Posho na Mishahara ya wabunge...

NI lazima kufikiri kwa makini sana kuhusu hili. Kinachopigiwa kelele siyo stahili za wafanyakazi bali ni posho za vikao ambao wanafaidika nazo wachache na sio wafanyakazi wote. Posho kama per diem ni lazima kwa wafanyakazi wote wanapotoka nje ya vituo vyao vya kazi hizi hata wao chadema wanazipokea mpaka sasa hivi bungeni na hawana tija ya kuziondoa. Imagine zikiondolew posho za vikao kwa watumishi wote wa serikali je tutaokoa mabilioni mangapi na tutakuwa tumeisaidia serikali kubana matumizi ya fedha zake kwani serikali zote ulimwenguni kwa sasa wanapunguza matumizi yasiyo ya lazima ili kuendana na hali ya uchumi wa kidunia. Pesa hizi tunaweza kuzielekeza katika kilimo na zikafanya mapinduzi makubwa ya kijani na tukasahau kabisa shida ya njaa hapa nchini.
 
Twanga kote kote hadi kieleweke, magamba yatavulika hadi pesa zirudi kwenye mkondo wa umma. Sera za kweli zinazogusa utaifa ndizo zinazokubalika.
 
Inasikitisha sana kuona kwamba mjadala wa Posho za Wabunge na Watumishi wa Serikali umechukua muda mwingi sana katika Bunge la bajeti na hii na vyombo vya Habari Tanzania,mimi nasikitika sana,naona Taifa letu linaelekea pabaya,na Wanasiasa wetu wamfilisika sana Mawazo

Hivi ni kweli Posho za Wabunge na Watumishi wa Serikali ndio sababu ya msingi ya Umaskini wa Taifa letu la Tanzania?
Mbona wanasiasa mumefilisika mawazo kabisa,kabisa kabisa ,kabisa,mnasahau kujadili mambo muhimu na kero za wananchi mnajadili Posho usiku na Mchana?Posho ni Pesa,ni kweli kwamba Posho ndio sababu la Umaskini wetu?kwelli ninyi Wabunge,wasomi na Ma Dr wengine ma Prof. Mnatuambia kwamba POSHO,POSHO,POSHO,POSHO ndio tatizo la Umaskini wa Watanzani? Mimi nasmea,mumefiliska mawazo! Tatizo la Tanzania ni:-

1.Katiba ya kizamani na Sheria mbovu zilizopitwa na Wakati.

2.Elimu Duni
Hatujawekeza kwenye Elimu vya kutosha na tumekimbilia kwenye Kilimo kwanza!Je Watu wasio na Elimu wanaweza kulima,kufuga na kufanya Uvuvi wa Kisasa?Je '' Si Elimu Kabla na Kilimo Kwanza''? au ''KILIMO KWANZA''!!!!

3.Uzalishaji Duni
Nchi yetu haizalishi,Viwanda vimeuzwa kwa wawekezaji wezi,Sekta ya Kilimo haijapewa kipaumbele na uzalishaji ni Duni

4.Rushwa na ufisadi

4.Wizi wa Rasilimali za Taifa Letu
Wawekezaji matepeli wanachimba madini yetu,dhahabu na kupora Mabilioni ya Utajiri wa Taifa letu na tuawasamehe Kodi juu,nadhani Posho ni kama tone la maji katika bahari ya wizi unaofanywa wa wawekezaji kwenye Sekta ya Madini na zinginezo

5.Ukosefu wa Ajira kwa Vijana
Kutokana na sababu nilizotaja hapo (1 hadi 4) imepelekea ukosefu mkubwa wa Ajira kwa mamilioni ya Vijana wa Kitanzania,Viwanda vimekufa,Kilimo Duni,Sekta Binafsi haikui,Ajira zitatoka wapi?Maelfu ya Vijana hawana Ajira!

6.Huduma za jamii zilizo Duni,kama maji,miundombinu ya usafiri,Makazi,Hospitali na Madawa na nk
Mamia ya akina mama wanafariki kwa kukosa Huduma bora za Afya hasa vijijini,Hospitali hazina Dawa,Foleni,Usafiri usio wa Uhakika( mfano wa Reli umekufa)

7.Mfumuko wa Bei na kupanda kwa Gharama za Maisha amabako si kwa kawaida

Wabunge,jadilini Wezi wa Madini yetu,je Madini tunaibiwa Shs. Ngapi?What is Posho za Wabunge Bwana!!!!!! Tuambieni nani anachimba Chuma Chetu,tuambie Dhahabu inapatikana kwenye Migodi yetu?Tuambieni mliowasamehe Kodi wamemsaidiaje mama Swema wa Kijiji cha Tujitegemee kule masasi Mtwara au kwigineko?Mnajadili Hoja za Posho?Posho?This is non-sense!
 
