Bramo
JF-Expert Member
- Oct 21, 2009
- 13,160
- 10,007
AHADI - ALIITOA AKIWA WAPI...
---2005 Alikuja na Maisha bora kwa kila Mtanzania,hili halina ubishi lilikuwa ni changa la macho kwa Watanzania,Kama haitoshi akasema anawajua kwa majina wala rushwa,lakini hatuoni hata mmoja aliyemchukulia hatua===hii ni kutaka sifa na popularity.
---Juzi amekuja na mpya ya kumpatia kila mwanafunzi Computer ambayo iko connected kwa internet, it's high time now kwa watanzania kuhoji uwezo wa RAIS wetu,ni kwamba anafanya Wa Tanzania ni wapumbavu sana kiasi kwamba hawawezi ku reason kuwa hilo sual haliwezekani???
Hata kwa wanafunzi tu wa vyuo vikuu hilo suala halitekelezeki leo anatuambia ataanza na shule za msingi,umeme ni tatizo..hivi jk anajua kuwa its only 10% ya wa Tanzania wana access na umeme na 0.05% ya watanzania ndo wanaweza kutuima computer na wana access na internet,hata kwa nchi ambazo zimeendelea kuzidi sisi hilo suala halipo,,yeye anataka kuhadaa Wa Tanzania aili aendelee kubaki madarakani!!!!!me nadhani pia JK na uwezo mdogo sana wa ku reason ndo maana hata hafikirii kuwa suala kama hilo watu wenye akili timamu hawawezi kusadiki,inahitaji mtu mwenye akili za mwenda wazimu kuamini ahadi kama hizo.
----WITO WANGU
Nawaomba wana JF wooote..mu influence watu wenu wa karibu wasimchague JK na CCM yake,watatoa ahadi nyingi sana,watasema watajenga fly over,watasema watajenga majumba angani--->tuwapuuuze na ahadi zao hizo...tuwaulize kati ya zile walizoahidi 2005 ni ngapi wametekeleza mpaka tuwape ajira nyingine kwa miaka mitano!!!!!!
Watakuja na gia ya kuwa wamejenga DOdoma University,tuwapuuze pia kwa sababbu kwanza ulikuwa ni ukumbi wa bunge wa zamani (chimwaga),halafu huo ni wajibu wake...tuipuuzie kete ya kipuuzi kama hii.
SAY NO TO CCM-----SAY NO TO JK-----WANYIMENI KURA
-----------------------------
[h=2]Miezi 22 kabla ya uchaguzi mkuu:Tujikumbushe ahadi za Kikwete 2010, ngapi zimetekelezwa hadi sasa?[/h]
- Kujenga reli mpya kutoka Dar es Salaam mpaka mikoa ya Kanda ya ziwa - Nzega, Tabora
- Mkoa wa Tanga kuwa Jiji la Viwanda - Tanga mjini
- Tabora kutumia maji ya Ziwa Victoria - Igunga
- Kulipa madeni ya chama cha Ushirika mkoa wa Shinyanga (SHIRECU) - Shinyanga
- Kumaliza migogoro ya Ardhi nchini - Dodoma
- Wakulima kuacha kutumia jembe la mkono - Dodoma mjini
- Kuwapatia trekta wakulima - Kata ya Mrijo, Dodoma
- Wananchi kutoondolewa kwenye Ranchi ya Misenyi - Kagera
- Kujenga Uwanja wa Ndege Misenyi - Kagera
- Kupanua Uwanja wa Ndege Bukoba - Bukoba Mjini
- Kujenga uwanja wa ndege mkubwa Kigoma - Kigoma Mjini
- Mtukula kupatiwa umeme kutoka Uganda - Kagera
- Mikoa ya Kagera, Kigoma, Lindi, Rukwa na Ruvuma kuunganishwa katika gridi ya taifa ya umeme - Kagera
- Kuimarisha Takukuru kwa miaka mitatu - Kagera
- Hukumu kwa waliopatikana na hati ya kuua albino - Mbeya
