Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 1,817
- 4,566
SIASA: Jeshi la Polisi jijini Dar es Salaam limetoa kibali kwa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kufanya Maandamano yaliyotangazwa kufanyika Januari 24, 2024 katika baadhi ya Mitaa ya Jiji la Dar
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Polisi Wilaya ya Kipolisi Kariakoo, Jeshi la Polisi limesema Maandamano hayo hayatazuiwa na Polisi iwapo tu hayataleta uvunjifu wa amani au kusababisha vitendo vya kihalifu
Jeshi la Polisi limeitaka CHADEMA kuhakikisha inazuia lugha za uchochezi na kejeli zinazoweza kusababisha uvunjifu wa Sheria. Pia, limeagiza kufuatwa kwa taratibu katika maeneo yote ambayo chama hicho kimetoa taarifa za kufanya maandamano
---
BARUA YA POLISI
Kumb.Na. GB.795/1054/01/03 23/01/2024CHAMA CHA DF.MOKRAS1A NA MAENDELEO
PO BOX31191
UFIPA STREET KINONDONI
DAR ES SALAAM
FAX / TEL NO (0222668866)
email :info@chadema.or.lz
websiteiwww.chadema.or.tz
YAH: TAARIFA YA MAAMDAMANO
Tafadhali husika na soino tajwa hapo juu na rejea barua yako yenyc Kumb: Na.C/ADM/MS/l 1/59 ya tarehe 16/01/2024.
Kwa mujibu wa Sheria, Kanuni na taratibu zinazohusu ’'taarifa za MAANDAMANO, hayatazuiwa na Jeshi la Polisi iwapo Maandamano hayo hayataleta uvunjifu wa amani, au kusababisha kutendeka kwa vitendo vya kihalifu.
Kwa barua hii viongozi wa CDM na wanachama mnalojukumu la kuzuia lugha za uchochczi, kcjeli zinazowcza kupclekea kutendcka kwa vitendo vya uvunjaji wa shcria. Mtalaztmika kufuata utaratibu wa kisheria katika macneo yotc kwa kadri mtakavyoclekezwa na wasimamizi wa shcria Polisi w .kiwa ni kiongozi
katika eneo bilo mlilolitolca taarifa.
Maandamano hayo yasisababishe uvunjivu wa amani/watu kuibiwa au kuporwa na yawe kwenyc njia zilizokubaliwa.Taarifa ycnu pia izingatie muda wa kilichoelezwa kwenye barua ycnu ikiwa ni pamoja na kutoanzishwa mambo mengine ambayo hayamo kwenyc taarifa iliyotol'ewa Polisi.
5. Aidha ukiukwaji wowote wa masharti hayo utalilazimisha Jeshi la Polisi kuchukua hatua za kisheria bila kusita ili kuzuia madhara ya kuvunjika kwa amani.
6. Naamini msingi wa taarifa yenu utabaki kuwa ni kudumishwa kwa amani na utulivu uliopo nchini
MKUU WA POLISI (W) KARIAJ^QO,uXi
DARES SALAAM^a ya KA^Ak..
DARES SALAAM^a ya KA^Ak..
NAKALA
Mkuu wa Wilaya ya Ilala - Kwa taarifa tafadhali.
Kamanda wa Polisi (M) Ilala - Kwa taarifa tafadhali.
PIA SOMA:
- Jeshi la Polisi: Hatujakubali au kukataa maandamano, tutawapa majibu tarehe 23
- Kama Jeshi litafanya usafi tarehe 23-24, basi CHADEMA ifanye maandamano tarehe 25 wapite njia zikiwa safi
- CHADEMA yatangaza Maandamano Kupinga Miswada ya Sheria za Uchaguzi iliyowasilishwa Bungeni
- Mbowe: Makubaliano na Jeshi la Polisi yamefikiwa kuwa maandamano yataendelea kama yalivyopangwa