Prof Tibaijuka lazima ajiuzulu

Barubaru

JF-Expert Member
Apr 6, 2009
7,161
2,323
Na Mwinyi Sadallah
23rd January 2012

Chama cha Wananchi (CUF) kimesema kwamba kitapinga Umoja wa Mataifa (UN) kuiongezea Tanzania mipaka ya eneo la kiuchumi la bahari Kuu kabla ya kupatikana muafaka kati ya Serikali ya Muungano na Zanzibar.

Tamko hilo limetolewa na Naibu Katibu Mkuu na Mkurugenzi mambo ya nje wa Chama hicho, Ismail Jussa Ladhu, alipokuwa akihutubia mkutano wa hadhara uliyofanyika katika uwanja wa Gombani ya Kale huko kisiwani Pemba jana.

Alisema Serikali ya Muungano imefanya makosa kuandaa kupeleka maombi ya kutaka kuongezewa mipaka ya eneo tengefu la kiuchumi la bahari kuu (EEZ) bila ya kushirikisha Zanzibar.

Jussa alisema wananchi wa Zanzibar wapo tayari kupoteza maisha lakini hawatokubali eneo la bahari Kuu la Zanzibar kuongezwa na kuwa sehemu ya eneo la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

“Wananchi wa Pemba simameni kidete kutetea maslahi ya Zanzibar hata kama tutamalizika sote haiwezekani eneo la bahari Kuu la Zanzibar kuwa la muungano,” alisema Jussa.

Alifafanua kuwa Januari 16 mwaka huu Waziri wa Ardhi nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka, alitangaza mpango wa Tanzania kuomba UN kuiongezea maili 150 sawa na kilometa 241.5 kutoka usawa wa mwambao wa Tanzania.

Profesa Tibaijuka alisema kazi ya kukamilisha andiko hilo ilianza mwaka 2007 na kugharimu Sh. Bilioni 5.2 na kushilikisha wataalamu kutoka sekta ya mbalimbali, ili iweze kulifanyia utafiti zaidi kuhusu rasilimali zilizoko chini ya bahari kwa lengo la kuinua uchumi wa nchi.

Jussa alisema mpango huo umelenga kuiwezesha serikali ya Muungano kuongezewa eneo hilo ili kufanikisha mpango wake kufanya utafiti na uchimbaji wa mafuta wakati SMZ imekwishaliondoa kwenye orodha ya mambo ya muungano.

Hata hivyo, alisema mpango wa Tanzania kuongezewa eneo la maili 150 kutoka usawa wa bahari ya Hindi umefanyika bila ya kuishilikisha SMZ.

Jussa ambaye pia mwakilishi wa jimbo la Mji Mkongwe, alisema alipohoji suala hilo ndani ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar (BLW) alitakiwa na serikali kuwa na subira na kutoa nafasi kwa serikali ya SMZ kulifuatilia.

Alisema suala la mafuta na gesi asilia tayari SMZ imeamua tangu mwaka 2009 kuliondoa katika orodha ya mambo ya muungano na haikuwa muafaka kwa serikali kupeleka maombi hayo bila ya kupata baraka ya Zanzibar.

“Wenzetu wanataka kuchimba mafuta na gesi asilia ya Zanzibar kwa kutumia mlango wa nyuma hatukubali kwa maslahi ya Zanzibar na nchi yetu,” alisema Jussa.

Kuhusu kufukuzwa kwa viongozi wanne wa CUF akiwemo Mbunge wa Wawi Hamad Rashid Mohammed, alisema viongozi hao wamekwenda kinyume na misingi ya kuanzishwa kwa chama hicho mwaka 1992.

Alisema CUF ilianzishwa kwa madhumuni makubwa ya kupingania haki za Zanzibar na wananchi wake ikiwemo mfumo wa Muungano.

Jussa alisema katika kupingania haki za Zanzibar ndiyo maana wapo watu wamepoteza maisha na wengine kupata ulemavu wa kudumu ndiyo maana chama kimeamua kuwafukuza viongozi hao baada ya kwenda kinyume na misingi ya kuanzishwa kwake.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa haki za Binadamu na mahusiano ya umma Salim Biman, alisema kwamba viongozi waliyofukuzwa ndani ya CUF waliweka maslahi binafsi mbele badala ya maslahi ya chama na wanachama wake.

Awali akisoma risala ya mikoa miwili ya wanachama wa CUF Kisiwani Pemba, Ayoub Yussuf Mgeni, alisema wanachama wanaunga mkono maamuzi ya Baraza Kuu la Uongozi kwa kuwatimu viongozi hao.