- Kununua meli kubwa kuliko MV Bukoba - Kagera
- Kuanzisha benki ndogondogo kwa ajili ya wajasiriamali
- Serikali kuvisaidia vyama vya ushirika - Mwanza
- Kuimarisha usalama Ziwa Victoria na Ziwa Tanganyika kwa kupeleka kikosi maalum chenye vifaa kupambana na wahalifu - Mwanza
- Wilaya ya Geita kuwa hadhi ya mkoa Januari mwakani - Geita
- Kulinda muungano kwa nguvu zote - Pemba
- Kuwajengea nyumba waathirika wa mafuriko Kilosa - Morogoro
- Kununua meli mpya kubwa Ziwa Nyasa - Mbeya mjini
- Kujenga bandari Kasanga – Rukwa
- Kumaliza tatizo la walimu miaka mitano ijayo - Songea
- Kufufua mgodi wa makaa ya mawe Kiwira - Mbeya
- Kuzuia hatari ya kisiwa cha Pangani kuzama - Tanga
- Kununua bajaji 400 kwa ajili ya kubeba wajawazito hasa vijijini - Iringa
- Kujenga barabara yenye kiwango cha lami kutoka Same mpaka Kisiwani – Kihurio na kuiunganisha na barabara kuu ya Moshi - Dar es salaam - Same mkoani Kilimanjaro
- Kumaliza tatizo la maji katika wilaya ya Same - Same Mjini
- Kuboresha barabara za Igunga - Tabora
- Kusambaza walimu 16,000 katika shule za sekondari zenye upungufu makubwa wa walimu - Kisesa Magu
- Kununua vyandarua viwili kwa kila kaya - Mbeya Mjini
- Kuzipandisha hadhi hospitali maalumu saba nchini kuwa za rufaa ili kuipunguzia mzigo Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MHN) - Hydom Manyara
- Kulinda amani nchini kwa kuzuia chokochoko za kidini, kikabila na kisiasa - Musoma
- Kulinda haki za walemavu - Makete
- Kujenga baabara ya Njombe - Makete kwa kiwango cha lami,urefu wa kilomita 109 - Iringa mjini
- Kujenga barabara Musoma – Mto wa Mbu Arusha - Arusha
- Kuanzisha jimbo la Ulyankulu- Shinyanga Mjini
- Kujenga barabara ya lami Manyoni-Kigoma – Kaliua,Tabora
- Kukarabati barabara ya Arusha Moshi - Arusha Mjini
- Kuboresha barabara ya Handeni, Kondoa, mpaka Singida - Dodoma
- Kuwafidia wanakijiji ng'ombe waliopotea wakati wa ukame mwaka 2009 - Longido
- Vijiji vyote vilivyoko kilomita 15 kutoka kwenye bomba kuu la mradi mkuu wa maji wa Ziwa Victoria - Shinyanga-Kahama kuunganishiwa maji - Shinyanga
- Tatizo la umeme kufikia kikomo Novemba mwaka huu mkoani Arusha – Arusha mjini
- Kukopesha wavuvi zana za kilimo - Busekera, Wilaya ya Musoma
- Kuwapatia maji wakazi wa Wilaya ya Longido - Longido
- Kujenga barabara ya lami kupitia pembezoni mwa Hifadhi ya Taifa ya Seregenti – Ngorongoro
- Utekelezaji wa mpango wa maendeleo ya kilimo kuwasaidia wafugaji kuweza kupata na kutunza mifugo yao vizuri - Mbulu mkoani Manyara
- Kusambaza maji nchi nzima - Babati vijijini
- Kusambaza umeme, utoaji wa huduma za afya, na uboreshaji wa kilimo cha umwagiliaji na utoaji ruzuku kwa wakulima. mwaka 2010-2015 - Babati vijijini
- Kuongeza mara tatu idadi ya wananchi wanaonufaika na ruzuku ya pembejeo za kilimo kwa mfumo wa vocha - Iringa
- Kuhakikisha Isimani inapata maji ya uhakika - Iringa
