Rais Omary al Bashir wa Sudan alipinduliwa kwa ongezeko la bei ya mkate, Watanzania tunachekelea Serikali kuongeza kodi lukuki

Ileje

JF-Expert Member
Dec 20, 2011
8,798
12,240
Watanzania ni watu wa ajabu sana sijui ni sababu ya upole na unyenyekevu au uoga! La sivyo wako katika lindi la ujinga!

Mwaka 2019 wananchi wa Sudan waliiondoa serikali ya Rais Omary al Bashir kwa kuongeza bei ya mkate kwa kufanya maandamano nchi nzima. Walifanikiwa na sasa Bashir anatumikia kifungo jela kwa ufisadi na matumizi mabaya ya madaraka.

Watanzania tumeongezewa kodi lukuki zingine zikipewa majina ya ajabu kama kodi za mshikamano sijui kodi za uzalendo nk, tumebaki tunanung'unika kimoyo moyo! Kodi ya miamala imepanda, bei ya mbolea imepanda, nauli za usafiri na usafirishaji zimepanda, bei ya mafuta imepanda lakini tunashindwa kuihoji serikali yetu tumebaki tunapiga makelele kama wehu!

Wakati huo huo serikali inapanga kujenga sanamu ya mabilioni ya fedha, gharama za kuendesha serikali inazidi kupanda kutokana na ukubwa wa serikali, ufujaji wa fedha za umma na ufisadi. Aidha serikali inazidi kukopa fedha kwa matumizi yale yale ambayo serikali inakusudia kutumia fedha za kodi mpya!

Watanzania tumebaki kukodoa macho kama vile hatuoni kinachoendelea na hakituhusu! Nani huyu aliyeturonga na kuzaliwa na udumavu wa akili? Kuna matumizi mabaya sana ya madaraka viongozi wetu wanafanya lakini tunashindwa kuwawajibisha!

Watanzania tuamke vinginevyo twafwa!
 
Muda si mrefu kila kitu kitapanda kwa sababu ya kodi nyingi kwenye mafuta, sasa nikimtumia mama yangu kule kijijni pesa ya kujitibia lazima akatwe pesa ya kutosha, huku nikikatwa tena pesa nyingi.
 
Acha kuwashauri watu ujinga wa kuanzisha uasi dhidi ya serikali yao pendwa. Mbona sisi chadema kila mara huwa tunawachangia viongozi wetu hela za kuendesha chama, hela za uchaguzi, na za kuwatoa jela viongozi wote wanaokamatwa licha ya kuaminishwa kuwa mwenyekiti wetu ni tajiri wa kutupwa. lkn hatuandamani, wala kulalamika kuwa michango yetu inaliwa na wajanja wachache ndan ya chama.
 
Watanzania ni watu wa ajabu sana sijui ni sababu ya upole na unyenyekevu au uoga! La sivyo wako katika lindi la ujinga!

Mwaka 2019 wananchi wa Sudan waliiondoa serikali ya Rais Omary al Bashir kwa kuongeza bei ya mkate kwa kufanya maandamano nchi nzima. Walifanikiwa na sasa Bashir anatumikia kifungo jela kwa ufisadi na matumizi mabaya ya madaraka.

Watanzania tumeongezewa kodi lukuki zingine zikipewa majina ya ajabu kama kodi za mshikamano sijui kodi za uzalendo nk, tumebaki tunanung'unika kimoyo moyo! Kodi ya miamala imepanda, bei ya mbolea imepanda, nauli za usafiri na usafirishaji zimepanda, bei ya mafuta imepanda lakini tunashindwa kuihoji serikali yetu tumebaki tunapiga makelele kama wehu!

Wakati huo huo serikali inapanga kujenga sanamu ya mabilioni ya fedha, gharama za kuendesha serikali inazidi kupanda kutokana na ukubwa wa serikali, ufujaji wa fedha za umma na ufisadi. Aidha serikali inazidi kukopa fedha kwa matumizi yale yale ambayo serikali inakusudia kutumia fedha za kodi mpya!

Watanzania tumebaki kukodoa macho kama vile hatuoni kinachoendelea na hakituhusu! Nani huyu aliyeturonga na kuzaliwa na udumavu wa akili? Kuna matumizi mabaya sana ya madaraka viongozi wetu wanafanya lakini tunashindwa kuwawajibisha!

Watanzania tuamke vinginevyo twafwa!
Moja ya move ya kuyapinga haya ni hili vuguvugu na KUANDIKWA KWA KATIBA MPYA YA WANANCHI...

Mambo yanakuwa hayawezekani kwa sababu sheria mama ya nchi [Katiba] inawapa mamlaka viongozi kujiamulia wamkamueje mwananchi na wewe mwananchi huwezi kuwa na "say" kwa sababu sheria haikuruhusu kunyanyua mdomo kupingana na viongozi kwa mambo yahusuyo fedha iwapo wameshayaamua wenyewe...

