Rais tunaomba usikilize vilio vya watanzania, mfumuko wa bei ni mkubwa mno

Mchokozi wa mambo

JF-Expert Member
Mar 27, 2014
201
159
Ni Tanzania pekee duniani mfanyabiashara anaweza kupanga bei aitakayo bila kujali chochote
Serikali kupitia waziri wa viwanda na biashara angalieni mfumuko wa bei nchini hasa bidhaa za msingi ni mkubwa mno.

Ukiuliza kila kitu unaambiwa ni sababu ya vita ya Ukraine na Urusi.

Sio kweli wafanyabiashara wengi sasa wanajificha kwenye vita hiyo kuumiza wananchi kwa kupanga bei kubwa na kunufaika juu ya hiyo vita.

Swali dogo tu hivi hapa Tanzania kila kitu tunachotumia kinatoka Urusi na Ukraine?

Bei ya Mafuta ya kula kwa lita ni 7000/= na baadhi ya mikoa ni 10,000/= na mafuta mengi yanazalishwa nchini.

Kwanini bei iko hivi. Wiki kama mbili binafsi nilifanikiwa kuona mfanyabiashara mmoja wa duka jumla unashusha shehena ya mafuta na kuficha nyumbani kwake ndani ya fensi na kupanga madumu kama 300 kuzunguka uwanja wa nyumba yake. Lakini mtaani ukiuliza unaambiwa bidhaa hii ni adimu sana sababu ya vita na ndio maana bei ni kubwa kitu ambacho si kweli.

Kwanini Serikali inafumbia macho wafanyabiashara wenye tamaa kuumiza raia wao?

Bei ya vifaa vya stationery nayo haikamatiki. Fikiria kufikia mwezi Machi mwanzoni ream ya karatasi ilikuwa ilikuwa Tsh 8000/= kwa pc1 na katoni yenye ream iliuzwa kwa Tsh 40000/= Ila kwa sasa ream 1 tu ni Tsh 15000/= mpaka 18000 baadhi ya maeneo huku katoni ikiuzwa kwa Tsh 65000/= .

Mbona Zanzibar vitu bei ni rahisi sana kwanini huku bara tunanyanyasika na huku Rais wetu umekaa kimya? Huna huruma na watu wa bara? Mbona Rais Mwinyi katangaza kushusha kodi kwa bidhaa za msingi kwa kipindi hiki cha mfungo ili bidhaa zishuke kwanini huku bara inashindikana?

Mheshimiwa Rais kauli yako uliyoisema kuwa bidhaa nyingi zitapanda kwa sababu ya vita na zitazidi kupanda sana imechukuliwa kama fimbo na wafanyabiashara kuumiza raia.

Serikali ya awamu ya tano bei ya Sukari ilipanda sana na ikawa sukari ni adimu sana lkn kwa umakini wao walihundua ni janjajanja ya wafanyabiashara walikuwa wameficha sukari ili wapandishe bei kwa kwa kuwa ni adimu.

Lkn tuliona Serikali imejitokeza na kutangaza bei kikomo kwa mikoa yote na huku ikifanya msako kukamata sukari iliyofichwa. Kwanin sasa inashindikana?

Kiukweli Rais bila kuwa mkali nchi hii hautafanikiwa kwa chochote. Watanzania wengi walishaharibika wakipata fursa wanawaza matumbo yao na kujinemeesha wao kwa wao.

Nchi hii kwa sasa ndo tuseme ni ya watu wachache? Hapo nchi jirani ya DRC bei za bidhaa za msingi zilipanda majuzijuzi tu, lakini tumeona Bunge wamemta waziri anayehusika na biashara ajiuzulu ndani ya masaa48.

Tanzania hapa kila kitu ni kusifia hata ujinga. Bunge letu mmekosa mamlaka kisheria kuchukua hatua mbalimbali kurekebisha mambo nchini?
 
Tanzania hapa kila kitu ni kusifia hata ujinga.

Bunge letu limekosa mamlaka ya kisheria kuchukua hatua mbalimbali kurekebisha mambo ya ajabu.

Ngoja tusubiri na tuone mwisho wake, japo tutakuwa tumechoka tukisubiri muafaka.
Tutakuwa tumeumia sn
 
Nchi zinazojitambua👇
AARD4K.jpeg
Nchi zisizojitambua hadi kauli zitapanda bei👇🐒🐒🐒
 
Hebu tuongee ukweli huu mfumuko wa bei uko tanzania pekee?,huu mfumuko kauleta samia?na kwamba huo mfumuko samia unataka afanye nini?
Serikali iwe inatoa bei elekezi katika zile bidhaa ambazo ni za muhimu na zilizokumbwa na huo mgogoro !! Vinginevyo wafanyabiashara watatumaliza !! Hawanaga huruma Hao ! Huwa wanajali maslahi yao tu !!
 
Kwani yeye ni mbara mpk awe na huruma na

Hebu tuongee ukweli huu mfumuko wa bei uko tanzania pekee?,huu mfumuko kauleta samia?na kwamba huo mfumuko samia unataka afanye nini?
Haiko Tanzania pekee ni kweli, ila shida kuna bidhaa zinalishwa na zinapatikana hapa Tanzania, hata vifaa vingi vya Stationery vinatoka China, South Africa, Indosea na India. Tanzania hapa kila mfanyabiashara hasa waagizaji wakubwa wanapandisha bei ukiuliza unaambiwa vita ya Urusi na Ukraine inasababisha.

Kuna mtu maeneo ya kwetu kaficha mafuta ya kula nyumbani na harusu mtu kuingia nyumbani anasubiri bei ipande zaidi tena ndo atoe bidhaa yake auze kwa bei ya juu. Nipo tayri kutoa hata ushirikiano kuonyesha hayo mafuta yalikofichwa lakini Serikali yetu ya sasa haijali.
 
Haiko Tanzania pekee ni kweli, ila shida kuna bidhaa zinalishwa na zinapatikana hapa Tanzania, hata vifaa vingi vya Stationery vinatoka China, South Africa, Indosea na India. Tanzania hapa kila mfanyabiashara hasa waagizaji wakubwa wanapandisha bei ukiuliza unaambiwa vita ya Urusi na Ukraine inasababisha.
Kuna mtu maeneo ya kwetu kaficha mafuta ya kula nyumbani na harusu mtu kuingia nyumbani anasubiri bei ipande zaidi tena ndo atoe bidhaa yake auze kwa bei ya juu. Nipo tayri kutoa hata ushirikiano kuonyesha hayo mafuta yalikofichwa lakini Serikali yetu ya sasa haijali.
Rostamu, Kinana, Makamba, Mwigulu wote wapo ndani ya nyumba unategemea nini?
 
Haiko Tanzania pekee ni kweli, ila shida kuna bidhaa zinalishwa na zinapatikana hapa Tanzania, hata vifaa vingi vya Stationery vinatoka China, South Africa, Indosea na India. Tanzania hapa kila mfanyabiashara hasa waagizaji wakubwa wanapandisha bei ukiuliza unaambiwa vita ya Urusi na Ukraine inasababisha.
Kuna mtu maeneo ya kwetu kaficha mafuta ya kula nyumbani na harusu mtu kuingia nyumbani anasubiri bei ipande zaidi tena ndo atoe bidhaa yake auze kwa bei ya juu. Nipo tayri kutoa hata ushirikiano kuonyesha hayo mafuta yalikofichwa lakini Serikali yetu ya sasa haijali.
Mwambie uyo hapo Kenya mafuta yamepamda na sehemu nyingine hayapo
 
Back
Top Bottom