Alisema viongozi hao ni wasaliti kutokana na kitendo chao cha kutetea maslahi binafsi na kuwapaka matope viongozi wa kitaifa kwa kutaka kuwagawanya kwa mtazamo wa Uunguja, Upemba na Utanzania Bara.

Alisema CUF kimefanya kazi kubwa kupingania misingi ya haki za binadamu na utawala bora hadi kufanikiwa kuundwa kwa serikali ya Umoja wa Kitaifa Novemba mwaka 2010.

Alisema tangu kundwa kwa serikali hiyo kesi za kisiasa, ubaguzi na ukikwaji haki za binadamu umeondoka kwa wananchi wa Zanzibar.

Aliongeza kuwa hatua kama hizo zinapaswa kuendelea kuchukuliwa kwa mwanachama yoyote anayetaka kuvuruga umoja wa kitaifa kwa wananchi wa Zanzibar.

Mapema Katibu Mkuu wa chama hicho, Maalim Seif Sharif Hamad, ambaye pia Makamu wa kwanza wa Rais, alipokea maadamano ya amani ambayo yalinzia huko Machomanne kupitia Mkanjuni huku wanachama wakiwa wamebeba mabango ya kumshutumu Mbunge wa Wawi aliyevuliwa uanachama Hamad Rashid Mohammed.

Baadhi ya mabango yalisomeka ‘Tumekukuta Wawi na shuka kiunoni, tumekupeleka Dodoma na suti leo watusaliti’; ‘Tamaa imekuponza, siasa hukuweza rudi Wawi ukavue’ na lingine likisema ‘Hamad umepanda upepo utavuna dhuruba’


CHANZO: NIPASHE

My Take:

Kwa kosa alilolifanya kupeleka ombi Un Pasi na kupata baraka za baraza la wawakilishi Znz wakti anajua fika suala la ardhi sio suala la muungano ni utovu mkubwa sana wa nidhamu na kutaka kufanya ubabe na kuvunja katiba ya Muungano na ile ya Zanzibar. Kiungwana anatakiwa ajiuzuru.
 
Hakika Jusa wewe ni shujaa sana kwa kuliona hili kwani kuna dhulma kubwa sana ilitaka kufanyika hapa. Ikiwemo ile ya kumega eneo la bahari kwa Znz na kuitumbukiza katika Muungano.

Lazima kieleweke na Prof lazima aondolewe hapo. Kwani ubabe hauna nafasi kwenye sheria. lazima sheria zifuatwe.
 
KAFU mnapingana wenyewe kwa wenyewe na mko nyumba moja hizi ni akili au Matope ? Sasa mnapinga mko kibanda maiti na wenzenu mko nao nyumba moja wame enda NY ?
 
Nadhani hapa mtamuonea bure tu huyu mama. Hakuna nchi mbili au mataifa mawili. Kuna nchi moja tu nayo inaitwa Tanzania. Prof. Tibaijuka anatumikia Jamhuri ya Muungano wa TAnzania. Na kinyume na wanasiasa wa CUF wanavyojaribu kushawishi, uamuzi huo ulipewa baraka na serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ndio maana Waziri toka kwenye serikali hiyo naye alikuwepo UN wakati wa kupeleka ombi hilo. Lakini vile vile kwa wanaofahamu mchakato wa mambo haya wanajua kabisa kuwa maamuzi haya ya kimataifa toka chini ngazi za wataalamu hadi inapofikia ngazi ya mawaziri serikali zote mbili hushirikiana vizuri sana.

Kuongeza eneo la bahari haiongezi eneo la bahari ya Tanganyika! Linaonekana eneo la bahari ya Tanzania ambayo Zanzibar ni sehemu yake. Kwa hiyo labda kama kuna sababu nyingine. Sioni mahali popote ambapo pana msingi wa kuliuliza Baraza la Wawakilishi juu ya hili kwani suala la eneo la Muungano ni eneo zima la Tanzania. Hakuna bahari ya Zanzibar!

