Posho na Mishahara ya wabunge...

Sichochei wala sina mtimanyongo na mtu yeyote. Sipingi posho za vikao kuondolewa kwa wabunge na wafanyakazi wengine wa serikali. Ila sasa kusema kweli wafanyakazi wengi wa serikali wananufaika sana na hizi posho za vikao. Kuna viongozi (wakubwa), kuna wahudumu na kuna wataalamu (sekretariat) wote hawa kukiwa na vikao nao wanapata posho kusupliment mishahara yao. Pia kuna meal allowance na extra duty (siyo overtime) allowance; sijui kuna mtu anajua zinalipwalipwaje. Wafanyakazi kwa sasa wana chuki na mtu aliyeanzisha hili suala kabla ya kuhakikisha kuwa mishahara yao inapanda kabla ya kuondoa posho za vikao ambazo wanasema huenda zikafuatiwa na kuondolewa kwa posho zingine kama meal allowance na extra duty allowance.

Mkuu hao wanaolalamika ni wale wenye channeli zao. Nimefanya kazi mikoani huku zaidi ya miaka 19 . Kama kuhudhuria vikao vyenye kupeana posho nadhani haviwezi kuzidi vikao 6 au 7.
Fahamu kwamba hata hao wenye kulalamika si zaidi ya 1/10 ya wafanyakazi wote wenye kuhudhuria vikao. zaidi ni wakuu wa vitengo. Na ikitokea kasemina basi jua ni mara moja kwa mwaka tena fedha za misaada toka USAID , Danida, SIDA GTz na donars wengine. Na mpaka kikao chenye kutoa posho kikafika kule Nanyumbu vijijini tayari wizarani watu walisha chota sana. Nyie mnaambulia 5,000 au 10,000 kwa siku.
SASA ili wafanyakazi waweze kuongezewa mishahara ni lazima hivi vi mianya vyenye kuwafaidisha hawa 1/10 ya wafanyakazi pamoja na wabunge vikusanywe na kuwekwa kwenye kapu moja la mishahara. Na si hili la posho zawabunge tu bali hata hizi per diem za rais mawaziri na wengine wenye kufanana na hao lazima ziguswe na kufanyiwa tathmini kuona kama pia zinaweza kupunguza tabaka lililopo kati ya maskini na tajiri.
 
Kimbunga toa andishi lako hapa javini tulione. Walimu ndio watumishi wengi zaidi nchini, wangapi wanapata sitting allowance kwa mwezi, kwa mwaka? wewe utakuwa afisa mipango tu wa Halmashauri fulani umeshaanza kutetemeka. Hunalo hilo!
 
Kimbunga toa andishi lako hapa javini tulione. Walimu ndio watumishi wengi zaidi nchini, wangapi wanapata sitting allowance kwa mwezi, kwa mwaka? wewe utakuwa afisa mipango tu wa Halmashauri fulani umeshaanza kutetemeka. Hunalo hilo!

Angalia Jigsaw alivyonena hapo juu. Andishi kama unalitaka nitakupa anuani ya chuo na reference ya chapisho ukalitafute usome uone. Hapa nilipo naendelea na utafiti kuhusu posho mbalimbali zinazolipwa serikalini ili serikali iweze kuzi consolidate kwenye mishahara. Huenda nikapendekeza mishahara ya serikali kima cha chini kiwe Shs. 750,000.00 na siyo shs. 315,000.00
 
POSHO zitaibua mengi!! POSHO Zinatugawa!!

Nadhani wewe ni mmoja ya wale vichwa maji ambao hawelewi POSHO ambazo CDM wanataka ziondolewe!

Basi ni hivi na ukawaeleweshe pia na wafanyakazi wenzako wa kada za chini ila usiwadanganye maana wewe inaonyesha huwa unapata hizi posho ndo maana unatetea, imekula kwako!

1. POSHO zinzotakiwa ziondolewe ni pesa wanazopata watumishi kwa kuhudhuria vikao
2. POSHO wanazopata watumishi wanapohudhuria semina/washa ukiondoa pesa ya kujikimu kwa sababu wamesafiri kwenda kwenda mbali ya kituo cha kazi hivyo wanahitaji hela ya kula,kulala,kusafiri ambayo wanatakiwa kuiretire wakirudi na pengine kiasi fulani kwa ajili ya usumbufu ambacho huwa ni kama Dola 50-80 kwa siku kwa private companies na hiki huwa hawa-retire.