- Kuiwekea lami barabara inayokwenda katika Hifadhi ya Taifa ya Ruaha, ambayo ndiyo hifadhi kubwa kuliko zote Tanzania - Iringa
- Kulinda usalama wa wananchi kwa ujumla ili kudumisha amani na sifa ya nchi -Ifunda
- Kutokomeza malaria 2015 - Bunda, mkoa wa Mara
- Kuwapa wanawake nafasi zaidi - Kilolo, Iringa
- Ahadi kuisadia Zanzibar kuendeleza miradi mbalimbali ya kijamii - Kibandamaiti Mjini Zanzibar
- Kuipandisha hadhi hospitali ya Mnazi Mmoja Zanzibar kuwa ya rufaa - Kibandamaiti mjini Zanzibar
- Kuisaidia Zanzibar kila panapohitajika msaada - Kibandamaiti
- Serikali kujenga upya bandari ya Mbambabay - Ruvuma
- Ununuzi wa Meli mpya yenye uwezo wa kubeba tani 400 - Mbambabay Ruvuma
- kufufua chama kikuu cha ushirika cha wakulima wa Mbinga (MBICU) – Ruvuma
- Ahadi Rais wa Marekani Barack Obama kuimwagia misaada Tanzania – Ruvuma
- Ahadi hakutakuwa na umwagaji wa damu baada ya uchaguzi-Dar es Salaam
- Mtwara kuwa mji wa Viwanda – Mtwara
- Ahadi ujenzi wa kwanda cha dawa ya kuua viluilui vya mbu - Kibaha
- Hospitali ya Tumbi kuwa ya mkoa - Kibaha
- Halmashauri ya manispaa ya Kibaha kutenga eneo maalumu la viwanda - Kibaha
---2005 Alikuja na Maisha bora kwa kila Mtanzania,hili halina ubishi lilikuwa ni changa la macho kwa Watanzania,Kama haitoshi akasema anawajua kwa majina wala rushwa,lakini hatuoni hata mmoja aliyemchukulia hatua===hii ni kutaka sifa na popularity.
---Juzi amekuja na mpya ya kumpatia kila mwanafunzi Computer ambayo iko connected kwa internet, it's high time now kwa watanzania kuhoji uwezo wa RAIS wetu,ni kwamba anafanya Wa Tanzania ni wapumbavu sana kiasi kwamba hawawezi ku reason kuwa hilo sual haliwezekani???
Hata kwa wanafunzi tu wa vyuo vikuu hilo suala halitekelezeki leo anatuambia ataanza na shule za msingi,umeme ni tatizo..hivi jk anajua kuwa its only 10% ya wa Tanzania wana access na umeme na 0.05% ya watanzania ndo wanaweza kutuima computer na wana access na internet,hata kwa nchi ambazo zimeendelea kuzidi sisi hilo suala halipo,,yeye anataka kuhadaa Wa Tanzania aili aendelee kubaki madarakani!!!!!me nadhani pia JK na uwezo mdogo sana wa ku reason ndo maana hata hafikirii kuwa suala kama hilo watu wenye akili timamu hawawezi kusadiki,inahitaji mtu mwenye akili za mwenda wazimu kuamini ahadi kama hizo.
----WITO WANGU
Nawaomba wana JF wooote..mu influence watu wenu wa karibu wasimchague JK na CCM yake,watatoa ahadi nyingi sana,watasema watajenga fly over,watasema watajenga majumba angani--->tuwapuuuze na ahadi zao hizo...tuwaulize kati ya zile walizoahidi 2005 ni ngapi wametekeleza mpaka tuwape ajira nyingine kwa miaka mitano!!!!!!
Watakuja na gia ya kuwa wamejenga DOdoma University,tuwapuuze pia kwa sababbu kwanza ulikuwa ni ukumbi wa bunge wa zamani (chimwaga),halafu huo ni wajibu wake...tuipuuzie kete ya kipuuzi kama hii.
