Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,484
- 30,162
Kwa kweli leo tarehe 24, inabidi iingie katika historia kwa nchi hii, kwa kuwa ni kwa mara ya kwanza, tokea tupate uhuru kwa serikali yetu kuruhusu maandamano ya amani ya chama cha upinzani!
Ingawa katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ya mwaka 1977, ibara ya 18(1) na 18(2) inaruhusu maandamano hayo ya amani, lakini wakati wote vyama vya upinzani, vilipokuwa vikiomba vibali hivyo kwa Jeshi la Polisi, jibu limekuwa kukataliwa kwa visingizio vya kuwa maandamano hayo, yataleta uvunjifu wa amani nchini!
Lakini wakati wote chama tawala cha CCM, kimekuwa kikifanya maandamano hayo, bila vikwazo vyovyote!
Wakati wao CCM wamekuwa wakilyatumia majeshi yetu, ili kutuogopesha sisi vyama vya upinzani ili tusiandamane!
Hata katika maandamano haya yaliyofanyika leo, alijitokeza Mkuu wa Mkoa wa Dar, kueleza kuwa wanajeshi wapatao 8,000 na Polisi wapatao 5,000 watashiriki kwenye yaafi, siku hiyohiyo iliyopangwa kwa maandamano hayo ya amani, yaliyotangazwa na Mwenekiti wa Chadema, Freeman Mbowe.
Nimetafakari kwa umakini na kujiuliza, hivi inawezekanaje hawahawa CCM, ambao kwa miaka yote, wamekuwa hawataki kabisa kuruhusu maandamano yoyote ya amani ya vyama vya upinzani, leo hii wakubali ",kiulaini" kabisa maandamano ya Chadema??
Ndiyo nikapata jibu kuwa huenda hata Rais wetu Samia Suluhu Hassan, ameshawachoka hao wahafidhina wake, ndani ya CCM, wasiotaka mabadiliko yoyote ndani ya nchi na wakiamoni pia wao CCM, ndiyo wamepewa "hatimiliki" ya kutawala nchi hii, milele na milele!
Nikapata jibu kuwa, yeye Rais Samia, ambaye pia ndiye Amiri Jeshi Mkuu, ametoa baraka, maandamano hayo yafanyike, kwa kuwa ameshawachoka wahafidhina ndani ya chama chake na wale wanaojiita chawa wa Mama!
Mungu ibariki Tanzania
Ingawa katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ya mwaka 1977, ibara ya 18(1) na 18(2) inaruhusu maandamano hayo ya amani, lakini wakati wote vyama vya upinzani, vilipokuwa vikiomba vibali hivyo kwa Jeshi la Polisi, jibu limekuwa kukataliwa kwa visingizio vya kuwa maandamano hayo, yataleta uvunjifu wa amani nchini!
Lakini wakati wote chama tawala cha CCM, kimekuwa kikifanya maandamano hayo, bila vikwazo vyovyote!
Wakati wao CCM wamekuwa wakilyatumia majeshi yetu, ili kutuogopesha sisi vyama vya upinzani ili tusiandamane!
Hata katika maandamano haya yaliyofanyika leo, alijitokeza Mkuu wa Mkoa wa Dar, kueleza kuwa wanajeshi wapatao 8,000 na Polisi wapatao 5,000 watashiriki kwenye yaafi, siku hiyohiyo iliyopangwa kwa maandamano hayo ya amani, yaliyotangazwa na Mwenekiti wa Chadema, Freeman Mbowe.
Nimetafakari kwa umakini na kujiuliza, hivi inawezekanaje hawahawa CCM, ambao kwa miaka yote, wamekuwa hawataki kabisa kuruhusu maandamano yoyote ya amani ya vyama vya upinzani, leo hii wakubali ",kiulaini" kabisa maandamano ya Chadema??
Ndiyo nikapata jibu kuwa huenda hata Rais wetu Samia Suluhu Hassan, ameshawachoka hao wahafidhina wake, ndani ya CCM, wasiotaka mabadiliko yoyote ndani ya nchi na wakiamoni pia wao CCM, ndiyo wamepewa "hatimiliki" ya kutawala nchi hii, milele na milele!
Nikapata jibu kuwa, yeye Rais Samia, ambaye pia ndiye Amiri Jeshi Mkuu, ametoa baraka, maandamano hayo yafanyike, kwa kuwa ameshawachoka wahafidhina ndani ya chama chake na wale wanaojiita chawa wa Mama!
Mungu ibariki Tanzania