Ileje
JF-Expert Member
- Dec 20, 2011
- 8,798
- 12,240
Watanzania ni watu wa ajabu sana sijui ni sababu ya upole na unyenyekevu au uoga! La sivyo wako katika lindi la ujinga!
Mwaka 2019 wananchi wa Sudan waliiondoa serikali ya Rais Omary al Bashir kwa kuongeza bei ya mkate kwa kufanya maandamano nchi nzima. Walifanikiwa na sasa Bashir anatumikia kifungo jela kwa ufisadi na matumizi mabaya ya madaraka.
Watanzania tumeongezewa kodi lukuki zingine zikipewa majina ya ajabu kama kodi za mshikamano sijui kodi za uzalendo nk, tumebaki tunanung'unika kimoyo moyo! Kodi ya miamala imepanda, bei ya mbolea imepanda, nauli za usafiri na usafirishaji zimepanda, bei ya mafuta imepanda lakini tunashindwa kuihoji serikali yetu tumebaki tunapiga makelele kama wehu!
Wakati huo huo serikali inapanga kujenga sanamu ya mabilioni ya fedha, gharama za kuendesha serikali inazidi kupanda kutokana na ukubwa wa serikali, ufujaji wa fedha za umma na ufisadi. Aidha serikali inazidi kukopa fedha kwa matumizi yale yale ambayo serikali inakusudia kutumia fedha za kodi mpya!
Watanzania tumebaki kukodoa macho kama vile hatuoni kinachoendelea na hakituhusu! Nani huyu aliyeturonga na kuzaliwa na udumavu wa akili? Kuna matumizi mabaya sana ya madaraka viongozi wetu wanafanya lakini tunashindwa kuwawajibisha!
Watanzania tuamke vinginevyo twafwa!
Mwaka 2019 wananchi wa Sudan waliiondoa serikali ya Rais Omary al Bashir kwa kuongeza bei ya mkate kwa kufanya maandamano nchi nzima. Walifanikiwa na sasa Bashir anatumikia kifungo jela kwa ufisadi na matumizi mabaya ya madaraka.
Watanzania tumeongezewa kodi lukuki zingine zikipewa majina ya ajabu kama kodi za mshikamano sijui kodi za uzalendo nk, tumebaki tunanung'unika kimoyo moyo! Kodi ya miamala imepanda, bei ya mbolea imepanda, nauli za usafiri na usafirishaji zimepanda, bei ya mafuta imepanda lakini tunashindwa kuihoji serikali yetu tumebaki tunapiga makelele kama wehu!
Wakati huo huo serikali inapanga kujenga sanamu ya mabilioni ya fedha, gharama za kuendesha serikali inazidi kupanda kutokana na ukubwa wa serikali, ufujaji wa fedha za umma na ufisadi. Aidha serikali inazidi kukopa fedha kwa matumizi yale yale ambayo serikali inakusudia kutumia fedha za kodi mpya!
Watanzania tumebaki kukodoa macho kama vile hatuoni kinachoendelea na hakituhusu! Nani huyu aliyeturonga na kuzaliwa na udumavu wa akili? Kuna matumizi mabaya sana ya madaraka viongozi wetu wanafanya lakini tunashindwa kuwawajibisha!
Watanzania tuamke vinginevyo twafwa!