SAY NO TO CCM-----SAY NO TO JK-----WANYIMENI KURA
-----------------------------
[h=2]Miezi 22 kabla ya uchaguzi mkuu:Tujikumbushe ahadi za Kikwete 2010, ngapi zimetekelezwa hadi sasa?[/h]
Sijachelewa kuwatakia Heri ya Mwaka Mpya 2014.Hongereni mliouona.
Wakuu tukiwa tunajadili mambo mbalimbali yaliyotokea katika Taifa letu kwa mwaka uliopita, kama yale ya Chadema na Zitto, Rasimu ya katiba mpya namba 2, kujiuzuru kwa waziri wa Maliasili na Utalii na kufukuzwa kwa mawaziri 3 na la mwisho kifo cha waziri wa fedha Mh W.A.Mgimwa, tusisahau kumkumbusha Rais Kikwete na chama chake kuwa kuna ahadi kadhaa bado hawajatekeleza kwa wananchi.
Ahadi ya Kuunganisha Gridi ya Taifa katika mikoa ya Ruvuma na Kigoma
Ahadi hii ilitolewa kwanza Septemba 16, 2005 katika uwanja wa Lake Tanganyika Kigoma kuwa kufikia mwaka 2010 mikoa hiyo ingekuwa imeunganishwa na grifdi ya Taifa ili wakazi wake nao wanufaike na umeme wa uhakika. Ahadi hii ilishindwa kutekelezwa.Octoba 10, 2010 iliahidiwa tena kuwa wazo la kuunganisha gridi ya Taifa katika mikoa hiyo bado ipo pale pale.Ahadi hii ilitolewa mjini Songea katika uwanja wa Majimaji.Je, tujiulize ikiwa imebakia miezi 22 tu toka sasa wamefikia wapi?Je kazi imeanza kweli huko Kigoma? Maana najua Songea bado hata kukata nyasi hawajaanza ili kuweka njia ya umeme.
Ahadi ya maji eneo la Mshangano na Ruhuwiko
Siku hiyo hiyo wakisaidiana na Waziri aliyefukuzwa Bwana Emmanuel Nchimbi waliahidi kuweka maji ya bomba katika maeneo husika, na si tena kina mama kwenda kutafuta maji zaidi ya kiliometa 10.Bwana mkubwa akachombeza kuwa CCM haipo tayari kutengeneza mazingira ya kuvunja ndoa za watu, kisa mama kafuata maji mtoni.
Uwanja wa Ndege Misenyi
Katika kampeni hizo hizo za mwaka 2010 Kikwete aliwaahidi wana Misenyi kuwa atajenga uwanja wa ndege wa kimataifa kabla ya 2015. Je wana wa mkoa wa Kagera tayari matayarisho yameanza?Na je imefikia wapi kazi hii? Maoni yenu tafadhali.
Meli Ziwa Nyasa
Ahadi hii aliitoa akiwa Mbambabay na huko Mbeya kuwa atanunua meli mpya ili kurahisisha usafiri wa wakazi wake katika Ziwa Nyasa.Je mipango hii bado ipo kweli au ndio wamesahau kama waliahidi?
Machinga Complex Temeke na Kinondoni
Bila kusahau wakazi wa Dar waliahidiwa kujengewa Machinga Complex zingine katika wilaya zao maana kwa wakati huo walikuwa wamejenga pale Ilala. Sasa akasema kila wilaya itapata machinga Complex yake.
Naomba maeneo mengine waongezee kama zimetekelezwa au Zipo nusu ya kumalizika.
Naomba kwa muda tuwasahau Chadema na Zitto maana CCM kwa matatizo hayo ndio wanapata pa kujisahaulisha zaidi.Wanajua wanachi wako "busy" kujadili mambo yasiyokuwa na tija kwao moja kwa moja bali kwa watu wachache.
Nawasilisha