Kama wapo watu wa CUF au wengine wanaoamini kitendo hiki kiko nje ya madaraka ya serikali ya Muungano; wafungue kesi ya Kikatiba kukipinga na kukizuia. Of course, I know no one will.
 
natamani ningekuwa rais ningeifanya zenj mkoa na hao vimbelembele kama jusa ningewarudisha kwao uaharabuni, hawa ndio wanaotududisha nyuima. Tanahitaji raisi mbabe ndio tuendelee. La sivyo hatutafika mahali. Huyu jussa ni ni mtu hatari na si mzalendo kabisa ni mamluki

Hilo aliwezekani hata kidogo. Kwani Tanganyika na Znz zimeungana KIMKATABA na sio KIKATIBA. Kuna mambo apo nje ya mkataba wa Muungano likiwemo hili la ardhi na makazi.

Sasa unapozungumzia maslahi ya eneo la milki ya arrdhi ni lazima uziusishe pande zote mbili kwani hili si suala la muungano. Alichofanya Tibaijuka ni ubabe kitu ambacho hakikubaliki. Ni mawili tu yanatakiwa hapo ima a withdraw hayo maombi na kuanza mchakato mpya kama nchi zote mbili zitakubaliana au kuanisha kila nchi itanufaika vipi in terms of eneo hilo.

kama OIC ilizimwa na Muungano kwanini na hili lisizimwe.

Tibaijuka amechamke lazima ajiuzuru tu hakuna mjadala.

 
Dhahabu na almasi pamoja na pamba ikiwemo makusanyo ya TRA tunawapa wao samaki na Mafuta ya kufikirika wanataka yabaki kwao...Jusa think Twice before you roll those dice
 
Hilo aliwezekani hata kidogo. Kwani Tanganyika na Znz zimeungana KIMKATABA na sio KIKATIBA. Kuna mambo apo nje ya mkataba wa Muungano likiwemo hili la ardhi na makazi.

Sasa unapozungumzia maslahi ya eneo la milki ya arrdhi ni lazima uziusishe pande zote mbili kwani hili si suala la muungano. Alichofanya Tibaijuka ni ubabe kitu ambacho hakikubaliki. Ni mawili tu yanatakiwa hapo ima a withdraw hayo maombi na kuanza mchakato mpya kama nchi zote mbili zitakubaliana au kuanisha kila nchi itanufaika vipi in terms of eneo hilo.

kama OIC ilizimwa na Muungano kwanini na hili lisizimwe.

Tibaijuka amechamke lazima ajiuzuru tu hakuna mjadala.


Dua la Kiarabu...!
 
Nadhani hapa mtamuonea bure tu huyu mama. Hakuna nchi mbili au mataifa mawili. Kuna nchi moja tu nayo inaitwa Tanzania. Prof. Tibaijuka anatumikia Jamhuri ya Muungano wa TAnzania. Na kinyume na wanasiasa wa CUF wanavyojaribu kushawishi, uamuzi huo ulipewa baraka na serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ndio maana Waziri toka kwenye serikali hiyo naye alikuwepo UN wakati wa kupeleka ombi hilo. Lakini vile vile kwa wanaofahamu mchakato wa mambo haya wanajua kabisa kuwa maamuzi haya ya kimataifa toka chini ngazi za wataalamu hadi inapofikia ngazi ya mawaziri serikali zote mbili hushirikiana vizuri sana.

Kuongeza eneo la bahari haiongezi eneo la bahari ya Tanganyika! Linaonekana eneo la bahari ya Tanzania ambayo Zanzibar ni sehemu yake. Kwa hiyo labda kama kuna sababu nyingine. Sioni mahali popote ambapo pana msingi wa kuliuliza Baraza la Wawakilishi juu ya hili kwani suala la eneo la Muungano ni eneo zima la Tanzania. Hakuna bahari ya Zanzibar!

Kama wapo watu wa CUF au wengine wanaoamini kitendo hiki kiko nje ya madaraka ya serikali ya Muungano; wafungue kesi ya Kikatiba kukipinga na kukizuia. Of course, I know no one will.


Barubaru na wenzake wanashangaza kwani wanajua kuwa Waziri Aboud kama sikosei naye yuo kwenye msafara wa NY; hao CUF na CCM najua ni kitu kimoja nilitegemea wawe wanajua kila kitu kuliko kuja kupayuka majukwaani kana kwamba kinachofanyika ni siri. Nadhani Jusa ni mtu hatari sana na serikali ya JMT im-mulike na tochi mchana kabla giza halijaingia
 
Nadhani hapa mtamuonea bure tu huyu mama. Hakuna nchi mbili au mataifa mawili. Kuna nchi moja tu nayo inaitwa Tanzania. Prof. Tibaijuka anatumikia Jamhuri ya Muungano wa TAnzania. Na kinyume na wanasiasa wa CUF wanavyojaribu kushawishi, uamuzi huo ulipewa baraka na serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ndio maana Waziri toka kwenye serikali hiyo naye alikuwepo UN wakati wa kupeleka ombi hilo. Lakini vile vile kwa wanaofahamu mchakato wa mambo haya wanajua kabisa kuwa maamuzi haya ya kimataifa toka chini ngazi za wataalamu hadi inapofikia ngazi ya mawaziri serikali zote mbili hushirikiana vizuri sana.