Tatizo kubwa la hizi posho za vikao wanapata wakubwa tu na wafanyakazi wa kada za chini ambao ndo wengi wengi haziwahusu kabisa kwa sababu huwa hawahudhurii vikao!

Posho za extra duty na meal kwanza ni msaada serikali hupewa na wahisani ili kuboresha masilahi ya watumishi umma angalau wawe na uhakika wa kupata lunch ili wafanye kazi kwa ufanisi. Hii ni sawa na kutoa uji na chakula cha mchana kwa watoto wa shule za msingi.

Hizi zinawahusu watumishi wote hivyo hazitaguswa na wala siyo pesa ya serikali kwa sasa hivi kwa ufahamu wangu.
 
Nakubaliana kabisa na wewe. Lakini pia huko tanroads kuna watumishi wa chini ambao wanapokea hizo posho. Mimi hapa naongelea kurekebisha vima vya chini si kwa watu kama hao ambao nasikia wanalipwa mamilioni.

Mheshimiwa tofauti na ilivyo sasa posho za vikao zikifutwa hata maamuzi serikalini na mashirika ya umma yatafanyika kwa haraka sana. Hali ilvyo hivi sasa huna pesa huwezi kuitisha kikao, mfano tenda imetangazwa pesa za mradi ziko tayari kama taasisi haina pesa za O/C kikao hakitaitishwa na hii itapelekea mradi kuchelewa kuanza ingawaje pesa zipo. Mfano mwingine kwenye mashirika yetu ya umma, kikao cha bodi kikiitishwa wale wajumbe wanaangalia zile agenda, wanazigawa mara mbili na kuamua leo tujadili hizi kesho au siku ingine tujadili hili kwenye "Kikao cha dharura", hapo watakula na kupokea sitting allowance na perdiem zao, bado kikao kingine kitagharamiwa kwa kiasi kile kile. Isitoshe kuna na kamtindo cha kuanza na vikao vya kamati siku moja au mbili kabla ya "Full Board" huu nao ni utafunaji tuu wa rasilimali za umma. Huku sekta binafsi ukihudhuria kikao sana sana utaambulia kuokoa pesa ambayo ungenunulia Lunch, lakini mambo yanakwenda kwa kasi ya karne ya 21. Najua wengi wamezoea kuishi kwa hizi posho lakini baada ya muda mtazoea kuishi kwa mishahara yenu na kama mna matumizi yasiyo ya lazima kama nyumba ndogo mtawaachia wasio na wake waoe. Niliyemkera kwa haya mawazo yangu namsihi anisamehe.
 
NATOA RAI KWA WATUMISHI WOTE WA SERIKALI KUTOIPIGIA KURA CDM 2015. HAKUNA SERIKALI AMBAYO HAITOI MARUPURUPU KWA WATUMISHI WAKE, HII NI KWA AJILI YA KUONGEZA KIPATO ZAIDI YA MSHAHARA ILI KUWEZA ANGALAO KUPUSH SIKU KUELEKEA MWISHO WA MWEZI. SERIKALI AMBAYO ITAKUWA HAITOI POSHO (MOTISHA) KWA WATUMISHI WAKE HIYO HAITUFAI. WAO (viongozi) WANA UHAKIKA KWA KUWA WATAKUWA NA MISHAHARA MIKUBWA HIVYO HATA KAMA WATAKOSA POSHO ZA VIKAO KWAO SI MBAYA. SASA SISI WA CHINI TUNASHABIKIA TU, LAKINI ISHU ITAKAPOTUGEUKIA TUTAJUA MBIVU NA MBICHI.
 
Nadhani wewe ni mmoja ya wale vichwa maji ambao hawelewi POSHO ambazo CDM wanataka ziondolewe!

Basi ni hivi na ukawaeleweshe pia na wafanyakazi wenzako wa kada za chini ila usiwadanganye maana wewe inaonyesha huwa unapata hizi posho ndo maana unatetea, imekula kwako!

