimarekani; Kidemnark

Sasa Unasema hizo trip 50 za US anapata waalimu 47? Oh, Tutafika kweli? Na ni Shule Gani hao 47 watafundisha?

Shule za Kata, Shule za Jamii, Shule za Serikali au Shule za Private?

 
Kama ni Peace Corps, basi ilianzishwa na John F. Kennedy. Haikuwepo kabla yake.

Hapana naongelea Waalimu, hata Nyerere alikuwa na Mwalim wa Kimerekani, au hujui hilo? wakati huo peace corps walikuwa hawajaanzishwa na Kennedy.
 

Nyerere alikuwa hafanyi ziara Nje tulikuwa na Waalimu wa Kinorway; Kiswidish; Australia; Kirusi; Kimarekani; Kidemnark

Sasa Unasema hizo trip 50 za US anapata waalimu 47? Oh, Tutafika kweli? Na ni Shule Gani hao 47 watafundisha?

Shule za Kata, Shule za Jamii, Shule za Serikali au Shule za Private?


Waalimu wanakuja wengi sana, kila mwaka tena wakujitolea kutoka nchi tofauti duniani, usibadili mada, hawa nnawaongelea mimi wamekuja mahsusi kwa kendeleza masomo ya sayansi pekee. Na hivi karibuni wanakuja wengine wa hayo hayo masomo ya sayansi kutoka India, hii ni effort aliyoitangaza Kikwete bungeni mwaka 2010 ya kupa kipaumbele masomo ya sayansi. na ameona baada ya kufanya vizuri kwenye vyuo vikuu sasa aje kwenye grass roots awapate wanasayansi kuanzia chini. Funguka.
 
Waulize waliosoma Mkwawa High School miaka ya 90 watakuambia vizuri habari za mwalimu mmoja wa kemia kutoka Uingereza Mr. Gordon alivyokua "mweupe" na kituko darasani. Aliiona syllabus ya A-level ya TZ kama Chuo kikuu kwao, mambo yalikuwa yanamwia vigumu.

Na Mkwawa hiyo hiyo ndio kuligunduliwa the "mpemba effect", unaijuwa?
 
Zomba,

..hivi ndivyo Jenerali Ulimwengu alivyo-summarise kuhusu mfumo wa elimu ya Tanzania.


Jenerali Ulimwengu said:
TUNAWEZA kuteua, kama Taifa: ama tutafute elimu endelevu ama tutafute ujinga endelevu.


Ninasema tunaweza "kuteua" si kwa sababu jamii inaweza kuteua, kwa makusudi, kuendeleza ujinga, na kwa kweli kila mara itakuwa inasema kwamba inatafuta elimu.


Kinachoifanya jamii hatimaye ionekane kama iliyoteua ujinga ni jinsi inavyoenenda katika kutafuta hiyo elimu inayosema inaitafuta.


Kwa mfano, tunateua kuendeleza ujinga na kujenga misingi ya ujinga endelevu nilioujadili huko nyuma kwa kukazana na ujenzi wa vyumba vya "madarasa' katika "shule' zisizokuwa na walimu wenye sifa za ualimu wala vitabu.


Tunaweza tukaangalia majengo mazuri na tukaamini kwamba tumepata shule, kumbe ni majengo matupu ambayo yangeweza kutumika kama maghala ya tumbaku au vyumba vya kuhifadhia maiti (mochuari).
 
Kama hujui aliyeiangamiza elimu, tuulize tuliokuwepo. Pitia juu huko tumeelezea kwa uchache.

Kwa kukujuza tu, somo la sayansi, ni moja uwe China uwe USA, uwe Tanzania, unaonesha hujui science ni nini.

technology has no ideology
 
Ninapata uoga sana kuona hii picha ya kuthamini na kusifia wataalam kutoka nje kuwa ni mwarobaini wa matatizo yetu. Ninatatizika kuona baadhi yetu tunaamini kwamba matatizo ya elimu hapa nchini yatatuliwa na waalim toka nje ambao watakuja na kukaa kwa kipindi kifupi sana. Je, uwepo wa hawa waalim unasaidia matatizo ya waalim nchini?
Ndio haya matatizo ya kuamini daktari toka India anayekuja na kukaa kwa wiki moja anaweza kutatua matatizo ya afya ya watanzania wakati yeye anakuja kibishara zaidi na hasa hasa 'ku-poach' wagonjwa wa kwenda kutibiwa kwao.
Let us wake up na kutukuza na kukitunza chetu,. Proudly Tanzanian!
 
Upuuzi mtupu. Ukilinganisha gharama za safari za JK na kile watakachochangia utajua nimaanishacho kwa kusema upuuzi mtupu. Kwani rais ni waziri wa elimu? Hili la kuomba walimu laweza kufanyika hata hapa hapa Dar kupitia ubalozi wa Marekani. Ingawa mleta mada ni shabiki wa JK angetafuta kitu kinachoingia akilini badala ya habari hii ya kidaku na kinazi.
Tatizo letu ni zaidi ya upungufu wa walimu wa sayansi. Kama kungelikuwepo na incentives vijana wangi wangejiunga na masomo ya sayansi na kuwa waalimu bora wa kizazi kijacho. Wanafunzi sasa hivi hawataki kusoma masomo ya sayansi. Nani anataka kusomea udaktari kwa miaka 6 kwa mshahara huu? Hata kozi nyingine za sayansi, watoto wanakwepa.
 
Back
Top Bottom