Kuongeza eneo la bahari haiongezi eneo la bahari ya Tanganyika! Linaonekana eneo la bahari ya Tanzania ambayo Zanzibar ni sehemu yake. Kwa hiyo labda kama kuna sababu nyingine. Sioni mahali popote ambapo pana msingi wa kuliuliza Baraza la Wawakilishi juu ya hili kwani suala la eneo la Muungano ni eneo zima la Tanzania. Hakuna bahari ya Zanzibar!

Kama wapo watu wa CUF au wengine wanaoamini kitendo hiki kiko nje ya madaraka ya serikali ya Muungano; wafungue kesi ya Kikatiba kukipinga na kukizuia. Of course, I know no one will.

Naomba nikuweke sawa kidogo kwani kuna mambo umeyasahau kidogo.

Tanganyika na Znz zimeungana kimkataba na sio kikatiba. Kuna mambo yamo katika mkataba huo nayo ndio mambo ya muungano. Suala la ardhi na makazi si suala la Muungano na ndio maana Znz kuna waziri wa wizara hiyo na Bara yupo.

Kumbuka kuwa Mamlaka ya Tibaijuka mwisho wake ni Chumbe akiwa Znz hana mamlaka yoyote ukilinganisha na waziri wa mambo ya nje au mambo ya ndani. hawa wana malka kote kote.

Kumbuka vile vile Znz ni nchi kamili yenye mamlaka kamili na hilo limebainishwa katika katiba ya Znz. Kwa msingi huo Katiba hiyo hiyo imeanisha eneo la Znz kiufasaha kabisa. sasa kwa ombi hilo la Tibaijuka ni lazima katiba ya Znz itabidi ibadilike kwa kuongeza eneo la milki yake au kupunguza miliki yake na hapo ili kubadilisha kipengele hicho cha katiba lazima BLW litahusika vilivyo kwani wao ndio wtunzi wa sheria za Znz na mambo yote yaliyo nje ya muungano.

Kumbuka kuwa katika Picha walopiga kule UN wakti wanawakilisha alikuweo Tibaijuka, balozi wa Tz katika UN, Mbunge wa Mafia na Katibu wa wizara kutoka Znz. Kwa mantiki hiyo inaonekana wazi Prof Tibaijuka alipata baraka zote za Bunge la Muungano dio maana akachukua muwakilishi wa Bunge.

Sasa upande wa BLW hawakuwa na taarifa zozote ongezeka hilo officially na aliku husishwa kwa lolote lile kitu ambacho Jussa amehoji. Ikumbukwe kuwa maombi haya yakifanikiwa lazima BLW litahusishwa katika kupitisha sheria za ongezeko la eneo la miliki la Znz.

sasa labda tujiulize.
Je Znz itaongezewa kiasi gani katika hicho kilicho ombwa? hilo ni suala ambalo limegubikwa na utata mkubwa na alijabainishwa katika mkataba au mbi hilo.

Lakini pia lazima ufahamu kuwa Tz na Znz zote zinaongozwa na Rules of Law. Na mihimili yote mikuu inajipambanua yaani Serikali, Bunge na Mahakama bila kuingilia katika utendaji kazi wake. Kila muhimili unajitegemea.

Limeanza baraza la wawakilishi kuhoji Serikali ya Znz kisha uzi utafuata. Kwani majibu ya Serikali ndio yatatoa mwangaza kwa sakata hilo. Lakin all in all Tibaijuka lazima ajiuzuru hapo.

Kwani mtiririko wa jambo hili unakuwa sawa kabisa na ule wa Tz kujiunga na OIC.

