Prof. Muhongo -> SYMBION -> Kikwete ->

Status
Not open for further replies.
Wakuu,

Kuna sekeseke linaendelea chini kwa chini ambalo likifumuka linaweza kupelekea Prof. Muhongo kuhamishwa Wizara au kupoteza nafasi yake.

Kifupi ni kuwa jamaa kaingilia maslahi ya wakubwa na kwa sasa mambo si mambo. Tutayasikia ya kusikika muda si mrefu.

Nimeandika ili wajue tayari tumejua, tuna taarifa za ndani zaidi na tunafahamu kinachoendelea kati yetu na wamarekani.

Likitokea hilo litakuwa limethibitisha udhaifu aliouzungumzia JJ. Mnyika, hebu tusubiri!
 
SYMBION powered by CIA na project za umeme wa vijijini wapi na wapi?. Hilo ni changa la macho, tutasubiri mpaka dakika ya mwisho. Viongozi wa Tanzania wengi mbumbumbu, someni CIA proposed world order after cold war.Hali tuliyonayo Tanzania ni mbaya kuliko tunavyoifilia, nchi imefika hatua haijui hata adui wake halisi ni nani, maadui wanakumbatiwa na viongozi wenye nyadhifa nyeti kabisa, lazima tuvune mabua
Njia mojawapo inayotumiwa na CIA kujipenyeza katika nchi ni kupitia miundombinu. Hawa wenzetu wana ujanja kutuzidi.
Wakishashika nguzo za umeme watatafuta kingine tena lakini lengo lao ni kuiweka nchi kiganjani. Itafika mahali wanasiasa wetu wanajikuta hawawezi kufanya maamuzi independently. Ndio maana kuna mahali nimesema haya madhara aliyotuletea Kikwete yatatuandamana hata miaka 30 baada yake kutoka mamlakani. It is a shame.
 
Kikwete kila siku kiguu na njia Marekani, tena bahati mbaya yeye mwenyewe anawaomba waje kuwekeza. Watashindwaje kutuibia na kuingia mikataba ya kinyonyaji?
 
Na mirahaba ya migodi yangu itajadiliwa? Teh teh teh...nilikuwa naota tu kama na mimi ni fisadi papa au nyangumi au na hallucinations!
 
hivi lini hii CCM tutairestisha ini pisi wawanawani 2015 mbali sana.
inakera sana kuona CCM kutwa kucha ni kutetea matumbo yao na sio maslahi ya wananchi
Prof Muhogo nakushauri wakikutisha itisha press conference sema kila kitu
halafu jiuzulu, hapo hapo andaa barua kabisa na itume after conference achia ngazi rudi kafundishe
CV yako inatisha huna haja kuinyenyekea CCM isiokuwa na lengo la kumkomboa Mtanzania.

istoshe ccm sio baba wala mama...bila ccm inawezekana
 
watajuta kumchagua Prof. Muhongo.,wakuu nisaidieni hivi kuna tofauti kati ya RICHMOND, DOWANS na SYIMBION. au mashine ni ile ile majina tofauti kama Ganja.
 
Mengi yalikuja na yamepita, yaliyopo yanafumbiwa macho, na hili nalo ni upepo tu, utapita. Kitu nina hakika hakitapita ni ufisadi ndani ya safu za CCM.

Let's not hope changes for the better while CCM is on power.
 
Tatizo la kuwa na viongozi wababaishaji ndo hilo. Mimi sitashangaa kama Prof atatolewa kwani wachapakazi hawawezi kukaa na wababaishaji. La sivyo inahitaji kuwa mwangalifu sana kwani yaliyotokea kwa baadhi ya wachapakazi tumeyashuhudia kwa macho yetu.

Katika hali kama hii ndo utakapojua kuwa bwana mkubwa (JK) anasimamia upande upi hasa. Tusubiri tuone
 
Prof wee komaa nao mpaka kieleweke watz zaidi ya 20mil wako nyuma yako na pia mola atakupigania its time to say NO to any none sense
Najua ukikomaa watanywea bse wanachofanya si haki mbele ya watz maskini na mungu
 
Symbion itatupa shida sana. It will cost us dearly na malipo yanaweza yakachukuwa muda mrefu-generations. Wakati wanakuja Dar watu walijadili sana hapa JF kuhusu potential problems na kuuliza -make up ya hii company. Haikuchukuwa muda tukamuona Bi Hillary Clinton mjini. Lakini ukiangalia wakubwa wanaoongoza Symbion utaona mzigo tuliojibebesha.

Na haitoshi tu kuangalia Symbion yenyewe, inabidi tuangalie other elements na kuunganisha dots. Kwa wadadisi wa mambo watagundua mahusiano ya karibu sana kati ya wafanyibishara wa kimarekani na ujasusi wao. Hyatt kwa sasa ni kama office ya hawa mabwana, kila kukicha tunaona ma-star wa basketball wanatembelea magogoni, tukienda mtaani tunaona volunteers wanamwagwa! Ukienda mbugani ndio basi tena. Ili mradi kama taifa hatumui bila kuona mmarekani.
 
Yaani Wamarekani ni majangili wa kutupwa. Si watu wazuri hata kidogo. Ukiacha barabara waliyojengwa huko kusini kwa ajili ya kurahisisha kuiba uranium yetu, miradi yao mingi ndani ya TZ iko kwenye kutusambazia virusi vya ukimwi na viwanda vyao vya kutengeneza vyandarua huko Arusha. They are evil people....

It is true mbona wasifanye miradi ya mikubwa ya umwagiliaji?Processing industries tuka- package bidhaa zetu hapa? vyandarua vya nini?kikichanika watatoa kingine? Watu wawe na mshiko watanunua vyandarua wenyewe.
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom