mbwigule
JF-Expert Member
- Jan 21, 2012
- 235
- 103
Tangu niliposikia Prof. huyu kateuliwa kushika wizara nyeti hiyo nilijua kazi ndiyo imeanza! namfahamu kama mtu mwenye msimamo na mchukia rushwa ila nilimwonea huruma kwa vile alikabiliwa na ugumu katika utekelezaji wa majukumu yake akiwa na timu iliyooza. Uozo wote ndani ya TANESCO na Wizara ya madini ukiwemo wa mikataba mibovu ya madini ni maslahi ya viongozi wa chama chake na serikali iliyopo madarakani. Tusubiri, tuone.Kuna sekeseke linaendelea chini kwa chini ambalo likifumuka linaweza kupelekea Prof. Muhongo kuhamishwa Wizara au kupoteza nafasi yake.
Kifupi ni kuwa jamaa kaingilia maslahi ya wakubwa na kwa sasa mambo si mambo. Tutayasikia ya kusikika muda si mrefu.