----Imekuwa kawaida watu wakiwa katika kipindi cha uchumba wanapenda kwenda outing kwa pamoja, utakuta mara nyingi haswa siku za weekend watu tunatoka out kujiburudisha/ kujiliwaza baada ya uchovu wa kazi na majukumu ya week nzima. Mnaweza kwenda kuhang out clubs, bar,beach, pub au restaurant.Inategemea sehemu gani mnayopendelea.
Hawa wachumba baada ya kuwa wanandoa, haswa kwa wanaume utakuta ni wachache wanaoambatana na wake zao au family zao kwenda outing. Hapa bongo siku za weekend bar nyingi zinajaa wanaume, na hawa wanaume ni watu ambao wanandoa zao.
Swali langu ni hili, je wewe mwanaume inakuwaje unamuacha mkeo nyumbani na kwenda bar peke yako?
Na wewe mwanamke inakuwaje ukubali mumeo aende bar peke yake na wakati ilikuwa kawaida yenu kwenda pamoja kipindi cha uchumba?
Haya wanajamii tujadili hapa, najua wapo wanandoa humu wanaoenda out haswa bar na kuwaacha wake/waume nyumbani.
Shemeji chrispin naomba agonge hii link wakati tunaendelea...!
http://www.thesun.co.uk/sol/homepage/sport/football/2703773/Arsenal-2-Liverpool-1.html
Now I propose outing ya mimi,My LOVE, wewe shem,Fidel80 na wapwa wengine close ili Fidel aelezee anayosema.
mimi nafikiri wanawake wavivu sana kuwa mbia waume zao the way they feel, wanataka kila mara waume ndo wapange what is next hata kupanga outing
Wakati mwingine wanawake pia tusipende tu kusubiri kutolewa out, inabidi na sisi tuwe mstari wa mbele kupanga outing na kuwatoa waume zetu. Mi wangu tuna sheria, kila nikimtoa mara moja yeye anarudisha mara tatu. so hajisikii kama anaumizwa na budget maana hata mimi nashiriki.
Hey Pretty hapa kuna maswali mawili
Unataka tuende na wake zetu bar au twende nao outing
Please specify hoja yako ieleweke
NN
mzima kipenzi nawackiliza hawa wakaka humu na stori zao wanazoenda kuongelea bar, mie mwenzenu kwa kweli najotokeaga tu nikirudi kanuna lakini ndio nimetoka hivyo jpili tupo hapo home nikiona anabadili tshirt na mie nabadili jeans, namwambia nakucndikiza uendako, anajua akinikatalia nitatoka tu mwenyewe anajikubalia tu safari inaanza.
Nyamayao hapa kweli umenena, hawa watu dawa ni kufuatana tu. Ukiona anaanza kujiandaa na wewe wajiandaa, mnaenda wote kuzitumia.
ndio Pretty ukisubiri kuambiwa tutoke utakaa sana....
Ni kweli tuna majukumu mengi lakini kuna wakati wa kutoka out ,utasikia eti ooh naenda kubadilishana mawazo na marafiki zangu kwani sisi hatutaki kubadilishana mawazo??
Hivi Nyamayao ungeolewa na wale jamaa wa Tarime huko Msoma ungethubutu kufanya hivyo?
hata langu la huko shy kwani wanatofauti sana bac? na ningetoka tu.
Na sijui kama unaelewa kuwa watu wa Tarime wakitembeza fito na vibao usoni ndo ishara ya upendo
outing zenyewe kama ni zike mnakwenda pamoja mnaagiza kinywaji/chakula kisha kila mtu gazeti basi afadhali nijipikie sima nyumbani! duh basi ukiwaona na wenzao wamechngamka kweli kweli. hivi ndoa huwafanya watu aje? mara mnakaa hamna cha kuambiana????????????? inatisha eti!!!!