Vikao vyenyewe vya posho ni vya kishkaji. Wake za watu wazuri wazuri, undugunise, pombe friends ndio wa kwanza kupewa barua za vikao. Mama yupo Idara ya misitu lakini anaitwa kwenye vikao vya HAKI ELIMU kuhudhuria kisa kuna posho. Huu mchezo wa posho posho unatakiwa utazamwe kwa kina. Sipendi kuongea pumba lakini inafika mahala pakujiuliza kwanini iwe mimi Tu, Hii nitabia mbaya na yakibinafsi ya mtu kujali tumbo lake pasipo kujali wale wanaomzunguka ambao ni wengi.
Tujaribu kubadirika na kuwa na roho za kibinadamu kuliko kukaa maofisini na kulalamikia hoja hii ya kuondoa hizi posho au hata kuzipunguza. Kwa mwanamapinduzi yoyote hili ataliona kama changamoto.
 
pinda ni mnafiki kwa nini anatetea hizo posho? huyo si mwenzetu tena
Pinda kumuongelea hapa ni sawa na kufufua mtu aliyekufa na kumshtaki. Tulishamuongelea sana kwa post`s zilizokwesha pita na udhaifu wake upo wazi. Yupo kwa maslahi ya waliomteua na si kwa maslahi ya taifa. Hawa ni kati ya lile kundi tunalosubiri liteketee ili tuweze kuanzisha Taifa lenye neema.
 
Salamu wana Jamii wenzangu!
Tanzania inaadhimisha miaka 50 ya Uhuru huku Taifa letu likiwa bado linaogolea kwenye wimbi kubwa la umaskini.Kumekuwa na juhudi za wazi kabisa za serikali za awamu zote toka awamu ya Kwanza hadi hiii ya nne kuapambana na Umaskini,naweza kusema juhudi hizi zimezaa matunda kwa kiasi Fulani lakini Ukweli umebaki pale pale kwamba nchi yetu na wanachi bado tu maskini sana.

Kwa majuma kadhaa sasa kumekuwa na mdadala mkali ndani ya Bunge la Bajeti la mwaka 2011,Wanasiasa na Vyama vya kijamii,kuhusiana na uhalali wa Posho wanazolipwa Wabunge na Watumishi wa Serikali na Taasisi za umma katika kipindi hiki cha mdororo wa Kiuchumi na unaoikumba Dunia na Taifa letu la Tanzania,kwa mtizamo wangu walioanzisha mjadala huu wana haki ya kutoa maoni yao kwakuwa nchi hii ni huru na tunaheshimu mawazo ya watu.Nasikitika sana kwa hoja nyepesi za kujibu hoja hii zinazotolewa na baadhi ya wanasiasa na viongozi wa andamamizi wa Serikali na mihimili ya Utawala wan chi yetu!

Baada ya kufuatilia kwa kina mjadala huu , mimi nimejiuliza swali moja tu,Ni kweli kwamba sisi watanzania Watanzania ya leo tunaoadhimisha miaka 50 ya Uhuru tukiwa Maskini tumegundua kwamba tatizo la Umaskini wetu ni Posho? Huu kweli si Mjadala wa Kipumbavu kwa Taifa maskini kama hili kuujadili wakati likiadhimisha miaka 50 ya Uhuru wake,huku sio kufilisika kisiasa na kifikra jamani!??
Tuwaambie watoto wetu kwamba Posho ndio suluhu ya matatizo linaikabili nchi yetu na tuwafundishe hivyo?
Mimi nasema,naomba mnisamehe mlio wakubwa kwangu,walimu wangu na wazee wangu,kama mnakaa kujadili Posho na mnasahau matatizo makubwa yanayowakabili Watanzani na sisi Vijana,mumefilisika sana kimawazo,mimi nasema Hasira ya Watanzania itawashukia muda si mrefu!!!Mbona mumeacha kujadili:

1.Wizi wa Rasilimali za Taifa Letu,Madini,Misamaha ya Kodi kwa Wawekezaji wababaishaji na Matapeli
Ninyi wabunge,kwanini Hamkatai Mikataba mibovu,kwanini mnanyamaza Kimya watu wanaiba Dhahabu zetu,wanachima Uranium Yetu,wanakula wanyamapori wetu,wanavuna Misitu yetu na kuuza magogo nchi zanje,wanavua Samaki wetu?wanatuacha sisi Maskini wa kutupwa na tunapiga miayoo na Maelfu ya Vijana wanakosa Ajira>>!!!! Hasira ya Vijana itawaka muda si mrefu!