1. POSHO zinzotakiwa ziondolewe ni pesa wanazopata watumishi kwa kuhudhuria vikao
2. POSHO wanazopata watumishi wanapohudhuria semina/washa ukiondoa pesa ya kujikimu kwa sababu wamesafiri kwenda kwenda mbali ya kituo cha kazi hivyo wanahitaji hela ya kula,kulala,kusafiri ambayo wanatakiwa kuiretire wakirudi na pengine kiasi fulani kwa ajili ya usumbufu ambacho huwa ni kama Dola 50-80 kwa siku kwa private companies na hiki huwa hawa-retire.

Tatizo kubwa la hizi posho za vikao wanapata wakubwa tu na wafanyakazi wa kada za chini ambao ndo wengi wengi haziwahusu kabisa kwa sababu huwa hawahudhurii vikao!

Posho za extra duty na meal kwanza ni msaada serikali hupewa na wahisani ili kuboresha masilahi ya watumishi umma angalau wawe na uhakika wa kupata lunch ili wafanye kazi kwa ufanisi. Hii ni sawa na kutoa uji na chakula cha mchana kwa watoto wa shule za msingi.

Hizi zinawahusu watumishi wote hivyo hazitaguswa na wala siyo pesa ya serikali kwa sasa hivi kwa ufahamu wangu.

Mkuu wewe ndio hujui kwa kuwa unachanganya private sekta na Serikali. Serikalini nani kakuambia kuna incidentals ya dola 50 ukiwa ndani ya nchi? Duh ingekuwa hivyo basi ingekuwa safi sana. Per diem ya dereva kwenda arusha ni Shs. 50,000.00 hiyo dola 50 ya incidentals imetoka wapi? Upo?

Kuhus meal allowance na extra duty allowance siyo kwamba zinalipwa kwa wafanyakazi wote. Hii inategemea kazi uliyofanya. Hii siyo sawa na ration allowance wanayolipwa polisi kama flat rate. Uliza uambiwe siyo kukurupuka na kuanza kuaita watu vichwa maji.
 
NATOA RAI KWA WATUMISHI WOTE WA SERIKALI KUTOIPIGIA KURA CDM 2015. HAKUNA SERIKALI AMBAYO HAITOI MARUPURUPU KWA WATUMISHI WAKE, HII NI KWA AJILI YA KUONGEZA KIPATO ZAIDI YA MSHAHARA ILI KUWEZA ANGALAO KUPUSH SIKU KUELEKEA MWISHO WA MWEZI. SERIKALI AMBAYO ITAKUWA HAITOI POSHO (MOTISHA) KWA WATUMISHI WAKE HIYO HAITUFAI. WAO (viongozi) WANA UHAKIKA KWA KUWA WATAKUWA NA MISHAHARA MIKUBWA HIVYO HATA KAMA WATAKOSA POSHO ZA VIKAO KWAO SI MBAYA. SASA SISI WA CHINI TUNASHABIKIA TU, LAKINI ISHU ITAKAPOTUGEUKIA TUTAJUA MBIVU NA MBICHI.
Kwani nyie watumishi wa serikali mko wangapi katika nchi hii?Wangapi kati yenu wana process malipo ya wazee wetu wa east africa?Wangapi kati yenu wana dhoufisha utendaji wa serikali?Wangapi wako kama wewe ambao watakuwa classed kama Unconscious Incompetence ( ignorant)?
 
hakuna ubishi we ni Nape squad, mm niko serikalini pia lkn swala la posho naunga mkono hoja litolewe kabisa,vikao vingi havina tija, bora zipelekwe kuboresha mashule,kama madawati,vifaa vya maabara, hospitali nk na kama kodi itakusanywa vema tuongezewe mishahara, Suala la fedha za kujikimu, uhamisho hizo ni stahili zako hata hela za likizo ni stahili zako sio posho.nasema tena POSHO zifutweeeeee.kama ww ni mwizi pia na huna uchungu na wananchi basi hufai ktk ufalme wa Tanzania.