Kwa hiyo, mbinyo (pressure) wa katiba Mpya uendelee kwa kasi sana. Hili likifanikiwa kwa kila mmoja kushiriki kwenye vuguvugu hili, itakuwa ni hatua nzuri ya mwanzo kurudisha mamlaka ya nchi mikononi mwa wananchi wenyewe...

Kutokea hapo, huo utakuwa mwanzo wa viongozi kuanza kuenzi na kuwaheshimu wenye nchi ambao ni umma...
 
Moja ya move ya kuyapinga haya ni hili vuguvugu na KUANDIKWA KWA KATIBA MPYA YA WANANCHI...

Mambo yanakuwa hayawezekani kwa sababu sheria mama ya nchi [Katiba] inawapa mamlaka viongozi kujiamulia wamkamueje mwananchi na wewe mwananchi huwezi kuwa na "say" kwa sababu sheria haikuruhusu kunyanyua mdomo kupingana na viongozi kwa mambo yahusuyo fedha iwapo wameshayaamua wenyewe...

Kwa hiyo, mbinyo (pressure) wa katiba Mpya uendelee kwa kasi sana. Hili likifanikiwa kwa kila mmoja kushiriki kwenye vuguvugu hili, itakuwa ni hatua nzuri ya mwanzo kurudisha mamlaka ya nchi mikononi mwa wananchi wenyewe...

Kutokea hapo, huo utakuwa mwanzo wa viongozi kuanza kuenzi na kuwaheshimu wenye nchi ambao ni umma...
Ni kweli kabisa kwani kutegemea hisani ya mtu ni utumwa ndani ya nchi yako mwenyewe!
 
U
Watanzania ni watu wa ajabu sana sijui ni sababu ya upole na unyenyekevu au uoga! La sivyo wako katika lindi la ujinga!

Mwaka 2019 wananchi wa Sudan waliiondoa serikali ya Rais Omary al Bashir kwa kuongeza bei ya mkate kwa kufanya maandamano nchi nzima. Walifanikiwa na sasa Bashir anatumikia kifungo jela kwa ufisadi na matumizi mabaya ya madaraka.

Watanzania tumeongezewa kodi lukuki zingine zikipewa majina ya ajabu kama kodi za mshikamano sijui kodi za uzalendo nk, tumebaki tunanung'unika kimoyo moyo! Kodi ya miamala imepanda, bei ya mbolea imepanda, nauli za usafiri na usafirishaji zimepanda, bei ya mafuta imepanda lakini tunashindwa kuihoji serikali yetu tumebaki tunapiga makelele kama wehu!

Wakati huo huo serikali inapanga kujenga sanamu ya mabilioni ya fedha, gharama za kuendesha serikali inazidi kupanda kutokana na ukubwa wa serikali, ufujaji wa fedha za umma na ufisadi. Aidha serikali inazidi kukopa fedha kwa matumizi yale yale ambayo serikali inakusudia kutumia fedha za kodi mpya!

Watanzania tumebaki kukodoa macho kama vile hatuoni kinachoendelea na hakituhusu! Nani huyu aliyeturonga na kuzaliwa na udumavu wa akili? Kuna matumizi mabaya sana ya madaraka viongozi wetu wanafanya lakini tunashindwa kuwawajibisha!

Watanzania tuamke vinginevyo twafwa!
uleee moshi wa mwenge anza nao kwanza!! ukifanikiwa baaso
 
Acha kuwashauri watu ujinga wa kuanzisha uasi dhidi ya serikali yao pendwa. Mbona sisi chadema kila mara huwa tunawachangia viongozi wetu hela za kuendesha chama, hela za uchaguzi, na za kuwatoa jela viongozi wote wanaokamatwa licha ya kuaminishwa kuwa mwenyekiti wetu ni tajiri wa kutupwa. lkn hatuandamani, wala kulalamika kuwa michango yetu inaliwa na wajanja wachache ndan ya chama.
we mpuuzi serikali yako ya kifisadi CCM ni wizi mtupu na kesi zao za kubumba ili kukusanya fedha za dhuluma. but time will tell
 
Bora hata jiwe kuliko huyu bi mkubwa, anajaribu kufurukuta lakini ndo anaharibu kabisaa! Unamuweka Mwigulu Nchemba kuwa waziri wa fedha what do you expect!

Some weeks ahead everything gonna be worse, mafuta ya kupikia yatapanda from 5,000 per litre to 6000.

Taabu saaana!

Madege ya kubeba abiria 262+ yamegeuzwa taxi za kutoka Dodoma-Dar halafu atakwambia ndege zilileta hasara Huku yeye akiendeleza hasara zaidi.

Huyu mama hafai kuwa rais atokee na CCM Kama nchi imewashinda waseme wazi!
 
Tanzania kabla ya kuchagua wanasiasa wananchi wana nguvu na thamani sana ila baada ya kuchagua wanasiasa wana nguvu maradufu ya kupanga hata hatma za wananchi. Huu ni upuuzi ambao wenye akili wasipoukemea kwa busara itafika wakati wasio na akili watatumia ujamaa wao kuangamiza taifa. It is a matter of time!
 
Back
Top Bottom