Mbona HAMYAKATAI haya kwa nguvu zenu zote >?????Mnakataa Posho?Posho?What is Posho na watu wanachota Utajiri Mkubwa wa Taifa Letu mumenyamaza?mbona hamjakataa hilo?mnasema tu kwenye majukwaa siasa,onyesheni kwa vitendo,susieni Bunge siku moja mseme tunaenda kuangalia Dhahabu yetu inavyoibiwa na watu wetu wanavyoangamizwa migodini na kunyang’anywa Utajiri wan chi yao,mnajadili Posho,Posho,Posho,What is Posho ni sawa tone tu la maji kwenye Mirahaba ya Dhahabu na Almasi inayoibiwa na mko Kimya?!!!!This is Non-Sense,naomba muondoe mijadala hii ya Kipumbavu,mjadili mambo ya maana ya kuliokoa Taifa Letu la Tanzania dhidi ya Umaskini baada ya Miaka 50 ya Uhuru.

2.Elimu duni na mifumo mibovu ya Elimu
Mbona Elimu imepewa Kisogo?Mnakaa Kimya,mnashabikia Kilimo Kwanza ?Kilimo kwanzaaa ehhee?Cha kutegemea mvua?Etii yee,ma power Tila yaKilima Hekta 1000 na mvua hainyeshi,Mbolea Hakuna na Mkulima mwenyewe Mumemnyima Elimu na Mtaji wa Kulimia hana!!! This is Non-Sense!!! Huu ni Upumbavu wa Wanaotudanganya mabo ni Mabeberu wan chi za Magharibi!Hakuna Maendeleo ya Taifa lolote bila ELIMU!!! Ndio maana namuunga mkono kwa nguvu zote Mheshimiwa EL kwamba ’’ELIMU KABLA NA KILOMO KWANZA’’ hii ndio sera mbadala wake Hakuna.Mkulima apewe Elimu kabla ndipo afundishwe Kilimo cha Kisasa!!!!
-Mbona Wanafunzi wa Vyuo Vikuu mnawafukuza wakidai Haki yao?
-Mbona Mikopo haitoshi kuwawezesha kusoma bila shida?
-Mbona shule za Kata zimetelekezwa bila maabara na Vifaa
-Mbona Hakuna Nyumba za Walimu
-Mbona Walimu hawalipwi Posho zao na Mishahara ili kuwaongezea Tija ya kazi
-Mbona Shule hazina Maabara za Kutosha?

3.Huduma Duni za Jamii kama Maji,Hospitali ,Mafoleni ya Dsm.Usafiri wa Reli,Ndege Mbovu nk

4.Miundombinu Hafifu,Barabara na Umeme kama Mshumaa,kidogo umewaka mara umweiziam

5.Mfumuko wa Bei za Bidhaa masokoni,wala Pesa haina thamani tena!

6.Ukosefu Mkubwa wa Ajira kwa Vijana na Maslahi duni ya Watumishi walio katika Ajira katika Sekta Rasmi na Zisizo Rasmi

7.Rushwa na Ufisadi

8.Ukosefu wa Usalama wa Raia,Wizi na Unyang’anyi wa kutumia Silaha,Mabomu yanalipuka katika maghala ya Silaha za Majeshi yetu
9.Uchafuzi Mkubwa wa Mazingira unafanywa na wamwekezaji wababaishaji wanachimba Dhahabu yetu na kutuachia mashimo makubwa,vumbi kutapakaa angani,Misitu inavyunwa na watu wanakula hadi nyama za Swala na walisahau siku nyingi kula ng’ombe.

10.Umaskini mkubwa wa Kipato miongoni mwa Mamilioni ya Watanzania waishio Mijini na Vijijini

11.Makazi duni na Mipango Miji mibovu na unya’anyi wa Adhi yetu na Wageni

13.Kuongezeka kwa Kasi kwa Deni la Taifa na hivyo kutishia nchi yetu kufilisika kama nchi za Ugiriki na Hispania zinakoelekea sasa

14.Ukabila,Udini na Ubaguzi wa kila namna Vinashamiri kila kukucha

15.Muungano usio Imara,kila leo kurushiana maneno na tumesahau umoja na mshikamano wa Taifa letu

16.Haki za Bindamu zinadharauriwa,Msongamano wa Wafungwa Magerezana,Rushwa katika Mahakama,Udharirishaji watoto na Wanawake,watu kujichukulia madaraka mkononi

17.Katiba ya Kizamani na Sheria Kandamizi
Na mengine Meengii!