NATOA RAI KWA WATUMISHI WOTE WA SERIKALI KUTOIPIGIA KURA CDM 2015. HAKUNA SERIKALI AMBAYO HAITOI MARUPURUPU KWA WATUMISHI WAKE, HII NI KWA AJILI YA KUONGEZA KIPATO ZAIDI YA MSHAHARA ILI KUWEZA ANGALAO KUPUSH SIKU KUELEKEA MWISHO WA MWEZI. SERIKALI AMBAYO ITAKUWA HAITOI POSHO (MOTISHA) KWA WATUMISHI WAKE HIYO HAITUFAI. WAO (viongozi) WANA UHAKIKA KWA KUWA WATAKUWA NA MISHAHARA MIKUBWA HIVYO HATA KAMA WATAKOSA POSHO ZA VIKAO KWAO SI MBAYA. SASA SISI WA CHINI TUNASHABIKIA TU, LAKINI ISHU ITAKAPOTUGEUKIA TUTAJUA MBIVU NA MBICHI.
 
Mheshimiwa tofauti na ilivyo sasa posho za vikao zikifutwa hata maamuzi serikalini na mashirika ya umma yatafanyika kwa haraka sana. Hali ilvyo hivi sasa huna pesa huwezi kuitisha kikao, mfano tenda imetangazwa pesa za mradi ziko tayari kama taasisi haina pesa za O/C kikao hakitaitishwa na hii itapelekea mradi kuchelewa kuanza ingawaje pesa zipo. Mfano mwingine kwenye mashirika yetu ya umma, kikao cha bodi kikiitishwa wale wajumbe wanaangalia zile agenda, wanazigawa mara mbili na kuamua leo tujadili hizi kesho au siku ingine tujadili hili kwenye "Kikao cha dharura", hapo watakula na kupokea sitting allowance na perdiem zao, bado kikao kingine kitagharamiwa kwa kiasi kile kile. Isitoshe kuna na kamtindo cha kuanza na vikao vya kamati siku moja au mbili kabla ya "Full Board" huu nao ni utafunaji tuu wa rasilimali za umma. Huku sekta binafsi ukihudhuria kikao sana sana utaambulia kuokoa pesa ambayo ungenunulia Lunch, lakini mambo yanakwenda kwa kasi ya karne ya 21. Najua wengi wamezoea kuishi kwa hizi posho lakini baada ya muda mtazoea kuishi kwa mishahara yenu na kama mna matumizi yasiyo ya lazima kama nyumba ndogo mtawaachia wasio na wake waoe. Niliyemkera kwa haya mawazo yangu namsihi anisamehe.

Mbona hatuelewani? Mimi naongelea posho zote za watumishi wa serikali ili tuzijadili kwa ujumla wake. Hivi leo tukitoa sitting allowance tukaona inafaa na kesho ikaibuka ya extra duty tuanze kulumbana tena? Baada ya hapo tulumbane kwa meal allowance? Mimi nataka tuliongelee hili suala katika muktadha wa maslahi ya watumishi wa umma/serikali wenye vipato vya chini ambao hutumia posho kama supplement ya kipato. Kila mtu anataka mshahara mzuri, watu hawataki posho. Serikali ipandishe mishahara iondoe poshe zote ambazo hazina mashiko iache per dier.

Hilo la vikao vya bodi sina comment kwa kuwa sijui kama bodi ambazo members wao siyo executive na hawalipwi mishahara itakuwaje posho za vikao zikiondolewa? Nadhani kwa bodi inatakiwa standardization huko serikalini. Kwenye sekta binafsi kuhusu boadi najua wanalipana kufuru. Kuna bodi kikao chake kimoja ni Million na nusu. Hilo siliongelei. Tuongelee pesa za walipa kodi.
 
Vijana wa Nape hao.Hata hivyo kwani mko wangapi ambao mnanufaika na hizi posho haramu?Kwanza we mtoa mada siyo mtumishi wa serikali, wewe uko kwenye payroll ya Nape.
 
Naomba wabunge wafutiwe posho(za vikao vya bunge) na badala yake ziende kwa watendaji kama madaktari,manesi,walimu,mahakimu na watendaji wa vijiji!

Kama mtumishi wa serikali naunga mkono hoja ya zitto.
 