 
Barubaru na wenzake wanashangaza kwani wanajua kuwa Waziri Aboud kama sikosei naye yuo kwenye msafara wa NY; hao CUF na CCM najua ni kitu kimoja nilitegemea wawe wanajua kila kitu kuliko kuja kupayuka majukwaani kana kwamba kinachofanyika ni siri. Nadhani Jusa ni mtu hatari sana na serikali ya JMT im-mulike na tochi mchana kabla giza halijaingia

Waziri Moh'd Abood hakuwepo kwa mujibu wa picha aliyokuwepo kwene blog ya Issa Michuzi. Yule mweupe uliyemuona ni mbunge wa Mafia naye aliwakilisha Bunge la Muungano. Suala mbona hakukuwa na mwakilishi toka Baraza la wawakilishi?

Kumbuka kuwa katika Rules of Law kuna mihimili mikuu mitatu katika nchi nayo ni Bunge, Makahakama na Serikali. Tanzania iliwakilishwa na Mihimili ya Bunge na Serikali na Znz iliwakilishwa na Serikali na BLW halikuwakilishwa na kutojulishwa kuhusu suala hili.

Na at the end of the day BLW watahisishwa katika kubadili kipengele cha Katiba hususan kila cha eneo la miliki.

Ndio maana wawakilishi wmeuliza hilo kwanini wao hawakujulishwa kuhusu ombi hilo wakti linagusa muungano. Na suala la ardhi ni jambo ambalo haliko katika mambo ya muungano?

Kuna siri hapo ambayo Tibaijuka ameificha nayo lazima ijulikane na kubainishwa.

Tusubiri tu majibu ya Serikali.

 
Muungano ni issue sensitive

je kulikuwa kuna ubaya gani ikafanyika public consultation juu ya hili ?

Je wananchi wamehusishwa vipi ?

serikali zote za CCM zinaweza zikawa ziko right lakini wanavyoifanya hii issue ni kui mishandle kama walivyofanya juu ya Kigamboni na uvumi juu ya kambi ya jeshi ya USA
 
IMG_1621.JPG





Habari yenyewe hii hapa:

MICHUZI: TANZANIA YAWASILISHA UMOJA WA MATAIFA ANDIKO LA KUDAI NYONGEZA YA ENEO LA BAHARI


mwenyemacho haambiwi Tazama
 
Mamlaka ya JMT ni kamili. Eneo la jamhuri ya Muungano ni eneo zima la bara na visiwani. Hakuna eneo lolote la 'nchi ya Zanzibar' ambalo si eneo la JMT. Kama lipo niambie. Katiba ya ZNZ inaweza kusema lolote lakini ikipingana na ile ya Muungano vipengele vyake ni batili. Zanzibar ni nchi kwa Wazanzibari tu; siyo nchi inayotambulika mahal popote duniani. Kuwa na jeshi, mahakama, na rais (mihimili mitatu ya dola) hakuifanyi ZNZ kuwa nchi vinginevyo miye ningetamba niko "nchi" ya Michigan! Kuongeza eneo la bahari kutakuwa na manufaa kwa Zanzibar na kwa Tanzania nzima. Wananchi wa ZNZ yawapasa wafurahi na kuunga mkono uamuzi huu wa serikali ya JMT.
 
Napendekeza mwanzisha maada ateuliwe kushika wadhifa wa TIBAIJUKA akijiuzulu.
 
Mamlaka ya JMT ni kamili. Eneo la jamhuri ya Muungano ni eneo zima la bara na visiwani. Hakuna eneo lolote la 'nchi ya Zanzibar' ambalo si eneo la JMT. Kama lipo niambie. Katiba ya ZNZ inaweza kusema lolote lakini ikipingana na ile ya Muungano vipengele vyake ni batili. Zanzibar ni nchi kwa Wazanzibari tu; siyo nchi inayotambulika mahal popote duniani. Kuwa na jeshi, mahakama, na rais (mihimili mitatu ya dola) hakuifanyi ZNZ kuwa nchi vinginevyo miye ningetamba niko "nchi" ya Michigan! Kuongeza eneo la bahari kutakuwa na manufaa kwa Zanzibar na kwa Tanzania nzima. Wananchi wa ZNZ yawapasa wafurahi na kuunga mkono uamuzi huu wa serikali ya JMT.

Je Zanzibar kujiunga na OIC sawa au si sawa?
 
natamani ningekuwa rais ningeifanya zenj mkoa na hao vimbelembele kama jusa ningewarudisha kwao uaharabuni, hawa ndio wanaotududisha nyuima. Tanahitaji raisi mbabe ndio tuendelee. La sivyo hatutafika mahali. Huyu jussa ni ni mtu hatari na si mzalendo kabisa ni mamluki

Huko kwenu mbona ndio wameja? Rudisheni kina manji, rostam etc!
 
Back
Top Bottom