Haya na mengine meengi ndiyo yanasababisha Taifa letu liendelee kuwa Maskini kwa wakati tukiadhimisha Miaka 50 ya Uhuru,Wanasiasa/Asasi za kijamii na Wabunge wetu,tujadiri haya ???na tuwafundishe watoto wetu haya na tuache kujadili mambo madogo madogo kama Posho huku tukiacha Taifa letu likiangamia kwa Umaskini.Kujadiri Posho na Kuacha haya ni KUFILISIKA KWA MAWAZO.

Natoa hoja ya kufunga Mjadala wa Posho kuanzia leo!
 
Nduguzanguni mh aliyekuwa mtt wa mkulima na hapo zamani aliyekuwa mwenye huruma kwa wanyonge mpaka analia akiona wanyonge wanaonewa, alichosema kuhusiana na posho za wabunge kwamba wanaombwa na kwamba zinaishia Dodoma ni kweli kabisa ........ kwa tetesi nilizopata nikwamba changudoa maarufu na wakali wote wapo dodoma kipindi hiki cha bunge wanakula posho!!!!
 
Bora kama machangudoa hao, vijana wetu wa vyuo vilivyoko dodoma wasalimike maana ni nguzo ya taifa, hatutaki mashangii kuendelea kupake pale kusubiria wanafunzi na sasa wako busy na mitihani ya malizia mwaka,
 
Wabunge walazimishwa kulipa kodi Kenya
Mamlaka ya ushuru nchini Kenya (KRA) imeagiza kuwa wabunge wote walipe kodi kulingana na katiba mpya nchini humo.

Wabunge wanasema hawawezi kulipa kiasi hicho cha pesa

Mamlaka hiyo imewataka wabunge hao walipe malimbikizi ya kodi hiyo kutoka mwezi Agosti mwaka jana, wakati katiba mpya nchini humo ilipoidhinishwa.

Kulingana na makadirio ya KRA, kila mbunge anatakiwa kila dola 10,000 kutoka mshahara wake. Takwimu zilizopo zinaonyesha kuwa wabunge nchini Kenya wapo kwenye orodha wa wawakilishi wanaolipwa mishahara mikubwa zaidi barani Afrika.

Agizo hilo la mamlaka ya ushuru hata hivyo limepingwa vikali na baadhi ya wabunge wanaosema kuwa huenda wakashindwa kumudu maisha kufuatia hatua hiyo wasiokuwa wakiitarajia. Akizungumza na BBC, Waziri wa Maji ambaye pia ni mbunge wa eneo la Kitui, Bi Charity Ngilu amesema kuwa kulipa pesa hizo itakuwa kibarua kigumu sana.

"Tulipoingia bunge tulielezewa pesa ambazo tutalipwa katika kipindi cha miaka mitano kisha wengi wakachukua mikopo, sasa kuja sasa hivi na kutuambia tulipe, itakuwa vigumu sana kwa kuwa hatuna biashara" alisema Bi Ngilu.

Wabunge wengi walitegemea kuwa agizo hilo kuwa walipe kodi litaanza kutekelezwa baada ya uchaguzi ujao mwakani. Kwa sasa wanamakubaliano na Rais Kibaki kuwa wasilipe kodi hiyo lakini hakuna muafaka ikiwa hali itakuwa hivyo. Mwaka jana wabunge waliongeza mishahara yao hadi dola 126,000.

Uamuzi huo ulikemewa vikali na raia nchini humo ambao wengi wanakipato cha chini ya dola moja kwa siku.
-----------------------------------------------------------------------

Hebu tuongozane hapa Tanzania: Mshahara wa Mbunge unakatwa kodi au wanakwepa kwa vipato vyao kuitwa posho?
 
jamani kwani wastaafu muhimu katika nchi hii ni wanajeshi peke yao?halafu kibaya zaidi akistafu anakabidhiwa kitengo mkuu wa wilaya mkuu wa mkoa mwenyekiti wa kamati flani sio kwa malipo yaleyale malipo mengine tena eti wanawaogopa kusitisha posho zao tehe tehe wana nguvu gani hawa wakati hawana sauti tena jeshini mbona waliodai uhuru wametupwa,makumbusho ya jemedali mkwawa kichefuchefu nyie wanakumbatia watu waliokuta amani imeshatengenezwa
 
WAKATI hoja ya kufutwa posho za vikao vya wabunge ikivuruga hata chama kinachodai kubuni hoja hiyo cha Chadema, baadhi ya wabunge wamependekeza bajeti ya masurufu hayo iongezwe kwa madiwani ili ‘wawe kama wabunge’.