By ?In2EastAfrica? - Sun Jun 19, 9:01 pm

??0? Comments?

55 views

?

While some Members of Parliament from the opposition camp have asked for a review of their allowances, which they claim are colossal, it has been reliably established that the payments are actually the collateral that enabled them to secure bank loans.

?

‘Daily News’ investigations have found that the majority of MPs, from both CCM and the Opposition, took loans ranging from 60m/- to 200m/- from CRDB and NMB banks whose final deductions would be due in 2015 when their tenure expires.

Last week, the Prime Minister, Mr Mizengo Pinda, defended the allowances paid to MPs, saying much as they were seen to be mouth-watering on paper they in actual fact only cover a small fraction of expenses the legislators are incurring to make them discharge their duties smoothly.

Ironically, two top CHADEMA leaders, who have been vocal and championed the debate to have MPs sitting allowances slashed, are among the biggest creditors. One has taken a 196m/- loan and another 100m/- both from CRDB Bank.

Records show that each MP (Daily News is in possession of the long list of the creditors) gets a 2,305,000/- monthly salary plus 5,115,000/- as constituency allowance, making the total deductible pay to 7,420,000,000/-.

The documents indicate that 883,000/- is deducted every month for five years to cover the 45m/- personal car loan each MP was advanced and a further 588,000/- paid as government taxes. However, the package does not cover per diem and sitting allowances which are only paid if an MP has attended Bunge sessions.

“So, the claim by the opposition MPs that they want the sitting allowances slashed is purely a publicity stunt,” said an impeccable source. The source, who preferred anonymity, said that the legislators, who are beneficiaries of the bank loans whose guarantors are the office of the National Assembly, are not allowed to divert them to another account without a written consent by the three parties.

For example, a document from NMB shows that a 200m/- loan attracts a monthly deduction of 19,815,340/- if it is to be paid within one year, 10,183,540/- ( for 24 months), 7,177,760/- (36 months), 5,722,600/- (48 months) while the same package is charged 4,871,740,000/- per month in a five-year period.

When contacted for comment on Sunday, the Acting Clerk, Mr John Joel, said that bank guarantees are only given to loans whose source of income must come from payments made by the National Assembly.

“The National Assembly does not guarantee personal loans by MPs who use other collaterals apart from salaries and some other allowances,” he said. On June 7, this year, Mr Zitto Kabwe Kigoma North – Chadema) wrote to the Parliament Clerk asking for a total ban on the sitting allowance, which he said was a misuse of public funds. He claimed that such allowance was uncalled for, adding that attending sessions was part of his official duties, thus not deserving to be paid.

However, he instructed the House Clerk to channel his sitting allowance through Kigoma Development Initiative (KDI) of which he is the Chairman of the Board of Trustees until a new system to permanently slash the payment has been put in place.

A number of Chadema MPs told this paper here on Friday last week that they disagreed with their fellow MP on slashing the allowances.

They said that Mr Kabwe was advancing his personal views to gain political gains while the party is heading towards picking a presidential candidate for the 2015 general elections. Last week, the Prime Minister, Mr ?Mizengo Pinda?, defended the allowances paid to MPs, saying much as they were seen to be mouth-watering on paper they in actual fact only cover a small fraction of expenses the legislators are incurring to make them discharge their duties smoothly.

Meanwhile, the National Assembly session resumes here on Monday morning with a debate on the 2011/12 budget estimates.

Source ?Tanzania Daily News
 
headline_bullet.jpg
Wapinzani waitega serikali
headline_bullet.jpg
Wasubiri ufafanuzi, kutoa msimamo

Mgaya(18).jpg

Msimamo wa Tucta umetolewa na Katibu Mkuu wake, Nicolaus Mgaya

Moto wa kupinga posho wanazolipwa wabunge za kuhudhuria vikao umeendelea kushika kasi na sasa Shirikisho la Vyama Huru vya Wafanyakazi (Tucta) limeungana na kambi ya upinzani kuzipinga. Msimamo wa Tucta umetolewa na Katibu Mkuu wake, Nicolaus Mgaya, ambaye ametaka kuondolewa kabisa kwa posho hizo na nyingine zinazolipwa kwa maofisa wa serikali kwa kuwa haziwanufaishi wananchi walio wengi.

Akizungumza na NIPASHE, Mgaya alisema kuwa hata kama suala hilo lipo kisheria, lakini sheria inaweza ikabadilishwa wakati wowote ili fedha hizo zikaelekezwa katika miradi ambayo itakuwa na manufaa kwa Watanzania wote badala ya sasa ambapo kundi dogo la watu wasiozidi asilimia mbili ya watanzania wote ndilo linalofaidika na posho hizo. "Kwa mfano, katika bajeti ya safari hii, kiasi cha Sh. bilioni 987 zimetengwa kwa ajili ya kulipana posho na posho kama hizi mara nyingi wanalipwa maofisa wa ngazi za juu serikalini kuanzia ngazi ya ukurugenzi na kuendelea ikiwa ni pamoja na wabunge," alisema.

Alifafanua kuwa ikiwa posho hizo zitaondolewa na kuelekezwa kwenye miradi ya maendeleo kama vile afya, elimu, maji na kilimo, thamani ya fedha hizo itakuwa ni yenye tija kubwa zaidi kwa kuwa itawagusa wananchi wengi na hasa maskini. Aidha, Mgaya aliitaka serikali kukifanyia kazi kilio cha Watanzania walio wengi cha kuhakikisha kuwa, posho hizo zinaondolewa kwa kuwa tayari hata baadhi ya mataifa wafadhili yameshaanza kuulizia juu ya suala hilo.

"Wiki hii (wiki iliyopita) tulikuwa na ugeni wa Rais Mstaafu wa Ujerumani, Profesa Horst Kohler, moja ya nchi ambazo hutupa misaada sisi watanzania na alihudhurua mdahalo mmoja uliofanyika hapa Dar es Salaam. Katika Mdahalo huo, naye aliligusia suala hili la posho kwa kuwa fedha za misaada wanazotupa zinatoka katika mifuko ya walipa kodi wao," alisema.Alisema siyo vizuri kwa Wajerumani kama alivyosema rais wao mstaafu na wafadhili wengine wanaotoa fedha kwa ajili ya kuwasaidia Watanzania wakasikia kwamba fedha wanazotoa kwa ajili ya maendeleo ya nchi zinaishia kwenye kulipana posho. Mkazi wa Dar es Salaam, Juma Pembe, alipinga wabunge kulipwa posho hiyo akisema kuwa ni kazi kwa kuwa jukumu lao ni kutunga sheria. Alihoji kama Waziri Mkuu, Mizengo Pinda anasema kiasi wanacholipwa wabunge ni kidogo, inakuwaje kwa watumishi wanaolipwa Sh. 135,000 kwa mwezi kuishi na kuzihudumia na familia zao.

Pembe alikosoa kauli ya Pinda kuwa fedha za wabunge zinaishia kwa wapiga kura na kuhoji ni wapiga kura wangapi wanawagawia fedha hizo.

UPINZANI WASUBIRI KESHO

Katika hatua nyingine, Kambi ya Upinzani Bungeni, imesema itaeleza hatua za ziada itakayochukua iwapo wakati wa kuhitimisha mjadala wa bajeti kesho, serikali haitatoa ufafanuzi bungeni jinsi itakavyofanya mabadiliko katika mfumo wa posho katika utumishi wa umma.

Kambi hiyo pia imeelezea ilivyokerwa na kauli iliyotolewa na Pinda ya kuhalalisha posho kwa wabunge kwamba zinahitajika kwa ajili ya kuwapa watu wanaowaomba fedha nje ya ukumbi wa Bunge.Imesema kauli hiyo inahamasisha siasa za fadhila.

Ilalamikia kauli ya Pinda kuwa wabunge wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wanamezea mate posho hizo kuwa inalenga katika kujaribu kuonyesha kwa umma kwamba hoja ya kutaka mabadiliko katika mfumo wa posho ni ya wabunge wachache.