Mbunge wa Viti Maalumu, Zarina Madabida (CCM) ndiye jana aliyeanzisha hoja ya kutaka wawakilishi hao wa wananchi katika halmashauri, waboreshewe maslahi pamoja na kuwepo hoja ya Serikali kutakiwa kujibana katika matumizi.

Madabida alitaka madiwani nchi nzima wapewe posho na kukopeshwa vyombo vya usafiri kwa maelezo kwamba ndiyo namna ya kuwafanya watekeleze majukumu yao vizuri ya kusimamia maendeleo kwenye maeneo yao.

Alisema diwani ni kiongozi muhimu katika kusimamia utekelezaji wa mipango yote ya kata na kumsaidia Mbunge ambaye naye anapewa posho kumudu majukumu yake.

Mbunge huyo alisema madiwani wanapata posho ya Sh 120,000 ambayo kwa maelezo yake ni kidogo ikilinganishwa na majukumu makubwa waliyonayo ya kusimamia maendeleo ya wananchi katika maeneo yao.

Alihoji kama Serikali haioni umuhimu wa kuongeza viwango vya posho za madiwani kulingana na kupanda kwa gharama za maisha.

Mbunge wa Ludewa, Deo Filikunjombe (CCM) alikwenda mbali na kuelezea kushangazwa na mfumo wa kuwanyima posho madiwani ulivyo wakati walikuwa pamoja wakati wa kampeni.

Alihoji iweje wakati wa kampeni wagombea wanatumia falsafa ya mafiga matatu; lakini baada ya uchaguzi figa la kwanza Rais, Serikali inalijali na figa la pili wabunge pia wanapewa posho nzuri lakini figa la tatu ambalo ni diwani linatelekezwa.

Naye Mbunge wa Kisesa, Luhanga Mpina (CCM) aliwahamasisha wabunge kutopitisha bajeti ya Waziri Mkuu, itakapowasilishwa bungeni keshokutwa, endapo hatatenga fedha kwa ajili ya malipo ya mishahara kwa madiwani.

Mpina akichangia hotuba ya bajeti juzi jioni, aliwaomba wabunge kutopitisha bajeti ya Waziri Mkuu mara itakapowasilishwa bungeni endapo haitakuwa imetenga fedha za mishahara ya madiwani.

Alisema ,kwa muda mrefu sasa Serikali imekuwa ikitoa ahadi ya kuanza kuwalipa mishahara madiwani lakini ahadi hiyo imekuwa haitekelezeki hatua ambayo mbunge huyo alisema inakwamisha usimamizi wa shughuli za maendeleo.

Mpina alisema hakuna sababu za msingi za kuifanya Serikali kushindwa kuwalipa mishahara madiwani huku ikifahamu kuwa madiwani ndio wasimamizi wa karibu zaidi wa shughuli za maendeleo katika ngazi za kata kuliko hata wabunge.

Akijibu maswali hayo ya wabunge, Naibu wa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Aggrey Mwanry alisema mbali na posho ya Sh 120,000, diwani pia anapokea Sh 40,000 kama posho ya kikao.

Alisema pia kuna posho ya madaraka kwa wenyeviti na mameya na viwango vyake ni kati ya Sh 100,000 na Sh 350,000.

Naibu waziri huyo alisema ni dhahiri kuwa utekelezaji wa mpango wa kupeleka madaraka kwa wananchi umesababisha rasilimali nyingi kupelekwa katika ngazi ya Mamlaka za Serikali za Mitaa na hivyo kuhitaji usimamizi wa karibu chini ya madiwani.

Alisema azma ya Serikali ni kuendelea kuboresha posho za madiwani kadri hali ya uchumi itakavyoruhusu. “Ndugu wabunge naomba mtambue kuwa serikali ni sikivu na itaendelea kutekeleza azma hiyo kama ilivyokusudia.”

Juzi wabunge wa Chadema wanadaiwa kushindwa kufikia muafaka wa kutafuta ujasiri wa kukataa kuchukua posho na kujikuta wakikubaliana na hoja wa Waziri Mkuu Mizengo Pinda, kuwa hawana ujasiri huo na wengi wao wanasema hawataki huku kimoyomoyo wakitaka.
 
Back
Top Bottom