Akizungumza na waandishi wa habari jana mjini Dodoma,Katibu wa Wabunge wa Upinzani, John Mnyika, alimtaka Pinda kufuta kauli zake hizo, "Na iwapo Bunge halitatoa ufafanuzi ikiwemo hatua mahususi kuelezwa bungeni kuhusu serikali itakavyoweza kufanya mabadiliko katika mfumo wa posho katika utumishi wa umma wakati wa kuhitimisha mjadala wa bajeti, tutakaa kama Kamati ya wabunge wa chama kwa mujibu wa kanuni za Kudumu za Bunge kifungu namna 109 na 110 kama sehemu ya kuweka msimamo wa pamoja kuhusu bajeti na kueleza hatua za ziada ambazo tutachukua kuhusu posho hizo (Sitting allowance) na ubadhirifu mwingine," alisema Mnyika.

Akizungumza hoja ya kutaka posho zifutwe, Mnyika alisema kuwa hoja hiyo imeainishwa katika ilani yao ya uchaguzi ya Agosti mwaka jana kifungu namba 5.5., kipengele cha tano kimeelezea jinsi CCM inavyotenga kiwango kikubwa kwa ajili ya posho. Alisema ilani hiyo imefafanua lengo la kupunguza posho hizo kwa zaidi ya asilimia 80 zikiendana na ongezeko la mishahara kwa watumishi wa umma kuendana na ujuzi, nafasi na wajibu. Aliongeza kusema kuwa suala hilo limezungumzwa katika vikao vya chama hicho na kuainishwa katika bajeti mbadala ya upinzani iliyosomwa na Waziri Kivuli wa Fedha na Uchumi, Zitto Kabwe.

Mnyika alisema posho hiyo haitajwi katika katiba ya nchi wala sheria yoyote na kwamba posho hiyo imetolewa kwa mujibu wa kifungu namna 10 (d), nne ambacho kinampa ridhaa Rais kutoa poshi zingine kwa Wabunge. Alisema mamlaka hiyo ndiyo iliyofanya kutolewe waraka wa Katibu Mkuu Kiongozi Ofisi ya Rais wa Oktoba 25, mwaka jana wenye kumbukumbu CAB 111/338/01/83. Alimtaka Rais Jakaya Kikwete kufuta posho hizo haraka badala ya kusubiri mabadiliko ya kisheria na kikatiba kama Pinda alivyoeleza bungeni.

PINDA AKOSOLEWA

Katika hatua nyingine, Chadema kimesema Pinda sio mtoto wa mkulima kwa kuwa ameonyesha mfano mbaya kwa Watanzania kutokana na kutetea posho za vikao anazolipwa Mbunge pamoja na watumishi wengine wa serikali. Kimesema awali kiliamini kuwa Pinjda ni mtoto wa mkulima, lakini kutokana na kauli aliyoitoa bungeni wiki iliyopita, ameonyesha kuwa anakumbatia matajiri na kujali maslahi ya watu wachache. Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano wa Chadema, Erasto Tumbo, aliwaambia waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam kuwa kauli ya Pinda imeonyesha dharau kubwa Watanzania zaidi ya milioni 40. Kutokana na kuali hiyo, Chadema kimemtaka Pinda kutafuta jina lingine la kujiita badala ya mtoto wa mkulima.

 
Kinachokataliwa sio posho ya kujikimu. Ugomvi wangu mimi ni posho ya kikao. Kwa nini wabunge walipwe posho za vikao wakati wanafanya kazi za kibunge? Basi na wafanyakazi wa idara mbalimbali za serikali basi nao walipwe posho kama hizo. Wawe madaktari, walimu, polisi, wahandisi, wahasibu, nk.
 
Hilo la vikao vya bodi sina comment kwa kuwa sijui kama bodi ambazo members wao siyo executive na hawalipwi mishahara itakuwaje .[/QUOTE said:
Watalipwa gharama za usafiri na perdiems. Siiting allowance inafidiwa na "Directors' fees"
 
wewe si bi magamba kwanini upigie CDM au na wafanyakazi wa magamba mlikuwa na mpango wa kuipigia cdm 2015... Poleni maana chama kinauwawa na wenyewe!

Cdm inawahitaji wafanyakazi ambao hawapokei posho za vikao kama wewe unapokea basi baki hukohuko magambani lasivyo vua kwanza gamba lako la ufisadi wa posho za vikao!
 
Back
Top Bottom